Sunday, July 07, 2013

TBS YAPIGA MARUFUKU UUZWAJI WA MAFUTA YA KUPIKIA YA 'OKI'.....WADAI YANA MADHARA KIAFYA.

http://www.ippmedia.com/media/picture/large/OKI.jpg 
Shirika la Viwango Tanzania (TBS), limebaini kuwa mafuta ya kula aina ya Oki na Viking yaliyoenea sokoni nchini, yamebainika kuwa hayafai kwa matumizi ya binadamu.
Kwa mujibu wa TBS, vipimo vyote vitatu vilivyotumika kuyapima kuonyesha ubora, vimefeli na vimeonyesha mafuta hayo kuharibika kwa haraka tangu yalipotengenezwa na mpaka leo.
Pamoja na Oki, mafuta mengine yenye walakini ni Asma, Vikingi, Partiner na Premier Gold ambayo huuzwa kwa dumu lenye ujazo wa lita 20 kwa bei ya kuanzia Sh 38,000 hadi 45,000, wakati bei ya mafuta ya kula yanayotengenezwa nchini kwa ujazo huo huuzwa kati ya Sh. 52,000 na Sh.55,000.

Baada ya kupimwa, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Udhibiti Ubora TBS, Lazaro Msasalaga, anasema ilithibitika kuwa mafuta ya Oki yanayozalishwa Malaysia na kupakiwa Singapore hayana ubora.
Alisema mafuta hayo yametengenezwa 2011 na kuonyesha mwisho wa kutumika ni Oktoba mwaka huu. Msasalaga alisema walipoyachunguza wamebaini hayana namba ya ufuatiliaji wakati suala hilo ni la muhimu kuwekwa.
Isitoshe, wawalipoyapima kutoka kipimo kimoja kwenda kingine, majibu yake yalishindwa na kuzidi kuonyesha mafuta hayo kuharibika kila walipoyapima.
Alisema kuna vipimo vya maabara ukipima vinaeleza mafuta kama yanafaa kutumika lakini kipimo hicho hakikufanikiwa.NA TALK BONGO

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...