Saturday, June 07, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JUNI 07, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAHAKAMANI KWA KOSA LA KUAGIZA MAITI IKATWE MIGUU...!!!


Mwandalizi mmoja wa mazishi nchini Afrika Kusini, anayedaiwa kuwaagiza wafanyakazi wake kuikata miguu ya maiti moja aliyodai kuwa ndefu sana alifikishwa mahakamani Ijumaa.
Ronel Mostert anayemiliki chumba cha kuhifadhi maiti ambacho pia huendesha shughuli za mazishi, alitoa amri hiyo kwa lengo la kuhakikisha kuwa maiti hiyo ingetosha katika jeneza. Anakabiliwa na kosa la kumkata miguu maiti.
Mfanyakazi mmoja aliimbia mahakama kuwa Ronel alimuagiza kuchukua kifaa kimoja cha kukata ili kuikata miguu hiyo ya marehemu na kwamba jambo hilo limekuwa likimsumbua sana kimawazo.
Mwili marehemu ulifukuliwa ili kusaidia katika uchunguzi wa polisi.Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Na BBC

MADEREVA WA UMMA WAGOMA BRAZIL

Mgomo wa wafanyakazi hao umesababisha uhaba wa magari ya usafiri
Maafisa wa polisi nchini Brazil wametumia gesi ya kutoa machozi ili kuwatawanya waandamanaji katika siku ya pili ya mgomo wa wafanyikazi wa sekta ya uchukuzi ambao umesababisha uhaba mkubwa wa usafiri wa uma katika mji wa Sao Paulo.
Takriban nusu ya vituo vya treni vilifungwa na kusababisha msongamano mkubwa wa watu katika barabara za mji huo mkubwa ambao unatarajiwa kuandaa michuano ya kombe la dunia kuanzia alhamisi ijayo.
Wafanyakazi hao wa treni wanataka mishahara yao kuongezwa kwa asilimia kumi.
Awamu nyengine ya majadiliano imefeli na wafanyikazi hao wanasema kuwa mgomo huo utaendelea kwa mda usiojulikana. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Na BBC

MWEGANE YEYA WA MBEYA CITY AAHIDI MAKUBWA TAIFA STARS, AMSHUKURU MUNGU KWA KUITWA NA MART NOOIJ


Mwagane-Yeya.pngnnnnnnnnnnnnnnNa Baraka Mpenja, Dar es salaam
MSHAMBULIAJI hatari wa Mbeya City fc, Mwegane Yeya amefurahishwa na kitendo cha kuitwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars chini ya kocha Mholanzi, Mart Nooij.
Akizungumza na mtandao huu, Mwegane amesema kuwa anamshukuru sana Mungu kwa kupata nafasi hiyo kwasababu Tanzania ina wachezaji wengi wenye viwango vya hali ya juu, lakini amechaguliwa yeye.
“Hii ni nafasi nyingine muhimu kwangu. Niliwahi kuitwa katika kikosi cha Young Future Taifa Stars na Kim Poulsen, lakini sikufanya vizuri kwasababu nilikuwa majeruhi. Naamini kwasasa nitaitumia vizuri nafasi hii”. Alisema Mwegane ambaye ni hatari kwa kufunga magoli ya kichwa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Friday, June 06, 2014

WARIOBA AZISHUKIA UKAWA NA CCM


Katika Bunge hilo, wajumbe wengi wa CCM walimshambulia Warioba na tume yake wakidai kuwa Rasimu ya Pili ya Katiba haikuzingatia maoni ya wananchi na Mabaraza ya Katiba. PICHA|MAKTABA 

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba amewashauri wajumbe wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) na CCM kuacha kuzunguka mikoani kufanya mikutano inayoeleza misimamo yao kuhusu mchakato wa Katiba Mpya kwa kuwa haina tija kwa taifa.
Ameonya kuwa mikutano hiyo inajenga mwelekeo mbaya kwa taifa na kuhatarisha mchakato wa Katiba na kuzitaka pande hizo kumaliza tofauti zao.
Akizungumza katika mahojiano maalumu yaliyofanyika Dar es Salaam jana, Warioba alisema: “Kwa mustakabali mwema wa taifa, ni muhimu makundi haya ‘ya-resolve’ (yamalize), matatizo yaliyopo kabla ya Agosti, ili Bunge Maalumu la Katiba likirejea, wote washiriki na kukamilisha mchakato wa kupata Katiba Mpya. Hili ni kwa masilahi ya taifa.”
Kauli ya Waziri Mkuu huyo mstaafu ambaye pia aliwahi kuwa Mwanasheria Mkuu, imekuja huku makundi ya Ukawa linaloundwa na wabunge wengi wa upinzani na viongozi wa CCM wakiendelea kung’ang’ania misimamo yao kuhusu Rasimu ya Katiba Mpya iliyowasilishwa kwenye Bunge Maalumu la Katiba.
Wakati CCM ikipinga mapendekezo ya kuwapo kwa mfumo wa serikali tatu uliomo kwenye Rasimu, Ukawa unaunga mkono mapendekezo hayo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

TIGO, AIRTEL NA ZANTEL ZAUNGANISHA HUDUMA




Meneja Mkuu wa Kampuni ya Tigo, Diego Gutierrez (Kulia) na Ofisa Mtendaji Mkuu wa DTBi, Mhandisi George Muhula wakitia saini ya makubaliano jijini Dar es Salaam jana baina ya Tigo na DTBi ya kusaidia wajasiriamali kujifunza teknolojia ya digitali na mawasiliano. Wanaoshuhudia ni Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof Makame Mbarawa na Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Dk Hassan Mshinda. Picha na Venance Nestory.


Kampuni za simu za mkononi za Tigo, Airtel na Zantel zimeunganisha huduma zao za kutoa, kutuma na kuweka fedha na sasa mteja anaweza kutuma fedha kutoka mtandao mmoja kupitia mwingine.

Taarifa ya pamoja na kampuni hizo iliyotolewa jana, ilisema kuwa wote wanaotumia huduma za kifedha za mitandao hiyo, wataweza kutumiana fedha kupitia simu zao za mikononi pasi na tatizo baada ya kampuni hizo kuunganisha huduma zao.

Huduma hiyo inayotarajiwa kuanza kutumika mwishoni mwa mwezi huu, itawafanya wateja wa mitandao hiyo kutumiana na kupokea fedha moja kwa moja kwenye akaunti zao tofauti na ilivyokuwa awali. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO IJUMAA JUNI 06, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MTAWA WA KANISA KATOLIKI ASHINDA KATIKA SHINDANO LA KUIMBA...!!!

Mtawa wa Italia anyakua ushindi
Mtawa mmoja kutoka Italia ambaye alipata umaarufu katika mtandao wa kijamii ameshinda shindano la kuimba nchini humo. Mtawa huyo, Sister Christina Scuccia alitokea kwa mara ya kwanza katika televisheni kushiriki shindano la The Voice.
Scuccia aliyeonekana amevalia mavazi yake ya utawa na msalaba shingoni, alijawa na furaha na kumshukuru Mungu kwa kumfikisha katika ushindi huo. Mtindo wake wa wimbo wa Alicia Keys, kwa jina 'No One', umetizamwa zaidi ya mara milioni 50 katika mtandao wa You Tube tangu auimbe.
Mtawa huyo mwenye umri wa miaka 25 amesema kuwa aliamua kushiriki mashindano hayo kufuata ushauri wa Papa mtakatifu Francis, kuwa kanisa liwakaribie zaidi watu wa kawaida. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Na BBC Swahili

DRC YAILAUMU RWANDA KWA KUWALINDA M23




DRC yailaumu Rwanda kuwalinda M23
Serikali ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo imeikashifu serikali ya Rwanda kwa kuwalinda wapiganaji wanaotuhumiwa kwa kusababisha mauaji ya halaiki chini ya nembo ya wapiganaji wa M23.
Afisa mmoja wa Serikali ya DRC ameiambia BBC kuwa imekuwa vigumu kwa serikali yake kuwahoji zaidi ya wapiganaji 500 ambao wamekita kambi nchini Rwanda licha yao kutuma ombi la kufanya hivyo yapata miezi saba iliyopita . Zaidi ya watu 800,000 walitoroka makwao haswa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemkrasia ya Congo wakati wa mapigano hayo ya wenyewe kwa wenyewe.

Rwanda imekuwa ikipinga madai hayo na kusema kuwa imeshirikiana na serikali ya DRC. Kundi hilo la M23 lichukua silaha mashariki mwa DRC kuanzia Aprili 2012, liliaumu serikali ya Kinshasa kwa kuwabagua jamii ya watutsi na pia kupuuza makubaliano ya awali ya kusitisha mapigano. Kundi hilo hata hivyo lilishindwa katika mapigano yaliyoongozwa na jeshi la Umoja wa mataifa likisaidiwa na majeshi ya serikali ya Congo mnamo November 2013. Wapiganaji hao walitorokea Rwanda na Uganda.


DRC yailaumu Rwanda kuwalinda M23
Katika mji wa Ngoma, mashariki mwa Rwanda mwandishi wetu alikumbana na wapiganaji hao ana kwa ana katika kambi nje ya mji. Wengi wao wanasema kuwa wamechoshwa na ngoja ngoja hiyo ambayo imedumu kwa kipindi kirefu sasa na wanasema kuwa wangependa kuomba hifadhi nchini Rwanda, kwani wanahofia kurejea ndani ya Congo.
 Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Serikali ya Congo imetangaza kuwa itawapa msamaha wapiganaji hao. Tulipoingia ndani ya kambi hiyo ,hali na taswira ilikuwa tulivu na shwari. Kulikuwa na hema kubwa nyeupe, majengo kadha mbali na bustani iliyolindwa na nadhifu. Wapiganaji hao wanalala sita katika chumba kimoja .

Thursday, June 05, 2014

G7 WAKUTANA BRUSSELS BILA URUSI

mkutano wa G7
Viongozi wa mataifa tajiri ya magharibi wanaokutana mjini Brussels wamesema kuwa wako tayari kuweka vikwazo zaidi kwa Urusi iwapo itaendelea kuvuruga amani mashariki mwa Ukrain. Taarifa ya pamoja ya mataifa ya G7 imesema kuwa Mambo yanayofanywa na Urusi nchini Ukrain hayawezi kubalika kamwe na lazima yakomeshwe.
Huu ndio mkutano wa kwanza wa viongozi hao tangu waifukuze Urusi kama mwanachama.
Urusi ilibumburushwa kutoka G7 kwa kosa lake kubwa zaidi, kuinyakua Crimea kutoka Ukrain. Viongozi wa mataifa hayo ya G7 wanakutana sasa kwa mara ya kwanza tangu wakati huo.
Ukrain vita vimechacha
Lakini huku wakikutana mapigano yamechacha kati ya serikali ya Ukrain na majeshi yanayo unga mkono Urusi mashariki mwa Ukrain. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Urusi imeendelea kukana kuhusika na mapigano hayo. Miongoni mwa mikutano iliyopangwa Alhamisi hii, waziri mkuu wa Uingereza Davin Cameron atakutana na rais Obama mjini Brussels, ambapo kwa upana zaidi watazungumzia Urusi. Kisha baada ya mkutano huo, David Cameron ataelekea Paris Ufaransa kwa mkutano wa faragha na rais wa Urusi Vladmir Putin.

D-Day barani Uropa

Katika wiki hii mataifa ya Uropa yamekuwa yakiadhimisha siku ya kuikomboa bara Uropa kutoka utawala wa ki Nazzi katika vita vya pili vya dunia miaka 70 iliyopita. Huku hayo yakitokea, juhudi za kidiplomasia zimeshika kasi miongoni mwa mataifa ya magharibi kumaliza uhasama kati yao na Urusi.
G7 wamepongeza uchaguzi mkuu uliofanyika nchini Ukrain na wameirai Urusi kumpokea na kushirikiana na rais mpya wa Ukrain Petro Poroshenko. Pia wameonya kuwa hawatasita kuiwekea Urusi vikwazo zaidi iwapo itakataa kusaidia kurejesha uthabiti Ukrain. Itakuwa ni mara ya kwanza kwa miaka 17 ambapo G7 inakutana bila Urusi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS JUNI 05, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.

.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Wednesday, June 04, 2014

ANGALIA MSAFARA WA RAIS WA KENYA UNAVYOKUWA BAADA YA KUPEWA KITISHO CHA KUUAWA NA AL- SHABAAB

Screen Shot 2014-06-04 at 9.53.41 AM 
Imefaamika kuwa baada ya kikundi cha kigaidi cha Al Shabaab cha Somalia kutoa onyo kwamba mashambulizi yake yanayofata yatawahusu viongozi wa Kenya, imebidi system ya ulinzi wa rais kwenye msafara ibadilike.
Mabadiliko yalianza kuonekana toka mwishoni mwa wiki iliyopita kwenye sherehe za 51 za kujitawala ambapo badala ya Rais kutumia gari aina ya Land rover iliyo wazi iliyokua pia ikitumika na marais wa awali, rais aliiingia kwenye uwanja wa michezo wa Nyayo na gari aina ya Land cruiser iliyo na vioo visivyo penya risasi.
Screen Shot 2014-06-04 at 9.53.52 AM 
Hiyo Land Cruiser ililoongozwa na gari lenye mitambo iliyo na uwezo wa kugundua bomu kwa zaidi ya kilomita 10, nyuma kabisa kulikua na gari lililo na uwezo wa kuhimili risasi na bomu au kilipuzi cha aina yoyote na inasemekana kwamba gari hilo huwa linatumika endapo msafara wa Rais umeshambuliwa kwa haraka Rais na wakuu wengine wanaondolewa na gari hilo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATANO JUNI 04, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

BOKO HARAMU WAFANYA MAUAJI


borno iliyoshambuliwa NIgeria
BBC imepata taarifa kuwa zaidi ya watu 20 wameuawa katika mashambulio katika vijiji vya jimbo la Borno.
Hii inatokea wakati bado kuna wasiwasi mkubwa juu ya hatma ya wasichana zaidi ya 200 waliotekwa nyara na kundi hilo yapata siku 50 zilizopita.
Wakaazi wa kijiji cha Attagara karibu zaidi na mpaka wa Cameroon na Nigeria wamesema kuwa watu waliovalia sare za kijeshi walikuja katika kijiji chao na kuwaagiza watu waje katika uwanja wa kanisa.
Wanadai kuwa walidhania watu hao walikuwa wnajeshi wa serikali waliokuja kuwapa ulinzi. Na baada ya wanajeshi hao kuwafyatulia risasai ndipo waligundua kuwa walikuwa wapiganaji wa Boko Haram. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Mbunge wa eneo hilo Peter Biye amethibitishia BBC tukio hilo na kusema kuwa watu wengi wameuawa na nyumba kuchomwa katika vijiji vingine 5 mbali na hicho.
'Jeshi lakanusha madai'
Wakati huo huo jeshi la Nigeria limekanusha madai katika vyombo vya habari kuwa mahakama ya kijeshi nchini humo imewapata na hatia baadhi ya maafisa wakuu wa jeshi kwa kuwasaidia wapiganaji wa Boko Haram.
Msemaji kutoka jeshi hilo amekanusha madai kuwa kuna majenerali 15 wa wa jeshi waliofunguliwa mashtaka ya kuwasaidia magaidi. Jeshi limesema kuwa taarifa hizo ni batili zilizolenga kulidhalilisha jeshi la nchi hiyo wakati mambo yako tete.

nyumba zimechomwa Borno
Hali imeendelea kuwa ya wasiwasi miongoni mwa wakaazi wa maeneo mengi kaskazini mashariki mwa Nigeria kutokana na mashambulio yaliyochacha. Wapiganaji wamekuwa wakishambulia kwa bomu maeneo ya umma na kuwaua watu zaidi ya 200 katika chini ya miezi miwili tu.
Suala la wasichana waliotekwa pia bado limekaa kama mwiba wa samaki kooni mwa serikali ya Nigeria ambapo shinikizo kutoka jamii ya kimataifa zinaendelea kutaka wakombolewe kwa haraka. Awali serikali ilikuwa imepiga marufuku maandamano yoyote kutokana na tisho la usalama lakini ssa polisi wametangaza kuwa maandamano ya amani yanaweza kufanywa.

Tuesday, June 03, 2014

RAIS WA MALAWI ANA MSIMAMO MKALI ZIWA NYASA



Rais wa Malawi, Peter Mutharika. PICHA|MAKTABA 

Wingu jeusi limeanza kutanda kuhusu hatima ya mzozo wa Ziwa Nyasa kutokana na msimamo wa hivi karibuni wa kiongozi wa Democratic Progressive Party (DPP), Peter Mutharika ambaye sasa ni Rais mpya wa Malawi.

Hiyo inatokana na msimamo wa Mutharika ambaye ni Profesa wa Sheria wa kupinga kuendelea kujadiliana na Tanzania kuhusu nani mwenye haki ya kumiliki ziwa hilo alioutoa wakati alipowatembelea wananchi wa Chipoko, kando ya ziwa hilo miezi michache kabla ya uchaguzi mkuu ambao ulimwigiza madarakani.

Pamoja na kwamba mazingira ya msimamo huo yanaweza kutofautiana na hali halisi ya sasa, tofauti za kisiasa baina yake na mtangulizi wake, Joyce Banda zinaweza kuongeza msukumo mpya wa kutaka kutoendelea na mazungumzo ya mpaka wa ziwa hilo.

Akizungumza na wananchi hao, Profesa Mutharika aliwatoa wasiwasi na kuwataka kuendelea na shughuli zao kama kawaida kwa maelezo kuwa ziwa hilo lipo kwenye himaya ya Malawi na kwamba kuendelea kujadiliana na Tanzania ni kupoteza muda. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMANNE JUNI 03, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.

.

.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

'MTOTO WA BOKSI' KUZIKWA LEO, NDUGU WA BABAKE WAJITOKEZA

Jeneza lenye mwili wa mtoto Nasra Rashid (4) likishushwa kutoka kwenye gari ili kuingiza katika chumba cha kuhifadhia maiti hospitali ya mkoa wa Morogoro Hospitali ya Taifa ya Muhimbi jijini Dar es Salaam. Picha na Juma Mtanda 

Ndugu wa baba wa mtoto, Nasra Mvungi (4) aliyefariki dunia usiku wa kuamkia juzi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, jana walijitokeza wakitaka wapewe mwili wa marehemu kwa ajili ya maziko.
Baada ya kuwasili hospitalini hapo saa 1:35 asubuhi, ndugu hao wakiongozwa na baba wa mtoto huyo, Rashid Mvungi walikutana na maofisa wa ustawi wa jamii wakiongozwa na Ofisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Morogoro, Oswin Ngungatuti wakitaka wakamzike mtoto wao kwa kufuata imani ya dini yao ya Kiislamu.
Hata hivyo, Ngungatuti alipinga hoja hiyo akisema suala la ndugu kuzika halina nafasi na kwamba mtoto atazikwa na ustawi wa jamii ambao ndiyo waliokabidhiwa mtoto huyo na polisi.
“Tutamzika kiserikali kwa kuzingatia imani ya dini yake lakini hatutawakabidhi maiti kwa namna yoyote,” Ngungatuti alisema na kuongeza kuwa wanafanya hivyo kwa kufuata misingi ya kisheria.
Akizungumzia suala hilo Mvungi alisema: “Ndugu zangu wanataka mtoto tupewe lakini kama sheria inakataza mimi sina neno ila kama ingekuwa ni matakwa yangu ningependa nipewe mwanangu nikazike mwenyewe.
Sakata hilo liliendelea mjini Morogoro ambako baada ya mwili kuwasili, watu wanne; wanawake wawili na wanaume walifika Ofisi za Ustawi wa Jamii na kujitambulisha kuwa ni bibi na wajomba wa marehemu wakitaka wapewe mwili wa mtoto huyo. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

NIGERIA YAANIKA `BUNDUKI` ZA MWISHO KOMBE LA DUNIA BRAZIL

412895_heroaKOCHA mkuu wa Nigeria, Stephen Keshi ametaja kikosi chake cha mwisho cha wachezaji 23 kwa ajili ya kombe la dunia mwaka huu nchini Brazil.
Mabingwa hao wa soka barani Afrika wanaenda kushiriki fainaili hizo kwa mara ya tano na wamepangwa kundi moja na Argentina, Iran na Bosnia.
Wachezaji wazoefu kama Vincent Enyeama, Austin Ejide, Joseph Yobo na Elderson Echiejile waliokuwa sehemu ya kikosi cha fainali za mwaka 2010 nchini Afrika kusini wamejumuishwa katika orodha hiyo ya mwisho. Mfungaji bora wa fainali za 29 za AFCON, Emmanuel Emenike, Godfrey Oboabona, John Obi Mikel na Victor Moses wanatarajia kucheza fainali zao za kwanza za kombe la dunia. Kikosi kizima: Walinda mlango: Vincent Enyeama, Austin Ejide, Chigozie Agbim
Walinzi: Joseph Yobo, Elderson Echiejile, Juwon Oshaniwa, Godfrey Oboabona, Azubuike Egwuekwe, Kenneth Omeruo, Efe Ambrose, Kunle Odunlami Viungo: John Mikel Obi, Ogenyi Onazi, Ramon Azeez, Michael Uchebo, Reuben Gabriel
Washambuliaji: Osaze Odemwingie, Ahmed Musa, Shola Ameobi, Emmanuel Emenike, Babatunde Michael, Victor Moses, Uche Nwofor. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

RAIA 130, 00 WA DRC WAFUKUZWA BRAZAVLLE

wakimbizi wa Congo wahangaika
Zaidi ya wakimbizi 130,000 kutoka Jamhuri ya Demokrasia ya Congo wamefukuzwa kutoka Congo Brazaville tangu mwezi Aprili. Wengi wao sasa wanaishi katika kambi za muda nchini DRC.

Serikali ya Brazzaville imesema kuwa watu hao walikuwa wahamiaji haramu lakini wengi wao wamekanusha hili wakisema kuwa wameteswa sana na polisi wa Brazaville. Umoja wa maaifa umetoa wito kwa Congo kukoma kuwafukuza watu hao. Hapo Jumatatu ujumbe kutoka pande zote mbili ulikutana mjini Kinshasa nchini DRC kujaribu kutafuta suluhisho.
Maelfu ya waliohamia kambi hizo za muda za DRC waliishi nchini Brazaville maisha yao yote na sasa wamepoteza kila kitu walichokuwa nacho. Wamedai kuwa polisi wa Brazaville waliwapiga, kuwabaka na hata kuwaua baadhi ya watu walioaminiwa kuwa raia wa DRC wakati wa msako wao.

Huu ni unyama

Upande wa DRC umelalamikia hatua hii na kusema kuwa Brazaville imekiuka haki za binadamu.
Richard Muye ni waziri wa mambo ya ndani wa DRC. Ameambia BBC, '' Mbona sasa wanawafukuza tena kwa wingi hivi bila kujali haki zao? Wanawatesa watu wote, wake waume na hata watoto.''

Brazaville yajitetea

Lakini waziri mwenzake kutoka upande wa Brazaville Raymond Zéphirin Mboulou amekanusha kuwafukuza wakongomani 130,000. Amesisitiza kuwa ni 2000 pekee waliofukuzwa kwa lazima nchini humo, na hiyo pia ni kwasababu walikuwa wahalifu.
"Walifanya uhalifu wa kuchukiza. Wizi, ubakaji ukahaba na mengine. Wameharibu mitaa yetu. Na hawakaribishwi hapa tena kwasababu hao wahamiaji ndio wanaowahangaisha raia wetu usiku na mchana."
Waziri huyo ameongeza kuwa wale wengine 128,000 walioondoka walifanya hivyo kwa hiari yao. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

NIGERIA YAKOMESHA 'BRING BACK OUR GIRLS'


Polisi wazuia maandamano Nigeria
Polisi nchini katika mji mkuu wa Nigeria, Abuja wamepiga marufuku maandamano ya watu wanaowaunga mkono zaidi ya wasichana wa shule mia mbili waliotekwanyara na kundi la wanamgambo wenye itikadi kali za kiislamu la Boko Haram mwezi Aprili.
Maandamano yamekuwa yakiandaliwa kila siku kwa kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja kuishinikiza serikali kutia bidii zaidi katika juhudi za kuwakomboa wasichana hao. Polisi wanasema maandamano hayo yanamepigwa marufuku kwa kuwa yanazua hatari kwa wenyeji.

Aibu kwa serikali

Kampeini ya 'Bring back our Girls, au warudisheni wasichana wetu,'' ambayo imekuwa ikifanywa nchini Nigeria na hata nje ya Nchi hiyo imeleta aibu kubwa sana kwa serikali ya Nigeria.
Waandamanaji wamekuwa wakikutana hadharani wakiishinikiza serikali hiyo kukoma kuzungumza tu katika vyombo vya habari na badala yake waongeze jitihada na kuhakikisha wasichana hao wamekombolewa.

Makosa sio ya serikali

Lakini wiki iliyopita, kundi tofauti lilianzisha kampeini sambamba, na hata kuvuruga ile ilyokuwa ikiendelea ambapo wanadai kuwa hasira zinastahili kuelekezewa hao watekaji nyara na wala sio serikali ya Nigeria.
Kundi hili linatumia nembo 'Release Our Girls Boko Haram'. Wameongeza jina Boko Haram kwa kusudi hapo mwisho. Polisi sasa wanasema kuwa maandamano haya yanatishia usalama kwa wananchi wa Abuja.
Lakini waandamanaji wanaoendesha kampeini ya 'Bring Back our Girls' sasa wanaona kama hili ni jaribio la serikali kuwanyamazisha na wamewasilisha ombi mahakamani kutaka kutolewe agizo la kuvunja amri hiyo ili waruhusiwe kufanya maandamano yao. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Sunday, June 01, 2014

GHANA YATANGAZA KIKOSI CHAKE KITAKACHOSHIRIKI KOMBE LA DUNIA, GYAN KUONGOZA KIKOSI

414047_heroa 
KOCHA mkuu wa timu ya taifa ya Ghana, Kwesi Appiah ametaja kikosi chake cha mwisho cha wachezaji 23 kwa ajili ya fainali za kombe la dunia zinazoanza kushika kasi mwezi huu nchini Brazil.  
Kikosi hicho cha Appiah kinajumuisha wachezaji 16 wanaokwenda kucheza fainali hizo kwa mara ya kwanza, huku nahodha Asamoah Gyan na Sulley Muntari wakiwa wakongwe wanaokwenda kucheza fainali zao za tatu mfululizo, wakati Jonathan Mensah, Michael Essien, Kwadwo Asamoah, Andre Ayew na Kevin-Prince Boateng wanakwenda kucheza fainali hizo kwa mara ya pili.  
Kocha huyo mwenye miaka 53 amewaacha majeruhi Jerry Akaminko, Jeffrey Schlupp na David Accam katika kikosi hicho kinachoelekea Miami kuweka kambi ya maandalizi ya mwisho ambapo kitacheza mechi ya kirafiki juni 9 dhidi ya Korea kusini Akaminko alipata majeruhi jana jumamosi katika kipigo cha bao 1-0 dhidi ya Uholanzi kwenye mechi ya kirafiki na atafanyiwa upasuaji utakaomfanya akae nje ya uwanja kwa miezi mitatu. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

GHANA YATANGAZA KIKOSI CHAKE KITAKACHOSHIRIKI KOMBE LA DUNIA, GYAN KUONGOZA KIKOSI


414047_heroa 
KOCHA mkuu wa timu ya taifa ya Ghana, Kwesi Appiah ametaja kikosi chake cha mwisho cha wachezaji 23 kwa ajili ya fainali za kombe la dunia zinazoanza kushika kasi mwezi huu nchini Brazil.  
Kikosi hicho cha Appiah kinajumuisha wachezaji 16 wanaokwenda kucheza fainali hizo kwa mara ya kwanza, huku nahodha Asamoah Gyan na Sulley Muntari wakiwa wakongwe wanaokwenda kucheza fainali zao za tatu mfululizo, wakati Jonathan Mensah, Michael Essien, Kwadwo Asamoah, Andre Ayew na Kevin-Prince Boateng wanakwenda kucheza fainali hizo kwa mara ya pili.  
Kocha huyo mwenye miaka 53 amewaacha majeruhi Jerry Akaminko, Jeffrey Schlupp na David Accam katika kikosi hicho kinachoelekea Miami kuweka kambi ya maandalizi ya mwisho ambapo kitacheza mechi ya kirafiki juni 9 dhidi ya Korea kusini Akaminko alipata majeruhi jana jumamosi katika kipigo cha bao 1-0 dhidi ya Uholanzi kwenye mechi ya kirafiki na atafanyiwa upasuaji utakaomfanya akae nje ya uwanja kwa miezi mitatu. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

TAIFA STARS YALAZIMISHA SARE YA 2 - 2 NA ZIMBABWE KATIKA MECHI YA MARUDIANO

DSC_457511 
Timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ imefanikiwa kuvuka hatua ya kwanza ya michuano ya kuwania kucheza michuano ya kombe la mataifa huru ya Afrika linalotarajiwa kufanyika mwakani.
Stars leo ilikuwa inacheza Zimbwabwe kwenye mchezo wa marudiano baada ya kuwafunga Zimbwabwe 1- 0 uwanja wa taifa wiki moja iliyopita, kwenye mchezo huo Stars imefanikiwa kufuzu baada ya kulazimisha sare ya 2-2.
Zimbwabwe walianza kufunga dakika ya 24, kabla ya Stars kusawazisha dakika kadhaa baadae kupitia Nadir Haroub ‘Cannavaro’ dakika ya 28. 
Muda mchache baadae  Thomas Ulimwengu aliongezea Tanzania bao la pili dakika ya 46, kabla ya dakika 10 baadae Zimbwabwe kusawazisha na kufanya matokeo 2-2.
Mpaka refa anapuliza kipenga cha mwisho matokeo yalibaki 2-2, na sasa Tanzania wanaingia hatua ya pili ambapo watacheza na Msumbiji. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

TANZIA: MAMA MZAZI WA MBUNGE ZITTO KABWE AFARIKI DUNIA

http://jambotz8.blogspot.com/ http://jambotz8.blogspot.com/Mama Mzazi wa Zitto enzi za uhai wake.
http://jambotz8.blogspot.com/ 
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAGEREZA 12 TANZANIA HAYAFAI KWA MATUMIZI YA BINADAMU...!!!




Mahabusu 


Wakati mamilioni ya fedha za Watanzania yakipotea kila mwaka kutokana na ufisadi na misamaha ya kodi, imebainika kuwa baadhi ya magereza nchini hayafai kutumiwa na wafungwa kutokana na kukosa sifa ukiwemo uchakavu wa majengo.

Ripoti ya utafiti uliofanywa na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kwenye magereza na vituo vya polisi 102 katika mikoa 12, inaeleza kuwa magereza 12 hayafai kutumiwa na binadamu.

Hali hiyo inaamanisha kwamba magereza hayo siyo tu ni hatari kwa wafungwa na mahabusu, bali pia kiwa watumishi wa Idara ya Magereza. Ripoti hiyo inaweka bayana kuwa magereza hayo yana hali mbaya kutokana na majengo yake kujengwa miaka mingi iliyopita, huku mengine yakikabiliwa na ukosefu wa mwanga wa kutosha.

Magereza yaliyotajwa kukosa sifa za kutumiwa na binadamu ni Rombo, Nzega, Geita, Ngudu, Kasungamile, Ukerewe, Mugumu, Musoma, Bunda, Ushora, Mang’ola na Bariadi.

“Hali kwenye haya magereza ni kinyume na Kanuni namba 10 ya Umoja wa Mataifa, inayozungumzia namna ya kuwahifadhi wafungwa ambayo inataka sehemu za kulala zikidhi vigezo vya kiafya, hali ya hewa, nafasi ya kutosha, joto na mwanga wa kutosha,” inasema sehemu ya ripoti hiyo. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

'JK VUA KOTI LA CCM, VAA LA UARAIS'




Mwenyekiti wa Kongamano la Katiba, Dk Ayub Rioba akizungumza na wajumbe mbalimbali waliohudhuria mdahalo ulioandaliwa na Muungano wa Asasi za Kiraia (Azaki) uliofanyika Dar es Salaaam jana. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa utetezi wa Haki za Binadamu, Onesmo Olengurumwa na Awadhi Ally Saidi aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya kukusanya maoni. Picha na Venance Nestory      

Dar es Salaam/Mwanza. Rais Jakaya Kikwete ameshauriwa kunusuru mchakato wa kupata Katiba Mpya ili usisimame kwa kuvua koti la Uenyekiti wa CCM na kubaki na Urais ili awaeleze wananchi nini cha kufanya kupata Katiba Mpya.
Ushauri huo umetolewa na viongozi mbalimbali wa vyama vya siasa na wasomi walioshiriki katika mdahalo wa Katiba uliofanyika jijini Dar es Salaam na Mwanza jana. Walisema kuwa Rais ana wajibu kuunusuru mchakato huo kwa kuwa yeye ndiye aliyeuvuruga kwa hotuba yake ya ufunguzi wa Bunge Maalumu la Katiba iliyoonekana kuelemea upande wa chama chake CCM.
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willibrod Slaa amesema Rais Jakaya Kikwete amekuwa kigeugeu juu ya Muundo wa Serikali za Muungano kama zilizopendekezwa kwenye Rasimu ya Kwanza na ya Pili ya Katiba.
Alisema kuwa Rais Kikwete alionyesha wazi kukubaliana na Muundo wa Serikali tatu, kwani kabla Rasimu ya Pili ya Katiba haijapelekwa kwenye Bunge Malaumu la Katiba ili kujadiliwa, alisaini kuonyesha kuwa amekubaliana na yaliyopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyoongozwa na Jaji Joseph Warioba. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JUNI 01, 2014 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.

.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

NDOTO ZA LUIS MONTES KUCHEZA FAINALI ZA KOMBE LA DUNIA ZAZIMA GHAFLA

Clash: Luis Montes came off worse than Segundo Castillo when the pair went for a 50-50 ball
Agony: It left Montes in severe pain as his team-mates urged the club doctor to come to his attention
 Mchezaji mwenzake akimuita daktari wa timu baada ya Montes kupata majeruhi kubwa
Worried: Montes' Mexican team-mates look on as their midfielder is lifted on to a stretcher
 Wasiwasi: Wachezaji wenzake wakimtazama Montes anapobebwa na machela.
NDOTO za Luis Montes kuichezea Mexico katika fainali za kombe la dunia mwaka huu nchini Brazil zimezima ghafla kufuatia kuvunjika mguu jana usiku kwenye mechi ya kirafiki dhidi ya Ecuador.
Nyota huyo mwenye miaka 28 alishuhudia timu yake ikishinda mabao 3-1 na yeye akifunga bao dakika ya 33, lakini dakika mbili baadaye alipata majeruhi mbaya.
Montes alibebwa na machela kutoka nje ya uwanja baada ya kugongana na mchezaji wa Ecuador,  Segundo Castillo, na kumuacha kocha wake Miguel Herrera akikiri wazi kuwa timu umwombee mchezaji huyo. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

AMUUA MKEWE KWA WIVU WA MAPENZI...!!!

Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya Ahmed Msangi
Watu wanne wamefariki dunia katika matukio tofauti likiwamo la mwanamke mmoja kudaiwa kuuawa na mume wake kutokana na wivu wa mapenzi.
Katika tukio la kwanza, Mkazi wa Kijiji cha Liwalanje, wilayani Mbozi, Christina Hayola (35) amefariki dunia baada ya kukatwa na kitu chenye ncha kali kifuani na miguuni na mtu anayedaiwa kuwa mume wake.
Kamanda wa Polisi mkoani Mbeya, Ahmed Msangi alisema uchunguzi wa awali umebaini kwamba chanzo cha mauaji ni wivu wa mapenzi na kwamba polisi wanamsaka mhusika.
Katika tukio la pili, Msangi alisema mkazi wa Isanga jijini hapa, Abdi Sanga aliuawa kwa vipigo baada ya kutuhumiwa kuwa wizi katika eneo la Forest.
Alisema marehemu anadaiwa alikuwa na mwenzake ambaye alitoroka baada ya kuiba vitenge vyenye thamani ya Sh70,000.
Katika tukio la tatu na la nne, alisema mwanafunzi wa Shule ya Msingi Ibumila wilayani Mbarali, Fitina Mwandosya alifariki dunia baada ya kudondoka kutoka kwenye trekta dogo aina ya ‘Powertiller’ alilokuwa amepanda akitoka kuvuna mpunga.
Alisema mwanafunzi huyo alipatwa na mkasa huo juzi wakati wanarudi na wenzake waliokwenda kuvuna mpunga wa shule.
Wakati huohuo mwanafunzi mwingine wa kidato cha pili Sekondari ya Makongorosi, wilayani Chunya, Aden Ngombe(17) amefariki dunia juzi baada ya kugongwa na lori aina ya scania alipokuwa akikatisha barabara.
Msangi alisema polisi walimkamata dereva wa lori na kubainika alikuwa amelewa pombe.
Katika matukio mengine watu wanne wanashikiliwa na polisi kwa tuhuma mbalimbali zikiwamo za kukutwa na bastola kinyume na sheria.
Kamanda wa polisi alisema aliyekamatwa na bastola ni mkazi wa Kijiji cha Itentula, Mbozi aliyekuwa na bastola aina ya Baby. risasi tatu. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Na Mwananchi

MWANAMKE ALIYEBADILI DINI NA KUPEWA ADHABU YA KIFO APATA UTETEZI

Bi.Meriam Ibrahim na mumewe
Afisa mmoja mwandamizi katika wizara ya maswala ya kigeni nchini Sudan amesema kuwa mwanamke aliyepewa hukumu ya kifo kwa kubadili dini yake ya kiislamu, Meriam Ibrahim atawachiliwa huru katika kipindi cha siku chache zijazo.
Abdullahi Alzareg ambaye ni katibu katika wizara hiyo amesema kuwa Sudan inatilia maanani uhuru wa kuabudu na kwamba serikali itamtetea mwananmke huyo.
Kumekuwa na shutma za kimataifa kuhusu hukumu aliyopewa mwanamke huyo.
Meriam Ibrahim anazuiliwa katika jela moja ambapo alijifungua mtoto wa kike juma hili.
Ameolewa na mkristo na pia amehukumiwa kuchapwa viboko mia moja kwa kuzini kwa sababu mwanamke wa kiislamu kuolewa na mkristo ni haramu kulingana na sheria za Sudan. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Na BBC

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...