Monday, May 19, 2014

'NAPE ALAANIWE KWA KUTUITA BOKO HARAM'


Mbunge wa viti maalumu kwa tiketi ya CUF, Amina Abdallah Amour amemjia juu katibu wa itikadi na uenezi wa CCM, Nape Nnauye kwa kuufananisha Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) na kundi la Boko Haramu na kutaka alaaniwe.
Ukawa iliundwa wakati wa Bunge Maalumu la Katiba na unahusisha wajumbe kutoka vyama vya NCCR-Mageuzi, Chadema na CUF.
Akizungumza bungeni mjini Dodoma juzi, mbunge huyo alisema kauli ya Nnauye ni ya uchochezi na inapaswa kulaaniwa.
Mbunge huyo alikuwa akichangia hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Wanawake, Jinsia na Watoto kwa mwaka 2014/2015 iliyowasilishwa na waziri wake, Sophia Simba.
“Gazeti la Uhuru (jana) lilimnukuu Nape Nnauye akisema Ukawa ni sawa na Boko Haramu… Hii ni kauli chafu na ya uchochezi. Haikubaliki na ninailaani kwa nguvu zangu zote,” alisema.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Mbunge huyo alihoji “wazazi wao hawajui watoto wao wanaishije, wanakula nini wala wanalala vipi…. Leo hii Nape Nnauye amethubutu kusema Ukawa ni sawa na Boko Haramu?”
Hata hivyo, wakati akihoji hivyo, baadhi ya Wabunge wa CCM nao walisikika wakihoji “na Intarahamwe Je?”.
Ukawa ilitumia jina hilo la Interahamwe wakati mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba akitangaza uamuzi wa kundi hilo kujitoa kwenye Bunge la Katiba, akiifananisha CCM na kundi hilo la nchini Rwanda.
Katika gazeti hilo, Nnauye amenukuliwa akisema Ukawa ni kundi hatari linaloeneza chuki na kusambaza uongo kwa Wananchi kwa nia ya kuwagawa na kusema silaha wanazotumia ni zaidi ya Boko Haramu.
Nnauye anadaiwa kutoa kauli hiyo katika mkutano wa hadhara uliofanyika mkoani Tabora, akisema silaha za uongo wanazotumia viongozi wa Ukawa ni hatari zaidi kuliko silaha za moto zinazotumiwa na Boko Haramu.
Viongozi wa CCM na wale wa Ukawa wamekuwa wakizunguka nchi nzima kufanya mikutano ya hadhara kufafanua kile kilichojitokeza ndani ya Bunge la Katiba na kusababisha Ukawa kususia Bunge hilo. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Chanzo: Mwananchi

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...