Sunday, June 23, 2013

The Finest : FA apata wakati mgumu kwa kulazimishwa na mashabiki kutaja jina la Lady Jay Dee.

Mwanamuziki Hamis Mwinjuma, maarufu Mwana FA, amepata wakati mgumu kwa kulazimishwa na mashabiki kutaja jina la Lady Jay Dee, baada ya kuliruka jina hilo alipokuwa akiimba wimbo wa Mabinti ambao ndani yake kuna jina la Jay Dee.
 
Tofauti na ilivyozooeleka katika wimbo wa Mabinti, kwa mara ya kwanza Mwana FA aliruka jina la mwanamuziki Lady Jay Dee ‘Anaconda’, hali iliyowafanya mashabiki wamtake arudie tena na kutenda haki.

Mwana FA alisita kwa muda na baadaye aliamua kurudia wimbo huo na alipofika katika kipengele cha kumtaja Jide aliimba kwa kumtaja, hali iliyoufanya ukumbi huo ulipuke kwa shangwe na mashabiki kumtaka arudie tena na tena.

Kutokana na hilo FA aliamua kufunguka; “Tunaishi na watu hivyo lazima mtagongana, hata mapacha wanakosana na kusameheana, lakini wakati mwingine shida inawafanya mnapatana,” alisema Mwana FA.
Awali shoo ilitangazwa kuwa ingekuwa ya watu 400 tu. Lakini mpaka inafika saa nne kasoro usiku, muda uliotangazwa kuanzwa kwa shoo hiyo watu waliokuwa wamefika walikuwa kama 250 tu.
Saa nne kamili mwanamuziki Hamis Mwinjuma, Mwana FA alikanyaga ‘red carpet’ akiwa na mbunifu wa mavazi Sheria Ngowi, na baada ya kuchukuliwa picha kadhaa alianza kuelekea nje ya ukumbi sehemu waliyosimama watu wakipata chakula na vinywaji, watu walizidi kufurika lakini kila aliyeingia alikuwa alwatan kidogo.

Waliendelea kuwasili mastaa na shoo inaanza Mashabiki wanaanza kuingia ukumbini saa tano kamili baada ya kupata vyakula na vinywaji nje, huku muziki wa taratibu ukipigwa na bendi ya muziki wa dansi ya Njenje. Mashabiki wanaendelea kubadilishana mawazo mpaka inapotimu saa tano na robo usiku, ambapo Mwana FA anapanda jukwaani.

Anaanza kazi kwa shoo ya aina yake baada ya kuimba hip hop live akiwa na bendi ya muziki wa dansi, kwenye shoo hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam.
FA alipanda jukwaani na wimbo wa Binamu akisindikizwa na wanamuziki Mandojo na Domokaya waliovalia suruali nyeusi na mashati meupe huku wakiwa wamevalia mikanda aina ya ‘suspender’, baadaye aliimba wimbo Unanijua Unaniskia na Bado Niponipo Kwanza ambao uliwapendeza mashabiki.

Alisimamisha shoo kwa muda na msanii Bernald Paul maarufu kama Benpol alipanda jukwaani na kuimba nyimbo zake tatu kwa kuziunganisha ukiwamo wa Maneno, Pete na Nikikupata na baadaye aliimba na Mwana FA wimbo wa Asubuhi aliomshirikisha Q Chief.
FA alipanda jukwaani na wanamuziki kadhaa katika vipindi tofauti akiwamo Linah Sanga ‘Linah’, Maua, Abdul Sykes ‘Dully Sykes’.
Baadhi ya nyimbo alizoimba ni pamoja na Kama Zamani, Alikufa kwa Ngoma, Habari Ndio Hiyo, Leo, Mabinti, Unanitega, Yalaiti na nyingine nyingi.

HII NDIO HALI YA MSANII BARNABAS TANGU KUPOKEA TAARIFA ZA MSIBA WA MAMA YAKE



Kiukweli inasikitisha sana tangu asubuhi hajatia kitu chochote tumboni analia ananyamaza,akipewa chakula hakitaki.mungu mjalie ndugu yetu mpe nguvu aweze kumzika mama yake kwa aman na upendo.







R.i.P mamaa BARNABAS, Maziko ni leo saa 10 katika makaburi ya mburahati,kuanzia asubuhi saa 5 tutakuwa na misa maalum kwa ajili ya marehemu mama barnabas.

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JUNI 23, 2013

DSC 0019 578e1

DSC 0022 d20cc
DSC 0023 43257

ASKOFU AITAKA SERIKALI KUWABANA WASIOTAKA NCHI ITAWALIKE.

RAIS Jakaya Kiwete akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa serikali na dini wakati alipohudhuria sherehe za miaka 25 ya Askofu wa jimbo kuu la Morogoro Telesphol Mkude wa pili kulia kwa rais katika viwanja vya shule ya ST Peter mkoani Morogoro jana.


SIKU chache baada ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kutaka Serikali iachwe ifanye kazi yake katika kudhibiti vurugu zinazoibuka kila kukicha, Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro, Mhashamu Telesphor Mkude naye ameitaka Serikali kuwadhibiti wote wasiotaka nchi itawalike.Askofu huyo amesema kuonya pekee hakusaidii, bali inawajibu wa kuwachukulia hatua kali ili kukomesha vitendo vinavyotishia amani nchini.Askofu Mkude aliyasema hayo jana wakati wa maadhimisho ya Jubilei ya miaka 25 ya uaskofu wake kwenye viwanja vya Seminari ya Mtakatifu Petro mjini hapa ambapo Rais Jakaya Kikwete alikuwa miongoni mwa wageni mashuhuri waliohudhuria.

RIHANNA AMPIGA SHABIKI WAKE NA KIPAZA SAUTA BAADA YA SHABAKI HUYO KUMKERA...!!!


MWIMBAJI nyota wa muziki wa R&B, Robyn Rihanna Fenty, anayefahamika zaidi kwa jina  la Rihanna, amenaswa na kamera akimpiga shabiki ‘mic’ usoni alipokuwa akifanya shoo huko Birmingham, Uingereza Jumatatu iliyopita.

Rihanna alifanya tukio hilo la kushtua alipojichanganya kwenye umati wa mashabiki, huku akiimba kwenye shoo hiyo ambayo ni sehemu ya ziara yake ya dunia inayojulikana kama ‘Diamond World Tour’ akiitangaza albamu yake ya saba ya ‘Unapologetic’ iliyotoka mwaka jana.

Ilidaiwa kuwa Rihanna mwenye umri wa miaka 25 alishindwa kudhibiti hasira zake baada ya shabiki huyo asiyefahamika kumng’ang’ania mkono wake.

Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo aliandika kwenye ukurusa wake wa Twitter: "Rihanna amempiga mtu mmoja na mic yake katika ajali haha oops."

Na Rihanna alijibu akisema kuwa alikusudia kumpiga shabiki huyo kwa sababu alikuwa akimzuia.

TAMASHA LA KILI MUSIC AWARDS NDANI YA UWANJA WA JAMHURI DODOMA.....OMMY DIMPOZ APIGWA CHUPA NA MASHABIKI JUKWAANI..!!

Ommy dimpoz arushiwa chupa na mawe jukwaaani dodoma na kushindwa kufanya show ya kilimanjaro muzik award dodoma. Wadau wa dom wasema kamwe msanii yoyote atakaye mdisi msanii wa dodoma awatamkubari kufanya show dom na watamshusha jukwaani kama walivyo fanya leo

 Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya,Linex akiwasalimia mashabiki na wapenzi wa Muziki waliofurika kwa wingi ndani ya Uwanja wa Jamhuri Mjini Dodoma leo,ambapo usiku huu kulikuwa na bonge moja la Show ya Kilimanjaro Tanzania Music Tour 2013.




 Msanii Ben Pol akighani moja ya nyimbo zake.

 

POLISI 7 WAFUNGWA JELA MIAKA 5 KWA KOSA LA MAUAJI HUKO KIGOMA

 

MAHAKAMA Kuu ya Tanzania Kanda ya Tabora imewahukumu kifungo cha miaka mitano jela askari saba wa Jeshi la Polisi mkoani Kigoma ambao walikuwa wakishtakiwa kwa mauaji.

Akitoa hukumu yake katika kikao cha Mahakama Kuu kilichokuwa kikifanyika mkoani Kigoma Jaji wa mahakama hiyo, Sam Mpaya Rumanyika alisema kuwa baada ya kupitia ushahidi mbalimbali Mahakama hiyo imewatia hatiani askari hao kwa kosa la kuua bila kukusudia.
Katika kesi hiyo namba 35 ya mwaka 2012 washitakiwa hao walifikishwa mahakamani hapo na kusomewa shitaka la kumuua Festo Stephano, mkulima wa kijiji cha Rungwe Mpya Wilaya ya Kasulu mkoani hapa katika tukio lililotokea Agosti 6, mwaka 2011.

Askari hao waliohukumiwa ni pamoja na Baraka Hongdi, Koplo Mawazo, Koplo Swahib, D/C Charles, D/C Shamsi, D/C Jerry na D/C Amrani ambao kwa pamoja walikana shitaka lao katika kesi hiyo namba 35 ya mwaka 2012.
Akitoa utetezi kabla ya hukumu hiyo wakili wa washitakiwa, Method Kabuguzi aliiomba Mahakama kuwafutia shitaka washitakiwa hao na kuwaachia huru kwani wote bado vijana na wameoa hivi karibuni.
Sambamba na hilo Kabuguzi alisema kuwa askari hao walikumbwa na mkasa huo wakati wakitekeleza jukumu lao la ulinzi wa taifa ambapo walimkamata mtuhumiwa wa kutumia silaha na ndipo kifo kikatokea wakati wakitekeleza majukumu yao.

Source: http://www.wavuti.com

AMANDA APIMA NGOMA, PRESHA YAPANDA YASHUKA

Stori:Gladness Mallya
MSANII wa filamu za Kibongo, Tamrina Poshi ‘Amanda’ hivi karibuni alijikuta akipandwa na kushukwa na presha  mara baada ya kwenda hospitali kupimwa Ugonjwa wa Ukimwi.Kikizungumza na Exclusive chanzo makini ambacho kilishuhudia tukio zima katika Hospitali ya Dokta Mvungi, Kinondoni, jijini Dar kilisema baada ya Amanda kupewa majibu ya vipimo na daktari, alianza kuhaha huku na kule kama mtu aliyechanganyikiwa, kisha presha ikampanda baadaye ikashuka.
Baada ya kuzinyaka habari hizo, paparazi wetu alimtafuta Amanda na kumuuliza juu ya tukio hilo ambapo bila hiyana alitiririka:
“Ile ilikuwa ni mara ya tatu kupima ngoma yaani wakati nikisubiri majibu, presha ilipanda ghafla mpaka daktari akawa na wakati mgumu wa kunipa majibu.



“Nilienda kuchukua majibu na sikutaka kuyaangalia, nilimpelekea daktari ambaye aliniambia niko safi yaani sikuamini nilitoka nikiwa naongea peke yangu, nilikuwa sijiamini si unajua tena ujana ni maji ya moto sasa presha ,” alisema Amanda.

Saturday, June 22, 2013

HATIMAE NDUGU YETU MPENDWA CHARLES HILILA AZIKWA LEO KIJIJINI KWAO



 

 NYUMBA YA MILELE ALIMOLALA MWANDISHI WA HABARI KITUO CHA MATANGAZO CHA CHANELL TEN

Habari Na Steven Kanyeph
Mwili wa aliyekuwa mwandishi wa habari wa chaneli ten Charles hilila umezikwa leo katika makaburi ya nyumbani kwao katika kijiji cha Dumida kata ya Tinde mkoani Shinyanga nakuhudhuriwa na mamia ya waombolezaji akiwemo mkuu wa mkoa wa shinyanga na viongozi wengine wa kiserikali , vyama vya siasa pamoja na viongozi wa kidini.

Mazishi hayo yametanguliwa na ibada ya misa takatifu iliofanyika katika kanisa la mama mwenye huruma Ngokolo mjini Shinyangsa na baade kufuatiwa na ibada ya mazishi iliyofanyika nyumbani kwao na kuongozwa na padre Emmanueli Makolo akisaidiana na padri Josephati Mahalu kabla ya maziko.
katika mahubiri padre Mahalu amewaasa wanajamii kudumisha upendo na kuwakumbusha kuwa kifo kipo mahali popote hivyo wanajamii wanapaswa kumrudia Mungu na kutenda matendo mazuri yenye kuleta amani na yanayompendeza Mungu.


Hali kadhalika mkuu wa mkoa wa Shinyanga Alli Nassoro Lufunga ametoa salamu za rambirambi kutoka katika serikali ya mkoa na kuwaomba wanahabari kudumisha upendo zaidi hasa katika umojawao kwani utawasaidia kufanya kazi kwa weledi na kuleta tija zaidi kwa wanajamii.
Marehemu Charles hilila amefariki juni 19 katika hospitali ya mkoa wa Shinyanga alipokuwa amelazwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa TB ya mifupa uliokuwa unamsumbua .
Aidha marehemu ameacha mjane na watoto watatu ,
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema mbinguni amina

*********************************************************************************


 

MEYA AZIMIA BAADA YA KUPIGWA NA POLISI

Meya wa Mji Mkuu wa Kampala nchini Uganda akiwa chini ya ulinzi wa polisi baada ya kukamatwa kwa tuhumza za kusababisha vurugu.

Kampala, Uganda. Watu wawili wameuawa kwa risasi nchini Uganda juzi, wakiwa katika mkusanyiko kwenye eneo la soko la Kisekka.

Meya wa mji mkuu wa Uganda, Kampala, Erias Lukwago, pia alizirai baada ya kupigwa na polisi hao waliofyatua risasi za mipira kuutawanya umati wa wafuasi wake.

Akiwa kitandani, Meya huyo amesema baada ya kupata kipigo hicho alipoteza fahamu na kukimbizwa hospitalini.

“Bomu ambalo lilinifanya nipoteze fahamu lilirushwa katika gari langu na kuingia ndani,” amesema.


Meya huyo ni mpinzani wa rais wa nchi hiyo, Yoweri Museveni, alieleza kwamba maofisa wa polisi walimpiga kifuani na kuzirarua nguo zake wakimtuhumu kwa kuchochea ghasia. 

NKAMIA AZUA VURUGU TENA BUNGENI SAFARI HII ATAKA KUMPIGA MBUNGE MWENZAKE...!!!

1625 cb219Mbunge wa Kondoa Kusini, Juma Nkamia (CCM), kwa mara nyingine ameingia katika kashfa nzito akituhumiwa kutaka kumpiga Mbunge wa Viti Maalumu CUF, Moza Abeid ndani ya Ukumbi wa Bunge.

Tukio hilo lilitokea mwanzoni mwa wiki ambapo imeelezwa kuwa Nkamia mbali na kutaka kumpiga mbunge huyo, pia alimtolea matusi mazito ya nguoni (gazeti hili haliwezi kuandika).

Kwa mara ya kwanza mbunge huyo aliingia katika kashfa baada ya kutoa kauli bungeni kuwa hazungumzi na mbwa, bali anazungumza na mwenye mbwa kabla ya kuingia katika mzozo na wahariri na baraza la habari aliposema kuwa Jukwaa la Wahariri na Baraza la Habari ni NGOs za kutafuta fedha.

Uchunguzi wa Mwananchi ambao umethibitishwa na Nkamia mwenyewe umebaini kuwa chanzo cha tukio hilo ni kutokana na kuzomewa kwa Nkamia katika kampeni za uchaguzi mdogo Kata ya Dalai Wilaya ya Chemba.

Kwa mujibu wa wabunge mashuhuda ambao waliliona tukio hilo, ilielezwa kuwa Nkamia, ambaye pia ni mwandishi wa habari, alianza kumshushia matusi Moza wakiwa ndani ya Bunge hadi walipotoka nje alimfuata na kutaka kumpiga.

MCHUNGAJI AZAA NA HAUSIGELI WA MIAKA 17 HUKO KIMARA....AVULIWA UCHUNGAJI, MKEWE AOMBA TALAKA...!!!

HAYA ni madai mazito! Mchungaji wa Kanisa la Kiroho la Kijito cha Utakaso au Healing Centre International lililopo Kimara-Mwisho, Dar, Thomas Mariki anadaiwa kuvuliwa kofia ya uchungaji baada ya kutuhumiwa kuzaa na ‘hausigeli’ wake, Sessy Mwambashi.

Akizungumza nasi Jumamosi kwa masikitiko, mke wa ndoa wa Mariki, Joyce Thomas Mariki alidai kuwa yeye na mchungaji huyo walioana mwaka 2004 katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Lungai Mwika, Moshi.
Alisema walijaliwa kupata watoto watatu lakini mmoja hakuwa bahati.


MATESO YAANZA
Mwanamke huyo alidai amani katika ndoa yake ilipotea baada ya kujifungua mtoto wa pili (marehemu), mumewe alianza kumtuhumu kuwa alitoka nje ya ndoa na huyo mtoto hakuwa wake.

MIMBA YA PENNY YACHOROPOKA..... PENZI LAKE NA DIAMOND LAKAA PABAYA...!!!

TAARIFA ya ndani zinazodai kwamba, mimba ya mchumba wa Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Nassibu Abdul ‘Diamond’, Peniel Mgilwa ‘Penny’ imechoropoka zimevujaKwa mujibu wa chanzo makini kilichojitambulisha kwa jina la wifi (jina kapuni) kwa Penny, ni kwamba mtangazaji huyo wa Runinga ya Channel 10 cha jijini Dar hivi sasa  hana ujauzito tena kama wengi wanavyodhani.
“Penny hana mimba jamani, yupo fiti kabisa na sidhani hata kama anatarajia kushika ujauzito leo wala kesho,” kilisema chanzo hicho.
 
Hata hivyo, wifi huyo alisema kwamba awali kulikuwa na dalili zilizoonesha kwamba Penny alikuwa ni mjamzito kutokana na mtangazaji huyo kutumia vitu vichachu kama vile maembe na mara kwa mara alikuwa akiumwa hadi kufikia kulazwa hospitali.
Inadaiwa kwamba Penny alipotoka hospitali alionekana kuwa fiti zaidi na hakuwa na dalili zozote za kuwa na ujauzito kama ilivyokuwa siku za nyuma.
Baada ya gazeti hili kupata habari hizo lililimpigia simu Penny ili kuthibitisha madai hayo:
Mwandishi: Mambo vipi, Penny pole sana.
Penny: Pole ya nini sasa?
Mwandishi: Si nimesikia kwamba unaumwa jamani na ukakumbwa na mkasa mwingine?
Penny: Mkasa gani huo unaousema maana mimi niko fiti tu.
Mwandishi: Nilisikia kwamba baada ya kuumwa na kulazwa hopsitali mimba yako ikatoka?
Penny: (Kimya kwa dakika 3) Asante ni mipango ya Mungu.
Mwandishi: Sasa unatarajia lini utapata tena mimba nyingine?
Penny :(Kwachuuuuuu). Simu ilikatwa na hata ilipokuwa ikipigwa tena haikuwa ikipokelewa.

ANGALIA PICHA ZA BOB JUNIOR AKIPEWA KICHAPO LOCATION...!!!


Bob Junior ameshare picha hizi kwenye ukurasa wake wa Facebook na kuandika: Kwa Dizaini hii lazima nirudi kwetu k…Aaaaah Maisha Haya Ya Bongo?,,,,COMING SOON Huu Mzigo…1 Love.


Bob Junior akiwa location kushoot video yake mpya, duuuuuuh...!!! kaaazi kweli kwelii

BOMU LA ARUSHA LAWATESA CCM, POLISI.

 
IGP SAIDI MWEMA. 
KATIBU MKUU MPYA WA CCM ABDULRAHMAN KINANA.

MLIPUKO wa bomu uliotokea wiki iliyopita katika mkutano wa kufunga kampeni za udiwani kwa CHADEMA mkoani Arusha na kuua watu wanne, umeiweka kwenye wakati mgumu serikali ya CCM, Jeshi la Polisi na Bunge.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alisema juzi bomu lililolipuliwa katika mkutano wa CHADEMA ni la kijeshi na limetengenezwa China na uzoefu unaonesha hutumiwa na wanajeshi kujihami wakiwa katika makabiliano na maadui vitani.

Wakati Pinda akitoa kauli hiyo bungeni, viongozi wa CHADEMA wamelihusisha Jeshi la Polisi na tukio hilo huku wakidai wanao ushahidi unaon
esha askari aliyevalia sare akilirusha kwenye mkutano huo.
Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kijamii, wamelidokeza Tanzania Daima kuwa kukiri kwa serikali kuwa bomu hilo limetengenezwa China, inapaswa iibane nchi hiyo ieleze iliyemuuzia na alivyoliingiza nchini.

“Kwanini isiundwe tume huru nchini ili nchi ya China iulizwe baada ya kutengeneza bomu hilo ilimuuzia nani? Na kama haikuiuzia serikali, basi ni dhahiri tuiulize China kwanini inafadhili vikundi vya kigaidi nchini kwetu ?.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...