Friday, September 06, 2013

GHASIA KUBWA ZALIPUKA BUNGENI KUPINGA MUSWADA.....!!!

vurugusugu_dd67c.jpg
Jana, Bingwa wa Dunia wa uzani wa kati (super middle), unaotambuliwa na Shirikisho la Ngumi Duniani (WBF), Francis Cheka alitembelea Bunge baada ya kutwaa taji hilo karibuni na jana hiyohiyo, Bunge hilo lilishuhudia ngumi kavukavu katika vurugu kubwa pengine kuliko zote zilizowahi kutokea katika ukumbi wake.Katika masumbwi hayo yasiyo rasmi, Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi 'Sugu' anadaiwa kumpiga kichwa Askari wa Bunge na kumchania sare na kung'oa kipaza sauti.
Mbilinyi jana alisema alikuwa anatafutwa na polisi huku akisema hilo limemshangaza akidai kwamba yeye ndiye aliyeshambuliwa na askari huyo.
Vurugu hizo zilitokea baada ya Naibu Spika, Job Ndugai kuamuru kutolewa nje kwa Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe.
Katika vurugu hizo Mbilinyi alibebwa juujuu na polisi hadi nje ya ukumbi huku akiwa hana viatu.
Pamoja na tafrani hiyo, Ndugai alisema wakati akihitimisha kikao cha Bunge kipindi cha asubuhi kuwa amewasamehe wabunge wote waliohusika na kosa hilo la utovu wa nidhamu na kuwaruhusu kurejea kipindi cha jioni kuendelea na Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba. Hata hivyo, wabunge wote CUF, NCCR-Mageuzi na Chadema ambao baada ya tukio hilo walitoka nje ya ukumbi, hawakurejea na baadaye walitoa msimamo wa pamoja wakisema hawatashiriki katika mjadala huo.

BAADA YA DAYNA, BABA LEVO NAE AFUNGUKA NA KUDAI KUIBIWA KORASI YA WIMBO MPYA WA DIAMOND "MY NUMBER ONE"...!!!

https://fbcdn-sphotos-a-a.akamaihd.net/hphotos-ak-prn2/q83/1185392_659474667396477_477324071_n.jpg
NARUDIA tena nina asilimia 100 DAIMOND PLATNUM amecopy KORAS yangu coz nimekuwa nikimuimbia kila tunapokutana kwa lengo la kumshirikisha kwenye wimbo wangu (SWEATY SWEATY) ni zaidi ya miezi saba au nane imepita akinizungusha tu.
Na kwa kudhibitisha Hilo mimi nina DEMO 5 za KORASI yangu ambazo nimefanya kwenye studio mbali mbali Ya kwanza 1 kwa MORE FIRE magomeni 2 STUDIO SINZA 3 kwa TUDY THOMAS mbezi 4 kwa G BAKUZA KIGOMA 5 kwa MR T TOUCH mwenge... 
Ninaweza kuwasikilizisha watu demo zote Tano lakini sio kuuachia huo wimbo coz ntaonekana walewale wategemea KICK. wakati MIMI KWA SASA sihitaji kick ya mtu coz msimu huu nina nguvu ya kutosha. na nina jiamini.. ukitaka kuamini angalia kilichotokea FIESTA MTWARA JUZI..

MAWAZIRI WATEJA WA MACHANGUDOA WATAJWA.......!!!



BAADHI ya Mawaziri na askari polisi wametajwa kuwa ni wateja wakubwa wa wanawake wanaouza miili yao(Machangudoa).

Hayo yameelezwa na jukwaa la wanaharakati wanawake vijana (YFF), walipokuwa wakiwasilisha ujumbe wao kwa njia ya sanaa ya ngonjera, katika tamasha la 11 la Mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP) linaloendelea eneo la Mabibo Jijini Dar es Salam.

"TATIZO LA UJENZI HOLELA NI KUBWA JIJINI DAR" SERIKALI

majengo_234e1.jpg
Serikali imekiri kuwa kumekuwa na ukiukwaji wa ujenzi ambao haufuati kanuni, taratibu na sheria zilizopo hususan katika Jiji la Dar es Salaam.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Hawa Ghasia ambaye alisema kuwa Serikali imeliona jambo hilo na sasa inapitia sheria upya ili kurekebisha hali hiyo.
Waziri aliyataja maeneo ambayo yanahusika na ukiukwaji ni pamoja na utoaji wa vibali vya ujenzi pamoja na ubadirishwaji wa matumizi ya ardhi na uvamizi wa viwanja vya wazi.
Maeneo mengine ni ukiukwaki wa maadili ya kitaaluma usiozingatia sheria ya mwaka 2007 ya sheria ya mipango miji na kanuni za udhibiti wa ujenzi.

Alikuwa akijibu swali la Muhammed Amour Chombo (Magomeni,CCM) aliyetaka kujua Serikali ina mkakati gani wa kukomesha utovu wa nidhamu dhidi ya waliopewa dhamana ya kusimamia sheria za mipango miji katika kuruhusu ujenzi.

CHEKA ATINGA BUNGENI NA UBINGWA WA WBF



Waziri Mkuu Mh, Mizengo Pinda wanne kushoto akiwa na bingwa wa dunia wa mchezo wa masumbwi nchini Fransic Cheka baada ya kukaribishwa bungeni mjini Dodoma wengine kushoto Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D'  na bingwa wa mabara Fransic Miyeyusho kulia ni promota wa mchezo wa masumbwi nchini Mohamed Bawaziri,  na promota wa mpambano wa ubingwa wa Dunia ambao cheka anao kwa sasa Catherini Matili .

MAJI MAREFU AKIWA NA MABINGWA WA MCHEZO WA MASUMBWI NCHINI

Thursday, September 05, 2013

ANGALIA PICHA ZA RAIS KIKWETE WALIPOKUTANA NA KAGAME HUKO KAMPALA LEO...!!!


Rais Jakaya Kikwete leo amefanya mazungumzo na Rais Paul Kagame wa Rwanda katika mkutano wa saba wa kimataifa wa nchi za maziwa makuu, unaofanyika Kampala, Uganda.
Haijafahamika mara moja walichozungumza, hizi ni picha za mkutano wao.
9676681299_b3707d20a5_c
9676687273_13e1849eb2_b
9679917620_3f83a214d0_b
Marais hao wamekutana wakati ambapo uhusiano kati ya nchi hizo mbili unaendelea kuzorota.

DULLY SYKES AMFANANISHA DIAMOND NA KANUMBA...!!! NI BAADA YA VIDEO MPYA YA DIAMOND KUTOKA

Baada ya kuachia video yake mpya iliyofanywa kwa gharama ya  takribani milioni arobaini na tano za kitanzania, mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya Diamond Platnumz amefananishwa na marehemu Steven kanumba kwa jinsi anavyothubutu kufanya mambo makubwa kukuza Sanaa na kipaji chake tofauti na wasanii wengine wenye majina makubwa nchini.

  Hayo yameongelewa na Msanii dully sykes katika mahojiano yake na mtandao wa Bongo5 hii leo... Katika interview hiyo Dully amemuelezea marehemu kanumba kama ni mtu aliyethubutu kutumia nguvu, hali na mali, kwa ajili tuu ta kukuza jina lake kitu ambacho ni nadra sana kwa wasanii hasa wa Tanzania.
“Kanumba alikuwa ana uwezo wa hata kuchukua nauli yake ya kwenda sehemu kama Ghana kwenye tamasha la movie lakini ilimradi kujitengenezea status yake. Kwahiyo Diamond ni mtu ambaye tayari ameshajitolea kwaajili ya kuutetea muziki wetu.” Alisema Dully sykes

KIZAAZAA CHATOKEA TENA BUNGENI.....WABUNGE WA CHADEMA WATOKA NJE YA BUNGE BAADA YA MBOWE KUAMRIWA KUTOKA NJE...!!!

Wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wametoka nje muda huu baada ya Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ambaye pia ni Mbunge wa Hai, Mhe. Freeman Mbowe kuamriwa atolewe nje na Naibu Spika wa Bunge Job Ndugai. 


Mbowe alisimama ili achangie lakini aliamriwa na Job Ndugai kukaa chini jambo ambalo hakuliafiki na kuendelea kusimama. Baada ya tukio hilo, Ndugai aliwaamuru askari wa bunge kumtoa nje Kiongozi huyo wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na ndipo mzozo ulipotokea.

Hali hiyo ilitokea wakati wa Majadiliano ya Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Mabadiliko ya Katiba wa mwaka 2013. Mbowe aligoma kutolewa nje ya bunge baada ya askari kufika alipokuwa amekaa kwa lengo la kumtoa nje, ndipo ilipotokea sintofahamu na mzozo mkubwa ndani ya bunge hali iliyopelekea wabunge wote wa Chadema kutoka nje.

Hali kama hii pia ilitokea jana wakati muswada wa marekebisho ya pili ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83 ukisomwa na kupelekea wabunge wa vyama vya Chadema, CUF na NCCR-Mageuzi kutoka nje wakishinikiza muswada huo usisomwe hadi maoni ya wadau kutoka Zanzibar yapatikane.

MAGAZETI LEO ALHAMISI SEPTEMBA 05, 2013

DSC 0020 2b75e
DSC 0021 88774

ATAFUNWA USO NA MWAJIRI WAKE NYUMBANI


IMG 4471 6ee8f
KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida mkazi wa Kijiji cha Nyabibuye Kakongo katika Wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma, Susuluka (16) anadaiwa kujeruhiwa vibaya usoni na bosi wake, Imani Paulo (36) kwa kung'atwa ng'atwa usoni na kisha kunyofolewa macho, pua na meno kubaki nje, kama ambavyo anaonekana pichani ukurasa wa mbele.

Tukio hilo ambalo tunaweza kulifananisha na dunia kuelekea kufika mwisho, limegusa hisia za watu wengi hasa wakazi wa Kibondo, huku wengine wakitokwa na machozi kutokana na kuguswa na ukatili ambao amefanyiwa kijana huyo.Tunaweza kufikiria kuwa tukio hilo ni sinema, lakini Mkuu wa Wilaya ya Kibondo, Venance Mwamotto, ameliambia Majira kuwa tukio hilo limetokea miezi miwili iliyopita.


Akizungumza na Majira katika mahojiano maalumu, Mwamotto, alisema kuwa kabla ya kijana huyo kujeruhiwa na bosi wake, alimtuma dukani ili akamnunulie soda.Aliliambia Majira kuwa baada ya kufika nyumbani alimkuta bosi wake akiwa amemkaba koo mbwa na kutokana na maumivu aliyokuwa akiyapata mbwa huyo, alianza kuhema akitoa ulimi nje.


DC Mwamotto alisema kuwa mtuhumiwa huyo ghafla alianza kuung'ata ulimi wa mbwa na kisha kumeza vipande jambo lililosababisha mbwa huyo kupiga kelele kutokana na maumivu.Aliongeza kuwa aliendelea kula vipande vya ulimi huo wa mbwa hadi alipoumaliza.

WABUNGE CHADEMA, CUF NA NCCR MAGEUZI WATOKA NJE....!!!

mbowe_chadema_08064.jpg
Wabunge wa Kambi ya Upinzani Bungeni jana jioni walitoka ndani ya Ukumbi wa Bunge, baada ya kupuuzwa kwa mwongozo wao wa kutaka kuahirishwa kujadiliwa kwa Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, hadi hapo Zanzibar itakaposhirikishwa.Wabunge waliotoka bungeni jana yapata saa 12.15 ni kutoka vyama vya Chadema, CUF na NCCR- Mageuzi huku Mbunge wa Vunjo na Mwenyekiti wa Taifa wa Tanzania Labour Party (TLP, Augustine Mrema akiendelea kubaki ukumbini.

Kitendo cha wabunge hao wa upinzani kilionekana kuwakera baadhi ya wabunge wa CCM, ambao walisikika wakiwakejeli kwa kupiga meza huku wakisema: "Kwendeni zenu, tumewazoea."
Wakati wabunge hao wakiondoka, Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, alikuwa akiwasisitiza wabunge wanaobakia wawe watulivu, maana kuna usalama wa kutosha ndani ya ukumbi huo.
"Mnaotoka nimewaona wote na mnanijua," alisikika Naibu Spika Ndugai akiwatahadharisha wabunge wa upinzani waliosusa mjadala huo.
Wabunge wa CCM waliendeleza vituko ambapo baada ya wapinzani kutoka, wabunge Juma Nkamia (Kondoa Kusini), Hilary Aeshi ( Sumbawanga Mjini) na Murtaza Mangungu (Kilwa Kaskazini) walikwenda kukaa katika viti vya kambi ya upinzani.

Kabla ya kutoka kwa wabunge hao wabunge wawili kutoka CUF waliomba mwongozo wa Spika, wakitaka muswada huo kuondolewa ili kuwapa nafasi Wanzanzibar kutoa maoni yao.
Mbunge wa Mkanyageni, Habib Mohamed Mnyaa (CUF) aliomba mwongozo akitaka muswada huo uondolewe, hadi hapo Wazanzibar watakaposikilizwa.

Alisema kuwa kwa maoni ya Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala wamesikiliza maoni ya wadau wengi, lakini Zanzibar hawakwenda kuwasikiliza wadau wa eneo hilo.

MUSEVENI AWAKUTANISHA RAIS KIKWETE NA KAGAME

museven_d895a.jpg
Rais wa Uganda, Yoweri Museveni ameitisha mkutano wa dharura wa marais wa nchi za Maziwa Makuu (ICGLR), kujadili hali ya usalama Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.Rais Jakaya Kikwete ni miongoni mwa waalikwa kwenye mkutano huo ambao pia unatarajiwa kuhudhuriwa na Rais wa Rwanda, Paul Kagame.


Wakati hali ya usalama Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ikidhoofika, katika siku za karibuni, uhusiano wa Tanzania na Rwanda umekuwa wa shaka hasa baada ya Rais Kikwete kuishauri Serikali ya Rwanda kukaa na wapinzani ili kumaliza mzozo uliolikumba eneo la Maziwa Makuu.

Rais Kikwete alitoa ushauri huo wakati akiwa katika sherehe za maadhimisho ya miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU), zilizofanyika mjini Addis Ababa, Ethiopia. Mkutano wa leo utafanyika kwenye Ukumbi wa Commonwealth Resort, Munyonyo katikati ya Jiji la Kampala.  Tembelea http://jambotz8.blogspot.com/ kila siku.

Kwa mujibu wa taarifa Rais Museveni ameitisha mkutano huo hasa kuzungumzia hatua ya Umoja wa Mataifa kupambana na Kundi la Waasi wa M23.

Mbali na viongozi hao wa Tanzania na Rwanda, viongozi wengine wanaotarajiwa kuhudhuria mkutano huo wanatoka Angola, Burundi, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Jamhuri ya Kongo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Kenya, Sudan, na Zambia.

SAKATA LA AGNESS MASOGANGE, AINGIZWA KWENYE CHUMBA CHA MATESO SAA 24. ... AWATAJA WALIOMTUMA

http://4.bp.blogspot.com/-LIqEEeOg9jY/UYOuPv4TsvI/AAAAAAAAfUY/LO4pQ528Ack/s1600/masogange.jpg

IMEVUJA! Staa muuza nyago kwenye video za wasanii wa muziki wa kizazi kipya na filamu za Kibongo, Agnes Gerald ‘Masogange’ na shosti wake, Mellisa Edward kabla ya
kupandishwa kizimbani kwa msala wa dawa za kulevya ‘unga’ Afrika Kusini waliingizwa kwenye chumba cha mateso kwa saa 24 ili kutaja waliowatuma.

Habari kutoka kwa chanzo chetu kilichopo jijini Johannesburg nchini humo zilidai kuwa baada ya kukamatwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oliver Tambo, walipelekwa polisi ambapo walichukuliwa maelezo.

Ilielezwa kuwa mwanzoni waligoma kueleza mzigo huo wa kilo 150 wa unga ulikuwa wa nani hivyo ikabidi polisi wa upelelezi watafute njia nyingine ya kuwalainisha kwa kuwabembeleza kuwa wakieleza ukweli wataachiwa.

MATESO SAA 24
Chanzo hicho kilisema kuwa baada ya mbinu hiyo kushindikana ndipo wawili hao wakaingizwa kwenye chumba maalum cha mateso ikiaminika kuwa watasema aliyewatuma.

MFANYABIASHARA ANUNUA NDEGE YA BOING 747 JUMBO NA KUIGEUZA NYUMBA YA KULALA WAGENI....!!!



Ndani ya ndege hii "nyumba ya kulala wageni" kuna vyumba 27, unapata utandawazi, vumba vina luninga, imesha aanza kuchukuwa wageni wa kulala na ipo karibu na uwanja wa ndege wa  Arlanda airport karibu na mji wa Stockholm, Sweden
The grounded Boeing 747 is now a fixed hostel at Arlanda airport, near Stockholm, where gusts can even pay to stay in the cockpit suite


Hii ni sehemu iliyokuwa ya rubani wa ndege hiyo unaweza kulala hapa kuanzia  £170 kwa usiku mmoja


The rooms are all kitted out with flatscreen TVs, WiFi and en-suites



Wednesday, September 04, 2013

WAZAZI WATELEKEZA WATOTO HOTELINI KWA MIEZI MITATU, WADAIWA MILIONI 3

Na Steven Kanyeph - SHINYANGA 
Wazazi ambao hawajulikani makazi yao maalumu wameitelekeza familia ya watoto wao wanne katika hoteli ya Ibanza iliyopo mjini Shinyanga kwa takribani miezi 3 ambapo mpaka sasa wanadaiwa kiasi cha shilingi milioni tatu. 

Mhasibu wa Hoteli hiyo bwana Julius Kiungu amemtaja bi Christina Peter ambaye ni mzazi wa watoto hao kuwa alifika katika hoteli ya Ibanza Mei, 15 mwaka huu akiwa na watoto wa wanne kwa lengo la kupumzika. Bi Chritina ambaye ni mzazi wa watoto hao alieendelea kuwepo katika hoteli hiyo kwa takribani wiki mbili lakini baada ya hapo aliondoka bila taarifa na kuwatelekeza watoto wake katika hoteli hiyo. Tembelea http://jambotz8.blogspot.com/ kila siku.

Mmoja wa watoto hao aliyejitambulisha kwa jina la Teddy Masumbuko mwenye umri wa miaka 20 amesema kuwa anashangazwa na kitendo cha mama yao kuondoka bila kutoa taarifa huku akimuacha na wadogo zake watatu wenye umri mdogo. Msemaji wa hoteli hiyo bwana Julius Kiungu anawaomba ndugu, jamaa na marafiki wa familia hiyo wafike ili kuwachukuwa watoto hao kwa ulinzi na usalama wa watoto hao.

MWANAMKE AKAMATWA NA DAWA ZA KULEVYA UWANJA WA NDEGE JNIA LEO MCHANA JIJINI DAR ES SALAAM TANZANIA

Jitihada za kurejesha heshima kwa viwanja vya ndege nchini zilizoanzishwa na waziri wa uchukuzu Dk. Harisson Mwakyembe zinaonekana kuzaa matunda baada ya mwanadada kutoka nchini Nigeria Anthonia Ojo (25) kukamatwa na kete 99 za madawa ya kulevya Dar es Salaam leo.

Zifuatazo ni picha mbalimbali za tukio zima la kunaswa kwa mtuhumiwa huyo ambapo anashikiliwa na polisi kwa uchunguzi zaidi wakati kete hizo zimepelekwa kwa ofisi ya Mkemia Mkuu kwa uchunguzi zaidi. 

ANTHONIA OJO AKIWASILI KITUO CHA POLISI CHA JNIA BAADA KUKAMATWA.
ANTHONIA OJO AKIELEKEA KWENYE GARI BAADA YA KUKAMATWA

MAGAZETI YA LEO JUMATANO SEPTEMBA 04, 2013

DSC 0018 857f5
DSC 0019 bd620

WAJUA KWANINI UNAHITAJI KULALA?

kulala_39d75.jpg
Wanasayansi wanaamini kuwa wamepata sababu moja mpya ya kwa nini tunahitaji usingizi.
Wanasema kuwa kulala kunasaidia katika kujenga celi mpya za ubongo.

Usingizi unasaidia kuzalisha upya celi za ubongo ambazo nazo hujenga kemikali inayojulikana kama Myelin ambayo ni muhimu katika kulinda ubongo wetu kwa ambavyo unafanya kazi.


Matokeo ya utafiti huu ambayo yalijitokeza katika panya wa mahabara, huenda yakachochea maelezo zaidi kuhusu umuhimu wa usingizi katika kukabarabati celi za ubongo na kukuza celi mpya pamoja na kuulinda kutokana na magonjwa.

Daktari Chiara Cirelli na wenzake kutoka chuo kikuu cha Wisconsin waligundua kuwa Panya hao walipokuwa wanalala, ndipo kemilaki hiyo ilikuwa inatengezwa kwa wingi na celi za mwili.

Tuesday, September 03, 2013

WIMBO MPYA WA DIAMOND - NUMBER ONE


MWANAMKE ANASWA NA SARE ZA JWTZ....!!!


JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limemkamata Saida Mohamed (30), mkazi wa Mwasonga Kigamboni, akiwa na sare za Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ). 
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleimani Kova, alisema mtuhumiwa huyo alikamatwa Agosti 31, mwaka huu, katika eneo la Mwasonga, Kigamboni.

Alisema Saida alikamatwa na suruali saba, mashati saba ya kombati, kofia 10, shati mbili nyepesi, fulana mbili na kofia moja aina ya bareti, vyote vikiwa mali ya JWTZ.

Alisema mtuhumiwa huyo, alikuwa na begi moja la kuwekea nguo za jeshi, cheo kimoja cha Koplo na mikanda miwili ya kijeshi.

Alisema uchunguzi unaendelea juu ya mwanamke huyo ili kubaini sababu za kumiliki sare za jeshi, kabla ya kufikishwa mahakamani.

Katika tukio jingine, polisi wamemkamata Husein Mkondoa (25), mkazi wa Gongolamboto Mzambarauni, akiwa anaendesha pikipiki huku akiwa amevaa nguo za kiraia na kofia ngumu ya kijani yenye nembo ya Polisi.

VIDEO MPYA YA GK - BARAKA AU LAANA


MAGAZETI YA LEO JUMANNE SEPTEMBA 3, 2013

DSC 0008 e4878
DSC 0009 047f4

RWANDA YAONGEZA USHURU KWA MIZIGO IPITAYO BADARI YA DAR TU

paul kagame 2d247
NI dhahiri sasa biashara ya kupitisha mizigo katika Bandari ya Dar es Salaam, imekuwa moto, baada ya Serikali ya Rwanda kupandisha tozo ya ushuru kutoka dola za Marekani 152 hadi 500 ambazo ni sawa na Sh 800, 000 za Tanzania.
Hali hii inawezekana kwa namna moja au nyingine, imetokana na mzozo kati ya Rais Jakaya Kikwete na Rais Paul Kagame wa Rwanda, ambao umepelekea wafanyabiashara wa Rwanda na Uganda kutishia kuacha kupitisha mizigo yao katika Bandari ya Dar es Salaam.


Itakumbukwa mzozo huo, umekuja baada ya Rais Kikwete kumshauri Rais Kagame akubali kukutana na waasi wanaoendelea na vita mashariki mwa nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), lakini ushauri huo unaonekana kupokelewa tofauti na Rais Kagame.
Siri ya kupandishwa kwa gharama hizo, imefichuka jana baada ya malori mengi ya wafanyabiashara wa Tanzania kukwama katika mpaka wa Rusumo mkoani Kagera.

Monday, September 02, 2013

FAMILIA: AFRIKA KUSINI YAKATALIA RIPOTI KIFO CHA NGWEA.....!!!


TAKRIBANI miezi miwili tangu alipofariki dunia mfalme wa freestyle wa Hiphop Bongo, Albert Kenneth Mangweha ‘Ngwea’ bado familia inalalama kuwa haijapokea ripoti ya kifo cha kijana wao.


Mama mzazi wa Ngwea, Denisia Mangweha (kulia) akiwa na aliyekuwa mchumba wa mwanaye aitwaye Misheily.
Habari za kiuchunguzi kutoka ndani ya familia zimeeleza kuwa ukiachilia mbali cheti cha kifo cha Ngwea walichopewa siku kadhaa baada ya mazishi ya mtoto wao, hawajawahi kuelezwa kwa kina juu ya kile kilichomsababishia mauti au hata mwenendo wa kesi au uchunguzi wa tukio hilo.
Ilidaiwa kuwa mara kadhaa familia hiyo ilikutana katika vikao vya ndani na kukubaliana kulifuatilia suala hilo katika Ubalozi wa Afrika Kusini jijini Dar. Huko walikumbana na vizingiti kwa maelezo imekataliwa kutolewa nchini humo.
Ilisemekana kuwa ndugu hao walipokwenda mara ya mwisho ubalozini hapo waliambiwa waandike barua ya kuomba kujua kinachoendelea ikiwa ni pamoja na ishu ya kama kuna kesi katika tukio hilo.


Habari nyingine zilidai kuwa huenda ripoti hiyo ilikwama sehemu au uchunguzi haujakamilika.

GEORGE BUSH ATANGAZA KIFO CHA MANDELA....!!!


Rais wa zamani wa Marekani George W. Bush amejikuta ‘akiingia chaka’ kwa kutangaza ‘kifo’ cha Rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela ambaye bado yuko hai.
 
Kosa hilo limetokea jana asubuhi (September 1) kwa bahati mbaya baada ya msemaji wa rais huyo wa 41 wa Marekani kujichanganya kwa kutosoma vizuri habari inayomhusu Mandela kupitia Washington Post hivyo kumfanya Bush aandike ujumbe huu,

“Barbara and I mourn the passing of one of the greatest believers in freedom we have had the privilege to know. As President, I watched in wonder as Nelson Mandela had the remarkable capacity to forgive his jailers following 26 years of wrongful imprisonment — setting a powerful example of redemption and grace for us all. 
He was a man of tremendous moral courage, who changed the course of history in his country. Barbara and I had great respect for President Mandela, and send our condolences to his family and countrymen.”

MAGAZETI YA LEO JUMATATU SEPTEMBA 2, 2013

DSC 0522 e0f47
DSC 0523 52ecd
DSC 0524 0ca06

NIMEPEWA MAJINA YA WABUNGE WAUZA DAWA ZA KULEVYA: WAMO CCM, CHADEMA

Khamisi_Kigwangala_e74fd.jpg
Mbunge wa Nzega (CCM), Dk. Khamis Kigwangallah, amesema amepokea majina ya wabunge, viongozi wa serikali na wafanyabiashara maarufu nchini ambao ni mapapa wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya.

Hata hivyo, Dk. Kigwangallah ambaye amepania kuwataja bungeni watu wanaojihusisha na biashara hiyo haramu, amesema baada ya kukabidhiwa majina hayo kutoka kwa wananchi, anafanya uchunguzi na kupata ushahidi ili kujiridhisha kabla hajachukua hatua ya kuwataja. Miongoni mwa majina ya wabunge aliyopewa wamo kutoka CCM na Chadema, na wafanyabiashara maarufu wote wanatoka mkoa wa Dar es Salaam.

"Nawashukru wananchi wamenipa ushirikiano hadi jana wamenikabidhi majina ya watu saba ambao ni wabunge wawili, kiongozi mmoja mwandamizi wa serikali na wafanyabiashara wanne, ambao wote ni mapapa wauza unga na siyo madagaa," alisema Dk. Kingwangallah. 

Alisema katika kuhakikisha anatekeleza alichoahidi amemwandikia barua Spika wa Bunge kumuomba atoe maelezo kwa kuwataja majina vigogo wanaojihusisha na dawa za kulevya na kwamba bado anasubiri kujibiwa. Dk. Kigwangallah amekabidhiwa majina hayo siku chache tu baada Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge), William Lukuvi, kulieleza Bunge kuwa kama serikali itaamua kutaja wanaojihusisha na biashara hiyo hakuna atakayesalimika ndani ya bunge kwa sababu pia wamo wabunge wanaotajwa.

MZEE MANDELA ATOKA HOSPITALI


nelson-mandela ba73e
RAIS wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela (95), jana aliondolewa hospitali na kurejeshwa nyumbani ambako ataendelea na matibabu ya maradhi ya mapafu. Hata hivyo, taarifa ya Serikali ya Afrika Kusini imesema uamuzi huo hauna maana kwamba Mandela amepata nafuu kwa vile hali yake bado ni mbaya na wakati mwingine hudorora zaidi.
 

Taarifa hiyo imeongeza timu ya madaktari wa Mandela inaamini ataendelea kupata matibabu katika makazi yake mjini Houghton kwa kiwango sawa na anayopata akiwa hospitalini mjini Pretoria.

Tangazo hilo limekuja siku moja tu baada ya maofisa wa serikali kukanusha ripoti kuwa shujaa huyo wa taifa hilo, alisharuhusiwa.
Mshindi huyo wa tuzo ya amani ya Nobel aliyekuwa amelazwa hospitali tangu Juni 8, mwaka huu anaheshimiwa duniani kwa kuongoza mapambano dhidi ya utawala wa kibaguzi wa wazungu wachache na kuhubiri upatanisho na maridhiano na jamii za weupe pamoja na kufungwa miaka 27 jela.

"Timu ya madaktari imetuhakikishia kuwa Mandela atapokea matibabu kwa sawa na anachopata hospitalini mjini Pretoria atakapokuwa katika makazi yake ya Houghton," taarifa ya Ofisi ya Rais ilisema.
"Lakini ikibidi, atarejeshwa hospitali," taarifa hiyo ilisema na kuongeza kwamba inamtakia Mandela afya njema.

DAUDI MWANGOSI ATIMIZA MWAKA MMOJA TANGU KUUWAWA KWAKE MKOANI IRINGA.


Ndugu zangu,

HUWEZI kutawala miili ya watu ukaacha mioyo yao. Ndiyo, mjumbe hauawi, ni kauli ya hekima ya tangu enzi za wahenga wetu.

Leo ni mwaka mmoja tangu mwandishi wa habari na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Wandishi wa Habari mkoani Iringa,Daud Mwangosi kuawa.

Ilikuwa ni Jumapili ya Septemba 2, 2012. Hakika, siku ile  itabaki katika kumbukumbu za Watanzania kwa mamilioni. Ni kwa kufikiwa na taarifa za kutisha za mauaji ya mwandishi wa habari. Haya yanaingia katika historia kuwa ni mauaji ya kwanza kwa mwandishi wa habari kufanyika hadharani tangu nchi hii ipate Uhuru. Wengi watakuja kukumbuka walikuwa wapi na walifanya nini siku walipopata taarifa hizo za kutisha. Binafsi, taarifa ile ya mauaji ya Daud Mwangosi siku ile ya Jumapili ya huzuni kwa Taifa ilinikuta nikiwa Iringa Mjini. N umbali wa mwendo wa saa moja  kwa gari kufika eneo la tukio, Nyololo, Mufindi.


Jioni ile nilikuwa nikifundisha soka ya watoto. Mara baada ya kupata taarifa zile kwa simu,  nilisitisha mazoezi yale ya watoto. Nikawapa taarifa zile.  Nilipowaambia kuwa nimepata taarifa sasa hivi kuwa mwandishi wa habari ameuawa Mafinga, mtoto mmoja akaniangalia na kuniuliza; “ Kwanini?”

Ndiyo, swali la mtoto yule ndilo umma wa Watanzania unapaswa uendelee kujiuliza hata leo; KWA NINI?


Mwandishi wa habari ni mjumbe katika jamii. Anapokuwa akifanya kazi yake hapaswi kuwa na hofu ya kudhuriwa kwa kukusudia na waliopata mafunzo ya  kutumia silaha.  Ndivyo ilivyo kwa watumishi wa Msalaba Mwekundu, wanapokuwa kazini kwenye maeneo hata ya vita.

Sunday, September 01, 2013

SAKATA LA MADAWA YA KULEVYA,DIAMOND APOKONYWA PASSPORT...MASANJA MKANDAMIZAJI NAE ATAJWA.....!!!


Ni mwendelezo wa Sakata la unga ambalo sasa ni janga kwa taifa letu. Orodha zinaendelea kutoka na kuwekwa wazi huku bunge likivutana kuhusu sakata hlo. 
 
Tetesi za kutoka ndani zinasema msanii wa muziki Naseeb Abdul au Diamond ambaye alijitapa wazi mbele ya kamera za habari kuwa anamiliki ukwasi zaidi ya bilioni moja kwenye akaunti yake, nyumba 5 za thamani Kijitonyama na Mikocheni na anatumia simu 6 za thamani ambazo zipo hewani muda wote tayari amenyang'anywa hati yake ya kusafiria na baadhi ya simu zake katika mwendelezo wa uchunguzi juu yake unaofanywa na vyombo vya dola.
Msanii pia wa maigizo Masanja Mkandamizaji ambaye anadaiwa kumiliki mkwanja mrefu na nyumba za thamani kubwa mpaka magari naye tayari ametajwa kuhusika na sembe.

Episode inaendelea,tuungane katka vita hii.

SOURCE: JF

MCHUNGAJI ATOA SIRI ALIVYOJIHUSISHA NA MADAWA YA KULEVYA....!!!

 Mchungaji Donald Mwakisambwe wa kanisa la Kipendekoste la Kiinjili Tanzania, kwenye ofisi za gazeti hili wakati akitoa ushuhuda wa kufanya biashara haramu ya madawa ya kulevya.

Kinara wa kimataifa wa kuuza madawa ya kulevya aliyezunguka sehemu mbalimbali duniani kuuza mihadarati, ameacha biashara hiyo na sasa anahubiri Injili kupiga vita dawa hizo. Kigogo huyo Mtanzania na mzaliwa wa Mbeya, ambaye sasa anajiita kiumbe kipya katika Kristo, ni Mchungaji Macdonald Mwakisambwe wa Kanisa la Kipentekoste la Kiinjili jijini Dar es Salaam. 
 
Akizungumza katika mahojiano maalumu na NIPASHE Jumamosi jana, Mwakisambwe alisema alianza biashara ya unga mwaka 1990 na kuifanya kwa miaka 10, akisafirisha dawa kwa maelfu ya wateja walioko Afrika, Asia, Ulaya na Amerika. Alisema katika kutimiza azma hiyo, alitumia pasi za kusafiria za mataifa mbalimbali zenye majina tofauti, zikimuonyesha kuwa ni raia wa Msumbiji, Tanzania, Kenya, Namibia, Afrika Kusini na Namibia.

MANDELA HAKUTOLEWA HOSPITALI....!!!

Serikali ya afrika Kusini imekanusha taarifa za vyombo vya habari kwamba aliyekuwa kiongozi wa afrika Kusini, Nelson Mandela, ambaye amelazwa hospitali tangu mwezi wa Juni, kwamba alirejeshwa nyumbani Johannesburg Ijumaa usiku.

Taarifa ya serikali imesema kuwa Bwana Mandela bado yuko hospitali mjini Pretoria na kwamba bado mahtuti, lakini hali yake imetulia.

Kulazwa kwa muda mrefu kwa kiongozi huyo kumewatia wasiwasi raia wa taifa hilo na ulimwengu kwa jumla.

Mandela ambaye ana umri wa miaka 95, alikuwa Muafrika wa kwanza kuwa rais wa taifa la Afrika Kusini, na anaheshimiwa na wengi kama baba wa taifa.

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI SEPTEMBA 01, 2013

DSC 0522 a7487
DSC 0523 38a54
DSC 0524 3c0ac

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...