Thursday, May 15, 2014

MWANAMKE AHUKUMIWA KUNYONGWA BAADA YA KUASI DINI...!!!

Serikali imesema kuwa Sudan sio nchi ya kwanza kutekeleza sheria za kiisilamu
Mahakama nchini Sudan imemhukumu kifo mwanamke mmoja anayedaiwa kubadili dini yake na kuolewa na mwanamume mkristo. Daktari Mariam Yahya Ibrahim Ishag, ambaye babake ni muisilamu alishitakiwa kwa kosa la kuasi dini pamoja na kufanya zinaa kwa kuolewa na mwanamume mkristo , kitu ambacho dini ya kiisilamu imeharamisha kwa wanawake.
Mariam mwenye umri wa miaka 28 pia ni mjamzito na ataadhabiwa kwa kuchapwa mijeledi miamoja kwa kosa la zinaa. Maafisa wakuu wanasema kuwa licha ya Mariam kulelewa kwa njia ya kikristo yeye bado ni muisilamu kwa sababu hiyo ndiyo dini ya babake. Alipewa siku tatu baada ya kuhukumiwa aweze kurejea katika dini ya kiisilamu lakini akakataa na ndio maana adhabu ikasalia.
Kwa kawaida wanawake waisilamu hawaruhusiwi kuolewa na wanaume wakristo ingawa wanaume waisilamu wanaruhusiwa kuwaoa wanawake wakristo. SShirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu Amnesty International linasema kuwa Bi Ishag alilelewa kama Mkristo muorthodoxi kwa sababu babake hakuwepo naye maishani mwake.
'Kesi ya kwanza'
Kesi ya Ibrahim ni ya kwanza ya aina yake kusikika nchini Sudan , kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters. Wanaharakati wa kutetea haki za binadamu, wamelaani uamuzi huo wa mahakama na kuitaka serikali ya Sudan kuheshimu haki na uhuru wa watu kuabudu. Maafisa wa balozi za mataifa ya magharibi pia wamekemea vikali kesi hiyo na kuelezea asiwasi wao kuihusu. Maafisa hao wamewataka maafisa wa sheria nchini humo kuangalia kesi hiyo upya na kuhakikisha kuwa Mariam anatendewa haki.
Waziri wa mawasiliano amesema kuwa sio Sudan peke yake ambako sheria za kiisilamu zinafuatwa na ambako sio sawa kwa mtu kubadili dini yake, hali hiyo pia ipo nchini Saudi Arabia na katika nchi zingine zinazofuata sheria za kiisilamu. Serikali ya Rais Omar al-Bashir inakabiliwa na changamoto nyingi za kiuchumi na kisiasa hasa baada ya kujitenga na Sudan Kusini ambako mafuta yake yalikuwa yanatoka mwaka 2011.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Chanzo: BBC 

IJUE HISTORIA YA KAMPUNI YA MABASI YA SCANDINAVIA EXPRESS ILIYOLETA HESHIMA KWA TAIFA...!!!


Kampuni ya mabasi ya Scandinavia Express ni kampuni pekee ya kitanzania iliyowahi kutokea kwa kuwa na huduma za uhakika na za viwango vya hali ya juu kabisa kulinganisha na huduma zinazotolewa na kampuni za sasa. Kampuni hii ilijijengea jina kubwa na sifa nzuri ndani na nje ya nchi kwa huduma bora walizokuwa wakizitoa kwa abiria wake na pia kuliletea sifa taifa la Tanzania kwa kujulikana kuwa na mabasi ambayo ni quality na high class.

Kampuni ya Scandinavia ilianzishwa zaiidi ya miaka thelathini na tano (35) iliyopita ikiwa na mabasi machache tu aina ya LEYLAND  na ilipofika mwaka 1982 kwa mara ya kwanza Scandinavia walinunua basi lao la kwanza la kisasa kutoka kampuni ya SCANIA TANZANIA COACHES aina ya SCANIA ambalo kutokana na ubora  wake na uzuri wake kwa kipindi hicho waliamua kulitumia kwa safari yao mpya waliyoianzisha ya Dar es salaam hadi Iringa.
BASI LA KWANZA LA KISASA KUNUNULIWA NA SCANDINAVIA 1982
Kadiri mahitaji ya usafiri yalivyokuwa yakiongezeka ndipo michirizi ya rangi ya BLUU,KIJIVU na NYEKUNDU ikaanza kuonekana katika mabasi mengi zaidi yaliyokuwa yakisafirisha abiria karibia kila kona ya Tanzania.
Ilipofika mwaka 2001 kampuni ya Scandinavia walianzisha safari yao ya kwanza kabisa kutoka nje ya nchi kwa safari ya Dare es salaam hadi Nairobi nchini Kenya,ambapo mafanikio ya ruti hiyo yalipelekea kuzaliwa kwa ruti nyingine kati ya Nairobi hadi Mombasa na Mombasa hadi Dar es salaam. Katika mwaka wa 2002 kampuni ya Scandinavia walipanua wigo wa huduma zao kwa kuanza ruti mpya ndani ya Afrika mashariki kwa safari za Dare es salaam hadi Kampala nchini Uganda.
Ilipofika mwaka 2003 kampuni ya Scandinavia ilipanua wigo zaidi kwa kuanza kwenda katika mji mkuu wa nchi ya Zambia Lusaka. Wakati huo wote kampuni ya Scandinavia ilikuwa chini ya mkurugenzi na mwanzilishi wake MR.MUHAMED ABDULLAH. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

UTALII WA NGONO WANAWIRI MALINDI NCHINI KENYA...!!!

jambotz8.blogspot.com
Utalii wa Ngono wanawiri Malindi Kenya
Unapouzuru mji wa Malindi uliopo kwenye mwambao wa Kenya unaonekana kama paradiso.
Hata hivyo mji huu ni kitovu kilichojificha cha biashara ya ngono ya watoto. Watoto wadogo wenye umri wa miaka hata 12 hutumiwa katika ukahaba na filamu za ngono na watalii ambao huwa tayari kulipa pesa nyingi kwa ajili ya ngono katika maeneo yaliyojificha. Maafisa wanasema biashara hii imependwa sana na wasichana hao wadogo na wavulana kiasi kwamba wengi wao huacha shule.
Kijana mmoja mwenye umri wa miaka kumi na saba ameiambia BBC kuwa aliacha shule kutokana na ufukara. Alivutiwa kuingia katika biashara ya ngono baada ya rafiki yake aliyekuwa akifanya kazi hiyo kukutana na mtalii aliyempeleka bara Uropa na sasa anaishi maisha ya ustaarabu. Maisha ni hayo hayo pia kwa wasichana.
jambotz8.blogspot.com
Utalii wa Ngono wanawiri Malindi Kenya
Msichana mmoja ameiambia BBC kuwa alianza biashara ya ngono akiwa na miaka 15, bila mamake kujua. Anaeleza ugumu wa biashara hiyo na jinsi wasichana wanavyogeuzwa kuwa watumwa wa ngono na hata kulazimishwa kushiriki tendo hilo na wanyama kama mbwa.
Hatahivyo anasema haoini ubaya wowote kwani ndiyo njia pekee inayomuwezesha kujimudu kimaisha.
Juhudi za mamake kumshawishi aiache biashara hiyo zimeambulia patupu. Ni suala linalowasumbua viongozi katika jamii hii. Naibu chifu wa kata ndogo ya Shela, Mayele anasema watu wengi hawatoi ripoti kwa serikali. Sasa Chifu huyo ameanzisha harakati kwa jina ''rudi shule'' ambapo watoto wakipatikana mjini wakati wa shule wanakamatwa na kupelekwa nyumbani, kisha wazazi wao kukamatwa na kufunguliwa mashtaka.
Anaamini kwamba mambo yataimarika, lakini changamoto bado ni nyingi.  
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Chanzo: BBC

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS MEI 14, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.

.

.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MTOTO AANGUKA TOKA GHOROFA YA 11 ANUSURIKA...!!!

Mtoto aanguka toka ghorofa ya 11 anusurika
Mtoto mwenye umri wa mwaka mmoja amenusurika kifo baada ya kuanguka kutoka ghorofa ya 11 ya jengo moja mjini Minnesota Marekani. Vyombo vya habari katika jimbo hilo vimeripoti kuwa Musa Dayib, amevunjika mkono mara mbili na kwa sasa anapumua kwa usaidizi wa mashine japo madaktari wanamtarajia kuishi. Musa aliteleza katikati ya mianya inayozingira sebule yao katika ghorofa ya 11 ya mjengo huo wenye nyumba na makazi ya watu.

Muuguzi mkuu katika zahanati aliyolazwa amesema kuwa Musa anatarajiwa kuishi baada ya kuanguka katika eneo lisilo kavu sana. Jamaa na marafiki wa familia hiyo ya kisomali wamepigwa na butwaa kutokana na tukio hilo. Tukio hilo lilizua mjadala kama ni muujiza au la kuwa amenusurika kifo lakini watafiti wameelezea kuwa mtoto ananafasi nzuri zaidi ya kuishi hata baada ya kuanguka ama kupatwa na janga lolote lile kwani mwili wao bado ni mwororo na mifupa ya mtoto huwa bado ni laini kinyume na mtu mzima ambaye tayari mifupa yake ni kavu na mwili wake ni mkubwa na mzito.

Abdirizak Bihi alisimulia muujiza huo kwa gazeti la The Star-Tribune. "baada ya kushuhudia yaliyotendeka hapa ninahofia usalama wa wazazi wa mtoto ambao hadi kufikia sasa wamepigwa na bumbuazi hawazungumzi na yeyote."
Dakta Tina Slusher, aliyemhudumia mtoto Musa, alisema hakuna vile mtu mzima angenusurika baada ya kuanguka umbali kama huo. Bila shaka huu ni muujiza wa Mwenyezi mungu kwa familia hiyo. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Chanzo: BBC

SEVILLA MABINGWA WA EUROPA

Sevilla ndio mabingwa wa ligi ya bara Uropa mwaka 2014.
Vigogo hao wa ligi kuu ya Uhispania la liga waliwalaza Benfica kutoka Ureno mabao 4-2 kwa mikwaju ya penalti.
Timu hizo zilikuwa zimetoshana nguvu suluhu bin suluhu katika muda wa kawaida na ziada katika mechi hiyo iliyochezewa mjini Turin Italia.
Ushindi huo ulidhibitishia mashabiki wa kandanda kote duniani ufanisi wa ligi kuu ya Uhispania La Liga kwani ulikuwa ushindi wa tatu kwa timu hiyo ya Sevilla katika kipindi cha miaka mitatu .
Kwa upande wake Benfica sasa itasubiri muda zaidi kwani hawajashinda katika fainali nane sasa.
Mara ya mwisho timu hiyo kushinda taji lolote barani Uropa ilikuwa ni miaka 50 iliyopita 1962 .
Mechi hiyo iliishia sare tasa na ulipowadia wakati wa kuamua kupitia mikwaju ya penalti ni kipa wa Sevilla Beto aliyeamua taji hilo litaenda Uhispania wala sio Ureno.
Beto aliokoa mikwaju miwili ya Oscar Cardozo na Rodrigo na kuitunuku Sevilla taji la Europa kwa ushindi wa mabao 4-2.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Wednesday, May 14, 2014

HII NDIO ORODHA YA WASANII WA KILI TOUR 2014

Ile orodha ya wasanii watakaoshiriki kwenye Kili Music Tour 2014 imetangazwa leo. Kwa mwaka huu zaidi ya wasanii 30 watashiriki katika ziara hiyo kwenye mikoa zaidi ya 10 nchini na itakayoanza ambao Mei hadi Septemba 2014. Wasanii hao ni pamoja na Diamond, Ommy Dimpoz, Linex, Proffesor Jay, Izzo Biznes, Kala Jeremiah, Fid Q, Snura, Weusi, Ben Pol, Mzee Yusuph, Shilole na Mwasiti.
 
Wengine ni Nay wa Mitego, Mwana FA, Khadija Kopa, Juma Nature, Warriors From the East, Madee, Young Killer, Jambo Squad, AY, Vanessa Mdee, Mashujaa Band, Rich Mavoko na Christian Bella. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

HAWA NDIO WATU 10 TANZANIA WANAOTISHA KWA UTAJIRI


 1. SAID BAKHRESA
Jina lake kamili ni Said Salim Awadh Bakhresa. Jarida la Forbes mwaka jana, lilimuorodhesha miongoni mwa matajiri 40 Afrika kwamba anamiliki utajiri wenye thamani ya dola milioni 620 (karibu shilingi trilioni moja). 
Hata hivyo, inadaiwa kuwa tabia ya usiri wa Bakhresa inafanya mali zake zisijulikane sana, ila ni tajiri zaidi ya kiwango hicho.

Ndiye mmiliki wa makampuni ya Bakhresa yanayotoa bidhaa zenye chapa ya Azam ambazo zinauzwa nchi mbalimbali Afrika. Ana viwanda vya nafaka na vinywaji, vyombo vya usafiri wa majini, uuzaji wa chakula, bidhaa za plastiki na kadhalika. Ndiye mmiliki wa Klabu ya Azam FC.

2. GULAM DEWJI

Huyu ni baba wa mfanyabiashara maarufu nchini, Mohamed Dewji ‘Mo’. Jarida la Forbes mwaka jana lilimtaja kuwa na utajiri wenye thamani ya dola milioni 560 (karibu shilingi bilioni 900). Mafanikio yake kibiashara yalianza mwaka 1970. Kiwanda chake cha 21st Century Textiles, kinatajwa kuwa moja ya viwanda vikubwa vya nguo Afrika. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
3. ROSTAM AZIZ
Inadaiwa anamiliki utajiri wenye thamani ya dola milioni 420 (shilingi bilioni 672). Anamiliki karibu asilimia 40 ya hisa Kampuni ya Vodacom Tanzania. Ni mmiliki wa Kampuni ya Caspian inayohusika na uchimbaji wa madini na ukandarasi nchini Tanzania, nchi kadhaa za Afrika na Asia.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO MEI 14, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

FERDINAND KUONDOKA OLD TRAFFORD

Mlinzi wa Manchester United Rio Ferdinand amesema ataondoka Old trafford msimu ujao baada ya klabu hiyo kukataa kumuongezea muda kwenye kandarasi yake.
Kauli hiyo inamaanisha Ferdinand ambaye amefunga mabao nane Old Trafford katika miaka 12 na kushiriki katika mechi 454 ataingia katika orodha ndefu ya wachezaji wakongwe mabalozi wa klabu hiyo.
Mwandishi wa BBC anasema kuwa mlinzi huyo anapania kuendelea kucheza lakini haijulikani ataichezea klabu ipi.
pics Rio
Ferdinand kuhama Old Trafford.
Ferdinand alisema katika barua ya wazi kwa klabu hiyo kuwa angelipenda kuwaaaga mashabiki wake kwa njia bora zaidi lakini kutokana na ati ati hangeweza .
Hata hivyo amesema kuwa amefikiria sana kuhusu hatima yake na umewadia wakati wake kuwaaga.
Ferdinand aliwasili United Agosti 2002 kutokea klabu ya Leeds timu hiyo ilipokuwaikikabiliana na Hungary Zalaegerszeg katika mechi ya ligi ya mabingwa barani Ulaya.
Ameshinda mataji 6 ya ligi kuu ya premia mbali na mataji mawili ya nyumbani .
Manchester Utd pia ilishinda taji la klabu bingwa duniani mbali na taji la mabingwa barani Uropa. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Chanzo: BBCswahili

WACHIMBA MADINI 200 WAFARIKI UTURUKI

157 wameaga dunia katika mkasa wa moto ndani ya mgodi
Mlipuko katika mgodi wa makaa ya mawe magharibi mwa Uturuki umesababisha vifo vya zaidi ya wachimbaji migodi 200 na kujeruhi wengine wengi kujeruhiwa kwa mujibu wa maafisa nchini humo.
Waziri wa kawi, Taner Yildiz, amesema kuwa zaidi ya wafanyikazi 780 walikuwa katika mgodi huo pale kuliposikika mlipuko katika kitengo cha kusambazia umeme.
Waokoaji wanajaribu kila mbinu kuwafikia mamia ya wachimba migodi.
Inahofiwa kuwa wachimbaji mgodi wengine wengi bado wamefukiwa chini ya mgodi huo.
Inakadiriwa kuwa wakati mlipuko huo ulipotokea wafanyikazi 780 walikuwa ndani ya mgodi huo japo inaaminika wengi waliweza kukimbilia usalama wao .
Bado idadi ya walionaswa ndani ya mgodi huo haijabainika.
Mgodi huo uko katika mji wa Soma, mkoani Manisa , takriban kilomita 250 kusini mwa Istanbul. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
157 wameaga dunia katika mkasa wa moto ndani ya mgodi
Jamaa za wachimbaji migodi hao wamekusanyika katika makundi karibu na mgodi huo ambao unamilikiwa na wawekezaji wa kibinafsi huku wengi wao wakilia hadharani na kububujikwa na machozi.
Waziri wa nishati Taner Yildiz ameimabia televisheni ya Uturuki kuwa huenda wengi wamekufa kutokana na sumu ya gesi aina ya carbon monoxide.
Amesema moto huo umesababishwa na hitilafu ya umeme.
Picha za televisheni zinaonyesha maafisa wa uokoaji wakiokoa wafanyikazi wa mgodi huo, huku nyuso zao zao zikiwa zimejaa vumbi.
Baadhi yao wanaweza kutembea na wengine wanabebwa na kupelekwa ndani ya magari ya kubebea wagonjwa yaliyoegezwa karibu na eneo la tukio. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Tuesday, May 13, 2014

TAZAMA VIDEO YA JAY Z AKIPIGWA NA SHEMEJI YAKE MBELE YA MKEWE BEYONCE

Screen Shot 2014-05-12 at 11.40.31 PM 
Ni video kamili ikionyesha kilichotokea kwenye lifti ambapo rapper Jay Z anaonekana akipigwa na shemeji yake ambae ni Solange kwa muda usiopungua dakika 2 kwa kutumia pochi na mateke na baada ya hapo wakatoka nje ya lift.
Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, haya yalitokea wiki iliyopita kwenye After Party ya Met Gala ndani ya Standard Hotel, NYC na ndani ya video inaonesha Jay Z, Beyonce na Solange wakiingia katika Lifti halafu Solange anaanza kumuwakia Jay z kabla ya kuanza kumvamia wakati huo Beyonce akiwa pembeni tu ametulia na wala haingilii.

Bodyguard aliekuemo katika lifti hiyo alianza kumzuia Solange lakini alifanikiwa kuponyoka kama mara tatu hivi na kuendelea kumpiga Jay Z pia kuna muda Solange alirusha teke na Jay Z akazuia lakini hakurudisha kwa aina yeyote ile, sio kwamba alishindwa kumpiga ili alifanya maamuzi ya kuwa mstaarabu tu. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAREKANI KUTAFUTA MATEKA NIGERIA

Marekani kusaidia kuwasaka wasichana waliotekwa na Boko Haram
Marekani imesema inapeleka vifaa vya uchunguzi nchini Nigeria kusaidia katika juhudi za kuwatafuta wasichana wanaozuiliwa na kundi la Boko Haram.
Wasichana hao walitekwa nyara kutoka shule moja Kusini mwa eneo la Borno mwezi mmoja uliopita.
Msemaji wa Rais Obama Jay Carney amesema kikosi cha maafisa 30 kiko nchini Nigeria tayari kushiriki juhudi hizo.
Amesema msaada huo wa Marekani kutoka wizara za mambo ya nje na ulinzi na pia kutoka idara ya uchunguzi ya FBI. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Hatua hiyo imechukuliwa wakati baadhi ya Jamaa za wasichana waliotekwa nyara wakielezea majonzi baada ya kutazama kanda ya video iliyotolewa na kundi hilo.
Marekani kusaidia kuwasaka wasichana waliotekwa na Boko Haram
Baadhi wameiambia BBC kuwa kanda hiyo imewapa matumaini lakini wameshangaa kuona wasichana hao ambao wengi ni Wakristu wamevalia mavazi ya Kiislam.

Akizungumza kwa uchungu nduguye mmoja wa wasicha waliotekwa ameiambia BBC ni heri kanda hiyo ingeonyesha maiti za wasichana hao kwa kuwa hiyo ingeondoa wasiwasi unaoendelea kukithiri na kuumiza mioyo ya wengi.
Kwenye kanda hiyo ya video kiongozi wa Boko Haram , Abubakar Shekau anasikika akiambia serikali ya Nigeria yuko tayari kubadilishana baadhi ya wasichana hao na wafuasi wake waliofungwa jela.
Hatahivyo wizara ya mambo ya ndani ya Nigeria imetupilia mbali pendekezo hilo.
Seneta Ali Ndume kutoka eneo ambapo wasichana hao walitekwa nyara anaisihi serikali kulegeza msimamo. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Chanzo: BBC

MAGAZETI YA LEO JUMANNE MEI 13, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

mg 2
mg 1
13 
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

TAARIFA YA WIZARA YA AFYA KUHUSU UGONJWA WA HOMA YA DENGUE


mg1
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid na Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii,Charles Pallangyo.
Utangulizi
Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii inapenda kutoa taarifa kwa Umma juu ya mwenendo wa ugonjwa wa homa ya dengue yaani “dengue fever” hapa nchini.Ugonjwa huu umethibitishwabaada ya sampuli zilizochukuliwa kutoka kwa watu waliohisiwa kuwa na ugonjwa huu jijini Dar es Salaam kupelekwa kwenye maabara yetu ya Taifa Dar es salaam na kuthibitisha kuwa na virusi vya homa ya dengue mnamo mwishoni mwa mwezi wa Januari 2014. Hadi sasa idadi ya wagonjwa ambao wamethibishwa kuwa na ugonjwa huuni 400 na Vifo 3. Kwa wiki iliyoshia tarehe 9 Mei 2014 ya idadi ya wagonjwa waliogundulika mkoani Dar es salaam ni 60 (42-Kinondoni, 14-Temeke na 4-Ilala) na idadi ya wagonjwa waliopo wodini mpaka sasa ni 13.
Aidha, mlipuko wa ugonjwa huu si mpya hapa nchini kwani uligundulika kwa
mara ya kwanza mnamo Juni 2010 mkoani Dar es Salaam ambapo idadi ya watu 40 walithibitika kuwa na ugonjwa. Pia, kati ya mwezi Mei hadi Julai 2013,wagonjwa 172 walithibitishwa kuugua ugonjwa huu.
Homa ya Dengue
Homa ya dengue ni ugonjwa unaosababishwa na kirusi ambacho kinaenezwa na mbu wa aina ya Aedes.
Dengue in ugonjwa uliosambaa duniani katika nchi za ukanda wa joto. Takribani asilimia 40 ya watu wote duniani wanaishi katika nchi zenye ugonjwa huu. Takwimu za Shirika la Afya Duniani zinathibitisha kuwa takribani matukio milioni 5 ya Dengue yanatolewa taarifa kila mwaka. Watu laki 5 hulazwa hospitali kwa kuathirika na Dengue kali. Homa ya Dengue imeshatokea katika nchi zipatazo 34 barani Afrika.
Hapa Afrika Dengue ni ugonjwa unaojulikana kwa kiwango kidogo sana. Licha ya kwamba milipuko ya kwanza imetokea tangu mwanzoni wa karne ya 19. Matukio ya Ugonjwa huu yameongezeka Afrika tangu miaka ya 1980, matukio mengi yakitokea nchi za ukanda wa Mashariki mwa Afrika ikiwa ni pamoja na Msumbiji, Somalia, Kenya, Komoro, Djibouti na Tanzania. Ikumbukwe kuwa jina “Dengue” linatokana na neno “Dinga” la kiswahili linalolomaanisha ugonjwa unaotakana na pepo yaani Kudinga pepo. Mabaharia wa Kispanish walipokuja kwenye pwani ya Afrika Mashariki walirudi kwao na kuuita “Dengue”.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...