Thursday, June 13, 2013

"BABY MADAHA ASITAKE KUPATA UMAARUFU KUPITIA JINA LANGU TENA ANIKOME" ...... JACK WOLPER

MWANADADA anayefanya vizuri katika tasnia ya filamu Jaqueline Massawe ‘Wolper Gambe’ amesema anamshangaa sana msanii wa muziki ambaye pia ni mwigizaji Baby Madaha kutumia vyombo vya habari kutengeneza ugomvi wakati hana mawasiliano naye yoyote na wala si rafiki yake au mtu aliyekaribu naye na hana mazoea naye.


“Nimelizika na umaarufu nilio nao sihitaji kujipeleka katika magazeti na kuongelea vitu ambavyo havina faida katika jamii, mimi sina urafiki na Baby Madaha, namshanga anavyotapatapa kuniandika vibaya kwa jambo lisilo nihusu, mambo hayo niliyafanya nikiwa Chipukizi”

“Nakumbuka mimi nilipigiwa simu na rafiki yake akiniomba namba mwenye nyumba lakini ghafla nikapiwa simu na mwandishi wa habari mara Polisi nikashangaa huyo mtu hata namba ya mwenye nyumba sijamtumia nasumbuliwa na watu utafikiri mimi ndio mtuhumiwa, lakini jambo ninalomshangaa mimi ni dalali?,” alihoji Wolper.
Hivi karibuni yalizuka maneno yakiwahusisha wasanii hawa wawili ikisemekana walikuwa wakigombea nyumba ya kupanga, huku Baby Madaha kuigizwa mjini na mwenye nyumba kwa kupangishwa nyumba hewa, Wolper amedai kuwa kwa sasa yeye amekuwa makini halipii nyumba kienyeji bali ulipia kwa mwanasheria wake tena kwa kufuata taratibu kwa kukwepa utapeli.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...