Saturday, August 09, 2014

WATU 6 WAUAWA KATIKA GHASIA SOMALIA

Wapiganaji wa Al-shabaab
Takriban watu sita wameuawa katika ghasia katikati mwa Somali.
Ijumaa usiku, wanamgambo kutoka kundi la Alshabaab walishambulia kambi moja ya wanajeshi wa Umoja wa Afrika katika mji wa Buloburde ,yapata kilomita 200 kazkazini mwa mji mkuu wa Mogadishu.
Vikosi vya Amisom viliuteka mji wa Buloburde kutoka kwa Alshabaab mapema mwaka huu,lakini wanamgambo hao bado wanadhibiti eneo kubwa la viungani mwa mji huo.
Wameendelea kutekeleza mashambulizi mjini Mogadishu ili kujaribu kuiondoa serikali inayoungwa mkono na jamii ya kimataifa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...