Thursday, June 13, 2013

KAULI YA BALOZI WA TANZANIA KUHUSU MSICHANA ANAYEDAIWA KUTAKA KUNYONGWA BAADA YA KUKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA EGYPT

.
Baada ya watu wengi kuzipata habari na bila kujua imekuaje kwa Mtanzania anaedaiwa kukamatwa na dawa za kulevya nchini Egypt na kwamba alikua anakaribia kunyongwa, balozi Mohamed Haji wa Tanzania nchini Egypt ameongea Exclusive na millardayo.com na kueleza yote anayoyafahamu kuhusu hii ishu. Namkariri akizungumza 1. Ni kweli kuna raia wawili Watanzania wamekamatwa na dawa za kulevya ambao ni Mbarak Abdallah Salim (28) na Sharifa Mahmud (27) wakazi wa Magomeni Kagera Dar es salaam, wanaundugu wa mtoto wa shangazi na mjomba. 2. Walikamatwa tarehe 16 May 2013 wakati wakiingia Misri, kwa mujibu wa maelezo safari yao ilianzia Dar es salaam kwenda Mombasa, Nairobi mpaka Misri.
.
3. Dawa za kulevya walizokamatwa nazo zimetajwa kwamba ni Heroine kilo saba. 4. May 18 2013 ndio tuliitwa kwenda kutazama Raia wetu, nikatuma maafisa wawili wazuri kwenda kutazama ili raia wetu wasimbambikiwe kesi. 5. Baada ya hapo waliwekwa rumande na tukapata nafasi ya kuwaunganisha na nyumbani huku Tanzania wakaongea kwenye simu kilichowapata. . 6. 26 May 2013 ndio walipelekwa Mahakamani kwa mara ya kwanza na kurudishwa rumande wote wawili. 7. Hawa ndio Watanzania wa kwanza kukamatwa na kesi kama hii na ikithibitishwa wamefanya kweli, hili kosa ndilo litakua doa la kwanza kwa Tanzania hapa Misri. 8. Ishu ya kunyongwa, tunajaribu kufanyia kazi lakini hakuna kumbukumbu za mgeni yeyote kwa sisi tunavyojua ambae amewahi kunyongwa kuhusu ishu ya dawa za kulevya. 9. Tunajitahidi kuwasiliana na mamlaka zinazohusika ili kujua siku gani watapelekwa tena Mahakamani alafu tutawafahamisha nyumbani. Kwa ushahidi unaweza kumsikiliza balozi hapa chini na pia kutazama video hapo chini ya ushahidi wa kukamatwa na dawa za kulevya…

PICHA ZA KALA JEREMIAH AKIAMKABIDHI MAMA MZAZI WA MANGWAIR TUZO YAKE

Mama mzazi wa marehemu Albert Mangweha akiwa ameshikilia tuzo aliyopewa kwa niaba ya mwanae, tuzo hii aliipata msanii Kala Jeremiah kwenye tuzo za Kilimanjaro ikiwa kama tuzo ya msanii bora ya Hip Hop 2013-14


 
 
 
 

MH: ZITO KESHO KUWA MGENI RASMI SHOW YA MWANA FA, HUKU SUGU AKIWA KWA JIDE

 
Ile the Big Square 1, show za magwiji wa muziki Tanzania mwana FA ‘The Finest’ na Lady Jay Dee ‘Miaka 13 ya Lady Jay Dee’ zitapigwa kesho June 14, huku presha ikiwa inaongezeka hasa kwa fans wanaotamani kuhudhuria show walioichagua na kuona ukubwa wa show kama walivyotarajia.

Show hizi kubwa zina nguvu sana kutokana na ukubwa wa majina ya wasanii husika. Kwa mujibu wa lady Jay Dee timu anaconda kesho itaungwa mkono na mheshimiwa Joseph Mbilinyi a.k.a Sugu.

Jide ambae hivi karibuni ameachia wimbo mpya unaopatikana kwenye album yake ‘Nothing but the truth’ inayoitwa Yahaya, amepost kupitia kupitia ukurasa wake wa facebook na pia katika akaunti yake ya Twitter kuonesha list ya wasanii watakaopanda jukwaani, na pia uwepo wa Sugu.

” Miaka 13 ya Lady JayDee, Ijumaa ya kesho shughuli inaanza rasmi saa 3:00 usiku...Ukiskia paaaa ujue show imeisha

1. Prof Jay 2. Juma Nature 3. Grace Matata 4. Hamza Kalala 5. Wakazi na ugeni wa Mh. Joseph Mbilinyi a.k.a SUGU

Nyimbo zote unazozipenda zitalia tar 14 June, pale Nyumbani Lounge sababu yaaaaa sababu yaaaaaa ?????????”


Kwa upande wa Mwana FA ambae atapiga show yake na Live band akiwa na kundi kubwa na maarufu kwa upigaji wa Live Band ‘Wananjenje’, yeye amepewa full sapoti na mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto kabwe.
Zitto ameweka wazi kupitia akaunti yake ya twitter kuwa anamsapoti sana msanii huyo.

“You have my full support “@MwanaFA”

"BABY MADAHA ASITAKE KUPATA UMAARUFU KUPITIA JINA LANGU TENA ANIKOME" ...... JACK WOLPER

MWANADADA anayefanya vizuri katika tasnia ya filamu Jaqueline Massawe ‘Wolper Gambe’ amesema anamshangaa sana msanii wa muziki ambaye pia ni mwigizaji Baby Madaha kutumia vyombo vya habari kutengeneza ugomvi wakati hana mawasiliano naye yoyote na wala si rafiki yake au mtu aliyekaribu naye na hana mazoea naye.


“Nimelizika na umaarufu nilio nao sihitaji kujipeleka katika magazeti na kuongelea vitu ambavyo havina faida katika jamii, mimi sina urafiki na Baby Madaha, namshanga anavyotapatapa kuniandika vibaya kwa jambo lisilo nihusu, mambo hayo niliyafanya nikiwa Chipukizi”

“Nakumbuka mimi nilipigiwa simu na rafiki yake akiniomba namba mwenye nyumba lakini ghafla nikapiwa simu na mwandishi wa habari mara Polisi nikashangaa huyo mtu hata namba ya mwenye nyumba sijamtumia nasumbuliwa na watu utafikiri mimi ndio mtuhumiwa, lakini jambo ninalomshangaa mimi ni dalali?,” alihoji Wolper.
Hivi karibuni yalizuka maneno yakiwahusisha wasanii hawa wawili ikisemekana walikuwa wakigombea nyumba ya kupanga, huku Baby Madaha kuigizwa mjini na mwenye nyumba kwa kupangishwa nyumba hewa, Wolper amedai kuwa kwa sasa yeye amekuwa makini halipii nyumba kienyeji bali ulipia kwa mwanasheria wake tena kwa kufuata taratibu kwa kukwepa utapeli.

MUME WA MTU ANASWA GEST AKIWA NA SHOGA WAKIFANYA UCHAFU WAO


Tukio hilo lililoshuhudiwa na watu kibao, lilijiri Juni 10, mwaka huu katika nyumba moja ya kulala wageni iliyopo Kinondoni jijini Dar.
Kunaswa kwa wanaume hao ambao ilidaiwa walikuwa kwenye harakati za kufanya Usodoma na Ugomora, kulifuatia mke wa mmoja wao kunasa meseji za kimapenzi walizokuwa wakitumiana wawili hao.
Mama huyo alipobaini meseji hizo chafu, wawili hao wakisisitiziana kukutana kwenye gesti hiyo usiku wa siku hiyo, alimpigia simu mmoja wa waandishi na  kumpa  mkasa  mzima ambapo  walikubaliana  saa  moja  zoezi  la  kuwanasa  litaanza.. 
Ilipofika saa 1:30 usiku, timu yetu, mama huyo, wapambe wake na polisi walikuwa wanafanya doria nje ya gesti hiyo.

Saa 5:30 usiku, mume wa mwanamke huyo akiwa na mwanaume anayedaiwa kuwa shoga walifika gesti hiyo bila kujua kama waliwekewa mtego wa kunaswa na kwenda kuchukua chumba namba 2.


 Wakiwa ndani, mke alimpigia simu mumewe na kuhoji alipokuwa akajibiwa alikuwa mitaa ya nyumbani kwao Manseze, Dar akipiga stori na rafiki zake.

Wawili hao wakiwa wanajiandaa na mchezo wao usiofaa, polisi aligonga mlango akijifanya mhudumu aliyetaka kumpatia taulo, jamaa bila kujua alifungua ndipo walipofumaniwa na kuibua varangati zito.
 
Kufuatia timbwili hilo, waliwekwa chini ya ulinzi na kutolewa pale gesti tayari kupelekwa kituoni ndipo mwanaume anayedaiwa kuwa shoga akatimua mbio mithili ya mwanariadha wa kimataifa, Usain Bolt wa Jamaika na wanandoa hao waliendelea kuzozana huku mke akimlalamikia mumewe na kumwambia wakifika nyumbani ampe talaka yake.

Hata hivyo, mwanamke huyo aliomba sakata hilo lisipelekwe polisi kwa madai alichotaka ni kumfumania mumewe na kwamba alikuwa na ushahidi wote.

GPL

RAIS JACOB ZUMA ASEMA KUWA AFYA YA NELSON MANDELA YAANZA KUIMARIKA

Rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela kulia na rais wa sasa Jacob Zuma
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amesema kuwa afya ya rais wa zamani wa taifa hilo Nelson Mandela imeanza kuimarika kidogo kutokana na matibabu anayopewa na Madaktari wake jijini Pretoria.
Zuma amewaambia wabunge kuwa Mandela anayefahamika kwa jina maarufu kama Madiba ameanza kuimarika na ni habari njema kwa raia wa nchi hiyo ambao wamekuwa wakikumbwa na wasiwasi kutokana na afya yake kuendelea kudorora.
Rais huyo ameongeza kuwa kila mmoja anakumbuka mchango wa Mandela ambaye alifungwa jela miaka 27 akiwa katika harakati za kupinga ubaguzi wa rangi nchini humo na baadaye kufanikiwa kuwa kiongozi wa kwanza mweusi nchini humo mwaka 1994.
Kiongozi huyo wa Afrika Kusini amewataka raia wa nchi hiyo na dunia nzima kuendelea kumwombea Mandela ili apate nafuu haraka na kuruhisiwa kurudi nyumbani.

Familia ya Mandela imesema kuwa imeguswa mno na salamu za heri njema zinazotumwa na watu mbalimbali duniani kumtakia kiongozi huyo wa zamani nafuu ya haraka.

Mandela mwenye umri wa miaka 94 alilazwa hospitalini Jumamosi iliyopita baada ya kuanza kusumbuliwa na mapafu tatizo ambalo limemsumbua kwa muda mrefu.

MAGAZETI YA LEO JUNI 13, 2013


.
 .

MWANA FA AFUNGUKA KUHUSU BIFU LAKE NA LADY JAYDEE

Baada ya kutibuana na Lady Jaydee, Mwana FA ameamua kuvunja ukimya na kuwataka mashabiki wachukulie poa maana ni hali ya kawaida tu katika maisha ya kibinadamu.....

Ugomvi wa wasanii hawa ulianza baada ya Mwana FA ku re -tweet post moja ya shabiki wake ambayo ilikuwa ikiiponda show ya Lady Jaydee...

Lady jaydee alijaribu kumuonya mara kadhaa lakini FA hakusikia na badala yake aliretweet post ya shabiki mwingine ikimponda Lady Jaydee....

Uvumilivu ulimshinda Lady Jaydee na kuamua kujibu mashambulizi kwa kumuita Mwana Fatuma na na mengine mengi.....

Wasikilize hapo chini wakifunguka

RAIS KAGAME AMGOMEA JK



RAIS wa Rwanda, Paul Kagame, amemshambulia kwa maneno makali Rais Jakaya Kikwete, akijibu ushauri alioutoa kwa serikali yake wa kukaa katika meza ya mazungumzo na waasi wa kikundi cha Democratic Force for the Liberation of Rwanda (FDLR), ili kumaliza mapigano. Shirika la Habari la Rwanda, linalojulikana kwa jina la News of Rwanda, jana lilimkariri Rais Kagame akitoa maneno ya kejeli na yenye mwelekeo wa kupuuza ushauri wa Rais Kikwete.

Kauli hiyo ya Rais Kagame, ambayo pia imesambazwa katika mitandao mbalimbali ya habari, inaonyesha kukerwa na ushauri wa Rais Kikwete ambao ameuita upumbavu uliojazwa ujinga.

Hii ni mara ya kwanza kwa Rais Kagame kutoa kauli hiyo tangu Rais Kikwete alipotoa ushauri huo, wakati akizungumza katika kikao cha Mkutano wa Umoja wa Afrika uliofanyika mapema mwaka huu, mjini Addis Ababa, Ethiopia.

Waasi wa FDLR ambao jamii yao ni Watutsi, walikimbilia nchini Kongo baada ya mapigano ya kimbari ya mwaka 1994, yaliyosababisha maelfu ya watu kupoteza maisha na wamekuwa wakiendesha chokochoko dhidi ya Serikali ya Rais Kagame.

Akizungumza katika sherehe ya kuhitimu mafunzo ya kijeshi maofisa 45 wa jeshi lake, Rais Kagame alisema ushauri wa kufanya mazungumzo na waasi wa FDLR ni ujinga na haupo katika historia ya Wanyarwanda.

Wednesday, June 12, 2013

KIFO CHA KASHI...YALIYOTABIRIWA NA MCHUNGAJI YAMETIMIA

Marehemu Jaji Hamisi ‘Kashi’.

KIFO cha msanii wa siku nyingi  katika tasnia ya filamu za Kibongo, Jaji Hamisi ‘Kashi’ kilichotokea Jumatatu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kimehitimisha maono ya mchungaji aliyetabiri kuwa mastaa wawili mmoja wa Bongo Fleva na mwingine wa Bongo Movie watafariki dunia ndani ya mwaka huu.

Marehemu Albert Mangwea.
TAARIFA ZA KIFO
Saa 5 asubuhi taarifa za kifo zilitua katika chumba chetu cha habari na haraka waandishi wetu wakafika nyumbani kwa baba mzazi wa msanii huyo Kinondoni Mkwajuni jijini Dar es Salaam na kuwashuhudia waombolezaji wakiangua vilio kufuatia kifo cha mpendwa wao huyo.
Akizungumza na paparazi wetu rafiki wa marehemu aliyejitambulisha kwa jina la Mwamtoro Mzura alisema wiki mbili kabla ya kifo hicho, Kashi akiwa anaendesha gari maeneo ya Karume, Ilala jijini Dar alikosea njia na kwenda kujikita kwenye ukingo wa barabara na kuumia miguu.
“Baada ya kupata ajali hiyo alikimbizwa Hospitali ya Amana na kupatiwa matibabu, kisha akaruhusiwa kurudi nyumbani, kuanzia siku hiyo hali yake ilianza kudhoofu,” alisema.
Mwamtoro alisema kuwa Ijumaa iliyopita hali yake ilibadilika na kuwa mbaya, hivyo akakimbizwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kupatiwa matibabu hadi Jumatatu iliyopita alipoaga dunia.

MASTAA WAFURIKA NYUMBANI KWAKE
Jacqueline Pentzel ‘Jack wa Chuz’, Sabrina Rupia ‘Cathy’, Mayasa Mrisho ‘Maya’, Seif Mbembe, Herieth Chumila, Happy Nyatawa ambaye alikuwa na marehemu katika Kundi la Shirikisho la Msanii Afrika.
Mastaa hao walinaswa na mapaparazi wetu nyumbani kwa baba mzazi wa Kashi.

TANGAZO LA MAFUNZO YA UALIMU DARAJA 'A' NA STASHAHADA MWAKA 2013/2014

clip_image002
Nafasi za Mafunzo ya Ualimu Ngazi ya Cheti Daraja A na Stashahada kwa mwaka wa masomo 2013/2014.
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi anawatangazia Wahitimu wa Kidato cha Nne mwaka 2012 na Kidato cha Sita mwaka 2013 kuwa muda wa kupokea maombi kwa ajili ya mafunzo ya Ualimu ngazi ya Cheti na Stashahada mwaka wa masomo 2013/2014 umeongezwa mpaka tarehe 28/06/2013.
Sifa za mwombaji ni kama zilivyoainishwa katika tangazo la Wizara lililopo katika tovuti ya Wizara www.moe.go.tz linalohusu “Nafasi za Mafunzo ya Ualimu Ngazi ya Cheti Daraja A na Stashahada kwa mwaka wa masomo 2013/2014”.Bofya hapa
Aidha, wahitimu wa kidato cha Sita kuanzia mwaka 2008 hadi mwaka 2013 wanahimizwa kutuma maombi yao.
Barua za maombi zioneshe Jina na anuani kamili ya mwombaji na kuambatisha nakala ya matokeo yake ya mtihani (wahitimu wa Kidato cha Nne 2012 na Kidato cha Sita 2013 waambatishe ukurasa wenye matokeo yao kutoka Baraza la Mitihani la Tanzania Au kuonesha namba yake ya mtihani)

Maombi yatumwe kwa:-

Katibu Mkuu,  

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi,

S.L.P.9121,

DAR ES SALAAM 

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi

SUGU AFUNGUKA KUHUSU WAUZA UNGA WANAVYO WATUMIA WANAMUZIKI KUBEBA UNGA


USHUHUDA WA SUGU 
Ukweli wa jinsi matajiri wauza unga wanavyowatumia wanamuziki wa Kitanzania kama punda, unapewa nguvu na ushuhuda aliowahi kuutoa Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’. Mbunge huyo ambaye anapewa heshima kwamba ni mmoja wa waasisi wa Bongo Fleva, alimweleza mwandishi wetu kuwa kabla hajawa memba wa jumba hilo la kutunga sheria, aliwahi kufuatwa na wauza unga kumshawishi awe anabeba mzigo kwenda nao nje ya nchi.
 
 “Jamaa waliniambia kwa sababu mimi nasafiri safiri sana, passport (hati ya kusafiria) yangu itakuwa imeshagongwagongwa sana, kwa hiyo ni rahisi kwenda nchi tofautitofauti kwa urahisi, kwa hiyo wakataka niwe nabeba unga. “Kigezo cha pili waliona kwa sababu mimi ni mwanamuziki,
kwa hiyo ni rahisi watu kuamini ziara zangu ni za kimuziki. Nilikataa, niliwaambia siwezi kufanya biashara hiyo kabisa,” alisema Sugu.
 
 Mwaka 2011, mbunge huyo aliwahi kugusia hilo, wakati akitoa hoja kuchangia bajeti ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kuwa serikali ni lazima iwasaidie wanamuziki wa Kitanzania kwa sababu wanaibiwa sana, hivyo kuwafanya vijana kuona kimbilio rahisi la kutajirika ni kuuza madawa ya kulevya. “Mheshimiwa spika, serikali isifanye ili kijana wa Kitanzania afanikiwe lazima auze unga, madawa ya kulevya,” alisema Sugu na kueleza mfano huo wa jinsi alivyofuatwa kushawishiwa na matajiri wa unga ili naye awe punda.

WASTARA AKIRI KUTOKEWA NA MZIMU WA SAJUKI KITANDANI...!!

SIKU chache baada ya staa wa sinema za Kibongo, Wastara Juma kumaliza eda na kurejea Bongo akitokea Uarubuni ameanza kuona maruweruwe ndani ya chumba alichokuwa akilala na mumewe marehemu, Sadick Juma Kiwoloko  ‘Sajuki’, Risasi Mchanganyiko lina habari za uhakika.
 
 
Wastara Juma akiwa na mumewe Sadick Juma Kiwoloko ‘Sajuki’ enzi za uhai wake.
 
Kwa mujibu wa Wastara siku hiyo akiwa amelala chumbani humo, usiku wa manane alihisi uwepo wa Sajuki kitandani kwake.
“Niliongea naye kwa kweli siwezi kukumbuka haswa ni nini tulichoongea lakini tulikuwa katika hali ya furaha sana,” alisema Wastara.
Pia, Wastara alisema kuwa wakiwa katika maongezi yao, aliuchukua mkono wake na kuuweka juu ya mwili wa Sajuki katika hali ya mapenzi na akapitiwa na usingizi.


“Asubuhi nilipoamka nilihisi kama nilikuwa na Sajuki  pale kitandani, kuangalia vizuri, mkono wangu ulikuwa juu ya shuka badala ya mwili wa Sajuki,” aliongeza.
Hata hivyo, Wastara alisema kuwa alihisi ni ndoto lakini alipochunguza alihisi kama kulikuwa na mtu aliyekuwa amelala naye pale kitandani.
“Sijui kama ni maruweruwe, ndoto au Sajuki alikuja kweli kitandani kwangu, kikubwa ninachokiamini ni kwamba mapenzi kwa marehemu mume wangu ndiyo yamepelekea hali hiyo,” alisema

FAMILIA YAMKATAA MTOTO WA NGWEA....!!!

SIKU chache baada ya aliyekuwa mkali wa Hip Hop Bongo, Albert Kenneth Mangweha ‘Ngwea’ kupumzishwa kaburini kufuatia kifo cha usingizini nchini Afrika Kusini kilichotokea Mei 28, mwaka huu, mambo kibao yanazidi kuibuka.

Habari zinadai kuwa familia ya marehemu Ngwea imemkataa mtoto aliyeletwa na mama yake makaburini akidaiwa kuwa ni mtoto wa Ngwea.
MTOTO WA NGWEA
Juni 6, mwaka huu wakati wa mazishi, mwanamke aliyejitambulisha kwa jina la Paulina Jeremiah, mkazi wa Kigamboni, Dodoma alitimba akiwa na mtoto huyo wa kike aitwaye Neema Albert na kudai kuwa alimzaa na Ngwea mwaka 2001, wakati msanii huyo akisoma Sekondari ya Mazengo.

Wakati akijieleza, ndugu wa Ngwea, Anthony Mangweha alikuwa akimsikiliza ambapo aliwataja wanandugu wa marehemu waliokuwa wakijua suala hilo.
Waliotajwa kujua kuwa mtoto huyo alikuwa wa Ngwea ni Frank, Jotam na Amani ambao waliwahi kutumwa na marehemu kwenda kumwangalia mkoani Dodoma.
Hata hivyo, ndugu huyo aliyekuwa akimsikiliza alimtaka mama Neema kupoa, hadi familia ikae kikao.
.
FAMILIA YAKAA KWA SAA 7, YATOA UAMUZI MZITO!
“Kweli wikiendi iliyopita familia ilikaa kikao kwa zaidi ya saa 7, pamoja na mambo mengine lakini wanadaiwa kufikia uamuzi mzito wa kumkataa mtoto huyo hadi mama Neema apeleke vigezo vya uthibitisho,” kilisema chanzo chetu ndani ya kikao hicho.
Akizungumzia suala hilo kwa sharti la kutotajwa gazetini, mmoja wa dada zake Ngwea alisema: “Ni kweli yule mtoto aliondoka na mama yake lakini kama akileta uthibitisho tutampokea.”

MWANAMKE AFUNGWA MIAKA 3 KWA KOSA LA KUMNG'ATA MUMEWE SEHEMU ZA SIRI HUKO IRAMBA SINGIDA ...!!!

 
MAHAKAMA ya Wilaya ya Iramba mkoani Singida umemhukumu mwanamke mmoja mkazi wa kijiji cha Kisana wilayani humo, Sayuni Ramadhani (42) kwenda jela miaka mitatu baada ya kukiri kosa la kumng’ata mumewe sehemu zake za siri.

Mwendesha mashitaka mkaguzi wa polisi, Vincent Ndasa alidai mbele ya hakimu mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Iramba, Kariho Mrisho kuwa Juni 4 mwaka huu saa 12.00 jioni katika kijiji cha Kisana, mshitakiwa kwa makusudi alizing’ata kwa meno sehemu za siri za mume wake, Onesmo Nathania (42) na kumsababishia maumivu.
Ndasa alidai kuwa siku ya tukio, wanandoa hao waliporejea nyumbani kutoka kwenye klabu cha pombe ya kienyeji kijijini hao, kulitokea kutokuelewana na hivyo kuanza kugombana.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...