Tuesday, June 04, 2013

Jokate aongea baada ya Diamond kukiri kuwa anajuta kumkosea na kuuvunja moyo wake

Hivi karibuni Diamond aliamua kuweka ‘ego’ pembeni na kukiri kuwa Jokate Mwegelo ndiye msichana katika maisha yake aliyemkosea sana na anajuta kumuumiza
Diamond alifunguka hayo kwenye kipindi cha Take One cha Clouds TV, kilichorushwa wiki iliyopita.

Akiongelea jinsi alivyomuumiza Jokate, Diamond alisema, “Kwasababu alikuwa too innocent halafu hakuwahi kunikosea kitu chochote Jokate kabisa, halafu nikamwingiza kwenye matatizo, watu wakamchukulia tofauti kwamba ‘Jokate kamchukulia Wema boyfriend wake’ wakati nilimfuata mimi kama mimi, nilimtafuta mwenyewe halafu then nikawa niko naye halafu ghafla nikarudisha mahusiano kwa Wema. Sikujiskia vizuri halafu still haikuwa vizuri so sometimes nikikaaga hivi nasema nilimkosea.”

Akijibu swali la kwanini alimuacha Jokate, Diamond aliongeza, “Sijui nilirogwa hata sijui, I don’t know, sijui hata kwanini, hakuwahi kunikosea chochote sio, sababu nilikuwa nikikaa naye alikuwa akinishauri vitu vingi vya maendeleo, sijui ulikuwa ni utoto sielewi yaani, sijui ni kitu gani, nilijikisa vibaya sana, halafu mtoto wa watu mstaarabu sana, alijitahidi kujenga career yake sasa hivi imekaa vizuri.”

Bongo5 imewasiliana na Jokate ili kutaka kufahamu upande wake baada ya kusikia kauli ya Diamond aliyesema anafurahi kuona Diamond amefunguka ukweli.

“Watu wengi hawajui the real issue, I’m glad kama ame-acknowledge I was innocent in that whole matter,” amesema Jokate.

MAPOKEZI YA MANGWEA JIJI ZIMA LAZIZIMA

 Gari iliyobeba mwili wa Albert Mangwea ikisukumwa na washabiki,wapenzi ndugu jamaa na marafiki mara baada kuanza kuondoka eneo la Eapoti hivi punde wakielekea Muhimbili kwa taratibu nyingine,Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi--Amen

ANGALIA PICHA MWILI WA ALBERT MANGWEA ULIVYOWASILI DAR

Gari maalum la Kubeba Mwili wa Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya,Marehemu Albert Mangwea likiwa tayari  kwa kubeba mwili.
Wadau mbali mbali wakiwa wamekusanyika kwa wingi kwenye uwanja wa Ndege Julius Nyerere kwa ajili ya kuupokea Mwili wa Marehemu Albert Mangwea uliowasili mchana huu kutokea nchini Afrika ya Kusini.
Wadau kibao wapo uwanjani hapa hivi sasa tayari kwa kuupokea Mwili wa Marehemu Mangwea.
Rafiki kipenzi wa Marehemu Albert Mangwea,Jay Mo akihojiwa na vyombo vya habari uwanjani hapa.

ANGALIA PICHA ZA MWANAMKE AZAA WATOTO WATANO KWA MPIGO NCHINI CZECH.

Mmoja wa watoto wa watano akiwa amejifungua mbele ya uangalizi wa jopo la madaktari siku ya jumapili nchini Czech.
Jopo la madaktari wakimchunguza mwanamke Alexandra Kinova miaka 23.
Alexandra Kinova kipindi cha ujauzito.

MAMA NA MPENZI WAKE WAMUUA MTOTO WA MIAKA 4 ILI WAFAIDI PENZI LAO

Wakati mwingine unaweza kudhani binadamu tunageuka kuwa wanyama, lakini huu sio mfano tosha kwani hata wanyama wakali kama simba huwa na huruma na huwalinda watoto wao hadi kufa, baadhi ya binadamu wamekuwa na roho ya ukatili isiyo ya kawaida hata kwa mtoto waliyemzaa wenyewe.
Huko Uingereza mama mmoja aliyejulikana kwa jina la Magdelena Luczack na mpenzi wake Mariusz Krezolek ambao walihamia uingereza wakitokea Poland, wamefikishwa katika mahakama kuu mjini Birmingham wakikabiliwa na mashtaka ya mauaji. 
Watu hao wanashtakiwa kwa kushirikiana kumuua kwa kumtesa wka vipigo na  kumyima chakula  kwa makusudi mtoto Daniel aliyekuwa na umri wa miaka minne tu,aliyefariki mwezi march mwaka jana akiwa na jeraha kichwani.
Magdalena ambae ni mama mzazi wa mtoto huyo anatuhumiwa kushirikiana kwa karibu na baba wa kambo wa mtoto huyo kusababisha kifo chake wakiwa na nia ya kutafuta amani na utulivu katika nyumba yao.

M2 THE P ANA USHAHIDI WOTE KATIKA KIFO CHA ALBERT MANGWAIR.

 
Na Mwandishi Wetu
MBIVU na mbichi sasa zinaweza kujulikana, kinachoombwa ni muda tu, kwani mng’amuzi halisi kuhusu kifo tata cha mwanamuziki mwenye kipaji kikubwa Bongo, Albert Mangwea ‘Ngwea’, yupo kwenye mazingira mazuri kueleza kilichotokea.

KWA NINI ANA USHAHIDI WOTE?
Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Mgaza Pembe ‘M2 The P’, ndiye mwenye ushahidi wote kwani aliambatana na Ngwea kila sehemu waliyotembelea mpaka nukta ya mwisho nchini Afrika Kusini.
M2 The P, alipatwa na matatizo sawa na marehemu Ngwea, isipokuwa mwenzake ilifikia hatua mbaya na kupoteza maisha huku yeye akibaki mahututi kwenye chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum (ICU) katika Hospitali ya St. Helen Joseph, jijini Johannesburg nchini humo.
Jambo la faraja ni kwamba, M2 The P yupo vizuri kwa sasa, atakaporuhusiwa kutoka, atajibu maswali mengi tata ambayo yamejitokeza tangu Ngwea alipofariki dunia Juni 28, mwaka huu, nchini humo  alipokwenda kwenye shughuli zake.

JAWABU LA SUMU 
Moja ya mambo yanayozungumzwa pembeni ni kwamba kuna uwezekano mkubwa marehemu Ngwea na M2 The P  waliwekewa sumu kwenye chakula au kupuliziwa ‘laivu’ kisha kutokea yaliyotokea, lengo likiwa kuwadhulumu mzigo wa fedha nyingi waliokuwa nao, hivyo kupona kwa mmoja huyo ni matakwa ya Mungu ili awe shahidi namba moja wa kifo cha Ngwea.

H0TUBA YA MAPENDEKEZO YA RASIMU YA KATIBA NA YALIYOMO KWENYE RASIMU HIYO NI HAYA HAPA .....



warioba 89a51
1.0. UTANGULIZI
Awali ya yote namshukuru mwenyezi mungu kwa kutuwezesha kufikia hatua hii ya leo ya kuzindua Rasimu ya Katiba. pia, niwashukuru ninyi nyote mliohudhuria halfa hii ikiwa ni mwendelezo wa mchakato muhimu wa Mabadiliko ya Katiba ya nchi yetu.
Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ilipitishwa Bungeni Novemba, 2011 na kufanyiwa mabadiliko Februari, 2012. Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliundwa kwa mujibu wa Kifungu 6(1) cha sheria hiyo (Cap.83). Wajumbe 34 wa Tume waliteuliwa na kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, mwezi Aprili, 2012. Kwa mujibu wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Tume imepewa miezi kumi na minane kukamilisha kazi yake kuanzia siku ilipoanza kazi rasmi ambayo ilikuwa Mei 2, 2012.
Tume iliandaa ratiba ya utekelezaji wa majukumu yake. Kufuatana na ratiba hiyo Tume ilijipanga kukusanya maoni ya wananchi katika kipindi cha miezi mitano kuanzia Mwezi Julai hadi Disemba, 2012. Kazi hiyo ilifanywa kama tulivyopanga. Tume ilijigawa katika makundi na ilitembelea mkoa yote thelathini.

Tume ilifanya mikutano 1,942 ambayo ilihudhuriwa na wananchi wapatao 1,365,337 ambao kati ya hao wananchi 333,537 walitoa maoni ama kwa mazungumzo ya ana kwa ana au kwa maandishi. Tume pia ilipata maoni ya wananchi wengi, wa ndani na nje ya nchi kwa njia mbali mbali kama vile; Mikutano ya hadhara, Fomu maalum za Tume, barua kupitia Masanduku ya Barua ya Tume, Mitandao ya Kijamii ya barua pepe; facebook ya Tume, Tovuti ya Tume; Makala mbalimbali kutoka kwenye magazeti na ujumbe mfupi wa simu.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE JUNI 04, 2013

1 c2a93
17 cdc7f

VITI MAALUMU VYAFUTWA, UBUNGE KUWA NA UKOMO


Tume ya Mabadiliko ya Katiba imependekeza katika rasimu ya Katiba Mpya ukomo wa wabunge na kufutwa kwa nafasi za Viti Maalumu bungeni.
Mwenyekiti wa tume hiyo, Jaji Mstaafu Joseph Warioba alisema jana, wanapendekeza kwamba ubunge uwe na ukomo wa vipindi vitatu vya miaka mitano, mitano akimaanisha kwamba kipindi cha mtu kuwa mbunge hakiwezi kuvuka miaka 15.

Rasimu hiyo ya Katiba imependekeza kutokuwapo tena kwa Viti Maalumu na badala yake, imetaka kuwapo kwa nafasi tano za uteuzi zibaki kwa Rais ambazo zitahusisha makundi maalumu ya watu wenye ulemavu pekee.

Jaji Warioba alisema Tume imependekeza kuwapo kwa
majimbo 25 ya uchaguzi kwa Tanzania Bara na 20 kwa Zanzibar ambayo kila moja litakuwa na wabunge wawili, mwanamke na mwanamume. Kwa mujibu wa rasimu hiyo, majimbo hayo ni mikoa 25 ya Tanzania Bara na wilaya 10 za Zanzibar. Kwa maana hiyo, Bunge la Muungano litakuwa dogo lenye wabunge 75.

Monday, June 03, 2013

MAPYA YAIBUKA KUHUSU KIFO CHA MANGWEA....ALIYELALA NAE ASIMULIA ALIYOYAONA WAKATI NGWEA AKIKATA ROHO..!!

HUKU mwili wake ukitarajiwa kuwasili Bongo kesho, kifo chake Albert Mangweha ‘Ngwea’ kilichotokea katika hali ya utata Mei 28, 2013 nchini Afrika Kusini, kimeibua mambo mapya, Ijumaa Wikienda lina mzigo wote.

MAMA MANGWEA NAYE AZIDIWA, AKIMBIZWA HOSPITALI YA MKOA
Habari kutoka msibani Moro jana zilisema mama mzazi wa marehemu Mangwea, Denisia Mangwea naye alizidiwa na kukimbizwa katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa matibabu zaidi.
Kwa mujibu wa baadhi ya waombolezaji msibani hapo, mama huyo alipata mshtuko wa moyo kufuatia kifo cha mwanaye ambapo taarifa za kifo hicho zilimshtua tangu Jumanne mpaka alipozidiwa jana. 

HABARI KUTOKA SAUZI SASA
Habari kutoka kwenye Jiji la Johannesburg ambako Ngwea alifia, mtiririko wa maelezo ya wenyeji wa Mangwea na Mgaza Pembe ‘M 2 The P’ nayo yanaibua mapya ambayo awali yalikuwa hayajulikani.
MAELEZO YA SAUTI ZA WENYEJI
Wakizungumza hewani kupitia redio moja ya jijini Dar, wenyeji wao wawili waliojitambulisha kwa jina moja moja la Godfrey na Godluck ambao walikuwa na Mangwea na M 2 The P, kila mmoja alisema lake huku maelezo yao yakionesha dalili ya kutofautiana au kuzua maswali masikioni mwa watu.

BINTI AANIKA MAKALIO MBELE YA WABUNGE KATIKA SHINDALO LA MISS TABORA


Mmoja wa washabiki wa muziki wa kizazi kipya ambaye alivaa vazi lililoacha  matako  nje....

Shabiki huyo  alipanda jukwaani kumkumbatia  msanii  maarufu nchini , Ommy Dimpoz  wakati alipokuwa akitoa burudani katika mashindano ya Redds Miss Tabora.

Tukio hilo la aibu lilitokea  mbele ya  wabunge....
Mbunge wa Jimbo la Sengerema  Bw.William Ngereja akiwa na Diwani wa kata ya Kitete manispaa ya Tabora Bw.Daniel Mhina ambaye alikuwa MC katika onesho hilo lililofanyika katika ukumbi wa Frankman Hotel mjini Tabora.

Sophia Simba, Anne Kilango nusura wazichape walipokutana gafla benki

Kushoto Mh. Sophia Simba na kulia ni Mh. Anna Kilango
UHASAMA wa kisiasa kati ya Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na watoto, Sophia Simba na Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango, umevuka mipaka na sasa ni uadui wa wazi wazi. Hali hiyo ilidhihirika wiki iliyopita mjini Dodoma, wakati wawili hao walipokutana katika Benki ya CRDB iliyopo bungeni na badala ya kusalimiana, waliishia kutofautiana.
Shuhuda wa tukio hilo, aliiambia MTANZANIA, kuwa tukio hilo lilitokea saa 6 mchana, baada ya Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, kuahirisha Bunge kutokana na vurugu zilizosababishwa na wabunge wa upinzani, wakati wa mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.


Shuhuda huyo alisema kuwa, kabla ya tukio hilo, Anne Kilango pamoja na wabunge wengine wa CCM, walikuwa ndani ya benki hiyo wakibadilishana mawazo.

Wakati wakiendelea kuzungumza, Sophia Simba aliingia ndani na kuanza kuwasalimia kila mmoja kama ilivyo kawaida.
 

MWANA FA NA JIDE KWA MARA NYINGINE WATAFANYA SHOW ZAO SIKU MOJA

Ikiwa ni siku chache baada ya wasanii kuahirisha show zao kufuatia kuondokewa mpendwa wetu Albert Mangwea, miongoni mwa show kubwa zilizoahirishwa ni ya Lady Jay Dee (Miaka 13 ya Lady JayDee) na ya Mwana FA (The Finest) zilizokuwa zifanyike siku moja (May 31),show hizi zinaweza kufanyika tena siku moja kwa kuwa wasanii hao wametaja tarehe inayofanana.

May 28 ambayo ndiyo siku aliyofariki Mangwea mwana FA alithibitisha kuahirisha show yake, lakini alipoulizwa siku ambayo anadhani atairudia show hiyo, yeye alifunguka kupitia akaunti yake ya twitter na kuitaja June 14.

 “Sina uhakika,but I'll pick June 14th kama brother tutakuwa tushampumzisha"@umykitwana”, alitweet Mwana FA a.k.a Binamu.
 
 
Kwa upande wake Lady Jay Dee ambae kwa sasa a.k.a yake mpya ‘Anaconda’ inaonekana ku-take over ametumia akaunti yake ya twitter kuiweka wazi tarehe ya show yake alipokua akijibu swali la fan wake ambae atasherehekea siku moja ya kuzaliwa na msanii huyo (June 15).

“@MteiHaikaJ Gud. Chukua hii tar 13 June Mahakamani, tar 14 June miaka 13 ya Jide na tar 15 June Bday ya Jide. Let's celebrate long week end.”Alitweet Lady Jay Dee June 2.

Kwa tweets za wakali hawa wa bongo fleva inaonesha kabisa kuwa show zao zinaweza kufanyika june 14 japo Mwana FA alisema hana uhakika, labda kama atatangaza siku nyingine tena. June 14,tunatarajia kuwa marehemu Ngwair atakuwa amekwisha pumzishwa kwenye nyumba yake ya milele huko Morogoro.
CHANZO : LEOTAINMENT

WABUNGE WAKUTWA KWENYE DANGURO LA UCHI DODOMA

 Watu wanaingia mmoja mmoja, wengine kwa makundi na baadhi wapo nje wakipunga kwanza upepo kabla ya kuingia.

Siku hizi wanawake wanaingia bure au kwa jina jingine ‘ladies free’ jambo linalosababisha ukumbi huu ufurike watu.

Katika ukumbi huu, yapo maeneo mawili. Kuna sehemu ya kawaida ambayo kiingilio chake ni kuanzia Sh5,000 hadi Sh10,000 kutegemeana na matukio au burudani ya siku hiyo.

Pia kuna eneo jingine ambalo ni kwa watu maalumu ama waweza kusema ni ‘VIP’ ambapo wateja wake hutakiwa kulipa Sh20,000.

Ukumbi wa VIP upo juu na ule wa kawaida upo chini. Hata hivyo maeneo yote haya hujaza watu kwa kiasi kikubwa.

Mwandishi wetu alifika katika ukumbi wa VIP saa tano usiku, hata hivyo bado watu ni wachache katika eneo hili ukilinganisha na kule kwa watu wa kawaida.

Ukumbi wa VIP si mkubwa kieneo . Kuna kaunta ya vinywaji, makochi madogo madogo aina ya sofa yenye meza mbele yake, viti vilivyoizunguka kaunta na katikati ya ukumbi huu kuna meza mbili za duara zenye mti wa chuma katikati.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU JUNE 03, 2013

1 a9412
17 20f78
5 173d6

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...