Tuesday, August 05, 2014

YANGA SC HAWATASHIRIKI KOMBE LA KAGAME 2014, WAGOMA KUBADILI KIKOSI...!!!

126
TAARIFA Mpya usiku huu! Yanga hawatashiriki michuano ya klabu bingwa kwa ukanda wa Afrika mashariki na kati, maarufu kwa jina la Kombe la Kagame inayotarajia kuanza kutimua vumbi Agosi 8 mwaka huu,, mjini Kigali, Rwanda.
Hii imetokana na Yanga kugoma kubadili kikosi chao kama walivyotakiwa na CECAFA leo hii.
Taarifa zinaeleza kuwa Yanga wamekomaa na kikosi B kama walivyopanga wakati CECAFA wamewataka kwenda na kikosi B.
Awali ilielezwa kuwa Yanga wanatakiwa kubadilisha kikosi hicho kufikia alfajiri ya kesho na kama haitafanya hivyo, basi timu itatolewa kwenye mashindo.
Kwa mana hiyo, mabingwa wa ligi kuu soka Tanzania bara, Azam fc wanaweza kupewa nafasi hiyo kama ilivyoelezwa awali. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...