Saturday, November 09, 2013

MWISHO WA UTEJA WA MIAKA 10 WA ARSENAL KWA MAN UNITED UMEWADIA?

article-2492557-1949D60F00000578-262_634x452_377d1.jpg
ILIKUWA Novemba 28, mwaka 2011, Arsenal ilipoondoka imetota vibaya Uwanja wa Old Trafford ikitandikwa mabao 8-2, siku ambayo Wayne Rooney alifunga Hat-trick na Ashley Young akafunga mawili. Danny Welbeck pia alifunga.
Kwa kiasi kikubwa Arsenal imekuwa ikinyanyaswa na Mashetani hao Wekundu, wakiwa wameweza kushinda mechi moja tu ndani ya misimu 10 na wao wakifungwa mechi 11.
Man United 2-1 Arsenal, Ligi Kuu Novemba 3, 2012
Van Persie alihitaji dakika tu kuwakumbusha mashabiki wa Arsenal kipi watakosa kwa kuuzwa kwake kwa Pauni Milioni 24 kwenda Old Trafford, akifunga bao la kwanza kwa guu la kulia. Patrice Evra akaifungia la pili United baada ya mapumziko na Santi Cazorla akaipatia bao la kufutia machozi Arsenal. Kipigo hicho kiliwaacha Arsenal na pointi 15 baada ya mechi 10, mwanzo mbaya zaidi katika historia yao kwenye Ligi Kuu ya England chini ya Wenger.
Man United 8-2 Arsenal, Ligi Kuu Novemba 28, 2011
article-2492557-0D9C44C500000578-470_634x401_176d4.jpg
.

SIMBA YAWEKA WAZI USAJILI MPYA

julio_31d1c.jpg
SIMBA imepanga kuongeza kiungo mkabaji, beki wa kati na mshambuliaji kwenye dirisha dogo la usajili ingawa pia imedai itaangalia kwa jicho la tatu nafasi ya kipa inayoonekana kusuasua.
Kocha Msaidizi wa Simba, Jamhuri Kihwelu 'Julio' alisema nafasi hizo ndizo zimeonekana zina mianya.
Julio, ambaye kikosi chake kina wachezaji 26 alisema wanahitaji kujipanga upya na watawasilisha mapendekezo yao kwa uongozi.
"Tumesuasua katika baadhi ya mechi na nafasi ambazo tunaweza kuongeza dirisha dogo ni mshambuliaji mmoja, beki wa kati na kiungo mkabaji ingawa pia tutaangalia nafasi ya kipa, nayo tunaweza kuongeza nguvu kwani pia inasuasua," alisema Julio, ambaye habari za ndani zinadai huenda naye akatolewa kwenye benchi la ufundi la timu hiyo.
Simba ilifanya vizuri katika mechi kadhaa za mzunguko wa kwanza ingawa ilikuja kupepesuka na kutoka kileleni ikagota nafasi ya nne.
Hata hivyo Julio alitetea uamuzi wao wa kuwapeleka wachezaji walioshuka viwango kwenda timu ya vijana baada ya baadhi ya mashabiki na wanachama kuponda mfumo huo.
"Hatuwezi kuacha jambo hilo, litaendelea hivyo hivyo hata kama hawataki, kwani ndiyo funzo la wachezaji wasiotaka kujituma.
Mchezaji ukishindwa kuonyesha kiwango unaenda timu B ili upandishe kiwango chako na ukipelekwa kule wale waliobaki timu kubwa lazima nao watajituma zaidi,"alisema Julio, ambaye ni mchezaji wa zamani wa Simba.

MAGAZETI LEO JUMAMOSI NOVEMBA 09, 2013

DSC 0283 8ca4a

DSC 0284 6d190

Friday, November 08, 2013

MAGAZETI YA LEO IJUMAA NOVEMBA 08, 2013

DSC 0008 4d1e7
DSC 0009 f4e40

HOTUBA YA MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE...!!!


Jakaya-Kikwete_4f6c2.jpg
HOTUBA YA MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, ALIYOITOA BUNGENI KUHUSU JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI, 7 NOVEMBA, 2013, DODOMA

Mheshimiwa Anne Makinda, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Dkt. Mohamed Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi;
Mheshimiwa Mizengo Pinda, Waziri Mkuu;
Waheshimiwa Mawaziri na Naibu Mawaziri;
Mheshimiwa Freeman Mbowe, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni;
Waheshimiwa Wabunge;
Mabibi na Mabwana;

Nakushukuru sana Mheshimiwa Spika kwa kukubali ombi langu na kutenga muda wenu ili niweze kuzungumza na Wabunge wa Bunge lako Tukufu kuhusu masuala muhimu kwa uhai, ustawi na maendeleo ya nchi yetu na watu wake.

Mheshimiwa Spika;
Nimeambiwa kuwa taarifa ilipotolewa kuwa ninaomba kuja kuzungumza na Waheshimiwa Wabunge, kumekuwepo na dhana mbalimbali. Wapo waliodhani kuwa nakuja kuzungumzia mchakato wa kuunda Katiba mpya na hasa matukio ya wiki chache zilizopita. Wapo waliodhani nakuja kuzungumzia "Operesheni Tokomeza". 

Tena wapo waliokwenda mbali na kufikiria kuwa nakuja kuwakaripia Waheshimiwa Wabunge waliotoa maoni yao kuelezea kasoro zilizojitokeza katika utekelezaji wa Operesheni hii muhimu. Na wapo pia waliodhani ninakuja kuzungumzia ushiriki wa majeshi yetu ya Tanzania katika Jeshi la Kulinda Amani la Umoja wa Mataifa nchini Kongo.

Mheshimiwa Spika;
Hayo si makusudio yangu. Kinachonileta mbele ya Bunge lako Tukufu ni kuzungumzia Jumuiya ya Afrika Mashariki na mustakabali wa Tanzania katika Jumuiya hiyo. Lakini, kwa sababu ya umuhimu wa masuala hayo niliyoyataja na rai niliyopewa kuwa niyasemee japo kidogo. Nimeona ni vyema nifanye hivyo.

Mheshimiwa Spika;
Kuhusu mchakato wa Katiba mpya, napenda kusema kuwa tumefikia hatua nzuri katika utekelezaji wake. Kama mjuavyo Tume ya Mabadiliko ya Katiba imekamilisha, kwa mafanikio, hatua ya mwanzo ya kusikiliza maoni ya wananchi kuhusu Katiba wanayoitaka. Pia walishatoa Rasimu ya Kwanza ya Katiba na kukamilisha mchakato wa Mabaraza ya Katiba. Kinachosubiriwa kwa hamu na sisi wote, ni Rasimu ya Pili ya Katiba ambayo inatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 15 Desemba 2013 au kabla ya hapo.

AZAM FC NA KOCHA WAKUBALI KUACHANA, YASEMEKANA JUMA KASEJA AMEJIUNGA YANGA

aje_7811f.jpg
Taarifa za kipa nyota, Juma Kaseja kutua Yanga zimewachanganya watu wengi. Ingawa zimekuwa hazina uhakika, lakini Salehjembe imepata taarifa za uhakika kwamba mchana wa jana ndiyo amemalizana na Yanga. Lakini bado watu wamekuwa wakihaha kutaka kujua kuhusiana na suala hilo.
Mmoja wa viongozi wa Yanga alisema; "Sitaki kulizungumzia kwa sasa, kama kuna walioandika sawa, lakini kumalizana
kwetu na Juma ni leo (Alhamisi). Tulimpa mkataba, anao yeye, hivyo tutakutana na kumalizana na tumegawanya makundi mawili, moja litakuwa uwanjani katika mechi dhidi ya Oljoro na lingine katika ishu hiyo ya Kaseja."
stewart_hall_62acc.jpg
Na Mahmoud Zubeiry
KOCHA Muingereza, Stewart John Hall ameamua kujiuzulu kufundisha klabu ya Azam FC baada ya kukubaliana na wamiliki wa timu hiyo na jana amewaaga wachezaji wa timu hiyo.
Stewart aliwaaga wachezaji na benchi la Ufundi mara tu baada ya mchezo wa mwisho wa mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baina ya timu hiyo na Mbeya City ulioisha kwa sare ya kufungana mabao 3-3 Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

KAMANDA WA M23 AJISALIMISHA UGANDA

131105144849_m23_304x171_getty_d4f56.jpg
Maafisa wa Serikali ya Uganda wanasema kuwa kamanda wa kijeshi wa wapiganaji walioshindwa katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, DRC, M23, amejisalimisha kwa utawala wa Uganda.
Ripoti kutoka Uganda zinasema kuwa mamia ya wapiganaji wamejisalimisha pamoja na kiongozi wao, Sultani Makenga.
Wapiganaji hao wamejisalimisha katika eneo la hifadhi ya Wanyama ya Pori ya Mgahinga, kwenye mpaka wa Uganda na DRC.
Mnamo Jumanne M23 walisema kuwa wamesitisha maasi yao ya miezi 20 Mashariki mwa Congo, baada ya kutimuliwa katika ngome zao Mashariki mwa Congo na wanajeshi wa Serikali wakishirikiana na askari wa kudumisha amani wa Umoja wa Mataifa.
Hata hivyo serikali za Uganda na DRC hazijaweza kuthibitsha madai haya.
Mapema wiki hii, M23 ilisema kuwa inamaliza uasi wake wa miezi kumi na tisa masaa chache baada ya majeshi ya serikali kudai ushindi dhidi ya waasi hao.
Ripoti zinasema kuwa Sultani Makenga na waasi wengine 1,700, wamesalimisha silaha zao na wanazuiliwa na jeshi la Uganda katika kambi ya jeshi ya Mgahinga, karibu na mpaka na DRC.
Mapema wiki hii, maafisa wa DRC walisema Makenga alitoroka na kuingia Uganda au Rwanda.
Uganda imekuwa mwenyeji wa mazungumzo ya amani kati ya waasi na serikali ya DRC , ingawa hakuna mkataba wa amani umefikiwa.

Thursday, November 07, 2013

POLISI WAFANYA JARIBIO KATIKA HOTELI YA GOLD CREST MWANZA KUONA JINSI WANANCHI WANAVYOWEZA KUJIAMI NA MATUKIO YA UVAMIZI

WAPINGA MAREKEBISHO SHERIA YA MAGAZETI


lissu_5a412.jpg
Wakati Serikali imewasilisha muswada wa marekebisho ya sheria mbalimbali ikiwemo Sheria ya Magazeti, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, imepinga marekebisho ya sheria hiyo kwa madai kuwa hayakufanyiwa tafakuri na utafiti.
Akiwasilisha maoni hayo bungeni jana, Msemaji wa Kambi hiyo kuhusu Sheria, Tundu Lissu, alisema mapendekezo hayo yamefikishwa bungeni bila kufanyia tafakuri au utafiti wowote.
"Mwanasheria Mkuu wa Serikali angefanya utafiti kidogo tu angegundua kwamba kifungu cha 55 hakina na hakijawahi kuwa na, sababu yoyote ya kuendelea kuwepo katika kanuni ya adhabu,"alisema .
Alisema hiyo inatokana na kifungu hicho hicho kutungwa upya, kwa maneno yale yale, kama kifungu cha 31 cha Sheria ya Magazeti kwamba kifungu hicho hakikupaswa kuwepo kwa sababu, makosa ambayo kifungu hicho kinafafanua hayako tena kwenye kanuni ya adhabu na badala yake, yako katika Sheria ya Magazeti.
"Inaelekea katika fasta fasta ya kupitisha muswada wa Sheria ya Magazeti, kifungu cha 55 kilisahauliwa katika kanuni ya adhabu wakati vifungu vyote vinavyohusu makosa ya uchochezi na kashfa ya kijinai vilipohamishiwa katika Sheria ya Magazeti,"alisema Lissu.

MBUNGE WA UKEREWE AFUTIWA DHAMANA NA KUAMRIWA AENDE SELO SIKU 14

560843761_fd884.jpg
Na mwanahabari Bundala William
DHAMANA ya mbunge wa jimbo la Ukerewe, Salvatory Machemli (CHADEMA) imefutwa na ameamuriwa na mahakama kwenda rumande siku 14 kwa kuwa wadhamini wake wamekosa sifa baada ya mshitakiwa na wadhamini wake watatu kushindwa kufika mahakamani ili kuwezesha kesi inayomkabili kusikilizwa kama ilivyopangwa.
Pia, Mbunge huyo ametakiwa kuwasilisha vitambulisho vyake katika kituo cha polisi na amezuiliwa kutoka nje ya wilaya bila kibali cha mahakama.
Hakimu mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya wilaya hiyo Faustine Kishenyi ametoa uamuzi huo leo baada ya upande wa mashitaka kuomba mshitakiwa afutiwe dhamana.


Wadhamini ambao ni Shellifu Ngelezya, Max Mhogo na Konsolata Machemli wamepoteza sifa hivyo udhamini wao umefutwa.
Mwendesha mashitaka wa jeshi la polisi, Inspekta Samweli Onyango amesema mshitakiwa kwa makusudi ameshindwa kufika mahakani zaidi ya mara tano bila kutoa taarifa wakati kesi yake ikitajwa.

MATOKEO YA LIGI YA MABINGWA ULAYA

ARSENAL YAIKALISHA BORUSSIA DORTMUND, ETO'O APIGA MBILI CHELSEA IKIUA WAJERUMANI...MESSI KAMA KAWA, AIPIGIA MBILI BARCA IKIINYANYASA AC MILAN ULAYA
article-2488571-193C99A200000578-202_634x431_c6de5.jpg
Zama za ushindi: Aaron Ramsey (kulia) na Mesut Ozil wakishangilia bao pekee la ushindi la Arsnal
BAO pekee la Aaron Ramsey dakika ya 62, limeipa Arsenal ushindi wa 1-0 ugenini dhidi ya wenyeji Borussia Dortmund nchini Ujerumani.
Hilo linakuwa bao la 13 kwa mchezaji huyo msimu huu na bao la tano katika michuano ya Ulaya msimu huu. Pamoja na kufungwa, wenyeji ndio waliocheza vyema usiku huu na kabla ya Arsenal kupata bao lake, hawakuweza kutengeneza nafasi hata moja ya kufunga.
Borussia ambayo inapewa sifa ya moja ya timu bora kabisa Ulaya kwa sasa, iliingia kwenye mechi hiyo ikiwa na kumbukumbu ya ushindi wa 6-1 dhidi ya Stuttgart katika ligi ya kwao, Bundesliga, lakini ilikalishwa na mtutu mmoja wa bunduki.

Wednesday, November 06, 2013

LULU AFUNGUKA KUHUSU YEYE KUCHUMBIWA...!!!

 
Muigizaji wa filamu nchini Elizabeth Michael aka Lulu amekanusha fununu zilizoandikwa kwenye gazeti la udaku liitwalo ‘Filamu’ kwamba amechumbiwa na muda mchache ataolewa.
 
Akizunguza jana  kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM, muigizaji huyo wa Foolish Age, alisema hajachumbiwa na mtu yeyote ila ni magazeti ya udaku tu ndio yamekuwa yakiandika kile yanachojisikia.
 
“Mimi sijachumbiwa na hakuna mtu yeyote aliyenichumbia na kama itatokea siku nikachumbiwa kila mtu atajua, na ni mimi mwenyewe ndiye nitakaesema,” alisema mrembo huyo.
  “Lakini sasa sijajua wao wamepata hiyo habari kutoka kwenye chanzo gani, by the way kwaajili kumekuwa na habari kila kukicha kila mtu anayejisikia kuandika anaandika ,anaamka anaandika, anaamka anandika. 

 "Kwa hiyo leo wameandika nimechumbiwa, kesho wataandika nimeolewa, kwa hiyo inategemea na mood ambayo wao waliamka nayo, kwamba ‘leo Lulu tumchumbie, tumuozeshe, tumuachishe’, I don’t know.
 
“Kuchumbiwa, kuolewa,kuwa mke ni vitu ambavyo tumeumbiwa binadamu, vipo kama ukiwa mpango wa mwenyezi Mungu nitachumbiwa na nitaolewa.” Lulu

ANGALIA PICHA ZA JUX KING OF PAMBA KWA WASANII WA BONGO

http://distilleryimage8.ak.instagram.com/d08bd338f3c411e289bf22000a1fa4a9_7.jpg

http://distilleryimage2.ak.instagram.com/ddfe26f6ef9611e2a63622000a9e28ec_7.jpg


http://distilleryimage11.ak.instagram.com/cbffd894453311e3984822000a1f9707_7.jpg 
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

UJUMBE MZITO WA LULU KWA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

MSANII wa filamu nchini, Elizabeth Michael ‘Lulu’, ameliomba Bunge kurekebisha sheria za Magereza katika vikao vyao vinavyoendelea mjini Dodoma.
Akizungumza na Tanzania Daima jijini Dar es Salaam juzi, Lulu alisema kutokana na kukaa huko kwa mwaka mmoja, ameona mambo mengi ambayo yanatakiwa kufanyiwa marekebisho.
“Unaweza ukamkuta mfungwa ana miaka zaidi ya 20 lakini hajawahi kufikishwa mahakamani wala kuulizwa chochote kutokana na kitu ambacho kimempeleka hapo, kiukweli hata kama ana makosa haiwezekani kumkalisha miaka yote hiyo pasipo kusikilizwa,” alisema.
Alisema yeye amekaa huko kwa muda mfupi lakini amepata shida sana kuyazoea mazingira hayo, kwani huwezi kuishi kama nyumbani, hivyo ni vizuri ukiwekwa utaratibu mtu anasomewa kesi yake kwa muda gani.
Lulu alilazimika kukaa gerezani kwa muda huo kwa tuhuma za mauaji ya aliyekuwa nguli wa filamu nchini, Steven Kanumba, aliyefariki dunia nyumbani kwake Sinza Vatican Aprili 7, mwaka jana

MAGAZETI YA LEO JUMATANO NOVEMBA 06, 2013

.
.
.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...