Tuesday, August 05, 2014

BENKI YA DUNIA YASAIDIA EBOLA

Wahudumu wa afya katika tahadhari ya kukabiliana na Ebola
Benki ya Dunia imetangaza kutoa msaada wa hadi dola milioni mia mbili, kutoka mfuko wa dharura wa msaada, ili kuzisaidia mataifa matatu ya Afrika magharibi kukabiliana na ugonjwa hatari wa ebola.
Pesa hizo zitasaidia Liberia, Sierra Leone na Guinea, ili kuboresha vifaa vya afya ya umma na kushughulikia matatizo ya uchumi yaliyosababishwa na ugonjwa huo.
Rais wa Bank ya Dunia Jim Yong Kim amesema amehuzunishwa sana kwa jinsi Ebola unavyoendelea kuvuruga mfumo wa afya kwa nchi tatu.
Kwa mwaka huu pekee karibu watu mia nane na tisini wamekufa kutokanana Ebola katika nchi za Afrika Magharibi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...