Wednesday, May 07, 2014

MAHABUSU ARUSHA WAVUA NGUO KUPINGA UBAGUZI


Ramani ya Tanzania
Mahabusu wa Gereza Kuu la Mkoa wa Arusha, jana walisababisha vurugu katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi mjini humo baada ya kuvua nguo na kugoma kushuka kwenye basi lililowachukua kwenda mahakamani wakipinga kitendo cha watuhumiwa wawili wa dawa za kulevya kuachiwa huru.
Watuhumiwa wanaolalamikiwa ambao mashtaka yao yalibadilishwa mara mbili ili wapewe dhamana ni Dharam Patel na Nivan Patel wanaodaiwa kukamatwa na kete 173 za heroini na misokoto 300 ya bangi, Aprili,2014.
Kwa mujibu wa watu waliokuwa katika eneo la mahakama hayo, mahabusu hao walikuwa wakipaza sauti kupinga madaraja(ubaguzi) miongoni mwa watuhumiwa, wenye uwezo kifedha na wasio nacho, hali ambayo imesababisha wengine kuachiwa na wengine kuendelea kusota magerezani kwa kisingizio cha "upelelezi haujakamilika"
Mahabusu hao walisikika wakipaza sauti kutoka ndani ya basi: "Wenzetu hata mwezi haujaisha wanafutiwa kesi, jamani sisi tumekosa nini? Tunataka haki itendeke kwa wote" walisema.
Kuachiwa kwa watuhumiwa wanaolalamikiwa na mahabusu wenzao kunasemekana kumetokana na hatua ya Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Arusha kubadilisha hati ya mashitaka na hivyo kuwawezesha kupata dhamana.
Kamanda wa Kikosi cha Polisi cha Kuzuia Dawa za Kulevya, Godfrey Nzowa ameliambia gazeti la Mwananchi kuwa ofisi yake haina taarifa za watuhumiwa hao kupewa dhamana lakini alisema kulikuwa na jaribio la kufanya hivyo.
Bwana Nzowa amesema baada ya kubainika njama hizo, ofisi yake ilipinga, akisema kuwa kosa la watuhumiwa lilikuwa wazi na hivyo kuonyesha hali ya kutoamini kuwa watuhumiwa wanaweza kupata dhamana kwa kosa hilo!
Hata hivyo Ofisi ya Mwendesha Mashitaka, DPP haijaweza kulitolea maelezo suala la mahabusu hao kulalamikia mahabusu wenzao kupendelewa katika utoaji wa haki kwa makosa wanayotuhumiwa.
Chanzo BBC 
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Monday, May 05, 2014

LUIS SUAREZ KAFNYA YAKE TENA

Screen Shot 2014-05-05 at 3.48.52 PM 
Wiki mbili baada ya kutangazwa kuwa mchezaji bora wa ligi kuu ya England kupitia chama cha wanasoka wanaocheza EPL mshambuliaji wa kimataifa wa Uruguay Luis Suarez ambae ni miongoni mwa mastaa wa soka waliowahi kumiliki headlines kwa kipindi kirefu, amechaguliwa tena kuwa mwanasoka bora wa England na chama cha waandishi wa habari za michezo Uingereza.
Suarez mwenye umri wa miaka 27 aliwashinda kwa kura nyingi wachezaji wengine akiwemo nahodha wa Liverpool na England Steven Gerrard.
article-2620532-1D69BE9B00000578-539_306x423 
Magoli 30 aliyofunga msimu huu kwenye EPL yameiweka Liverpool kwenye nafasi ya kutwaa ubingwa wa Premier League baada ya miaka 24.  Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Hii ndio listi ya washindi wa tuzo hiyo tangu mwaka 1990 mpaka leo
1989–90     John Barnes          
1990–91     Gordon Strachan
1991–92     Gary Lineker
1992–93     Chris Waddle
1993–94     Alan Shearer
1994–95     Jurgen Klinsmann
1995–96     Eric Cantona
1996–97     Gianfranco Zola
1997–98     Dennis Bergkamp
1998–99     David Ginola
1999–00     Roy Keane
2000–01     Teddy Sheringham
2001–02     Robert Pires
2002–03     Thierry Henry
2003–04     Thierry Henry
2004–05     Frank Lampard
2005–06     Thierry Henry
2006–07     Cristiano Ronaldo
2007–08     Cristiano Ronaldo
2008–09     Steven Gerrard
2009–10     Wayne Rooney
2010–11     Scott Parker
2011–12     Robin van Persie
2012–13     Gareth Bale

MAGAZETI YA LEO JUMATATU MEI 05, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAPIGANO MAKALI YAANZA TENA SUDAN KUSINI

Wanajeshi wa Sudan Kusini
Mapigano makali yamekuwa yakiendelea katika mji wa Bentiu nchini Sudan Kusini ambapo vikosi vya serikali vinajaribu kuurejesha mji huo uliotekwa na waasi.
Mwandishi wa Habari wa BBC aliyeandamana na kikosi cha Umoja wa Mataifa nje ya mji huo anasema amesikia milio ya bunduki na silaha nzito nzito ambapo pia ameona kikosi cha majeshi ya serikali kikijipanga.
Hata hivyo amesema bado haijajulikana ni kundi gani kwa sasa linaloshikilia mji huo wa wenye utajiri wa mafuta.
Kwa upande serikali nchini Sudan kusini inasema majeshi yake yameudhibiti mji wa huo na ngome ya waasi ya Nasir.
Baadhi ya wakimbizi wa Sudan Kusini waliokimbia makazi yao hivi karibuni kutokana na vita
Mjumbe wa Umoja wa mataifa mjini humo anasema mji huo umedhibitiwa upya na kikosi cha serikali katika operesheni kubwa iliyoanza hapo jana Jumapili.
Shambulio hilo linajiri siku mbili baada ya rais Salva Kiir kumwambia Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani John Kerry, kwamba yupo tayari kufanya mazungumzo ya amani ya moja kwa moja na kiongozi wa waasi, Riek Machar. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Chanzo BBC

HUKUMU YA WANAJESHI WABAKAJI DRC LEO

Wanajeshi wa serikali ya DRC
Hukumu inatarajiwa kutolewa baadaye leo kwenye kesi inayowahusu wanajeshi 39 wanaotuhumiwa kuendesha ubakaji na uhalifu wa kivita nchini Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo.
Wanajeshi hao wanatuhumiwa kusababisha machafuko yanayoendelea kwenye mji mdogo wa Minova ulio mashariki mwa nchi hiyo mwaka 2012.
Waasi wa M23 ambao wanadaiwa nao kujihusisha na vitendo vya ubakaji
Wakati wa machafuko hayo maelfu ya wajeshi wa serikali walikuwa wakirudi nyuma baada ya kupoteza mji wa Goma kwa waasi wa M23 .
Ripoti ya Umoja wa Mataifa inasema kuwa wanajeshi hao waliwabaka karibu wanawake na wasichana 135.
Matukio ya ubakaji yameenea katika eneo la mashariki mwa Congo na yanaidiwa kufanywa na askari wa pande zote mbili waasi na wale serikali. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Sunday, May 04, 2014

DIAMOND AIBUKA KIDEDEA KWA KUNYAKUA TUZO SABA (7) ZA KTMA 2014

Msanii wa kizazi kipya, Nasib Abdul a.k.a Diamond Platinumz leo May 3, 2014 amedhihirisha kuwa yeye ni msanii mkali kwa kuchukua tuzo saba katika Tuzo za Kilimanjaro 2014 (KTMA).
Diamond amejinyakulia tuzo:
Msanii Bora wa Kiume,
Video Bora ya Mwaka.
Mtumbuizaji bora wa Muziki wa Kiume.
Wimbo Bora wa Afro Pop.
Wimbo Bora wa Mwaka.
Mtunzi Bora wa mwaka Kizazi Kipya.
Wimbo Bora wa Kushirikisha/Kushirikiana.
Hakika Diamond ameonyesha ukali wake, na kuonyesha kuwa yeye ni bora zaidi na anapendwa na watu.  Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

TAZAMA PICHA 40 ZA MATUKIO YALIYOJILI KWENYE TUZO ZA KTMA 2014 USIKU WA KUAMKIA LEO, DIAMOND AVUNJA REKODI

Wanamuziki Ommy Dimpoz na Vanessa Mdee wakifanya vitu vyao stejini. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

BOMU LAUA WATU WATATU MOMBASA

Moja kati ya milipuko iliyowahi kutokea Mombasa
Watu watatu wanaripotiwa kuuawa katika mlipuko uliotokea katika mji wa Mombasa nchini Kenya.
Kwa mujibu wa taarifa bomu la mkono lilitupwa kwenye basi katika kituo cha mabasi cha Mwembe Tayari ambao hupendwa kutembelewa na watalii na kusababisha vifo hivyo na wengine kujeruhiwa.
Mlipuko mwingine umetokea katika mtaa wa kifahari wa Nyali.
Kamishna mkuu wa polisi Mombasa, Nelson Marwa, amesema watu 6 wamejeruhiwa na kuwa watu waliotekeleza shambulizi hilo walitoroka kwa Pikipiki.
Kenya imekuwa ikikumbwa na matukio ya mashambulio yanayodaiwa kutekelezwa na kundi la kiislamu la Alshabaab la nchini Somalia.
Aidha nchi hiyo imekuwa katika tahadhari tangu mwezi Septemba mwaka jana ambapo wanamgambo wa Alshabaab walivamia kituo cha biashara cha Westgate kilichopo mji mkuu wa Nairobi na kuua watu wapatao 67.
Al Shabaab ni kundi ambalo lina uhusiano na kundi la kigaidi la Al Qaeda ambalo limeapa kulipiza kisasi kufuatia Kenya kutuma majeshi yake nchini Somalia mwaka 2011ambayo yameungana na yale ya Umoja wa Afrika AMISOM. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Chanzo BBC

WATU 2000 WAFUKIWA KWA UDONGO AFGHANISTAN


Juhudi za uokoji zinaendelea siku ya pili Kaskazini mashariki mwa Afghanistan ambapo watu wapatao elfu mbili wanasadikiwa kufa kutokana na maporomoko ya ardhi katika maeneo ya vijiji kwenye mkoa wa Badakhshan.
Vijiji hivyo vimefunikwa na udongo wenye ukubwa wa karibu mita kumi kwenda juu baada ya sehem ya mlima mmoja kuporomoja kutokana na mvua kubwa zinazonyesha. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI MEI 04, 2014 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.

.

Saturday, May 03, 2014

MWENGE WA UHURU WAWASHWA RASMI JANA MKOANI KAGERA,TAYARI KUKIMBIZWA KATIKA WILAYA 127

 Makamu wa Rais wa, Dk. Mohammed Gharib Bilal, akiwasha Mwenge wa Uhuru wakati wa Sherehe za uzinduzi wa mbio za Mwenge huo zilizofanyika kwenye Uwanja wa Kaitaba, mjini Bukoba Mkoa wa Kagera leo. Mwenge huo unatarajia kuitimisha mbio zake Oktoba 14 mkoani Tabora, ambapo zinatarajia kufungwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Kikwete.
Makamu wa Rais, Dk. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Mwenge wa Uhuru, Kiongozi wa mbio za Mwenge Taifa, Rachel Kasanda, baada ya kuuwasha rasmi wakati wa Sherehe za uzinduzi wa mbio za Mwenge huo zilizofanyika kwenye Uwanja wa Kaitaba, mjini Bukoba Mkoa wa Kagera jana. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

ABSALOM KIBANDA AFUNGUKA NDANI YAMAANDIMISHO YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI DUNIANI

DSC_0017
Baadhi ya waandishi wa habari na wadau kutoka asasi mbalimbali nchini wakifanya usajili kwenye kongamano la siku moja lilioandiliwa kuadhimisha Uhuru wa vyombo vya Habari Duniani 2014 lililofanyika jijini Arusha.
Na Waandishi Wetu, Arusha
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF), Absalom Kibanda ametoa wito kwa waandishi wa habari nchini kuyapa uzito matukio yanayowatokea waandishi wa habari na kuyapigia kelele kwa nguvu zote ili kuyakomesha.
Kibanda aliyasema hayo jana mjini Arusha katika kongamano lililoandaliwa kama sehemu ya maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani na kuongeza kwamba wakati umefika kwa waandishi wa habari kuondoa tofauti zao na kuungana pamoja kuongeza nguvu waliyonayo kukabiliana na ukatili unaoendelea dhidi ya waandishi wa habari katika miaka ya hivi karibuni.
“Baadhi ya wahariri huwa hawayaandiki madhila yanayowasibu waandishi wa habari na kuyapa uzito unaostahili aidha kwa huyapuuzia au kudharau kwa kuwa hayawahusu moja kwa moja,” alisema Kibanda.
Aliongeza kwa kusema kuwa vyombo vya habari mara nyingi vimekuwa vikinyooshewa vidole na kulaumiwa kwa kutokufanya kazi kwa uadilifu jambo ambalo linatafsiriwa kuwa ni la uonevu, vinatumiwa vibaya na hakuna anayesimama kuvitetea kutokana na mchango wake mkubwa katika jamii. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI MEI 03, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

POLISI NIGERIA WAOMBA PICHA ZA WANAFUNZI


Waandamanaji nchini Nigeria wakidai wasichana waliotekwa katika mji wa Chibok, Borno warejeshwe
Polisi nchini Nigeria wamewataka wazazi wa wanafunzi wasichana zaidi ya 200 waliotekwa kuwasilisha picha za mabinti hao.
Wasichana hao walichukuliwa na watu wanaoshukiwa kuwa wanamgambo wa Kiislam kutoka shuleni kwao katika jimbo la Borno zaidi ya wiki mbili zilizopita.
Polisi wa jimbo la Borno wameiambia BBC kuwa serikali inataka kuthibitisha bayana ni nani ambaye ametoweka kwa sababu vitabu vya kumbukumbu vya shule vilichomwa moto katika shambulio hilo.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

WATU 30 WAFA KWA MOTO VITANI UKRAINE


Majeshi ya Ukraine pamoja na vifaru kuelekea kwenye mapambano
Polisi wa Ukraine wanasema kuwa zaidi watu 30 wameuawa katika moto ulioanza baada ya makabiliano kati ya vikosi vya wanamgambo wanaounga mkono Urusi na wafuasi wa serikali katika mji wa kusini magharibi wa Odessa.
Haijulikani ni nini kilichosababisha moto huo katika jengo la chama cha wafanyikazi ,huku ripoti zikiarifu kwamba pande zote mbili zilikuwa zikitumia mabomu ya petroli.
"Waziri wa mpito wa Mambo ya Ndani nchini Ukraine Arsen Avakov amesema kuwa harakati za serikali kudhibiti mji wa mashariki wa Sloviansk uliopo mashriki mwa Ukraine zinaendelea na kwamba vikosi vyake vimeliteka jengo la Televisheni karibu na Kromartosk.Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Friday, May 02, 2014

JK: MISHAHARA ITAPANDA NA KUPUNGUZWA KODI


Rais Jakaya Kikwete akiangua kicheko wakati walimu (juu), walipokuwa wakipita kwa maandamano, huku wakiimba ‘Shemeji mshahara bado’ wakati wa sherehe za Siku ya Wafanyakazi (Mei Mosi) zilizofanyika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam jana. Walimu walimwita shemeji kwa kuwa mkewe, Salma ni mwalimu kitaaluma. Picha na Silvan Kiwale. 
Dar/mikoani. Rais Jakaya Kikwete ametoa ahadi mbili za kuwafurahisha wafanyakazi. Kwanza ametangaza nia ya kuongeza mishahara yao na pili, kupunguza kodi inayokatwa kwenye mishahara hiyo mambo ambayo ameahidi kutekelezwa katika Bajeti ya mwaka 2014/2015 inayotarajiwa kuwasilishwa bungeni hivi karibuni.
Akizungumza kwenye maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi (Mei Mosi), yaliyofanyika kitaifa Dar es Salaam jana, Rais Kikwete alisema anatambua kuwa wafanyakazi wana hamu ya kujua Serikali itasema nini kuhusu masilahi yao.
Alisema malalamiko ya wafanyakazi wengi ni kutaka kuona kima cha chini cha mshahara kinaongezwa huku kodi kwenye mishahara (Paye), ikipungua.
“Mimi na wenzangu serikalini hatuna upungufu wa dhamira ya kufanya hivyo, tumethibitisha miaka iliyopita na tutaendelea kuwa hivyo,” alisema. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Huku akishangiliwa na wafanyakazi waliofurika katika Uwanja wa Uhuru, Rais Kikwete alisema: “Najua kuwa nyongeza tuliyotoa mwaka jana si kubwa kama wafanyakazi walivyotaka iwe... hata mimi nisingependa iwe hivyo.”

HII NDIO TAARIFA RASMI YA YANGA KUHUSU USAJILI WA DOMAYO NA KAVUMBAGU

Didier-Kavumbagu-na-Frank-Domayo-wakisaini-kuichezea-klabu-ya-Azam-FCUongozi wa klabu ya Young Africans unapenda kuwajulisha wanachama wake, wapenzi wa soka na wadau kwa ujumla kuwa taarifa za kuhama kwa wachezai wake Didier Kavumbagu na Frank Domayo kwenda kujiunga na Azam FC zisiwakatishe tamaa, ni mapenzi ya wachezaj wenyewe kwani walishakubaliana na uongozi kila kitu juu ya kuendelea kuitumikia Yanga kabla ya siku mbili hizi kuonekana wakiwa wamejiunga na wana ramba ramba.
Yanga tayari ina wachezaji watatu wenye mikataba inayoendelea na kama kanuni za VPL kwa wachezai wa kimataifa kuwa watatu zitatumika wachezaji Haruna Niyonzima, Hamisi Kizza na Emmanuel Okwi ndio watakaoendelea, hivyo uongozi uliomba mwongozo kwa TFF juu ya taratibu zitakazotumika kwa msimu ujao kabla ya kuwasainisha Kavumbagu na Twite.
Awali uongozi wa Yanga ulikuwa kwenye mazungumzo na wachezaji hao tangu mwanzoni mwa msimu wa 2013/2014 juu ya kuongezewa muda wa mikataba yao ili waweze kuendelea kuitumika Yanga kwa ajili msimu mpya ujao 2014/2015.
Didier Kavumbagu na Mbuyu Twite ambao mikataba yao ilikuwa mwishoni waliongea na uongozi tangu mapema mwaka jana mwezi wa Septemba juu ya kuweka sahihi zao na kuendelea kuitumikia Yanga na kukubaliana mambo yote ya msingi kikubwa kilichokuwa kinasubiriwa ni maamuzi ya TFF juu ya usajili wa wachezaji wa kigeni msimu mpya wa 2014/2015 kwani Azimio la Bagamoyo linapaswa kuanza kutekelezwa msimu huu. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MEI 02, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

HAMAD RASHID KUGOMBEA URAIS 2015

Hamad_Rashid6_3bea3.jpg
Mbunge wa Wawi (CUF), Hamad Rashid Mohamed amesema anapanga kujitosa kwenye kinyang’anyiro cha urais katika Uchaguzi Mkuu mwakani.
Akizungumza katika mahojiano maalumu hivi karibuni mjini Dodoma, Hamad Rashid alisema: “Kama Mwenyezi Mungu akinijalia uhai na uzima mwakani, ninatarajia kuingia kwenye kinyang’anyiro cha urais ama wa Muungano au wa Zanzibar.

“Ila sijaamua kama ni Bara au Zanzibar; kama ni chama cha CUF au kingine, hayo yote yatakuja baadaye,” alisema Hamad Rashid.
Mohamed ambaye ana mgogoro mahakamani na chama chake cha CUF, ametoa kauli hiyo wakati tayari viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), CUF kikiwamo wanajipanga kusimamisha mgombea mmoja wa urais katika uchaguzi ujao.
Mbali na CUF, vyama vingine vinavyounda Ukawa ni NCCR-Mageuzi na Chadema ambavyo pia vinakusudia kusimamisha mgombea mmoja kwa nafasi za ubunge na udiwani, lengo likiwa kukabiliana na nguvu ya chama tawala, CCM.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

WATU 19 WAUAWA KATIKA MLIPUKO NIGERIA

Waliojeruhiwa walikimbizwa hosipitalini
Maafisa nchini Nigeria wanasema kuwa watu 19 wameuawa baada ya mlipuko kutokea katika kituo cha basi katika mji mkuu wa taifa hilo Abuja.
Kwa mujibu wa mkurugenzi wa idara ya kushughulikia mikasa na hali ya dharura- FEMA- Abbas G Idriss, watu 60 walijeruhiwa vibaya lakini sitaka kati yao wametibiwa na kuruhusiwa kwenda nyumbani. Amesema kuwa magari sita yameharibiwa katika mlipuko huo.
Mlipuko huo umetokea katika eneo la Nyanya, karibu na kituo cha basi ambako zaidi ya watu sabini waliuwawa katika shambulizi la tarehe14 mwezi Aprili.
Ripoti za awali zimesema kuwa watu kadhaa wameuwawa na wengine wengi kujeruhiwa.
Waandishi wanasema kuwa mlipuko huo umesababishwa na bomu lililotegwa ndani ya gari. Mmoja wa walioshuhudia kisa hicho amesema aliona miili 20 ya watu waliouwawa. Hakuna kundi lililodai kuhusika katika shambulizi hilo lakini kundi la wanamgambo wa kiislamu la Boko Haram limewahi kutekeleza mashambulizi kama hayo mjini Abuja
Mengi ya mashambulizi ya Boko Haram yamekuwa yakitokea katika maeneo ya kaskazini mashariki mwa Nigeria.
Lakini shambulizi la bomu la tarehe 14 Aprili lilizua hofu kwamba huenda wanamgambo hao wameanza kupanua maeneo wanayoendeleza harakati zao. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...