Thursday, May 22, 2014

UNYAMA: MTOTO AFICHWA KWENYE BOKSI NA KUFUNGIWA NDANI KWA MIAKA MINNE...!!!


Rashid Mvungi  akimuangalia mtoto wake Nasrah Rashid (4) ambaye ni mlemavu wa viungo aliyefungiwa chumbani na kufichwa kwenye boksi bila ya kufanyiwa usafi tangu akiwa na umri wa miezi tisa. Picha na Hamida Shariff 

Alikuwa akitoa maelezo hayo huku akiwa amemshikilia mtoto huyo aliyetapakaa uchafu ikiwamo haja kubwa na ndogo alizokuwa akitoa ndani ya boksi na kusema kwamba mara ya mwisho alimwogesha Julai mwaka jana.

Morogoro. Mwanamke aliyetambuliwa kuwa ni Mariamu Said mkazi wa Kiwanja cha Ndege, Morogoro juzi alishushiwa kipigo na wananchi kutokana na kumficha mtoto wa marehemu mdogo wake kwenye boksi kwa miaka minne.

Tukio hilo lilitokea juzi saa nne asubuhi baada ya majirani zake kutoa taarifa kwa Ofisa Mtendaji wa Kata ya Kiwanja cha Ndege, Dia Zongo kuhusu mtoto huyo, Nasra Rashid, kufichwa ndani ya boksi tangu akiwa na umri wa miezi tisa. Zongo alisema majirani hao walimweleza pia kuwa jirani yao huyo hamfanyii usafi mtoto huyo wala kumtoa nje.

Baada ya kupata taarifa hizo, Zongo alimtafuta Mwenyekiti wa Mtaa huo, Tatu Mgagala na kuongozana naye hadi kwenye nyumba hiyo na kumhoji mwanamke huyo ambaye alikuwa akijibu kwa kubabaika. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS MEI 22, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.

.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

NGASSA, SAMATTA KUGOMBEA TUZO MOJA

 Mchezaji wa Yanga, Mrisho Ngassa pamoja na Mbwana Samatta wa TP Mazembe, wanaumana katika kuwania tuzo za mwanamichezo anayependwa zaidi na watu zinazoendeshwa na Kampuni ya Bongo 5 Media Group kupitia tovuti yake ya bongo5.com.
Wengine wanaowania tuzo katika kipengele hicho ni Ramadhan Singano (Simba SC), Juma Kaseja (Yanga) na bondia Francis Cheka.
Inaonekana kuwa Ngasa na Samatta watakuwa na ushindani mkubwa zaidi hasa ikizingatiwa kuwa wachezaji wote wana mashabiki wengi na pia kila mmoja anacheza mchezo unaopendwa na wengi.
Akizungumzia tuzo hizo, mhariri mkuu wa bongo5.com, Fredrick Bundala, alisema watu wengi walijitokeza kupigia kura kuchagua watu wanawataka kushinda tuzo mbalimbali.
Bundala alivitaja vipengele vingine na majina ya waliopendekezwa kuwa ni pamoja na Nisher, Adam Juma, Nick Dizzo, Mecky Kaloka, Jerry Mushala wanaowania tuzo ya Mwongozaji Bora wa Video za wasanii.
Video Bora kwa Wanaume ni My Number ya Diamond, Jikubali ya Ben Pol, Mirror ya Baby, Love Me ya Izzo Bizness, Barnaba na Shaa, Muziki Gani ya Nay wa Mitego na Diamond.
Alisema wanaowania Tuzo ya Video ya Mwanamuziki wa Kike ni Amani ya Moyo ya Feza Kessy, Closer ya Vanessa Mdee, Sugua Gaga ya Shaa, Yahaya ya Lady Jaydee, Nakomaa na Jiji ya Shilole.
Bundala alifafanua kuwa wananchi wanatakiwa kuchagua jina moja kutoka katika majina matano ya kila kipengele kilichotajwa.
“Wiki moja baada ya majina ya washiriki watano kutangazwa, mchujo wa kwanza utafanyika katika kila kipengele,” alisema Bundala.
Aliwataka Watanzania kuwapigia kura wale wanaowapenda kwa kutuma ujumbe mfupi na baadaye kufuata maelekezo rahisi ya kupiga kura pia kupitia tovuti www.tuzozetu.com. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

YAYA AITIA KIWEWE MANCHESTER CITY

Yaya Toure amekoleza moto kwenye sakata lake kutaka kuihama Manchester City akisema hajui hadi sasa atakapokwenda kucheza msimu ujao.
Wakala wa mchezaji huyo, Dimitri Seluk alibainisha kuwa Yaya anaweza kuondoka kwa sababu anadhani kwamba amekuwa akichukuliwa kama mtu asiyeheshimika na wamiliki wa klabu hiyo.
Hivyo kwa sasa, Toure ambaye ana miaka 31, hajaamua hatima yake kuhusu klabu atakayochezea msimu ujao.
Alipoulizwa kama anaweza kuichezea klabu nyingine msimu ujao, alijibu: “Ndio. Hatujui katika soka nini kitatokea. Kamwe hatuwezi kujua hilo.”
Katika mahojiano maalumu na mtandao wa BE IN SPORTS, nyota huyo wa timu ya taifa ya Ivory Coast alisema: “Kwa sababu ya msimu mzuri niliokuwanao klabu ya Man City, kila mtu ananizungumzia na kila kitu kiko wazi.
“Wakala wangu Dimitri, siku zote amekuwa akizungumza na watu kwa simu na anajua cha kufanya kwa sababu siku zote nimekuwa nikimuamini sana.
“Hatujui kesho itakuwaje, lakini kwa sasa akili yangu iko katika Kombe la Dunia na baada ya kumalizika kwake tutajua nini kimetokea.”
Toure alisaini mkataba mpya wa miaka minne kuichezezea City Aprili mwaka jana.
Hata hivyo, majaaliwa yake yamebaki kuwa na mashaka kutokana na wakala wake kuwalaumu wamiliki wa City kwa kutoonyesha heshima kwa kiungo huyo alipotimiza miaka 31. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

WAZIRI AJIUA BAADA YA KUSHINDWA KATIKA UCHAGUZI

Shughuli ya kuhesabu Kura Malawi
Naibu waziri wa serikali za mitaa wa Malawi amejipiga risasi na kujiua nyumbani kwake mjini Lilongwe.
Godfrey Kamanya alikuwa anayegombea kutetea kiti chake cha ubunge katika jimbo la Nzonzi Kusini amejiua alfajiri ya leo katika mojawapo ya vyumba vya nyumba yake iliyopo Area Ten mjini Lilongwe.
Mwili wa marehemu umehifadhiwa kwenye hospitali kuu ya Kamuzu mjini humo, na jeshi la polisi litatoa taarifa rasmi ya kifo hicho baada kukamilisha uchunguzi.
Haijajulikana sababu za Kamanya kujiua japokuwa ameacha barua ya maelezo ambayo polisi wataitoa baadae.
Matokeo ya kura bado hayajatangazwa rasmi katika kile kinachosemekana kuwa uchaguzi wenye ushindani mkali sana.
Afisa mkuu wa uchaguzi, amesema kuwa mfumo wa elektroniki umeharibika na maafisa wanatumia matokeo kwa njia ya barua pepe. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Wednesday, May 21, 2014

MELI YA KIKWETE KUKAMILIKA 2016

http://jambotz8.blogspot.com/
Siku kama ya leo mwaka 1996, ilikuwa ni vilio kila kona ya nchi, lakini Kanda ya Ziwa iliathirika zaidi na kuzama kwa meli ya Mv Bukoba na kuteketeza mamia ya wananchi.
Kuzama kwa Mv Bukoba inaelezwa ni kutokana na kuwa ubovu. Tukio hilo ambalo haliwezi kufutika vichwani mwa wakazi wa Kanda ya Ziwa, lakini kilio chao cha kupatiwa meli mpya licha ya Rais Jakaya Kikwete kuahidi Serikali kununua mwaka 2010, haijanunuliwa hadi sasa.
Hata hivyo, inaelezwa kuwa ujenzi wa meli hiyo mpya iliyoahidiwa na Rais Kikwete kwa Ziwa Victoria unatarajia kukamilika mwaka 2016.
Akizungumza ofisini kwake wiki hii, Ofisa Masoko wa Huduma za Meli Mwanza Obedi Nkongoki alisema mjenzi wa meli hiyo Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Denmark (Danida) kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania.
http://jambotz8.blogspot.com/
“Ujenzi huu unahusisha meli nne ingawa Rais aliahidi tatu; Ziwa Victoria moja, mbili Ziwa Tanganyika na nyingine Ziwa Nyasa ambazo zinatarajiwa kukamilika 2018, huku ya Ziwa Victoria ikitarajiwa kukamilika 2016,” alisema Nkongoki. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATANO MEI 21, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.

.

.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

VIFO VYA BOMU NIGERIA VYAFIKIA 118

Maafisa nchini Nigeria wamesema kuwa wamepata maiti 118 kufuatia shambulio la bomu katika mji wa Jos.
Mabomu mawili yalilipuka mojawepo ikiwa imefichwa ndani ya gari na kulipuka katika soko moja kubwa. Dakika 20 baadaye mlipuko wa pili ulitokea karibu na hospitali.
Inahofiwa kuwa kuna maiti zaidi zilizonaswa kwenye vifusi vya majengo yaliyo poromoka kutokana na shambulio hilo.
Kufikia sasa hakuna kundi lililodai kuhusika na shambulio hilo lakini wengi wanaamini kuwa Kundi la wapiganaji wa kiislamu la Boko Haram lilihusika.
Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan amejitokeza kukemea mashambulio hayo na kusema kuwa amejitolea kuangamiza kabisa ugaidi. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Na BBC Swahili

JESHI LA KENYA LAWASHAMBULIA AL-SHABAAB

Wanajeshi wa Kenya wanaendelea kukabiliana na Al Shabaab Somalia
Jeshi la Kenya limeishambulia ngome ya Al Shabab ya Jilib huko Somalia.
Katika mahojiano na BBC, msemaji wa Jeshi la Kenya Willy Wesonga amesema kuwa oparesheni hiyo kutoka angani imefaulu kuwaangamiza baadhi ya wakuu wa Al Shabab.
Ngome hiyo inadaiwa kuwa eneo ambapo wapiganaji hao wa kiislamu wanafanya mazoezi na mikutano yao.
Kikosi cha Kenya kinadai kuishambulia ngome hiyo baada ya kupokea taarifa kutoka kwa wakaazi wa wilaya hiyo ya Jilib.
Wapiganaji wa Al shabab wamezidisha mashambulio nchini Kenya tangu nchi hiyo iingize wanajeshi wake ndani ya Somalia kuwasaka wapiganaji hao haramu mwaka wa 2011
Wesonga anasema jeshi la Kenya linalishambulia Al shabaab kama sehemu ya vita vikuu duniani dhidi ya ugaidi, na pia kuwazuia wafuasi wa kundi hilo kutekeleza mipango yao, yanayohatarisha usalama wa kieneo.
Hayo yanajiri wakati kundi la Al Shabab likidai kufanya shambulizi huko Mandera na kuwaua maafisa wa usalama wa Kenya. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Na BBC Swahili

Monday, May 19, 2014

VAN GAAL AMTEUA VAN PERSIE KUWA NAHODHA MPYA MAN UNITED

Double Dutch: Louis van Gaal (right) sees Robin van Persie as his perfect captain at Manchester United
 Waholanzi wawili: Louis van Gaal (kulia) anaona Robin van Persie ndiye nahodha aliyekamilika katika klabu ya Manchester United.
LOUIS van Gaal  anatarajia kumteua mshambuliaji wake hatari Robin van Persie kuwa nahodha wa kikosi chake mara atakapojiunga na Manchester United baada ya kumalizika kwa kombe la dunia majira ya kiangazi nchini Brazil.
Jumamosi iliyopita Van Persia aliifungia bao muhimu timu ya taifa ya Uholanzi katika mechi ya kirafiki dhidi ya Ecuador na kulazmisha sare ya 1-1.
Van Gaal amekuwa na mahusiano mazuri na RVP ambaye ni nahodha wa timu ya taifa na sasa anatarajia kumpa jukumu hilo katika klabu ya Man United na kumpiga chini Rooney ambaye angekuwa nahodha wa kudumu katika utawala wa David Moyes.
A sign of things to come? Van Persie (right) poses with Kluivert (left), Louis van Gaal's assistant manager
Class: Holland captain van Persie scored a fantastic volley in their 1-1 draw with Ecuador on Saturday

SAKATA LA IPTL LAZIDI KUWAVURUGA WABUNGE


KABWE_b5fd6.jpg
Dodoma. Sakata la fedha za IPTL limechukua sura mpya baada ya baadhi ya wabunge kudai kurubuniwa na wenzao kwa fedha ili wakwamishe Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini, wakidai balozi mmoja yuko nyuma ya mpango huo.
Katika sakata hilo, Sh200 bilioni zilizohifadhiwa kwenye akaunti ya Escrow zilitolewa na kulipwa kwa Kampuni ya Pan African Power (PAP), ambazo Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali amesema anachunguza akishirikiana na Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru).
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Kabwe Zitto ameonya kuwa kuwaingiza mabalozi katika sakata la ufisadi wa zaidi ya Sh200 bilioni za IPTL ni kuibua mgogoro wa kidiplomasia na nchi husika.
Akizungumza na gazeti hili jana, mbunge huyo alisema kuwa kiongozi yeyote atakayegundulika kufaidika na hongo hiyo, kamati yake itaweka wazi jina lake na hakuna atakayeachwa bila kuchukuliwa hatua za kisheria.
Zitto alitoa kauli hiyo jana baada ya kubainika ujumbe mfupi wa maandishi (sms) unaodaiwa kusambazwa, ukifichua kile kinachodaiwa ni kuhongwa kwa baadhi ya wabunge ili wakwamishe bajeti ya wizara hiyo.
Ujumbe huo unasomeka: "Spika wa Bunge la Jamhuri, sisi wabunge waadilifu tunakiri kwamba Mhe. Mkono ametufuata na kutupatia fedha kila mmoja milioni 3 ili tukwamishe bajeti ya Nishati na Madini.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

COSMAS CHEKA ATAMBA KUTETEA UBINGWA WAKE WA TPBO

IMG_8710Cosmas Cheka ‘kulia’
Na Mwandishi Wetu BONDIA Cosmas Cheka anatarajia kupanda ulingoni juni mosi kwa ajili ya kutetea taji lake la ubingwa wa TPBO anaoshikilia kwa kupambana na Suma Ninja katika ukumbi wa vijana social hall wa Morogoro
Akizungumzia mpambano huo Cheka amesema amejiandaa kupigana kwa raundi kumi hivyo mashabiki waje kuona kazi anayoifanya akiwa ulingoni. Bondia huyo ambaye anatamba sambamba na kaka yake Fransic Cheka aliyekuwa bingwa wa WBF ambao alivuliwa kizembe amesema yeye anataka afike mbali zaidi ya kaka yake huyo.
Pambano hilo linalosimamiwa na TPBO litasindikizwa na mapambano ya utangulizi kati ya Kudura Tamimu atakaeevaana na Sadiki Yusufu, wakati Mohamed Matimbwa ataoneshana umwamba na Twaha Kassimu
Siku hiyo pia kutakuwa na uuzwaji wa DVD kali za ngumi wakiwemo mabondia wakali wanaotamba Duniani na hapa nchini kama Mohamed Matumla vs Fransic, Miyeyusho, Japhert Kaseba Vs Thomas Mashali , Floyd Mayweathar, Manny Paquaio, Saul ‘canelo’ alverez , Mike Tyson, Mohamed Ali, Ferex Trinidad, Miguel Cotto na wengine wengi
DVD hizo za ngumi kali zitakuwa zikiuzwa na kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila ‘Super D’ Pamoja na kutambua sheria na taratibu za mchezo huo siku hiyo pia kutakuwa na vifaa vya mchezo huo wa masumbwi vitakavyotolewa zawadi kwa mabondia na Kocha Super D ambaye ameahidi kutoa, Gum Shit ,Clip Bandeji,DVD za Mafunzo kwa mabondia, Bukta, Protector na vifaa mbalimbali kwa mabondia watakaoonesha uwezo wa hali ya juu wa kutupiana masumbwi. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATATU MEI 19, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.

.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

'NAPE ALAANIWE KWA KUTUITA BOKO HARAM'


Mbunge wa viti maalumu kwa tiketi ya CUF, Amina Abdallah Amour amemjia juu katibu wa itikadi na uenezi wa CCM, Nape Nnauye kwa kuufananisha Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) na kundi la Boko Haramu na kutaka alaaniwe.
Ukawa iliundwa wakati wa Bunge Maalumu la Katiba na unahusisha wajumbe kutoka vyama vya NCCR-Mageuzi, Chadema na CUF.
Akizungumza bungeni mjini Dodoma juzi, mbunge huyo alisema kauli ya Nnauye ni ya uchochezi na inapaswa kulaaniwa.
Mbunge huyo alikuwa akichangia hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Wanawake, Jinsia na Watoto kwa mwaka 2014/2015 iliyowasilishwa na waziri wake, Sophia Simba.
“Gazeti la Uhuru (jana) lilimnukuu Nape Nnauye akisema Ukawa ni sawa na Boko Haramu… Hii ni kauli chafu na ya uchochezi. Haikubaliki na ninailaani kwa nguvu zangu zote,” alisema.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

ASKOFU "HOFU YA MUNGU ITATUPA KATIBA MPYA"


Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu akiongoza watu mbalimbali kumpongeza Askofu Mkuu mpya wa Jimbo la Songea, Damian Dallu katika Kanisa la Mtakatifu Mathias Mulumba Kalemba mjini Songea jana. Picha na Joyce Joliga 


Kwa ufupi
Hayo aliyasema jana katika Ibada maalumu ya kumsimika rasmi iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Kiaskofu la Mtakatifu Mathias Mulumba lililopo Mjini Songea ambayo ilihudhuriwa na maelfu ya waumini, viongozi wa chama na Serikali, viongozi wa madhehebu ya dini pamoja na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Anne Makinda.

Songea. Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Songea, Damian Dallu amesema Katiba Mpya itapatikana iwapo wajumbe wa Bunge la Katiba watakuwa na maadili ya kiroho kwa kufuata maagizo ya Mwenyezi Mungu bila kupindisha ukweli wa mchakato wa maoni ya Katiba.

Amesema kupotosha ukweli wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba unaweza kuipeleka nchi kubaya.

Hayo aliyasema jana katika Ibada maalumu ya kumsimika rasmi iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Kiaskofu la Mtakatifu Mathias Mulumba lililopo Mjini Songea ambayo ilihudhuriwa na maelfu ya waumini, viongozi wa chama na Serikali, viongozi wa madhehebu ya dini pamoja na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Anne Makinda. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...