Thursday, November 07, 2013

MATOKEO YA LIGI YA MABINGWA ULAYA

ARSENAL YAIKALISHA BORUSSIA DORTMUND, ETO'O APIGA MBILI CHELSEA IKIUA WAJERUMANI...MESSI KAMA KAWA, AIPIGIA MBILI BARCA IKIINYANYASA AC MILAN ULAYA
article-2488571-193C99A200000578-202_634x431_c6de5.jpg
Zama za ushindi: Aaron Ramsey (kulia) na Mesut Ozil wakishangilia bao pekee la ushindi la Arsnal
BAO pekee la Aaron Ramsey dakika ya 62, limeipa Arsenal ushindi wa 1-0 ugenini dhidi ya wenyeji Borussia Dortmund nchini Ujerumani.
Hilo linakuwa bao la 13 kwa mchezaji huyo msimu huu na bao la tano katika michuano ya Ulaya msimu huu. Pamoja na kufungwa, wenyeji ndio waliocheza vyema usiku huu na kabla ya Arsenal kupata bao lake, hawakuweza kutengeneza nafasi hata moja ya kufunga.
Borussia ambayo inapewa sifa ya moja ya timu bora kabisa Ulaya kwa sasa, iliingia kwenye mechi hiyo ikiwa na kumbukumbu ya ushindi wa 6-1 dhidi ya Stuttgart katika ligi ya kwao, Bundesliga, lakini ilikalishwa na mtutu mmoja wa bunduki.
Dortmund; Weidenfeller 6, Grosskreutz 7, Papastathopoulos 6, Subotic 7, Schmelzer 6, Sahin 5, Bender 5 (Hofmann 75, 5), Blaszczykowski 6 (Aubameyang 74, 5), Mkhitaryan 6, Reus 6 (Schieber 86), Lewandowski 6.
Arsenal: Szczesny, Sagna, Mertesacker, Koscielny, Gibbs, Ramsey, Arteta, Cazorla/Monreal dk75, Ozil, Rosicky/Vermaelen dk91 na Giroud/Bendtner dk90.
article-2488608-193CB05A00000578-420_634x435_4e9d9.jpg
Katika mechi nyingine, Barcelona imeifunga AC Milan mabao 3-1 Uwanja wa Camp Nou, Lionel Messi akifunga mawili dakika ya 30 na 83, wakati lingine limefungwa na Busquets dakika ya 40, huku Pique akijifunga dakika ya 45 kuwapatia wageni bao la kufutia machozi.
Barcelona: Valdes; Dani Alves, Pique, Mascherano, Adriano; Xavi/Song dk88, Busquets, Iniesta/Fabregas dk78, Alexis, Messi na Neymar/Pedro dk85)
AC Milan: Abbiati; Abate, Zapata, Mexes, Emanuelson; Muntari, Montolivo, De Jong, Poli/Birsa dk74', Kaka/Matri dk84, Robinho/Balotelli dk46.
article-2488599-193C611A00000578-296_634x441_49e6a.jpg
Nayo Chelsea imeifumua 3-0 Schalke 04, mabao ya Samuel Eto'o dakika ya 31 na 54 na Demba Ba dakika ya 83.
Chelsea: Cech, Ivanovic, Azpilicueta, Mikel, Cahill, Terry, Willian, Ramires, Eto'o/Ba dk77, Oscar/Lampard dk81 na Schürrle/De Bruyne dk78.
Schalke: Hildebrand, Uchida, Aogo, Neustädter, Höwedes, Matip, Draxler/Clemens dk62, Jones, Szalai, Boateng/Kolasinac dk77 na Fuchs/Meyer dk67.
Chanzo:bongostaz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...