Tuesday, July 09, 2013

MBONA MAJANGAAA....!!! AGNESS MASOGANGE AKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA AFRIKA KUSINI

 

HATIMAYE  wale Wanawake wawili walionaswa  na  madawa ya  kulevya  Afrika  kusini wametambuliwa kuwa  ni  mabinti  wa  KITANZANIA ..
Mabinti  hao  wanadaiwa kuingiza shehena ya dawa za kulevya zenye thamani ya zaidi ya Sh. bilioni 6.8 nchini Afrika Kusini wakitokea Tanzania.
Akizungumza na mwandishi wetu  jana, Kamanda wa Polisi Kitengo cha Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Geofrey Nzoa, alisema haijafahamika wanawake hao wanatoka mikoa gani.
Kamanda Nzoa aliwataja wanawake hao kuwa ni Agnes Jerald (MASOGANGE)  ambaye alisema hajapiga hesabu ya umri wao, ila alizaliwa mwaka 1988 kwa maana hiyo ana umri wa miaka 25 na Melisa Edward ambaye alisema amezaliwa mwaka 1989 kwa maana hiyo atakuwa na umri wa miaka 24. Wawili hao bado wanaendelea kuhojiwa na polisi wa Afrika Kusini.

CHELSEA WAANDAA DAU LA JUU ZAIDI KUMSAJILI ROONEY....!!!



Target: Chelsea are set to launch a bid for Wayne Rooney despite David Moyes saying he is not for saleAnasakwa vibaya sana: Chelsea wameamua kutuma ofa kwa David Moyes ingawa alitangaza kuwa hafanya biashara, lakini wakali hao wa darajani wanamhitaji jembe  Wayne Roonye

Will he stay or will he go? Rooney's future at Manchester United has been debated this summerAtabaki au ataondoka? Maisha ya baadaye ya Rooney katika klabu yake ya  Manchester United bado hayajulikani

New man in charge: David Moyes says he does not want to sell RooneyKocha mpya wa United: David Moyes amesema hamuuzi Rooney kwa sasa

Welcome back, Jose: Frank Lampard and John Terry will be pleased to see the return of Mourinho to Chelsea Karibu tena Jose: Malejendari, Frank Lampard na John Terry wamefurahi kuona ujio wa Mourinho katika klau yao ya Chelsea

WAKATI MZEE MANDELA AKIENDELEA KUPATA MATIBABU FAMILIA YAKE WAZIDI KUTIBUANA



Mandla Mandela aendelea kulikoroga
WAKATI mgogoro kati ya watoto wa Mandela na wajukuu ukizidi kutokota kuhusu uhalali wa uchifu wa Mandla Mandela, yeye amejibu mapigo akisema Mfalme Buyelekhaya Dalindyebo wa kabila la abaThembu ”hana akili timamu”.
Hiyo inatokana na madai yaliyotolewa na mfalme huyo kwamba Mandla hakuwa chifu sahihi wa ukoo wa Madiba. Alidai kwamba hakukuwa na cheti chochote halali kilichotiwa saini wakati mandla alipotawazwa kuwa chifu mwaka 2007 – sherehe ambazo zilisimamiwa na Mandela mwenyewe.
Gazeti la Mail & Guardian wiki iliyopita liliripoti kuwa uchifu wa Mandla ulilalamikiwa kabla ya Mandela kulazwa hospitalini, ikielezwa kama kweli anafaa kuendelea kuwa chofu ikizingatiwa kuwa mama na baba yake walimzaa bila kuoana.
Mgogoro unaoendelea hivi sasa kati ya Manla na shangazio yake, Makaziwe Mandela, na wanafamilia wengine unaonekana kama kichocheo kwa baadhi ya wanafamilia hiyo ambao wangetaka Mandla avuliwe uchifu.

WEMA SEPETU ANASAKWA NA POLISI BAADA YA KUMTUKANA MENEJA WA HOTELI WAKATI YUKO POMBE...!!!



Msanii wa filamu za Bongo ambaye pia ni Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu anasakwa na Jeshi la Polisi Kituo cha Kawe, Dar es Salaam kwa tuhuma za kufanya fujo hotelini, kumtukana matusi ya nguoni na kumpiga makofi meneja wa hoteli hiyo, Godluck Kuyumbu. Songombingo hilo lilijiri saa tano usiku wa Jumatano iliyopita kwenye hoteli hiyo  iliyopo Kawe Beach, jijini Dar. 
Akizungumza na mwandishi wetu , meneja huyo alisema siku ya tukio majira ya saa nane mchana, Wema alifika kwenye mgahawa wa hoteli hiyo akiwa ameongozana na marafiki zake wapatao kumi.


Meneja huyo akaendelea kusema, ilipofika  saa tano usiku, Wema na marafiki zake  walionekana kuzidiwa na kilevi, wakaanza kufanya fujo kwa kupiga kelele, kitendo kilichowakera wateja waliokuwa katika mgahawa huo, wengi wakiwa ni Wazungu ambao waliondoka kutokana na fujo hizo. 


Aliongeza kuwa mmoja wa marafiki wa Wema ambaye ilidaiwa ni mpenzi wake, aliyejulikana kwa jina moja la D, alichukua glasi na kuipasua chini kwa makusudi huku meneja huyo akishuhudia.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Akutana na Waandishi Wa Habari Nakutoa maamuzi ya Kamati ya Ushauri (RCC) ya kupeleka Makao makuu ya Mkoa mpya Mkwajuni Wilayani Chunya.


  
Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na Usalama Mkoa wa Mbeya, Abbasi Kandoro ambaye pia ndiye Mkuu wa Mkoa Mbeya akiongea na vyombo vya habari ofisini kwake.
 Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mbeya wakimsikiliza mkuu wa mkoa Mbeya akiongea na waandishi wa habari.Picha na Habari na Mdau Joseph Mwaisango
--
Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mbeya hatimaye yatoa ufafanuzi na kupigilia Msumari maamuzi ya Kamati ya Ushauri (RCC) ya kupeleka Makao makuu ya Mkoa mpya Mkwajuni Wilayani Chunya.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE JULAI 10, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

"NGUVU YA UMMA" INAVYOGHARIMU UHAI WA WAMISRI...!!!


 

Miili  ya wafuasi  wa Rais  aliyeondolewa madarakani nchini Misri ikiwa imehifadhiwa
 


 
MAAFISA wa Afya Misri wamesema takriban watu 42 wameuawa kwa kupigwa risasi mjini Cairo nje ya kambi ya kijeshi ambapo wafuasi wa Rais aliyeondolewa madarakani Mohammed Morsi walikua wamekusanyika na wanaamini anazuiliwa hapo. Watu wengine 300 wamejeruhiwa.

Kundi la Muslima Brotherhood limewataka raia wa Misri kuwapinga wale linawaita wanaopokonya raia uhuru na demokrasia.

Brotherhood imelaumu jeshi kwa kuwaua raia wake.
Katika kikao na waandishi wa habari, wafuasi hao walimlaani vikali mkuu wa jeshi Abdel Fattah Al-Sisi na kumtaja kama muuaji aliyewashambulia raia wenzake.

Haya yanajiri huku ghasia zikiendelea baada ya kuondolewa mamlakani kwa aliyekuwa rais Mohammed Morsi.

NDEGE YA RAIS WA SOMALIA 'YASHIKA MOTO'

somali f9f1f
Rais wa Somalia, Hassan Sheikh Mahamud
*******
NDEGE iliyokuwa inambeba rais wa Somalia, imelazimika kutua kwa dharura mjini Mogadishu baada ya moja ya mabawa yake kushika moto. (HM)
Msemaji wa Hassan Sheikh Mohamud, alisema kuwa haijulikani kwa nini injini ya ndege ilisita kufanya kazi.
 
Rais Hassan Sheikh Mohamud, alielezea kuwa rais hakujeruhiwa lakini wazima moto walifanya kila hali kuzima moto huo.
Bwana Mohamud alichaguliwa kama rais wa Somalia mwaka jana katika mpango ulioungwa mkono na Umoja wa Mataifa, katika hatua za kumaliza vita vya miaka mingi.
Mwandishi wa BBC Mohamed Mwalimu, alisema kuwa magurugumu ya ndege yaliharibiwa vibaya baada ya tukio hilo.

Rais alikuwa anaelekea katika mji mkuu wa Sudan Kusini, Juba, wakati ndege hiyo ilipolazimika kurejea Mogadishu.
Moja ya ripoti zilizotolewa za mwanzo kuhusu tukio hilo, ilitoka kwa akaunti ya Twitter ya kundi la al-Shabab lakini haikusema kama imeshambulia ndege hiyo.

 
Wanajeshi wa Muungano wa Afrika pamoja na wale wa Somalia, wanaounga mkono bwana Mohamud wamewaondoa wapiganaji wa al-Shabab kutoka mji mkuu Mogadishu, mwaka jana ingawa kundi hilo bado hufanya mashambulizi ya mara kwa mara ya kuvizia.
Serikali mpya ni ya kwanza kwa zaidi ya miaka 10 kutambuliwa na serikali ya Marekani na shirika la fedha duniani (IMF). 

Chanzo: bbcswahili

HILI NDILO GHETTO LA DIAMOND THE PLATNUMZ...!!!

Photo by diamondplatnumz
Photo by diamondplatnumz


Monday, July 08, 2013

RAIS WA ZANZIBAR DK. ALI MOHAMED SHEIN AWAASA WAISLAMU NCHINI

 

Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein amewataka Waislamu wote nchini kuishi na Watanzania wenzao katika misingi ya kuheshimiana, kuvumiliana na kupendana, kama Uislamu ulivyofundisha.

Dk Shein aliyasema hayo jana katika ufunguzi wa msikiti wa Masjid Taqwa, uliopo Ilala Bungoni, jijini Dar es Salaam, katika hotuba ilyosomwa kwa niaba yake na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Mwinyihaji MakameKatika hotuba hiyo ya ufunguzi wa msikiti huo, Dk Shein alisema kuwa ni wajibu kwa Waislamu kufanya kila jitihada katika kuilinda amani na utulivu alioubariki Mwenyezi Mungu hapa Tanzania. 

Alisema kuwa kuna kila sababu kwa Waislamu kumshukuru Mwenyezi Mungu kwamba wanaweza kufanya ibada zao katika mkusanyiko mkubwa kama huo wa ufunguzi wa msikiti bila ya hofu, woga wala bughudha ya namna yoyote.Dk Shein alipongeza jitihada zinazochukuliwa na wasimamizi wa msikiti huo katika kuimarisha na kuitunza historia yake tangu ulipoanzishwa mnamo mwaka 1927, ambapo historia hiyo inadhihirisha kuwa msikiti huo ni miongoni mwa misikiti mikongwe katika Jiji la Dar es Salaam.

MKE WA RAIS MSTAAFU BENJAMIN MKAPA, MAMA ANNA MKAPA AMETENGWA...!!!

MAMA ANNA MKAPA.

MKUTANO wa wake za marais uliofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi wazito, akiwemo Rais wa zamani wa Marekani, George W. Bush na Mkewe, Laura, umeacha kitendawili kizito kuhusu mke wa Rais wa zamani, Benjamin Mkapa, Mama Anna Mkapa. Imebainika kuwa katika mkutano huo, ambao mke wa Rais Jakaya Kikwete, Salma alikuwa ni mwenyeji wao, Mama Anna Mkapa hakuhudhuria, lakini pia imeonyesha wazi kwamba hakupewa fursa kulingana na hadhi yake. 

Mkutano huo wa Kimataifa ulifanyika katika Hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam, Juni 2-3 mwaka huu, uliozungumzia nafasi ya wanawake kuinuka kimaendeleo, ukizihusisha taasisi zinazoendeshwa na wake wa marais, wakiwemo wale wastaafu.



HAKEEM NA FATIMA WAAGA SHINDANO LA BBA USIKU WA LEO; MWANAMZIKI WA KIBONGO ATUMBUIZA

 Ikiwa leo ni siku ya 42 ndani ya jumba la BBA,kama inavyokuwaga siku zote kila jumapili huwa ni eviction day yaan lazma mshirik hata mmoja aage mashindano
Mwanadada Fatima kutoka Malawi ndiye aliyekuwa wa kwanza kuaga mashindano ya BBA kwa usiku wa leo.Mshiriki mwenzake kutoka Malawi  Natasha hakuamini kilichotea na kuanza kulia huku Fatima akimwambia Natasha  "No drama, no drama. It's not about you, chill out "kasha akaagana na wenziwe na kutoka nje ya jumba la BBA. 
  Hakeem kutokea nchini Zimbabwe nae ameyaaga mashindano usiku wa leo huku akiwa haamini kabisa kile kilichotokea kutokana na utani aliokuwa akiwatania wenzake kwamba wanatoka leo.Na cha zaidi amemuacha mchumba wake CLEO katika wakat wa majonzi.
 .Usiku wa leo ndania ya BBA ulipambwa na msanii mahiri kutoka TANZANIA aitwaye WAKAZI aliyeimba nyimbo zake WEEKEND na TOUCH.
Live Show: Wakazi sizzles on stage

HIZI NDIYO SABABU ZA MH ZITTO KABWE KUTOSHIRIKI TAMASHA LA MATUMAINI


Kupitia account yake ya facebook Mh. Zitto Kabwe amepost hotuba hii akielezea kushindwa kwake kufika katika tamasha la siku ya matumaini.
POST YAKE AMEANZA KWA KUANDIKA HIVI.

Global Publishers leo 7.7.2013 waliandaa Tamasha la Matumaini. Bahati mbaya sana sikuweza kuwahi kutokana na safari nilizonazo. Hii ni hotuba niliyopanga kuitoa na kuwatumia waandaaji.


TAMASHA LA MATUMAINI

Leo nilikuwa niwe nanyi kwa ajili ya siku hii muhimu sana kwa nchi yetu, siku ya matumaini kama inavyoandaliwa na Kampuni ya Global Publishers. Napenda kutoa shukrani zangu za dhati kabisa kwa ndugu yangu Erick Shigongo kwa kuandaa tamasha hili kila mwaka. Nasikitika kuwa sitaweza kufanya pambano la ngumi na ndugu Ray na pia kuchezea timu yangu ya Wabunge wa Simba dhidi ya watani zetu Yanga. Hata hivyo naamini kuwa tamasha litakuwa na mafanikio makubwa na nipo nanyi japo sipo Dar es Salaam.


Ilikuwa niwepo Dar es Salaam leo, lakini nimeshindwa kuondoka Marekani kwa sababu Spika wa Bunge Mama Anna Makinda ameniagiza kwenye safari nyingine ndefu kwenda visiwa vya Cayman na baadaye Namibia kwa shughuli za Umoja wa Wabunge wa Jumuiya ya Madola. Sikuweza kukwepa jukumu hili la kitaifa maana limekuja ghafla na mimi nipo huku jirani na maeneo hayo. Naomba radhi sana kwamba sipo nanyi leo.

Sunday, July 07, 2013

BABU CHA MIAKA 92 AFUNGA NDOA NA BINTI ALIYEMZIDI MIAKA 70...!!!

 
Musali Mohammed al-Mujamaie (kulia) akiwa na mkewe, Muna Mukhlif al-Juburi.
Mkulima mmoja nchini Irak mwenye miaka 92 amemuoa mwanamke waliyetofautiana miaka 70 katika ndoa tatu kwa mpigo sambamba na wajukuu zake wa kiume wawili.

Musali Mohammed al-Mujamaie alimuoa mke mwenye umri wa miaka 22, Muna Mukhlif al-Juburi katika sherehe iliyodumu kwa masaa manne.

Wajukuu zake wa kiume, wenye umri wa miaka 16 na 17, nao walifunga ndoa kwenye sherehe hiyo iliyofanyika kaskazini mwa Baghdad Alhamisi iliyopita, kwa mujibu wa ripoti.

Mzee Mujamaie alisema kwenye siku hiyo maalum alikuwa akisubiria kwa muda mrefu kutokana na harusi za wajukuu zake kuwa zinaahirishwa mara kadhaa ili aweze kuunganisha na sherehe yake.

TBS YAPIGA MARUFUKU UUZWAJI WA MAFUTA YA KUPIKIA YA 'OKI'.....WADAI YANA MADHARA KIAFYA.

http://www.ippmedia.com/media/picture/large/OKI.jpg 
Shirika la Viwango Tanzania (TBS), limebaini kuwa mafuta ya kula aina ya Oki na Viking yaliyoenea sokoni nchini, yamebainika kuwa hayafai kwa matumizi ya binadamu.
Kwa mujibu wa TBS, vipimo vyote vitatu vilivyotumika kuyapima kuonyesha ubora, vimefeli na vimeonyesha mafuta hayo kuharibika kwa haraka tangu yalipotengenezwa na mpaka leo.
Pamoja na Oki, mafuta mengine yenye walakini ni Asma, Vikingi, Partiner na Premier Gold ambayo huuzwa kwa dumu lenye ujazo wa lita 20 kwa bei ya kuanzia Sh 38,000 hadi 45,000, wakati bei ya mafuta ya kula yanayotengenezwa nchini kwa ujazo huo huuzwa kati ya Sh. 52,000 na Sh.55,000.

Baada ya kupimwa, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Udhibiti Ubora TBS, Lazaro Msasalaga, anasema ilithibitika kuwa mafuta ya Oki yanayozalishwa Malaysia na kupakiwa Singapore hayana ubora.
Alisema mafuta hayo yametengenezwa 2011 na kuonyesha mwisho wa kutumika ni Oktoba mwaka huu. Msasalaga alisema walipoyachunguza wamebaini hayana namba ya ufuatiliaji wakati suala hilo ni la muhimu kuwekwa.
Isitoshe, wawalipoyapima kutoka kipimo kimoja kwenda kingine, majibu yake yalishindwa na kuzidi kuonyesha mafuta hayo kuharibika kila walipoyapima.
Alisema kuna vipimo vya maabara ukipima vinaeleza mafuta kama yanafaa kutumika lakini kipimo hicho hakikufanikiwa.NA TALK BONGO

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...