Wednesday, August 06, 2014

PINDA: TUNGEJUA TUNGEAMUA AINA YA MUUNGANO KWANZA

Waziri Mkuu Mizengo Pinda PICHA|MAKTABA

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda amesema kama Serikali ingejua, ingeanza kwa kura za maoni ya wananchi kuamua aina ya muungano wanaoutaka, kabla ya kuendelea na mchakato wa Katiba.
“Tungejua kama hali ya aina hii itajitokeza, basi tungeanza na kura ya maoni, tungewauliza wananchi kama wanautaka muungano na kama ndiyo, basi uwe wa aina gani au serikali ngapi, mtu angesema moja, mbili, tatu na kadhalika,” alisema Pinda jana kwenye Viwanja vya Bunge mjini hapa.
Pinda alikuwa akijibu swali kuhusu hatima ya Bunge Maalumu kutokana na wajumbe wa Bunge hilo ambao ni wanachama wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kususia vikao hivyo wakishinikiza kile walichokiita kujadiliwa kwa rasimu iliyowasilishwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba na siyo vinginevyo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Miongoni mwa mambo ambayo yamezua mvutano mkubwa ni muundo wa muungano wa serikali tatu uliopendekezwa na tume hiyo, pendekezo ambalo linaungwa mkono na wajumbe wa Ukawa ambao wamesusa Bunge, wakati upande mwingine wenye wabunge wengi wa CCM ukitaka muundo wa serikali mbili uendelee.
Pinda alisema baada ya kupata majawabu ya aina ya muundo wa muungano wanaoutaka wananchi kwa matokeo ya kura ya maoni, basi ungekuwa wakati mwafaka wa kwenda kukusanya maoni ya wananchi kuhusu mambo mengine katika Katiba.
“Lakini ndiyo hivyo, hatukuliwaza hili kwa hiyo ndiyo tunapata taabu yote hii kwa sababu kama mnavyoona bado hatujakubaliana, lakini wenzetu mpaka sasa hawajafika bungeni na mambo kama hayo. Lakini bado tuna imani kwamba busara zitatumika ili mchakato huu uwe wa maridhiano ya wote,” alisema Pinda na kuongeza:
“Katika kukusanya maoni ambayo tunayafanyia kazi sasa, Tume ya Jaji Warioba (Joseph, Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba) ilikusanya maoni mchanganyiko na utakuta pengine suala hili la aina ya muungano halikuwa na mchango wa watu wengi.”
Alisema kama suala la aina ya muungano lingekuwa limetafutiwa suluhu mapema, mambo mengine yote yangejadiliwa na kuafikiwa kwa kuzingatia suala hilo ambalo linaonekana kuwa ni nguzo muhimu ya Katiba.
Alisema jitihada bado zinaendelea ili kuwashawishi Ukawa warejee bungeni na kwamba katika meza ya majadiliano hakuna kinachoshindikana.
“Ninaamini kwamba hizi tofauti zinaweza kuondoka kwa majadiliano, ni suala la kukubaliana kwamba ninyi chukua hiki na sisi tunabaki na hiki na hapo mchakato unaendelea,” alisema.
Alisema imekuwa vyema kwamba kanuni za Bunge Maalumu zimebadilishwa ili kuwezesha wajumbe kujadili maeneo mengine katika Rasimu ya Katiba ambayo hayana utata na kwamba suala la muungano linaweza kupewa fursa baadaye na wakati huo mwafaka unaweza kuwa umepatikana. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na Mwananchi

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...