Tuesday, August 12, 2014

BUNGE MAALUMU LA KATIBA MTEGONI TENA LEO

Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba,Samuel Sitta. PICHA |MAKTABA

Mjadala kuhusu masuala ya Muungano unatarajiwa kurejea upya katika kamati za Bunge Maalumu leo, wakati zitakapoanza kujadili sura za saba, nane, kumi na moja, 18 na 15 za Rasimu ya Katiba.
Kamati zimepewa siku sita kujadili sura hizo tano ambazo zina jumla ya ibara 79, huku miongoni mwake zikigusa masuala mengi ambayo msingi wake umejengwa juu ya mfumo wa serikali tatu.
Miongoni mwa masuala hayo ni pamoja na baraza la mawaziri, tume ya kusimamia na kuratibu uhusiano baina ya Serikali ya Muungano na Serikali za Nchi Washirika (Tanganyika na Zanzibar), Sekretarieti ya Tume ya Uhusiano na Uratibu, Masuala yanayohusu Benki Kuu na Fedha pamoja na uteuzi wa watumishi katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Suala la aina ya muungano lilianza kujadiliwa katika sura ya kwanza na ya sita katika awamu ya kwanza ya Bunge iliyomalizika mwishoni mwa Aprili mwaka huu na kuzua mvutano mkali ambao hatimaye ulisababisha baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalumu kususia mchakato huo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

UNYAMA HUU: BINTI WA KAZI AMWAGIWA UJI NA MKE WA BOSI WAKE KISA WIVU WA MAPENZI...!!!


MSICHANA mmoja mkazi wa eneo la Minga katika Manispaa ya Singida (muuza duka), amenusurika kifo baada ya kumwagiwa uji wa moto na mke wa tajiri yake na kumsababishia maumivu makali kutokana na kile kinachosadikiwa kuwa ni wivu wa kimapenzi.

Muuguzi wa zamu katika Hospitali ya mkoa wa Singida, wodi namba mbili ya wanawake, Anna Sprian amefahamisha kuwa binti huyo amejeruhiwa sehemu za sikio la upande wa kulia na mgongoni, ambapo amesema hali ya mgonjwa huyo inaendelea vizuri kutokana na matibabu anayoyapata hospitalini hapo.
Akizungumza Agosti 10, 2014 kwa tabu, binti huyo Jackline Lasway (23), maarufu kwa jina la Pendo, amesema majeraha ya moto yapo katika sehemu ya sikio la upande wa kulia na mgongoni.
Pendo amesema kuwa tukio hilo limetokea Jumamosi Agosti 9, 2014 saa nane mchana wakati akiwa dukani kwa bosi wake aliyemtaja kwa jina la, Charles Kamnde.

Amesema akiwa anaendelea na kazi zake za kuuza bidhaa mbalimbali dukani hapo, ghafla alitokea mke wa bosi wake akiwa na chupa yenye uji wa moto na kuwa alimmwagia usoni ambapo baada ya kumwagiwa uji huo alitaka kujiokoa ili usimmwagikie usoni na ndipo ulimuunguza kwenye sikio la kulia na mgongoni na kuwa baada ya mke wa bosi wake kumkosa uso alitoa kisu kutaka kumchoma kifuani. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMANNE AGOSTI 12, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.

.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

BBC YAZINDUA OFISI MPYA DAR

Wafanyakazi wa BBC wakiwa kazini kupeperusha matangazo ya Dira ya Dunia redio
Idhaa ya kiswahili ya BBC imezindua rasmi studio zake mjini Dar es Salaam kwa mbwembwe na haiba kuu.
Uzinduzi huo ni matokeo ya mkakati na uwekezaji wa miaka mingi wa shirika la BBC duniani kuhakikisha kuwa matangazo yake yanawafikia wasikilizaji katika hali ya ubora wa hali ya juu na ya kisasa zaidi.
Katika hafla hiyo iliyoandaliwa katika ofisi hizo hizo mpya zilizoko eneo la Mikocheni, mkuu wa kitengo cha uandishi wa habari katika BBC, Nicki Clarke, ameshukuru serikali ya Tanzania, kwa kuwaruhusu kujenga studio hizo za kisasa zitakazoinua tasnia ya habari nchini humo na uhuru wa habari kwa ujumla.
Naye mkuu wa ofizi ya Dar es Salaam, Hassan Mhelela mbali na kuwataka wafanyakazi wa BBC Tanzania, kuzidi kuonyesha ushirikiano pamoja na utendaji kazi wa pamoja, pia ametangaza kuanishwa rasmi kwa ushirikiano kati ya BBC na chuo kikuu cha Dar es Salaam kitengo cha uandishi wa habari.
Eric David Nampesya akizipa taabu Tumba kwenye sherehe ya ufunguzi wa ofisi za BBC Dar es Salaam
Ushirikiano huo amesema kuwa unalenga kusaidia kutoa mafunzo kwa wandishi wa habari chipukizi walioko mafunzoni katika chuo hicho, ambao kwa nyakati tofauti, watakuwa wakijiunga na BBC ili kupata mafunzo katika uandaaji vipindi vya redio na televisheni pamoja na utangazaji.
Kwa upande wa BBC, kuanzishwa kwa ofisi hii, yenye studio za kisasa kabisa za redio na televisheni mbali na kuongeza ubora wa vipindi lakini pia kutawezesha matangazo ya redio na televisheni kufanyika moja kwa moja kutokea Dar es Salaam.
Na kuanzia sasa matangazo ya Amka na BBC yatakuwa yakiandaliwa Dar es Salaam.
Itakumbukwa kuwa Tanzania mbali na kuwa na wasikilizaji wengi wa idhaa ya kiswahili ya BBC, lakini pia ndiko kunakozungumzwa zaidi lugha ya kiswahili.
Tanzania pia ina rekodi ambapo mtangazaji wa kwanza au sauti ya kwanza iliyosikika mwaka 1957, ilikuwa ya mtanzania Oscar Kambona ambapo alikuwa mwanafunzi mjini London. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Monday, August 11, 2014

BUNGE LAKODI VIPAZA SAUTI KWA SH. 8.9 MILLION KILA SIKU....!!!


Kwa maana hiyo Bunge, hilo linatumia Dola 5,400 sawa na Sh8.91 milioni kwa siku kugharimia vipaza sauti katika vyumba 12 vinavyotumiwa na kamati hizo na kwa siku 16  ambazo kamati zitakutana, gharama hizo zitafikia Sh142.56


Wakati kukiwa na malalamiko kwamba Bunge la Maalumu la Katiba linagharimu fedha nyingi za walipakodi, uongozi wa taasisi hiyo umetumia Sh142.56 milioni kukodi vipaza sauti kutoka Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).

Katibu wa Bunge Maalumu, Yahya Khamis Hamad alithibitisha kukodiwa kwa vipaza sauti hivyo kwa ajili kamati zote 12 na kwamba kila gharama ya chumba kimoja kwa siku ni Dola 450 za Marekani (Dola moja ni wastani wa Sh1,650).

Kwa maana hiyo Bunge, hilo linatumia Dola 5,400 sawa na Sh8.91 milioni kwa siku kugharimia vipaza sauti katika vyumba 12 vinavyotumiwa na kamati hizo na kwa siku 16  ambazo kamati zitakutana, gharama hizo zitafikia Sh142.56. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MREMA AWATAMBIA UKAWA, AMUONYA MBATIA

Mbunge wa Vunjo, Augustine Mrema (TLP)

Mbunge wa Vunjo, Augustine Mrema (TLP) amedai kitendo cha yeye kubaki kwenye Bunge Maalumu la Katiba kumetumiwa vibaya na wahasimu wake wa kisiasa jimboni kwake.

“Ukawa na ubunge wa Vunjo vimegeuka propaganda chafu dhidi yangu. Wamediriki kuwaambia wananchi wangu kuwa nimeahidi kuwaachia jimbo langu,” alisema.
Mrema ambaye pia ni mwenyekiti wa taifa wa TLP, alitoa kauli hiyo jana jimboni kwake katika mkutano na waandishi wa habari aliouitisha kuelezea kwa nini hakuwaunga mkono Ukawa.
Mrema alisema malengo ya Ukawa siyo katiba bali Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 na ndiyo maana tangu waliposusia Bunge agenda yao imebadilika na kuwa muungano wa kuelekea uchaguzi 2015.
“Mimi nimeamua kubaki bungeni kwa ajili ya masilahi mapana ya wananchi wa jimbo langu la Vunjo na Watanzania kwa jumla. Sitishwi na Ukawa na nitatetea kiti changu 2015,” alisisitiza.
Mrema alitumia mkutano huo kumshambulia mbunge wa kuteuliwa na Rais, ambaye ni James Mbatia kutokana na uamuzi wake wa kutangaza nia ya kuwania ubunge wa Jimbo hilo mwakani. Kwa mujibu wa Mrema, ndiye Mtanzania pekee mwenye sifa na aliweza kugombea ubunge katika majimbo matatu tofauti na kushinda.
“Mimi ni Mtanzania pekee ambaye nimewahi kuwa mbunge wa majimbo matatu tofauti ya Moshi Vijijini, Temeke na Vunjo. Sifa hizo hazipo kwa wengine,” alisema. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ZESCO YATIBUA SHEREHE YA SIMBA DAY...!!!

Mabao matatu yaliyofungwa na Jackson Mwanza, Clatons Chama na Winston Kalenga, yamesababisha siku ya Simba ‘Simba Day’ kuwa chungu baada ya Zesco kuizamisha miamba hiyo kwa mabao 3-0.
Safu ya ulinzi ya Simba iliyoshindwa kuelewana iliizawadia Zesco ya Zambia mabao matatu, wakati wa mchezo huo wa kuadhimisha siku muhimu ya klabu hiyo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ikiwa inatumia mchezo huo kwa ajili ya kutambulisha wachezaji wake wapya iliyowasajili, Simba iliendeleza rekodi yao ya kutoshinda katika mchezo wa Simba Day tangu kuanza kuiadhimisha siku hiyo.
Ukihudhuriwa na mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Fedha, Adam Malima, ambaye aliwataka Simba kucheza kimataifa zaidi, kikosi hicho cha kocha Zdravko Logarusic kilijikuta katika siku mbaya msimu huu.
Simba ilianza kuruhusu bao la kwanza dakika ya 14, wakati Mwanza akiunganisha kwa kichwa krosi safi kutoka wingi ya kushoto. Mabeki wa kati wa Simba, Donaldi Mosoti na Joseph Owino walionekana kushindwa kujua nani wa kumkaba na kumuacha Mwanza akiruka peke yake.
Mshambuliaji mpya wa Simba, Paul Kiongera alishirikiana vizuri na Amissi Tambwe, lakini hawakuwa makini kwani Tambwe alikosa nafasi kadhaa za wazi.
Nafasi ya kwanza kwa Tambwe ilikuwa dakika ya saba, wakati shuti la Kiongera lilipopanguliwa na kipa wa Zesco, lakini Tambwe alishindwa kuumalizia mpira huo vizuri.
Simba ilikuwa na kipindi cha pili kibaya zaidi, kwani mabeki wake wa kati walisababisha penalti kwa kumwangusha Chama aliyekuwa anakwenda kufunga na mshambuliaji huyo kuukwamisha mkwaju huo wavuni.
Dakika tano za nyongeza zilikuwa mbaya zaidi kwa Simba, ambapo shambulizi la kushtukiza lilizaa bao baada ya mabeki wa Simba kwa mara nyingine wakishindwa kuondoa krosi ndogo ambayo ilimaliziwa kiufundi na Kalenga. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATATU AGOSTI 11, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MADAKTARI WATOA TAHADHARI YA EBOLA

madaktari wakitoa huduma dhidi ya Ebola
Shirika la Madaktari wasio na mipaka Medecins Sans Frontiers wametahadharisha kuhusu wizara ya afya nchini Liberia kuzidiwa nguvu na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola katika eneo la Afrika Magharibi.
Mratibu wa mambo ya dharura wa shirika hilo nchini humo amesema serikali haikutilia maanani vya kutosha madhara ambgayo yangesababishwa na ugonjwa huo na kwamba mfumo wa afya kwa sasa upo katika hali ya kushindwa.
Nchini Siera Lione, majeshi yameweka vizuizi katika maeneo yaliyoathirika na ugonjwa huo.
Raia wa Uingereza ambaye ni mfanya biashara katika eneo la Kanema kaskazini mwa nchini hiyo anaeleza madhara wanayopata kutokana vizuizi vya zilivyowekwa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAREKANI KUENDELEA KUISHAMBULIA IRAQ

Wapiganaji wa Kurdi
Marekani imeendeleza mashambulizi ya anga kaskazini mwa Iraq kwa lengo la kuwasaidia Wakrud katika mji wa Erbil dhidi ya wapiganaji wa kiislam wa kundi la Jihad.
Wapiganaji wa kundi hilo la Kiislam hivi karibuni wameendelea kuimarisha ngome yao katika eneo hilo ikiwa ni pamoja na kuiteka ngome kubwa ya Iraq katika mji wa Mosul. Jeshi la Marekani limesema limefanya mashambulizi dhidi ya wapiganaji wa Sunni waliokuwa wamejificha katika milima iliyo eneo la wakimbizi la Yazid.
Hata hivyo Uingereza imesema inaendelea kutoa misaada ya kibinadamu kwa Wakurdi ambapo Ofisa wa zamani wa mambo ya kigeni wa Uingereza Alistair Burt anasema nchi hiyo inaweza kusaidia eshi la Wakurdi.
Wakati huo huo vikosi vya majeshi ya Iraq na vyombo vya usalama vimesambaa katika katika maeneo mbalimbali ya mji wa Baghdad huku kukiwa na hali ya wasiwasi kufuatia kauli iliyotolewa na waziri mkuu wa nchi hiyo ya Iraq Nouri al-Maliki inayodaiwa kuwa ni ya utovu wa nidhamu kwa Rais wa nchi hiyo Fuad Masum.
Amesema kuwa Rais wa Jamhuri hiyo amevunja katiba mara mbili,mara ya kwanza ni pale alipojiongezea muda wa kukaa madarakani,wakati alistahili kutangaza kuvunja bunge. Hata hivyo kipindi chake kiliisha august saba alhamisi iliyopopita.
Hata hivyo papa Francis ameelezea gogoro wa Ira kwamba msingi wake mkubwa ni masuala ya tofauti za kidini. Melfu ya watu nchini Iraq wamekuwa wakilazimishwa na wapiganaji wa kiislam ambao wameimarisha ngome ao kaskazini mwa nchi hiyo.Katika ujumbe wake wa jumapili ,papa Francis ametoa wito kwa dunia kukomesha uhalifu huo unaoendelea nchini Iraq. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Saturday, August 09, 2014

WASALITI UKAWA: WAJIANDAE KUWA 'WABUNGE WA MAHAKAMA'

Mjumbe wa Bunge la Katiba (Chadema) Said Arfi  akisaini karatasi ya mahudhurio bungeni jana, kabla ya kwenda  kushiriki mjadala wa kamati  yake.

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema kuwa wabunge wote walio wanachama wake, lakini wanakiuka msimamo wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kwa kuingia katika Bunge la Katiba, wajiandae kuongeza idadi ya ‘wabunge wa mahakama’.
Kauli hiyo ya tahadhari imetolewa na Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hatua ya baadhi ya wabunge wa chama hicho kuonekana mjini Dodoma, kunakofanyika vikao vya Bunge Maalumu la Katiba (BMK) ambalo Ukawawamesusia kuhudhuria.
“Ni bora wawe wabunge wa mahakama kama mwenzao (akimlenga Zitto Kabwe), kuliko kuendeleza usaliti ndani ya chama. Tunatarajia kukaa na wenzetu kushauriana nini cha kufanya dhidi ya wote wanaoenda kinyume na  msimamo wa Ukawa,” alisema Tundu Lissu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI AGOSTI 09, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

LIPUA LIPUA YA KAMATI ZA BUNGE MAALUMU LA KATIBA

Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba wakitoka kwenye ukumbi wa Bunge mjini Dodoma wakati wa mapumziko ya mchana. Picha na Emmanuel Herman.

Kamati za Bunge Maalumu la Katiba zilizoanza vikao vyake juzi mjini Dodoma, zimejikuta zikifanya kazi kwa kulipua kutokana na uchache wa muda uliotengwa, ikilinganishwa na ukubwa wa kazi ya uchambuzi wa ibara za rasimu ya Katiba hiyo.
Kamati hizo zimetengewa siku 14 kwa ajili ya kujadili na kuchambua sura 15 za rasimu hiyo na siku mbili za kuandaa taarifa ambazo zitaanza kuwasilishwa kwenye Bunge Maalumu, Septemba 2, mwaka huu.
 Hata hivyo, baadhi ya wajumbe wamekuwa wakilalamikia ufinyu wa muda uliotengwa na kwamba kazi imekuwa ikifanyika kwa kulipua, ili kuhakikisha kwamba wanamaliza katika muda uliopangwa.
 Malalamiko hayo yanatokana na ukweli kwamba baadhi ya sura za rasimu zina ibara nyingi ambazo ni vigumu kuzijadili kwa kina, kuzifanyia marekebisho kisha kuzipigia kura kwa lengo la kuzipitisha.
 Waraka wa mgawanyo wa sura kwa siku za mjadala katika Kamati za Bunge Maalumu unaonyesha kuwa kamati zilipaswa kujadili sura ya pili na ya tatu za rasimu hiyo siku ya kwanza zilipoanza kuketi, sura hizo zina jumla ya ibara 13, kazi ambayo baadhi ya wajumbe walisema ilikuwa ni vigumu kuikamilisha kwa siku moja.
 Mwenyekiti wa Kamati namba tano, Hamad Rashid Mohamed juzi alikiri kuwapo kwa changamoto ya muda lakini akasema: “Hiyo ndiyo hali halisi, lazima tutumie muda huo ambao tumepewa na tufanye kazi kwa ufanisi”. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WABUNGE WA CCM WAMEGUKA KATIBA MPYA...!!!




Kwa nini tukae siku 87 au 90 wakati tunajua upande wa pili haujakamilika? Kwa mujibu wa sheria inatakiwa ridhaa ya theluthi mbili. Mwigulu Nchemba 

Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimeanza kumeguka baada ya baadhi ya wabunge wake ambao ni Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, kuunga mkono kauli ya Naibu Katibu Mkuu wake, Mwigulu Nchemba.

Nchemba ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha, Jumanne iliyopita akichangia wakati wa mjadala wa mabadiliko ya kanuni, alilitaka Bunge Maalumu la Katiba lijitathmini kama lina ulazima wa kuendelea wakati hakuna uhakika wa kupatikana kwa theluthi mbili.


Alisema kitendo cha Bunge hilo kukaa kwa siku 84 bila uhakika wa kupatikana kwa theluthi mbili kwa pande zote mbili inayohitajika kupitisha Rasimu ya Katiba Mpya, hakiwezi kueleweka kwa Watanzania.

Nchemba alisema ni vyema kujua idadi ya wanaoshiriki awamu ya pili ya Bunge hilo ili kutoa uthibitisho  kimahesabu kama uamuzi wa kuendelea kwa Bunge unaweza kuwa na maana.

Jana Mwigulu Nchemba alizidi kusisitiza kauli aliyoitoa akisema ni msimamo wake binafsi kama mtoto wa maskini. Alisema anatambua jinsi walipa kodi watakavyoumia, rasimu hiyo itakapokwama kupita kutokana na kukosekana kwa theluthi mbili ya pande zote.


Hata hivyo, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye  juzi alijibu akisema kauli ya Nchemba ni mtazamo wake binafsi na hakuongea kama kiongozi wa chama hicho.

Lakini jana wabunge mbalimbali wa CCM walijitokeza hadharani wakisema wanaunga mkono kauli ya Nchemba ili hesabu ijulikane badala ya kuendelea kutafuna fedha za wananchi bila tija.

Ali Keissy

Mbunge wa Nkasi Kaskazini, Ali Keissy, alisema msimamo wa Nchemba ndiyo msimamo sahihi ambao unapaswa kufuatwa kuliko kuendelea na Bunge wakati wakijua kuwa theluthi mbili haitapatikana.

“Kama kuna wabunge wa CCM wanaounga mkono kauli ya Mwigulu kwa asilimia 100 basi mimi naunga mkono kwa asilimia 500 na wako wabunge wengi tu wa CCM wanaunga mkono,” alisema. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WATU 6 WAUAWA KATIKA GHASIA SOMALIA

Wapiganaji wa Al-shabaab
Takriban watu sita wameuawa katika ghasia katikati mwa Somali.
Ijumaa usiku, wanamgambo kutoka kundi la Alshabaab walishambulia kambi moja ya wanajeshi wa Umoja wa Afrika katika mji wa Buloburde ,yapata kilomita 200 kazkazini mwa mji mkuu wa Mogadishu.
Vikosi vya Amisom viliuteka mji wa Buloburde kutoka kwa Alshabaab mapema mwaka huu,lakini wanamgambo hao bado wanadhibiti eneo kubwa la viungani mwa mji huo.
Wameendelea kutekeleza mashambulizi mjini Mogadishu ili kujaribu kuiondoa serikali inayoungwa mkono na jamii ya kimataifa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...