Wednesday, September 04, 2013

WAZAZI WATELEKEZA WATOTO HOTELINI KWA MIEZI MITATU, WADAIWA MILIONI 3

Na Steven Kanyeph - SHINYANGA 
Wazazi ambao hawajulikani makazi yao maalumu wameitelekeza familia ya watoto wao wanne katika hoteli ya Ibanza iliyopo mjini Shinyanga kwa takribani miezi 3 ambapo mpaka sasa wanadaiwa kiasi cha shilingi milioni tatu. 

Mhasibu wa Hoteli hiyo bwana Julius Kiungu amemtaja bi Christina Peter ambaye ni mzazi wa watoto hao kuwa alifika katika hoteli ya Ibanza Mei, 15 mwaka huu akiwa na watoto wa wanne kwa lengo la kupumzika. Bi Chritina ambaye ni mzazi wa watoto hao alieendelea kuwepo katika hoteli hiyo kwa takribani wiki mbili lakini baada ya hapo aliondoka bila taarifa na kuwatelekeza watoto wake katika hoteli hiyo. Tembelea http://jambotz8.blogspot.com/ kila siku.

Mmoja wa watoto hao aliyejitambulisha kwa jina la Teddy Masumbuko mwenye umri wa miaka 20 amesema kuwa anashangazwa na kitendo cha mama yao kuondoka bila kutoa taarifa huku akimuacha na wadogo zake watatu wenye umri mdogo. Msemaji wa hoteli hiyo bwana Julius Kiungu anawaomba ndugu, jamaa na marafiki wa familia hiyo wafike ili kuwachukuwa watoto hao kwa ulinzi na usalama wa watoto hao.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...