Saturday, August 17, 2013

WAISLAMU MSIKITI WA MTAMBANI 'WAMTEKA' ASKARI POLISI.... !!!


Baadhi ya waumini wa Kiislamu Msikiti wa Mtambani wakiwa wamemzunguka askari Polisi, Jonathan Tossi (katikati aliyeshika kamera) wakimuhoji baada ya kumshikilia kwa muda, hata hivyo walimuachia kwa masharti ya kumtaka afute picha zote alizopiga eneo hilo.
Askari Polisi wakizunguka doria eneo la Msikiti wa Mtambani jijini Dar es Salaam kuhakikisha kuna amani.
Askari wa Jeshi la Polisi, Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) wakizunguka kufanya doria maeneo mbalimbali ya jijini la Dar es Salaam kuhakikisha kuna amani. (Picha kwa hisani ya Gazeti la Jambo Leo.)

TAARIFA YA HARAKATI YA JUMUIYA NA TAASISI ZAKIISLAM TANZANIA KWA VYOMBO VYA HABARI..!!!


Bismillar Rahmanir Rahiim
JUMUIYA NA TAASISI ZA KIISLAM (T)
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI JUU YA KUCHUKULIWA NA POLISI SHEIKH PONDA ISSA PONDA TOKA HOSPITALI

Jana asubuhi majira ya saa nne na nusu askari wa jeshi la Polisi na watu wanaoaminika kuwa usalama wa taifa walikwenda hospitali ya Muhimbili (MOI) na kumchukua Sheikh Ponda Issa Ponda. Juhudi za Sheikh Mwenyewe, mkewe na waislam waliokuwepo pale hospitali kutaka abaki hospitalini kuendelea na matibabu hazikuzaa matunda. Mpaka Sasa bado tunafuatilia kujua mahali Kiongozi huyo wa Kiislam alikopelekwa.

Tumepokea kwa masikitiko makubwa sana habari hizi na tunashindwa kuamini kama mambo haya yanaweza kufanywa na Serikali inayodai kutawala kwa kufuata utawala bora unaojali sheria, uadilifu, utu na uhuru wa kujieleza.

Kitendo cha kumpiga risasi Sheikh Ponda na kisha kumchukua toka hospitalini na kumpeleka Gerezani kwa kukiuka taratibu ni kinyume cha haki za binadamu, utawala bora na uhuru wa maisha ya mtu. Matibabu ni haki mojawapo kwa binadamu yoyote hata kama kuna wanaomtuhumu. Tuhuma juu ya mtu si sababu ya kukiuka taratibu, kuvunja sheria na hata kumtisha unayemtuhumu kwani njia hiyo haiwezi kutatua tatizo bali inalifanya kuwa kubwa zaidi.

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI AGOSTI 17, 2013

.

.

MWAKYEMBE ATIMUA WOTE WALIOHUSIKA KUSINDIKIZA MSAFARA WA MADAWA YA KULEVYA KWENDA SAUZI AFRIKA

Waziri wa Uchukuzi,Mh.Dkt. Harison Mwakyembe akiongea na waandishi wa habari jana  ofisini kwake jijini Dares salaam juu ya hatua zilizochukuliwa na Wizara ya Uchukuzi juu ya sakata la madawa ya kulevya yaliyokamatwa huko Afrika Kusini hivi karibuni.Dkt. Mwakyembe amewafukuza kazi mtandao mzima uliohusika kusaidia kusafirisha madawa hayo, pia Waziri Mwakyembe ameliagiza jeshi la Polisi kuwakamata wafanyakazi hao na kuwaunganisha na wenzao kujibu mashitaka ya jinai.
Waziri wa Uchukuzi,Mh.Dkt. Harison Mwakyembe akionyesha picha ya Msanii Agness Gelard maarufu kwa jina la Masogange mbele ya waandishi wa habari,masogange alikamatwa na madawa ya kulevya huko nchini Afrika Kusini hivi karibuni.
waandishi wa habari wakimsikiliza kwa makini Waziri wa Uchukuzi akiwa anafafanua hatua zilizochukuliwa na Serikali kuushughulikia mtandao mzima uliosaidia kupitisha madawa ya kulevya.

ANGALIA PICHA ZA RAIS KIKWETE AKIWASILI NCHINI MALAWI JANA

8E9U4456 8E9U4461 8E9U4487 8E9U4488

WABUNGE 11 WA TANZANIA WANUSURIKA KIFO BAADA YA BUS WALILOKUWA WAKISAFIRI​A KUANZA KUUNGUA


wabunge wakoswa ca547
Wakati msafara wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu ukielekea Wilayani Missenyi kukagua sehemu utakapojengwa uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Omukajunguti, gari aina ya Costa lenye namba za usajili T 570 BYU lilowabeba Waheshimiwa Wabunge 11 lilipata hitilafu na kutaka kuungua.
P.T
wabunge tena 5ee72
Ajali hiyo ilitokea eneo la Mwanzo Mgumu kilometa moja kutoka mpakani mwa Wilaya ya Bukoba na Wilaya ya Missenyi ambapo gari hilo aina ya costa lilianza kutoa moshi mwingi kwa upande wa nyuma wakati likiwa kwenye mwendo mkali na kuleta hofu kubwa kwa abiria walikuwemo ndani ya gari hilo.

WAKILI WA PONDA ANENA JUU YA SHEIKH PONDA

Wakili wa Sheikh Ponda

Wakili wa Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Sheikh Ponda Issa Ponda (54) ambaye kwa sasa anakabiliwa na kesi mpya ya kufanya uchochezi katika maeneo mbalimbali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Nassor Jumaa, amesema kuwa amesikitishwa na hatua  ya vyombo vya dola kumuondoa Ponda aliyekuwa  amelazwa katika wodi ya Kitengo  cha Taasisi ya Tiba  ya Mifupa  na Upasuaji wa Mishipa ya Fahamu(MOI)  alikokuwa akipatiwa matibabu na kisha kumwamishia katika gereza la Segerea.


Wakili Jumaa alisema amesikitisha na kitendo hicho kwani hakimu Hellen Riwa juzi muda mfupi baada ya wakili mwandamizi wa serikali Tumaini Kweka kumaliza kumsomea shitaka Ponda, hakimu Liwa alitoa amri ya Ponda aendelee kukaa chini ya ulinzi lakini cha kushangaza leo,wanausalama wamemtoa wodini na kumpeleka katika gereza la Segerea na kwamba atalazimika kurudishwa tena mahakamani siku kesi yake itakapojatwa Agosti 28 mwaka huu, ambapo upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.

Thursday, August 15, 2013

WATUMIA MIFUKO YA RAMBO BADALA YA KONDOMU KWA WATAKAOPATA WANACHANGIA......!!!


KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida baadhi ya wananchi mk o a n i Ki l ima n j a r o , wamelazimika kutumia mifuko ya plastiki (malboro) kujikinga na maambukizo ya ugonjwa wa Ukimwi, huku wengine wakichangia kondomu, jambo ambalo ni hatari na linaelezewa kuwa moja ya chanzo cha ongezeko la maambukizo mapya ya ugonjwa huo mkoani humo.  

Takwimu zinaonesha kuwa kiwango cha maambukizo ya ugonjwa wa Ukimwikatika Mkoa wa Kilimanjaro, kimepanda kutoka asilimia 1.9 mwaka 2007/2008 hadi kufikia asilimia 3.8 mwaka 2011/2012. 
Akizungumza na gazeti hili ofisini kwake, Mkurugenzi Mtendaji wa shirika lisilokuwa la kiserikali, linalojihusisha na mapambano dhidi ya Ukimwi mkoani Kilimanjaro (KACA) Faraji Swai alisema wananchi wa maeneo ya vijijini wako hatarini zaidi kupata maambukizo ya ugonjwa ya ukimwikutokana na kwamba wengi bado hawajafikiwa. 

Alisema Shirika la Kacakatika utoaji elimu ya mapambano dhidi ya Ukimwi kwa jamii, wamefika katika baadhi ya vijiji mkoani Kilimanjaro na kuwakuta wananchi wakitumia mifuko ya plastiki (malboro) kama kinga ya kujikinga na maambukizo ya Ukimwihuku wengine wakichangia kondomu jambo ambalo liliwashangaza.

HIZI NDIZO NCHI 25 MASKINI ZAIDI DUNIANI

 
TAKWIMU za nchi masikini dunian,Tanzania mwaka 2010 ilishika nafasi ya tatu kwa umaskini duniani, lakini Tanzania kwa sasa imepiga hatua hata na kwenye 25 Tanzania haimo katika nafasi ya nchi masikini duniani.

BARNABA NA AMINI WALITAMBULISHA KUNDI LAO JIPYA LIITWAYO 'GEMENIH'


Wale wakali toka jumba la vipaji Tzee- THT walioishi kama pacha kwenye jumba hilo (Amini & Barnaba) wameungana na kuunda crew yao mpya kimziki iitwayo “GEMENIH” wakimaanisha wao ni kama mwezi na nyota angani. 
 
“Yap, Tumeungana kufanya kazi pamoja kama kundi nje ya THT tukiwa ni matunda ya THT na tumeamua kujiita hivyo kutokana na kutegemeana kwetu kwenye kazi na umuhimu wa uwepo wa kila mmoja kwenye mziki wa bongo kama umuhimu wa nyota na mwezi angani.” Barnaba alilidokeza BK. 
 
Kundi hilo kwa sasa lina-bang hewani na ngoma yao ya ‘Why me’ huku wakiwa na mipango mingi ya utendaji wao wa kazi kama Gemenih. Pia waliongeza kitu juu ya Gemenih na THT.
“Kikubwa ni kwamba, watu wasidhani tumetoka au tuna ugomvi na THT ila tumehitimu mafunzo pale na kutunukiwa vyeti nasi ni matunda ya THT na bado tunashirikiana nao kwa kuwapa ushauri hata kuwatungia nyimbo. Kwa ufupi tumewaachia wengine nafasibaada ya sisi kufuzu mafunzo pale.” Amini aliongeza. 
 
Gemenih ipo chini ya meneja aitwaye Moses Clemence ambaye ndiye ana-control mambo yote yahusuyo vijana hao.

HATARI!! MAGUNIA 405 YA BANGI YAKAMATWA KATIKA OPARESHENI YA KUSHITUKIZA ARUMERU, ARUSHA....!!!


Katika Operesheni ya Kuzuia Uhalifu na Madawa ya Jeshi la Polisi mkoa wa Arusha liliingia kijijini hapo majira ya saa 2 za asubuhi Agosti 13 mwaka huu.

Ilikuwa ni ziara ya kushtukiza katika kijiji hicho hali iliyowafanya wanakijiji kutaharuki na kuanza kukimbia na kutokomea milima wakiziacha nyumba zao zikiwa wazi.

Uongozi wa Kijiji hicho nao ulitoweka kusikojulikana kwa kuhofia mkono wa Jeshi la Polisi.
Kamishna wa Operesheni hiyo ACP Ngonyani alisema safari hii waliamua kwenda baada ya mavuno kutokana na ukweli kwamba zikiwa bado shamabni ni kazi nzito sana ya kufyeka.

POLISI WAMKAMATA ALIYEMUUA BILIONEA ERASTO MSUYA.....!!!


Polisi wamefanikiwa kumtia mbaroni mfanyabiashara tajiri wa madini ya Tanzanite huko Mirerani anayetajwa kuwa ndiye aliyepanga na kukodi watu waliomuua bilionea Erasto Msuya.

Habari za uhakika kutoka ndani ya Jeshi la Polisi zimedai kuwa mfanyabiashara huyo alikamatwa mwishoni mwa wiki na jana na juzi alikuwa akihojiwa na makachero.

Kwa mujibu wa vyanzo hivyo, mfanyabiashara huyo ndiye aliyetoa fedha za kununulia pikipiki mbili zilizotumika katika mpango huo na pia alitoa fedha kwa ajili ya kununua simu mpya na laini mpya.

“Tumewakamata watu wametupa mwanga mzuri na huyo mfanyabiashara ndiye aliyetoa fedha za kununua pikipiki na siku moja kabla ya tukio zilihifadhiwa nyumbani kwake,” alidokeza polisi mmoja.

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI AGOSTI 15, 2013.


.

.

HAYA NDIO MAPOKEZI YA FEZA KESSY UWANJA WA NDEGE DAR



Mwakilishi wa Tanzania katika jumba la Big Brother 'The Chase' aliyetolewa Jumapili Agosti 11 Feza Kessy amewasili leo jioni Tanzania katika uwanja wa kimataifa wa Mwl J.K Nyerere jijini Dar es Salaam.

Katika mapokezi watu mbalimbali walijitokeza kumpokea Feza Kessy akiwemo Vanessa Mdee,Mama mzazi wa Feza kessy,ndugu jamaa na marafiki pamoja na Meneja wa Uhusiano wa Multichoice Tanzania 'Barbara'.




MAJANGAAAAAAA... MTU NA MDOGO WAKE WAOANA HUKO BAGAMOYO....POLISI WAINGILIA KATI....!!!

MWANAFUNZI wa kidato cha pili jina kapuni (16), amejikuta akiozeshwa na wazazi wake kwa mwanaume aliyetambulika kwa jina la Kaizilege Jabiri (31) ambaye ni mtoto wa mama yake mkubwa...
Kaka mtu akitiwa mbaroni
Tukio hilo lilitokea Juni 14, mwaka huu jijini Dar nyumbani kwao Mlandizi, Bagamoyo, Pwani ambako mwanaume huyo alifunga ndoa na binti huyo na kurejea naye nyumbani kwake, Ubungo Kisiwani, Dar huku baadhi ya watu wakihofia uhai wa ndoa hiyo.

Baada ya kuanza maisha ya ndoa kama mke na mume, Agosti 6, mwaka huu taarifa zikafika kwenye Kituo cha Polisi cha Ubungo ambapo maafande walisema hiyo haiwezekani.
“Polisi walipopata habari walisema hakuna ndoa hapo, wakajipanga kwenda kuvamia nyumbani kwa wanandoa hao,” kilisema chanzo.
Dada  mtu akiwa ameshika tama.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...