Sunday, November 17, 2013

HASSAN DILUNGA ATUA YANGA

dilunga a6713
SAA chache baada ya kufunguliwa kwa Dirisha Dogo la Usajili kwa msimu wa 2013/14, vinara wa Ligi Kuu ya Vodacom, Yanga jana walifanikiwa kumsajili kwa mkataba wa miaka mitatu kiungo Hassan Dilunga kutoka Ruvu Shooting ya Pwani.

Kwa mujibu wa kanuni, klabu za Ligi Kuu na Daraja la Kwanza zenye fursa ya kusajili wachezaji katika dirisha dogo ni zile ambazo hazijatumia nafasi zote 30 za wachezaji, usajili uliofunguliwa jana Novemba 15 na kutarajiwa kufungwa Desemba 15.

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili wa klabu ya Yanga, Abdallah Bin Kleb, alisema jana kwamba usajili wa kiungo huyo ni utekelezaji wa maagizo ya Kocha Mkuu, Ernie Brandts, aliyoyaacha na benchi lake la ufundi kwa ajili ya kuboresha kikosi.

"Kocha aliacha mapendekezo ya usajili tuyafanyie kazi, la kwanza lilikuwa ni kuhakikisha tunampata Kaseja ili kuongeza nguvu miongoni mwa makipa, ambao tuliukamilisha mwishoni mwa wiki na sasa tumelimaliza la kiungo Hassan Dilunga," alisema Bin Kleb na kuongeza.

Kikubwa kuhakikisha kuwa, tunatekeleza maagizo yote yaliyo katika ripoti ya benchi la ufundi na kuyafanyia kazi ili kujiweka katika mazingira mazuri ya kuboresha kikosi chetu kwa ajili ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu na michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Usajili wa Dilunga kiungo aliyeteuliwa kikosi cha timu ya taifa, 'Taifa Stars', inayojiandaa kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya Harambee Stars, ametua Jangwani siku chache baada ya mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu walipomsajili mlinda mlango wa zamani wa Simba na Stars, Juma Kaseja, aliyekuwa hana timu tangu kumaliza mkataba wake na Wekundu wa Msimbazi.

MAREKANI YAIWEKA PABAYA TANZANIA, YAIITA KITOVU CHA ‘BIASHARA’ YA BINADAMU


UzaMtuClip 79203
Marekani imetoa ripoti inayozungumzia usafirishaji wa binadamu ya mwaka 2013, huku ikiitaja Tanzania kuwa kinara wa kunyanyasa wasichana, kuwatumikisha katika ngono na usafirishaji wa binadamu.
Ripoti hiyo iliyotolewa na idara ya nchi hiyo inayohusika na diplomasia (US Department of State, Diplomacy in Action), pia inaitaja Tanzania kuwa ni kitovu cha njia ya kusafirisha wanawake, watoto na wanaume ambao hutumikishwa kwenye kazi za mashambani na biashara ya ngono.


Ripoti hiyo iliyozinduliwa Julai mwaka huu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Seneta John Kerry inaweka bayana kwamba biashara ya usafirishaji wa binadamu hufanywa na baadhi ya ndugu na marafiki ambao hutoa ahadi kwa wahusika kwamba wanakwenda kuwasomesha au kuwatafutia ajira nzuri mijini.
"Unyonyaji wa wasichana wadogo na utumikishaji majumbani ndilo tatizo linaloongoza, ingawa kesi za watoto kusafirishwa kwa ajili ya biashara ya ngono katika mpaka wa Tanzania na Kenya zinaongezeka. Pia, wasichana wananyonywa kwenye maeneo ya utalii," inasema sehemu ya ripoti hiyo.

Saturday, November 16, 2013

KILI STARS YAPANGWA NA ZAMBIA, BURUNDI CHALLENGE 2013

9_e471e.jpg
Kikosi cha Taifa Stars amacho kinaundwa na wachezaji wengi wa Bara
Na Prince Akbar, Dar es Salaam
TANZANIA Bara maarufu kama Kilimanjaro Stars imepangwa katika Kundi B kwenye michuano ya CECAFA Challenge pamoja na Zambia, Burundi na Somalia.
Katika michuano hiyo inayotarajiwa kuanza Novemba 27 mjini Nairobi, Kenya, wenyeji Harambee Stars wamepangwa na Ethiopia, Zanzibar na Sudan Kusini katika Kundi A.
Mabingwa watetezi, Uganda wamepangwa Kundi C pamoja na Rwanda, Sudan na Eritrea. Ratiba ya michuano hiyo inatarajiwa kutolewa wiki ijayo.

MAKUNDI CHALLENGE 2013:
KUNDI A- Kenya, Ethiopia, Zanzibar, South Sudan
KUNDI B- Tanzania, Zambia, Burundi and Somalia
KUNDI C- Uganda, Rwanda, Sudan and Eritrea.

MGAO WA UMEME KUANZA LEO NCHI NZIMA

aa_29e0f.jpg
Meneja Uhusiano wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Badra Masoud akieleza kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu kuwepo kwa upungufu wa umeme kwenye gridi ya Taifa kuanzia tarehe 16 hadi 26 November, 2013 kutokana na upungufu wa gesi kutoka katika Kisiwa cha Songosongo kilichopo Wilaya ya Kilwa, Mkoa wa Lindi Unaosababishwa na Matengenezo ya Kiufundi kwenye visima vya gesi unaofanywa na Kampuni ya Pan Afrika ili kuboresha upatikanaji wa gesi ya kutosha kwenye visima hivyo.

SHIRIKA LA UMEME TANZANIA
MPR/PR/12
Shirika la Umeme Tanzania(TANESCO) linasikitika kuwajulisha wateja wake wote kwamba kutawepo na upungufu wa umeme kwenye gridi ya Taifa kuanzia tarehe 16 hadi 26 November, 2013 kutokana na upungufu wa gesi kutoka katika Kisiwa cha Songosongo kilichopo Wilaya ya Kilwa, Mkoa wa Lindi Unaosababishwa na Matengenezo ya Kiufundi kwenye visima vya gesi unaofanywa na Kampuni ya Pan Afrika.
Lengo la matengenezo hayo ni kuboresha upatikanaji wa gesi ya kutosha kwenye visima hivyo.
Kutokana na Matengozo hayo Mikoa iliyounganishwa katika gridi ya Taifaa itaathirika kwa kukosa umeme kwa baadhi ya maeneo kwa nyakati tofauti.
Uongozi unaomba radhi kwa usumbufu utakaojitokeza kwa baadhi ya maeneo yatakayokuwa yakikosa umeme.
Imetolewa na: BADRA MASOUD
MENEJA UHUSIANO

RATIBA YA SHUGHULI YA KUAGA MWILI WA DKT. SENGONDO MVUNGI LEO - JUMAMOSI NOVEMBA 16 2013

Mvungi_01_f96b1.jpg
NOVEMBA 15, 2013 – UWANJA WA NDEGE WA MWALIMU JK NYERERE
Saa 12:50 jioni
Kuwasili kwa mwili wa Marehemu – Uwanja wa Ndege wa Mwalimu JKN
KESHO, NOVEMBA 16, 2013 – VIWANJA VYA KARIMJEE
Saa 2:00 – 3:30 asubuhi
Kuwasili kwa Wageni, Wananchi na Waombolezaji
Saa 3:30 asubuhi
Kuwasili Mwili wa Marehemu
Saa 4:00 – 5:45 asubuhi
Ibada ya Misa Takatifu, Viwanja vya Karimjee
Saa 5:45 – 6:55 mchana
Salaam za Rambirambi na Neno la Shukurani
Saa 6:55 – 8:40 Mchana
Kuaga Mwili wa Marehemu
Saa 9:00 Alasiri
Msafara kupeleka mwili wa marehemu Kibamba Msakuzi
KESHO KUTWA, NOVEMBA 17, 2013 – NYUMBANI KWA MAREHEMU - KIBAMBA, MSAKUZI
Saa 2:30 – 4:30 asubuhi
Ibada ya Misa nyumbani kwa marehemu
Saa 5:00 asubuhi
Kuanza safari ya kwenda Chanjale, Kisangara Juu, Mwanga, Kilimanjaro

TATOO NA MUONEKANO MPYA WA RAY..... VYAWACHEFUA WASHABIKI WAKE

 
Huu  ni  muonekano  mpya wa  Vicent  Kigosi ambao ni moja ya maandalizi ya movie  yake  mpya ...
Ni  muonekano  ambao  kwa  kiasi  flani  umewachefua  mashabiki  wake  ambao  dakika  chache  baada  ya  picha  hizo  kuwekwa  walijimwaga  kwa  comment  ambazo hazikumuunga  mkono  kwa  asilimia  zote.



  Je nageukia bongoflava au kuna nini kinakuja?. Aliadika  Ray  kwenye  moja  ya  picha  zake.

Friday, November 15, 2013

MAGAZETI YA LEO IJUMAA NOVEMBA 15, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
..



.

LOWASSA: TULIOHUZUNIKA, TUTASHINDA PAMOJA

lowassapx a10b6
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa amesema waliofurahi na kuhuzunika naye pia watashinda pamoja naye.
Bila kufafanua kauli yake jana, Lowassa aliwaambia wakazi wa Monduli mkoani Arusha kuwa: "Kumbukeni kaulimbiu yangu wakati wa Uchaguzi Mkuu uliopita, tulifurahi pamoja, tulihuzunika pamoja na tutashinda pamoja".
Mbunge huyo wa Monduli alikuwa akizungumza kwenye mkutano wa hadhara mara baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa wodi mbili za ghorofa za wazazi katika Hospitali ya Wilaya ya Monduli.
Katika hotuba yake fupi, pia alitamba kwamba atayashinda majaribu. Hata hivyo, hakufafanua majaribu hayo... "Kuna vita kubwa, lakini ambacho naweza kusema ni kuwa nayaweza yote kwa yeye anitiaye nguvu."
Kuhusu afya yake ambayo mara kadhaa imeelezwa kuwa siyo imara, kiongozi huyo alisema kwa sasa ni nzuri na imeimarika kupita kipindi kingine chochote.

Thursday, November 14, 2013

MAGAZETI YA LEO NOVEMBA 14, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
.

LIST MPYA YA MATAJIRI 50 AFRIKA, WATANZANIA WAKO WANNE

dangote
Mtandao wa Forbes maarufu kwa kutoa taarifa kama hizi, umetoa list mpya ya matajiri 50 kutoka Africa na kuhusisha vyanzo vya pesa zao, umri wao pamoja na kiasi cha pesa wanachomiliki.
List imeongozwa na Mnigeria Aliko Dangote (kwenye picha hapo juu) na mtanzania wa kwanza ameonekana kwenye namba 27 akiwa na utajiri wa dola bilioni moja. Cheki list yote hapa.
Watanzania hawa wanne ni Rostam Aziz kwenye namba 27, Reginald Mengi namba 34, Bakhresa namba 38 na Mohammed Dewji namba 38.

1
2
3
4
5

MZEE MIAKA 80 AJIUA KISA WIVU WA MAPENZI, MKEWE ADAIWA KUTEMBEA NA MWANAYE WA MIAKA 12


Mke wa marehemu, Asha Ali (50) anayetuhumiwa kutembea na mwanaye wa miaka 12.

Stori: Gladness Mallya na Chande Abdallah
AMA kweli duniani kuna mambo! Mzee Juma Kondo (80) mkazi wa Mkuranga mkoani Pwani amejiua kwa kunywa dawa ya macho hivi karibuni kutokana na wivu wa kimapenzi, Risasi Mchanganyiko limefukunyua.


Kwa mujibu wa chanzo chetu kilichopo jirani na familia hiyo, mzee Juma na mkewe, Asha Ali (50) walikuwa na mgogoro wa muda mrefu uliotokana na mambo ya mapenzi.
Mzee huyo alikuwa akimtuhumu mkewe kutembea na mtoto wao wa mwisho ambaye ana umri wa miaka 12 (jina kapuni).
“Mpaka marehemu anachukua uamuzi wa kujiua, mgogoro mkubwa kati yao ulikuwa ni kumlalamikia mkewe kutembea na mtoto wao huyo anayesoma darasa la tano,” kimesema chanzo hicho.

Waandishi wetu walizungumza na mke wa marehemu, Asha ambaye alikiri mumewe kujiua kutokana na wivu huo wa mapenzi.
“Ndani ya ndoa yetu tulikuwa na mgogoro na mume wangu alikuwa akinituhumu kutembea na mwanangu kitu ambacho hakikuwa cha kweli, binafsi siwezi kulala na mwanangu kwa sababu mimi siyo kuku.

Mtoto wa mwisho wa marehemu mwenye umri wa miaka 12 anayesoma darasa la tano anayetuhumiwa kutembea na mama'ke.

MAELEZO MAPYA ALIYOYATOA MOHAMED MORSI JINSI ALIVYOPINDULIWA EGYPT.

Morsi 1 
Rais Mohamed Morsi aliepinduliwa madarakani nchini Misri July 2013 amesema alitekwa nyara na wanajeshi ambao ndio walimtoa kwenye madaraka ambapo kikundi cha wanasheria waliojitolea ambao hawako kwenye upande wa Morsi, wametangaza hii baada ya kukutana na Morsi gerezani.

Rais huyu aliepinduliwa anataka kulishtaki jeshi na anasema hakutakua na utulivu Misri mpaka hawa watu waliompindua watolewe na wale waliohusika na umwagaji damu za Wamisri  watakapowajibishwa.
morsi gerezani

FUTURE YOUNG TAIFA STARS YAICHAPA TAIFA STARS 1-0 ANGALIA ILIVYOKUWA


Mshambulia wa Taifa Stars, Mrisho Ngasa (kulia) akichuana na mchezaji wa Future Young Taifa Stars, Kabanda katika mchezo kirafiki uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam. (Picha na Francis Dande)
Kiungo wa Taifa Stars, Athuma Idd "Chuji" akichuana na mchezaji wa Future Young Taifa Stars,Paul Nonga.

ALIYEMUUA GWIJI LA SHERIA YA KATIBA DAKTA MVUNGI AKAMATWA DAR

kova1 e15c3
Kamanda wa Kanda Maalum Dsm, Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Polisi (ACP) Suleiman Kova.

Na Damas Makangale, Moblog
Siku moja baada ya nguli ya sheria za katiba nchini, Dakta Sengodo Mvungi kuaga dunia nchini Afrika Kusini, Jeshi la Polis Kanda Maalum Ds, linamshikilia mtuhumiwa mmoja John Ikondia Mayunga (56) kwa kosa la kushiriki kikamilifu kwenye mauaji ya mwanasheria huyo na mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Kanda Maalum Dsm, Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Polisi (ACP) Suleiman Kova amesema mtuhumiwa huyo ni mkazi wa kiwalani walipata taarifa kwa raia wema kwamba alishiriki kikamilifu kwenye tukio hilo lilosababisha kifo cha Dakta Sengodo Elibariki Mvungi.

"mnamo tarehe 12/11/2013 Polisi walipata taarifa kutoka kwa raia mwema kwamba kuna mtu ambaye amehusika na tukio la mauaji ya Dakta Mvungi na kwamba kipindi hicho mnamo saa 12 jioni mtuhumiwa alikuwa maeneo ya mtaa wa Twiga Jangwani akiwa anaangalia Televisheni," amesema Kamishina Kova. Marehemu Dakta. Sengodo Mvungi.

CCM YATOA POLE MSIBA WA DR.SENGONDO MVUNGI


 KINANA_MKUTANO_WA_SHIRIKISHO_LA_CCM_VYUO_VIKUU_MORO_PIX_NO_2_529d1.jpg
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Abdulrahaman Kinana amesikitishwa na taarifa ya kifo Cha Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Dr Sengondo Mvungi kilichotokea Jana katika Hospitali ya Millpark nchini Afrika ya Kusini.

Kwa niaba ya Chama Cha Mapinduzi, Katibu Mkuu anawapa pole wanafamilia, Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Warioba na Uongozi wa Chama Cha NCCR-Mageuzi. Hakika Taifa limepoteza Mtaalamu wa Sheria, Kiongozi Mzalendo na hodari katika kipindi ambacho mawazo yake yanahitajika kwa kiasi kikubwa kuliendeleza Taifa hili.
Mwenyezi Mungu aiweke roho ya marehemu mahali pema peponi.

Imetolewa na:
KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA
ITIKADI NA UENEZI
13/11/2013
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.
Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) umepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha mjumbe wa tume ya mabadiliko ya katiba Dr Sedondo Mvungi ambacho kimetokea katika hospitali ya Millpark nchini Afrika kusini.

Uongozi wa UVCCM Taifa unatoa pole kwa familia na ndugu wa marehemu, pia UVCCM inatoa pole kwa uongozi wa NCCR- Mageuzi na kwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji Warioba pamoja na Vijana nchini kote ambao wamenufaika na Utaalamu na mafunzo. 
Kama vijana tulihitaji sana mchango wa mawazo, hekima na utaalamu kutoka kwake, hakika tumepoteza kiongozi shupavu, muadilifu na mzalendo ambae ni mfano wa kuigwa kwa Vijana wa Taifa hili.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...