Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph
Warioba amesema kuendelea vikao vya Bunge Maalumu la Katiba bila kuwapo
maridhiano baina ya pande zinazovutana na upande mmoja ukibaki nje ya
Bunge, ni sawa na kutumia vibaya fedha za Watanzania.
Amesema kauli kwamba akidi ya wajumbe wa Bunge
hilo imetimia na vikao vinaweza kuendelea haiwezi kuzaa Katiba
itakayokubaliwa na wananchi wote na ni tofauti na Sheria ya Mabadiliko
ya Katiba inavyoeleza katika sehemu ya kufanya uamuzi.
Akizungumza katika mahojiano na mwandishi wetu
ofisini kwake Dar es Salaam jana, Jaji Warioba alisema, “Kama uwezekano
wa kukutana upo, kwa nini Bunge liendelee kutumia fedha wakati mnajua
kuwa mwisho hamtafikia uamuzi? Jambo la msingi ni kujitahidi kuafikiana
na Bunge liwe na wajumbe wote.”
Kauli ya Warioba imeungwa mkono na Naibu Waziri wa
Fedha, Mwigulu Nchemba wakati akichangia hoja ya mabadiliko ya kanuni
ya Bunge hilo kwa kulitaka bunge hilo kujitathimini iwapo baada ya
mjadala litaweza kufikia uamuzi, ili kuepuka matumizi mabaya ya fedha za
walipakodi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz