Saturday, August 09, 2014

WASALITI UKAWA: WAJIANDAE KUWA 'WABUNGE WA MAHAKAMA'

Mjumbe wa Bunge la Katiba (Chadema) Said Arfi  akisaini karatasi ya mahudhurio bungeni jana, kabla ya kwenda  kushiriki mjadala wa kamati  yake.

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema kuwa wabunge wote walio wanachama wake, lakini wanakiuka msimamo wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kwa kuingia katika Bunge la Katiba, wajiandae kuongeza idadi ya ‘wabunge wa mahakama’.
Kauli hiyo ya tahadhari imetolewa na Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hatua ya baadhi ya wabunge wa chama hicho kuonekana mjini Dodoma, kunakofanyika vikao vya Bunge Maalumu la Katiba (BMK) ambalo Ukawawamesusia kuhudhuria.
“Ni bora wawe wabunge wa mahakama kama mwenzao (akimlenga Zitto Kabwe), kuliko kuendeleza usaliti ndani ya chama. Tunatarajia kukaa na wenzetu kushauriana nini cha kufanya dhidi ya wote wanaoenda kinyume na  msimamo wa Ukawa,” alisema Tundu Lissu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Baadhi ya wabunge wa  Ukawa hasa kutoka Chadema, akiwamo Leticia Nyerere (Viti Maalumu), John Shibuda (Maswa Mashariki) na Said Arfi (Mpanda Mjini) wameripotiwa kuonekana mjini Dodoma wakijiandikisha kuhudhuria vikao vya Bunge Maalumu la Katiba tofauti na msimamo wa vyama vinavyounda umoja huo, ambao umeahidi kutorudi bungeni mpaka Rasimu ya Pili ya Katiba iliyowasilishwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, itakapojadiliwa.
Mbali ya kuonekana Dodoma, posho  imetajwa kuwa moja ya sababu ya wabunge hao kushawishika kurudi na kuendelea na mchakato huo wa kutunga Katiba uliogomewa na Ukawa.
“Msimamo wa Chadema kwa wasiofanya kama ilivyopangwa na chama unaeleweka. Hatutarajii kumwogopa yeyote; awe Nyerere, Shibuda au Arfi. Tunafahamu kuwa hawa wote wapo Dodoma na wamesaini posho, hivyo watatueleza wakati utakapofika,” alisema Lissu.
Alisema kuwa ana uhakika kuwa Katiba Mpya haiwezi kupatikana. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...