Thursday, June 26, 2014

UBABE BUNGENI, MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI NUSURA AMPIGE KAFULILA

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema (kushoto) akizuliwa na Mawaziri na Manaibu Waziri kutomfuata Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila baada ya kupandwa na hasira kufuatia mbunge huyo kumtuhumu kwa kumuita mwizi kwenye ukumbi wa Bunge, mjini Dodoma jana. Picha na Edwin Mjwahuzi 
Kwa ufupi
“Profesa Muhongo aliliambia Bunge kuwa Serikali ililipa fedha hizo ili kuondokana na kesi hiyo lakini ninazo nyaraka za Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), kuteua kampuni mbili za uwakili kwenda kuiwakilisha katika kesi nchini Uingereza,” alisema Kafulila.


Kama siyo kuzuiwa na mawaziri, Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema jana angezua tafrani bungeni kutokana na kitendo chake cha kutaka kumpiga Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila. 

Sakata hilo lilitokea jana asubuhi baada ya Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Azzan Zungu kuahirisha kikao cha Bunge hadi jioni, ikiwa ni muda mfupi baada ya Werema na Kafulila kurushiana maneno bungeni. Jaji Werema alichukia baada ya Kafulila kumwita mwizi, akijibu mapigo baada ya mbunge huyo kuitwa tumbili na mwanasheria huyo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS JUNI 26, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MSEKWA ATOBOA SIRI YA CCM KUNG'ANG'ANIA SERKALI MBILI...!!!


Spika mstaafu wa Bunge, Pius Msekwa akikusanya baadhi ya vitabu alivyoviandika  alipokuwa akifanya mahojiano na wahariri wa gazeti hili nyumbani kwake jijini Dar es Salaam. 

Makamu Mwenyekiti mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Pius Msekwa ametoboa siri ya chama hicho kung’ang’ania Muungano serikali mbili akisema hiyo ndiyo sera yake pekee iliyopitishwa na wanachama wake wote kwa kura ya maoni.
Msekwa alieleza hayo katika mahojiano maalumu na wahariri wa gazeti hili yaliyofanyika nyumbani kwake Oysterbay, Dar es Salaam.
Msekwa ambaye katika habari iliyochapishwa na gazeti hili jana alieleza kuwa binafsi, hana tatizo na suala la idadi ya Serikali katika Muungano, alisema kamwe hawezi kukishauri chama chake kukubaliana na mapendekezo ya Rasimu ya Katiba iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba ya muundo wa serikali tatu.
“Siwezi kuishauri CCM kukubali serikali tatu. Hili la Serikali mbili ni sera ya CCM, siyo tu sera ya kawaida, bali hii ni sera pekee iliyopitishwa na wanachama wote kwa kura ya maoni,” alisema Msekwa ambaye pia ni Spika mstaafu wa Bunge.
Alisema tofauti na sera hiyo ya serikali mbili, sera nyingine za chama hicho huanzia katika ngazi ya Kamati Kuu, kujadiliwa na Halmashauri Kuu ya Taifa (Nec) na kupitishwa na Mkutano Mkuu wa Taifa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WALIOVUNJA 'MOCHWARI' WAPATA DHAMANA

Watu sita kati ya 12 wanaotuhumiwa kwa uchochezi na kuvunja chumba cha kuhifadhia maiti katika Kituo cha Afya Kaigara wilayani hapa, jana wamepata dhamana baada ya kutimiza masharti ya mahakama.
Mwendesha mashtaka wa polisi, Cleophace Waane Maatu aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni pamoja na Georgina Angelo, Triphory Joseph, Georgia Triphory, Shafii Abdul, Venanti Benard na Shamim Yusuph.
Aliiambia mahakama kuwa mnamo Juni 16, mwaka huu watuhumiwa hao walifanya uchochezi na kuvunja chumba cha maiti cha kituo hicho na baadaye kutoa mwili wa binti aliyedaiwa kufariki na kunyofolewa viungo vya mwili.
Maatu alisema mtuhumiwa wa kwanza ni shangazi wa marehemu, Georgina Angelo aliyekuwa ametoroka na kukamatwa na polisi kwa kuhusika na uchochezi kwenye mazishi ya binti huyo katika Kijiji cha Bukono wilayani hapa.
Alisema Triphory Joseph na mkewe Georgia ambao ni wazazi wa binti aliyefariki akifanya kazi za ndani mkoani Arusha na Georgina Angelo wanatuhumiwa kwa uchochezi wa kuvunja mochwari ya kituo hicho.
Alisema katika vurugu hizo, pia siku hiyo saa 11:00 jioni walivamia shamba la Valentina Maxmilian na kukatakata migomba pamoja na mazao mengineyo kisha kuchoma nyumba mbili, vitu vyote vikiwa na thamani ya Sh20 milioni.
Watuhumiwa wengine sita hawakutimiza masharti ya dhamana na kesi hiyo itatajwa tena Julai 10, mwaka huu.
Kesi hiyo imevuta hisia za wengi kufuatia kifo cha binti huyo kuzua sintofahamu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MLIPUKO WAUA WATU 21 NA KUJERUHI 50 NIGERIA



Moto ukiteketea kulikolipuka bomu nje ya kituo cha biashara Abuja, Nigeria.

Kumetokea shambulizi la bomu mbele ya soko lenye shughuli nyingi katika mji mkuu wa Nigeria Abuja na kuwauwa zaidi ya watu 21.

Taswira ya majonzi na kilio ilitanda katika mji wa Abuja, mamia ya watu waliokuwa wakinunua bidhaa katika soko hilo wakijikuta wakivuja damu kutokana na majeraha ya mlipuko huo na wengine kuishia mauti.

Bomu hilo lililipuka mbele ya kituo kikubwa cha biashara, kinachotembelewa na watu wengi.

Walioshuhudia walisema sehemu za miili ya wanadamu zilitapakaa kila mahali sakafuni.

Magari yalichomeka kabisa na vioo katika madirisha ya nyumba zilizokuwa karibu kuvunjika vyote. Watu waliokuwa na hofu walielekea kwenye mahospitali yaliyo karibu ambapo walishuhudia magari ya wagonjwa yakisongamana kila mahali yakiwaleta wagonjwa na miili ya waliokufa.

John Tobi Wojioa aliwasili mahali hapo muda mfupi baadaye akimtafuta jamaa wake. Alitaja alichoona kama mafuriko ya damu:

"Kulikuwepo magari ya wagonjwa wa shirika la FRCS (federal Road Safery Corps) na ya mashirika mengine yaliyokuwa yakiingia na kuondoka yakibeba miili ya waathirika. Kwenye barabara alama za damu za nyayo za wanadamu zilionekana kila mahali," alisema Bwana Wojioa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Saturday, June 21, 2014

MARCIO MAXIMO KUTUA BONGO JUMANNE

417570_heroaMaandalizi ya msimu wa ligi kuu ya Tanzania yameanza kupamba moto huku vilabu vikijaribu kujiimarisha tayari kwa mapambano, kwa upande wa klabu ya Yanga wameanza kwa kuimarisha benchi la ufundi kwa kumuajiri kocha Marcio Maximo.
Kocha huyo mbrazil anayeheshimika zaidi nchini, Marcio Maximo atatua Jangwani ndani ya siku nne kuanzia leo Jumamosi. Bosi huyo ambaye anasifika zaidi kwa msisitizo wake katika nidhamu za wachezaji atatua Jumanne ikiwa ni mapema kabla ya uchaguzi wa Simba utakaofanyika Juni 29 Jijini Dar es Salaam. Mwanaspoti linajua kwamba Maximo yuko jijini Brasilia akifanya kazi ya uchambuzi wa mechi za Kombe la Dunia kwenye televisheni ya Taifa ya Mexico na mkataba wake unamalizika Jumatatu.
Yanga imethibitisha kwamba Maximo ameshaanza maandalizi ya safari hiyo tangu juzi ambapo katika hilo pia amewajulisha baadhi ya maofisa wa Ubalozi wa nchi hiyo nchini kuwa atakuwa Tanzania mapema wiki hii kumalizia maongezi yake na mabosi wa Yanga.
Yanga wamemleta Maximo mapema kufanya maandalizi ya uhakika katika kikosi cha timu hiyo ikiwa ni kuwawahi wapinzani wao wa jadi Simba ambao bado wapo katika mchakato wa uchaguzi.
“Ilikuwa kuna baadhi ya viongozi waende Brazil kumalizia mazungumzo na kusainishana mkataba  lakini hilo limebadilishwa. Maximo ndiyo atakuja Dar es Salaam kuepuka gharama,”alisisitiza mmoja wa viongozi wa Yanga.
Source: Mwanaspoti

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JUNI 21, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MSF: "UGONJWA WA EBOLA HAUDHIBITIKI TENA"

Raia anayeugua ugonjwa w Ebola
Afisa mwandamizi wa shirika la madaktari wasio na Mipaka Medicine San Frontiers ameelezea kuwa mkurupuko wa ugonjwa wa Ebola katika mataifa matatu ya magharibi hauwezi kudhibitika.
Mkurugenzi wa Oparesheni katika shirika hilo Bart Janssens ameliambia shirika la habari la A.P kwamba ugonjwa huo utasambaa hadi katika mataifa mengine iwapo hakutakuwa na mwitikio wa kimataifa.
Ugonjwa wa Ebola tayari umesababisha vifo vya takriban watu 330 nchini Guinea,Sierra leone na Liberia.
Bwana Janssens amesema kuwa shirika la MSF limefikia kikomo cha uwezo wake wa kukabiliana na ugonjwa huo.

VITA VIKALI VYAENDELEA NCHINI IRAQ

Wapiganaji wa kundi la JIhad la Isis
Mapigano yanaendelea katika mji uliopo kazkazini magharibi wa Tal Afar nchini Iraq ambapo wapiganaji wa kiislamu wamekuwa wakikabiliana na vikosi vya serikali tangu jumatatu.
Wanamgambo wa ki sunni kutoka kundi la Jihad la ISIS wanaudhibiti mji huo ambao uko katika barabara inayoelekea Syria.
Kwengineko kuna makabiliano makali katika mji wa Baiji ambapo wapiganaji wamekizunguka kiwanda kikubwa cha kusafisha mafuta.
Uzalishaji wa mafuta katika kiwanda hicho umesitishwa na hivyobasi kusababisha ununuzi wa mafuta katika maeneo mengine ya taifa hilo kwa hofu ya kupotea kwa bidhaa hiyo.
Watu wanaomuunga mkono kiongozi wa dhehebu la Shia Muqtada Al Sadr sasa wanaelekea katika mji mkuu wa Baghdad.

Wednesday, June 18, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMATANO JUNI 18, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


IMG-20140618-WA0000_b70f2.jpg
IMG-20140618-WA0001_2c722.jpg
IMG-20140618-WA0015_1691e.jpg
IMG-20140618-WA0016_e5359.jpg
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ROBO TATU YA WALIOFAULU WACHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO



Akizungumza na waandishi wa habari jana, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Kassim Majaliwa alisema kati ya waliochaguliwa wavulana ni 31,352 na wasichana ni 22, 733.PICHA|MAKTABA

Robo tatu ya wanafunzi waliofaulu kidato cha nne kwa kupata daraja la kwanza hadi la tatu (Division I – III), wamechaguliwa kujiunga na kidato cha tano. Idadi hiyo ya wanafunzi watakaojiunga katika shule za Serikali mwaka huu, imeongezeka kutoka 33,683 mwaka jana hadi kufikia 54, 085 sawa na asilimia 75.6 ya wanafunzi 71,527 wenye sifa ya kujiunga na kidato cha tano Tanzania Bara.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Kassim Majaliwa alisema kati ya waliochaguliwa wavulana ni 31,352 na wasichana ni 22, 733.

“Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano 2014 ni kutoka shule za Serikali na zisizo za Serikali. 
Kati yao wavulana 14, 826 sawa na asilimia 27.41 wamechaguliwa kusoma masomo ya sayansi na wengine 16, 526 sawa na asilimia 30.5 wamechaguliwa kusoma masomo ya sayansi ya jamii,” alisema. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MBASHA APANDISHWA KIZIMBANI KWA UBAKAJI

Mwimbaji wa nyimbo za Injili na mfanyabiashara, Emmanuel Mbasha. PICHA|MAKTABA 

Mwimbaji wa nyimbo za Injili na mfanyabiashara, Emmanuel Mbasha amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala kwa mashtaka ya ubakaji. Mbasha ambaye pia ni mume mwa mwimbaji maarufu wa Injili nchini, Flora Mbasha alipandishwa kizimbani jana na kusomewa mashtaka mawili ya ubakaji.
Wakili wa Serikali, Nassoro Katuga alidai kuwa mshtakiwa huyo alitenda makosa hayo kwa nyakati tofauti kati ya Mei 23 na 25, mwaka huu, eneo la Tabata Kimanga, Ilala, Dar es Salaam.Wakili Katuga alidai kuwa katika tarehe hizo, mshtakiwa alimbaka mtoto (jina linahifadhiwa), mwenye umri wa miaka 17, kinyume cha sheria.
Hata hivyo, Wakili Katuga alisema upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika. Ingawa dhamana ya mshtakiwa huyo ilikuwa wazi, aliswekwa mahabusu, baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana ambayo yalikuwa kuwa na wadhamini wawili, mmoja akiwa ni mfanyakazi wa taasisi inayotambulika, ambao watasaini hati ya dhamana ya Sh5 milioni kila mmoja.
Hakimu Wilberforce Luhwago anayesikiliza kesi hiyo aliiahirisha hadi kesho itakapotajwa kwa ajili ya kuangalia iwapo mshtakiwa amekamilisha masharti ya dhamana. Mbasha alifikishwa mahakamani hapo asubuhi akiwa amevaa shati jekundu la mikono mirefu, suruali ya rangi ya udongo na kandambili nyekundu.
Mahakamani hapo alikuwa ameambatana na wanaume wawili. Wakati akisubiri kupelekwa mahabusu, saa 7:35, watu hao aliokuwa ameambatana nao walikwenda kumnunulia chakula na maji kabla ya kuongozwa na polisi kwenda kupanda basi la Magereza kuungana na mahabusu kuelekea Gereza la Keko saa 7:05. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WAKUU WA POLISI WAFUTWA KAZI NCHINI KENYA

Inspekta wa polisi Kenya, David Kimaiyo
Idara ya polisi nchini Kenya imefanya mabadiliko ya dharura katika afisi kuu za Kaunti ya Lamu, kutokana na mashambulio yaliyosababisha vifo vya watu 60 wiki hii. Inspekta mkuu wa polisi nchini Kenya David Kimaiyo amechapisha katika mtandao wa jamii Twitter, maelezo ya wakuu wa polisi katika kaunti hiyo waliofutwa kazi mara moja, wakiwemo makamanda wa polisi.
Afisa mkuu wa kituo cha Polisi, OCS, pia amehamishwa kituo mara moja. Hatua hii tayari imepokewa kwa hisia tofauti huku wakenya wengi wakielezea kutoridhishwa na adhabu hiyo.
Miongoni mwa walioandika malalamiko yao kwa Bwana Kimaiyo, wamesema kuwa mabadiliko yalistahili kufanyika hadi ngazi ya juu zaidi, baadhi hata wakimtaka yeye mwenyewe kama Inspekta wa polisi kujiuzulu.
Tangu kutokea shambulio la Jumapili usiku katika kijiji cha Mpeketoni, karibu na kisiwa cha Lamu pwani ya Kenya, lawama zimeelekezwa kila upande, huku baadhi wakidai kuwa wanasiasa wamehusika na wengine wakilalamikia utepetevu wa polisi katika kutekeleza majukumu yao.
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta alihutubia taifa Jumanne akisisitiza kuwa ana imani kuwa mashambulio hayo yalichochewa kisiasa. Ametoa matamshi hayo licha ya taarifa kutoka kwa kundi la wapiganaji wa kiislamu wa AL shabaab waliodai kuwa wao ndio waliohusika.
Matamshi ya rais Kenyatta yame kejeliwa na wanasiasa wa upinzani nchini humo waliodai kuwa rais huyo hana ufahamu wa yale yanayoendelea nchini mwake.

Seneta kutoka chama kikuu cha upinzani, Moses Wetangula amesema matamshi ya rais sio ya kweli. '' Badala ya kuitisha usaidizi wa wenzetu wenye teknolojia bora, hata tutumie ndege zisizo na rubani kuwalipua huko waliko, tunakaa hapa Nairobi na kudai AL shabaab hawakuhusika.'' Wetangula aliambia bunge la Kenya. '' Huu ni mzaha,'' Aliongeza bwana Wetangula.
Lakini uchunguzi uliofanywa na BBC umeonesha kuwa huenda kuna uzito kwa madai ya rais Kenyatta. Wakaazi wengi wa Mpeketoni waliozungumza na BBC wametueleza kuwa, wanaamini shambulio la Jumapili usiku linatokana na mzozo wa ardhi kati ya jamii zinazoishi huko. Wakaazi hao wamesema kuwa Al shabaab wamedakia tu kujigamba kwa yaliotokea huko ila wao wanaamini kuwa ni jambo lililokuwa likitokota kwa muda mrefu.
polisi waimarisha usalama
Huku hayo yakiarifiwa, polisi wanasemekana kuimarisha doria katika eneo la Lamu na vitongoji vyake. Wanajeshi wachache wametumika kuimarisha usalama hasa katika kijiji cha Mpeketoni. Katika taarifa zilizotufikia ni kuwa Polisi wameimarisha usalama katika mkoa wa magharibi mwa Kenya kutokana na duru walizopokea kuwa huenda eneo hilo likalengwa kwa shambulio.
Al shabaab wamefanya mashambulio ya mara kwa mara katika sehemu mbali mbali nchini Kenya tangu majeshi ya Kenya yaingie nchini Somalia mwaka wa 2011, katika oparesheni ya kuwafagia kutoka nchini humo. Shambulio la punde zaidi linadaiwa kufanywa kama kulipiza kisasi ya kuuawa kwa masheikh 2 wa kiislamu katika mji wa Mombasa pwani ya Kenya hivi majuzi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

DAKIKA 90 ZA MECHI ZA KOMBE LA DUNIA ZA JUNI 17

Kwenye mechi zilizochezwa usiku wa June 17 2014 matokeo yake ni Russia 1 (Kerzhakov 74′ ) – 1 Korea Republic goli lao lilifungwa na K Lee kwenye dakika ya 68.
Game nyingine ilikua ya Brazil vs Mexico iliyoisha kwa 0-0 huku ile ya nyingine ya mwanzo ikiwa ni Belgium 2 ( Fellaini 70′ + Mertens 80′) – 1 Algeria (Feghouli aliefunga kwa penati dakika ya 25 ) Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MASHABIKI WA SOKA WALIPULIWA

Mlipuko watokea Yobe watu wakitizama kombe la dunia
Shambulio limetokea katika jimbo la Yobe nchini Nigeria wakati watu wakitazama mechi za kombe la dunia. Jimbo hilo limewekwa katika hali ya hatari huku maafisa wa usalama wakijaribu kukabiliana na mashambulio yanayofanywa na wanamgambo wa Boko Haram kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.
Wakaazi wanasema walisikia sauti ya mlipuko mkubwa nje ya eneo la kutazama sinema mjini Damaturu ambapo mashabiki wa soka walikua wamejumuika kutazama mechi za kombe la dunia. Walioshuhudia wanasema mshambuliaji wa kujitolea mhanga aliyekuwa amebebwa kwa baiskeli alijilipua karibu na mgahawa katika jimbo la Yobe wakati mechi kati ya Brazil na Mexico ikiendelea.
Yobe imekumbwa na mashambulizi ya Boko Haram katika miaka iliyopita.
Duru kutoka hospitalini zinasema malori kadhaa yamewasafirisha majeruhi kupata matibabu na polisi wanasema maafisa wamepelekwa katika eneo hilo. Mfanyikazi mmoja wa hospitali ameaimbia BBC kuwa waliopelekwa hapo wana majeraha mabaya huku baadhi yao wakipoteza miguu na mikono.

Wiki iliyopita maafisa wa utawala katika jimbo la Adamawa ambalo liko katika eneo hilo la Kaskazini mwa Nigeria walipiga marufuku watu kujumuika katika maeneo ya umma kutazama mechi za kombe la dunia kutokana na hofu ya Usalama. Hatua hiyo ilichukuliwa baada ya shambulio kutokea katika eneo la burudani na kusababisha mauaji ya watu kadhaa.

Majimbo ya Borno, Yobe na Adamawa yako katika hali ya tahadhari kuanzia mwezi Mwezi 2013 kufuatia mashambulizi ya kila mara ya wapiganaji wa kundi la kiislamu la Boko Haram. Takriban watu 2,000 wamepoteza maisha yao yangu visa vya uasi kuanza kutekelezwa mwaka wa 2009. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...