Wednesday, May 01, 2013

Kimenuka! Sasa hivi vimini ‘No’ kwenye filamu, bodi ya filamu imeona ilivalie njuga suala hili.

TAARIFA iliyotua kwenye dawati la gazeti hili hivi karibuni inaeleza kuwa, mavazi yasiyo ya heshima vikiwemo vimini yamepigwa marufuku...
kuvaliwa na wasanii kwenye filamu wanazorekodi na yoyote atayekiuka atakiona cha mtemakuni.Chanzo chetu makini kilichoomba hifadhi ya jina lake, kimeeleza kuwa waliotoa agizo hilo ni Serikali ya Tanzania kupitia Bodi ya Filamu lengo likiwa ni kuhakikisha maadili ya taifa yanazingatiwa.
Ikaelezwa kuwa hatua hiyo imekuja kufuatia uwepo wa filamu nyingi mtaani ambazo wasanii wanaoshiriki huvaa mavazi yasiyo ya heshima, mazingira yanayoiharibu jamii. 

“Kama wanavyosema vijana huko mtaani kwamba kimenuka na kweli kimenuka! Sasa hivi vimini ‘no’ kwenye filamu, bodi ya filamu imeona ilivalie njuga suala hili ili kulinda maadili ya taifa,” kilieleza chanzo hicho.


Katika kujua ukweli wa jambo hili, mwandishi wetu alimtafuta Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), Simon Mwakifwamba ambaye alikiri kuwepo kwa utaratibu mpya wa Bodi ya Filamu wa kuzipitia filamu zinazoingia mtaani na kwamba zinazokiuka maadili zinafungiwa. 
Mwakifwamba alisema ni kweli mavazi ya nusu utupu hayataruhusiwa tena kuonekana kwenye filamu kama ilivyokuwa huko nyuma na wale watakaojifanya vichwa ngumu watashughulikiwa.
“Sasa hivi kuna sheria mpya kabisa, hakuna kuvaa nguo zisizo za maadili na ukikiuka basi filamu yako haioneshwi au kama unaweza urudie na kuondoa vipande vilivyoharibu filamu hiyo,” alisema Mwakifwamba huku kukiwa na maelezo kuwa, hilo pia litasimamiwa na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo chini ya Waziri Fenella Mukangara.

WOSIA WANGU KAMA IKITOKEA NIMETANGULIA KUFA KABLA YA RUGE AU JOE KUSAGA:..........JIDE

Watu wanashtuka mtu akiongelea kifo, Utafikiri hawafahamu fika kuwa kila nafsi itakionja, Kwenye maisha yangu nimepitia mambo mengi, magumu na mepesi
Na bado naendelea ku experience mambo magumu zaidi kadri ninavyozidi kuwa mkubwa.

Siku za karibuni nimekuwa nikipigwa vita sana na watu wenye uwezo mkubwa kifedha , ki umri na hata wenye ukubwa wa connection katika hii industry ya muziki. Wanaomiliki chombo cha habari.

Nasimama na kusema kuwa sitokata tamaa, kwani lengo lao kubwa ni kuona na kuhakikisha nimeanguka kabisa na sipo katika ramani ya muziki.

Watu hao ambao vita yao ilikuwa baridi miaka kumi iliopita, sasa inazidi kuwa moto baada ya kutambua kuwa mimi ni mtu mwenye maamuzi yangu na misimamo yangu bila kuburuzwa.
Wanapita kila mahali kuhakikisha kila mrija unaoniingizia chochote unakatika, na hiyo ni kutaka kuuthibitishia umma wa Tanzania kuwa hakuna msanii anaeweza ku survive bila wao.

HUYU NDO MODAL KUTOKA GERMANY, ALIYEAMUA KWENDA KAZINI AKIWA UCHI WA MNYAMA

 
A STUNNING model gives fellow commuters a wake-up call to remember by riding the train completely starkers. The brunette wore only glasses and shoes for her nude ride to work. And in place of clothes, she daubed herself with words describing what they might have expected her to have been wearing. Model rides without clothes Skin full view ... model rides without clothes TNI Press
The woman carried out the stunt in Dusseldorf, Germany. After boarding a train without blushing, the lady ensured she purchased a ticket before taking her seat as normal. THE model showed her flawless figure to fellow commuters on the train in Germany as part of an art project Stunned passengers gawked open-mouthed as the woman showed off her flawless figure.
Naked model on a train in Germany Wake-up call ... but some passengers on the train still managed to stay asleep TNI Press But remarkably, some of them gave barely a sideways glance as she walked through the carriage in the buff. The model’s naked journey was part of a project put together by Swiss artist Milo Moire. Entitled The Script System, the stunt was intended as a way of "shaking up the ordinary". Swiss artist dreamed up scheme to have naked model take a train ride in Germany Stunt ...

 Swiss artist dreamed up scheme TNI Press Milo Moire said the model walking around the train without clothes was meant to make people think outside the box on their commute. He wrote on his website: “Radical nudity becomes the defence shield against the stereotypes and makes the artist invisble.” And he went on to say that the timing of the early morning stunt meant ordinary performance art was out of the question.TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

ANGALIA PICHA ZA DIAMOND PLATNUMZ AKIWA NYUMBANI KWA MTOTO WA KAMANDA KOVA UINGEREZA


Taarifa mbalimbali za michezo kutoka TFF ikiwemo ligi kuu ya Vodacom kuingia raundi ya 25 hapo kesho.

Afisa Habari wa TFF Boniface Wambura.
LIGI KUU YAINGIA RAUNDI YA 25
Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inaendelea katika raundi yake ya 25 kesho (Mei Mosi) kwa mechi tano zitakazochezwa katika miji ya Dar es Salaam, Turiani, Morogoro na Mlandizi.
Licha ya kuwa tayari Yanga imetawazwa kuwa mabingwa wa VPL msimu huu (2012/2013), mechi dhidi ya Coastal Union itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni moja kati ya zitakazovuta macho na masikio ya washabiki wa mpira wa miguu nchini.
Mechi hiyo namba 172 itachezeshwa na mwamuzi Simon Mberwa kutoka Pwani akisaidiwa na Said Mnonga na Charles Chambea wote wa Mtwara wakati mwamuzi wa mezani atakiwa Hashim Abdallah wa Dar es Salaam. Kamishna wa mechi hiyo ni David Lugenge kutoka Iringa.
Viingilio katik mechi hiyo itakayoanza saa 10.15 jioni ni sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya bluu na kijani, sh. 8,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, sh. 15,000 kwa VIP C na B wakati VIP A itakuwa sh. 20,000. Tiketi zitauzwa uwanjani siku ya mchezo.
Mtibwa Sugar itakuwa mwenyeji wa African Lyon katika mechi namba 170 itakayochezeshwa na mwamuzi Dominic Nyamisana wa Dodoma kwenye Uwanja wa Manungu ulioko Turiani mkoani Morogoro. Nayo Kagera Sugar iliyo katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi hiyo itakuwa mgeni wa Polisi Morogoro kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Kambi ya Upinzani Bungeni imetoa tuhuma nzito kwa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.

Kambi ya Upinzani Bungeni imetoa tuhuma nzito kwa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana ikidai kuwa anajihusisha na mtandao wa ujangili nchini.
                                        Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana. 
Hata hivyo, Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Emmanuel Nchimbi amejibu tuhuma hiyo akisema ni za uongo huku akiituhumu kambi hiyo kuwa imedanganya wakati inajua ukweli kuhusu tuhuma dhidi ya Kinana.
Akiwasilisha maoni ya upinzani kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii mwaka 2013/14, Msemaji wa Kambi ya Upinzani kuhusu Maliasili, Mchungaji Peter Msigwa alisema vitendo vya ujangili vimekuwa vikilitia doa taifa kwenye jumuiya za kimataifa.
“Kwa bahati mbaya ni kwamba wahusika wengi ambao wanatajwa kwa ushahidi ni makada maarufu na wengine ni viongozi waandamizi wa CCM,” alisema Mchungaji Msigwa.
“Tumeshuhudia watuhumiwa wengine wa ujangili ambao Ikulu imediriki kuwapatia nafasi kubwa za uongozi wa taifa hili, licha ya kutajwa kwenye ripoti ya uchunguzi kuhusiana na ujangili.”
Alisema mwaka 2009, meli ya Kampuni ya Wakala wa Meli ya Sharaf Shipping inayomilikiwa na Kinana ilikamatwa China ikiwa na makontena yenye nyara za Serikali ikiyasafirisha kwenda Hong Kong.

RAIS KIKWETE AUNGA MKONO HOJA YA MBATIA KUHUSU MITAA YA ELIMU.

Rais Kikwete. Mbunge wa kuteuliwa, James Mbatia. 
RAIS Jakaya Kikwete amekubaliana na hoja ya Mbunge wa Kuteuliwa, James Mbatia kuhusu kufanyiwa marekebisho kwa mitalaa ya elimu nchini ili iendane na viwango vya elimu inayohitajika.

Rais Kikwete alisema hayo jana alipokuwa akizungumza na wenyeviti na wamiliki wa shule na vyuo vya binafsi kwenye Ukumbi wa Benjamin Mkapa, Mbeya.

Katika kikao cha Tano cha Bunge, Januari mwaka huu, Mbatia aliwasilisha hoja binafsi kuhusu ubovu wa elimu na mitalaa, hoja aliyodai kufinyangwa na Bunge kabla ya kupatiwa majibu stahiki na hata kuzua mjadala mkali miongoni mwa wadau wa sekta hiyo.

Akizungumza jana, Rais Kikwete alisema: “Mitalaa na mihutasari ya elimu itarekebishwa ili kuzingat
ia mazingira ya sasa ya dunia na ni lazima tuwe na viwango vya elimu vya kimataifa.”

RAIS OBAMA AMPONGEZA MWANAUME SHOGA ALIYEJITANGAZA HADHARANI


Mchezaji wa mpira wa kikapu nchini Marekani mwenye asili ya Afrika Jason Collins amejitangaza kuwa yeye ni shoga hatua ambayo imewashitua watu wengi hususani wapenzi wa mchezo huo.

Jason Collins anakua mchezaji wa kwanza wa kimataifa mwanaume ambaye bado anacheza mpira wa kikapu kutangaza kuwa ni shoga huku akisema kuwa yeye ni mwanamme mweusi na ni shoga.

Rais wa Marekani Barack Obama amempongeza mwanababa huyo shoga mwenye umri wa miaka 34 anayecheza katika ligi ya NBA kwa kujitangaza hadharani.

Rais Obama ambaye mwaka jana alitangaza kuunga mkono ndoa za mashoga alimpigia simu Collins na kumpongeza kwa ujasiri alioonyesha na amesema atamuunga mkono.

Mchezaji wa zamani wa NBA John Amaechi mwaka 2007 alijitokeza hadharani na kutangaza kuwa ni shoga lakini yeye alifanya hivyo akiwa tayari amestaafu kucheza kikapu.

Naye Rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton alimpigia simu Collins na kusema kuwa hatua hiyo ni muhimu kwa wanamichezo wa kimataifa na ni historia kwa jumuiya ya mashoga na wasagaji.

Binti wa Bill Clinton, Chelseea ambaye amesema kuwa alimfahamu Collins wakati wakiwa wanachuo katika chu kikuu cha Stanford na meandika katika ukurasa wake wa tweeter kwamba anaona fahari kubwa kwa rafiki yake Collins kwa kuwa na ujasiri wa kuwa mchezaji pekee wa NBA shoga na kuweka hadharani hali yake.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO TAREHE 01.05.2013

.
.
.

Tuesday, April 30, 2013

YALIOJILI KWENYE BIRTHDAY KICK YA MTU MZIMA CHIDY BENZ@NEW MAISHA CLUB


 Chidy akimlisha keki joketi

 Hapa akimlisha keki moja kati ya mafuns wake katika siku yake zakuzaliwa

 Totozzilikuwa zaukweli na zakumwaga

 Makiss na ma hug yalihusika sana siku hiyooooo

 Hii hapa keki ya king kong chidy beeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeenz

BABA MZAZI WA CHRIS BROWN, AMEZUNGUMZA KUHUSU MAPENZI YA CHRIS NA RIHANNA

.
Gazeti la New York Daily News limefanya Exclusive interview na baba mzazi wa mwimbaji staa Chris Brown na kutoa maoni yake kuhusu mahusiano ya kimapenzi ya mwanae na Rihanna RiRi.
Clinton Brown amesema “sioni maisha marefu kwa Chris Brown kuwa na Rihanna, sijawahi kupendezwa na kurudiana kwao, unajua ni lazima kwenye uhusiano wa kimapenzi uwe na mtu sahihi ambae ni hitaji la kweli na linaloweza kuwa lako kwenye maisha, lakini sio kama hivi”
Clinton amesema hapendi kutumia mifano lakini anadhani watu wameona mahusiano ya mastaa kama Whitney Houston, Michael Jackson, Amy Winehouse na wengine”
Kuhusu mrembo ambae angependa kuona anaolewa na mwanae, Clinton amemtaja Jordin Sparks kwa kusema “nimempenda Jordin, ni msichana mdogo lakini mwenye upeo mkubwa… ana akili na heshima”
.

DOTNATA AFUNGUKA BAADA YA KUGUNDUA KAWEKEWA SUMU KWENYE JUICE

http://1.bp.blogspot.com/-Xf5pb-ynWck/UFeJceXxqJI/AAAAAAAAIqE/ajgKiv17IsI/s1600/DOTNATA2.jpgMuigizaji wa filamu nchini Dotnata Rubagumya anadai kuwekewa sumu kwenye juice na mtu asiyemfahamu ambayo imemsababishia matatizo makubwa ya kiafya.
Amesema alianza kuhisi kupandwa na pressure ambapo alilazwa kwenye hospitali ya IMTU na kuambiwa imepanda hadi kufikia 284 huku wakimweleza huenda ni kwakuwa amenenepa sana.Baadaye alifanyiwa uchunguzi wa moyo kwenye hospitali ya Lugalo kabla ya kupelekwa TMJ kwa vipimo zaidi.

Anasema tatizo hilo lilimsabisha ashindwe kuhema, sauti kukata na mara nyingi alikuwa akitapika.
“Nimezidiwa usiku wa kuamkia Jumatano nikakimbizwa tena TMJ ndo sasa ikabidi wanichunguze kwa makini kwanini nakuwa hivi ndo wakagundua nimelishwa sumu takriban mwezi wa nane sasa huyo mtu aliyenipa sumu aliipitisha kwa njia ya juice,” amesema Dotnata ambaye kwa sasa ameokoka.
Akizungumzia sababu za kuwekewa sumu, Dotnata amesema:
“Kila mwanadamu ana mawazo jinsi anavyowaza katika akili yake labda hakupendezewa na mimi niendelea kuishi hivi, labda alifikiria akiniua mimi yeye hatokufa. Lakini natamka wazi kwamba sitokufa nitaishi ili niyasimulie mema ya Mungu. Nimejifunza mtu anaweza kuwa rafiki yako kumbe ndio mbaya wako siwezi kujua ni kwasababu gani, namwachia Mungu.”
Msikilize zaidi hapa.
NA BONGO CLAN BLOG

Wabunge waliosimamishwa warejea kwa ari Bungeni

Dodoma. Baada ya kutumikia adhabu ya kutohudhuria vikao vitano vya Bunge, wabunge watano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), jana waliingia bungeni wakionekana kuwa na ari mpya.
Wabunge waliosimamishwa Aprili 17 ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa.
Wengine ni Highness Kiwia (Ilemela), Ezekiel Wenje (Nyamagana), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ (Mbeya Mjini) na Godbless Lema (Arusha Mjini).
Jana asubuhi Mchungaji Msigwa alikuwa miongoni mwa wabunge waliowahi kuingia mapema ndani ya Ukumbi wa Bunge na kufuatiwa na Lissu muda mfupi baada ya kikao kuanza.
Ndani ya Ukumbi wa Bunge, Msigwa alipata nafasi ya kuuliza swali namba 115 lililokuwa liulizwe na Joyce Mukya kuhusu Kampuni ya Kamwene Woodworks . Kwa upande wake, Lissu aliomba mwongozo wa Spika kuhusu kukwama kwa Bajeti ya Wizara ya Maji.
Wabunge wengine haikujulikana sababu za kutofika jana licha ya kuwa adhabu yao ilikwisha tangu April 25 huku taarifa zikieleza kuwa Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema alikuwa apelekwe mahakamani kujibu staka la uchochezi.
Mwananchi

Mitambo ya analojia Mbeya kuzimwa leo saa 6:00 usiku.

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imesema mitambo ya Analojia mkoani Mbeya itazimwa rasmi leo saa 6:00 usiku.
                                      Innocent Mungi, alisema Mkoa wa Mbeya.
Akizungumza na waandishi habari jana, Meneja Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Innocent Mungi, alisema Mkoa wa Mbeya umekuwa wa mwisho katika hatua za kuzima mitambo hiyo, katika awamu ya kwanza.

Mungi alisema uzimaji wa mitambo ya analojia na kuhamia katika mitambo ya Digitali katika awamu ya kwanza, ulihusisha Mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma, Tanga, Mwanza, Moshi na Arusha.

Alisema wakazi wa Mbeya walikwishafahamishwa kuhusu kuzimwa kwa mitambo hiyo kwa kufanya maandalizi yaliayohitajika ili kuepuka usumbufu ambao ungejitokeza.
 

Aliwataka Watanzania kuacha kunung’unika wanapokabiliwa na changamoto mbalimbali na hasa yanayohusu matatizo ya ving’amuzi na badala yake, wachukue za kutafuta ufumbuzi
Alisema baadhi ya Watanzania wamekuwa wakitumia muda mrefu kunung’unika na kushindwa kuchukua hatua za kukabiliana na changamoto zinazowakabili.

Shambulio lafanyika mjini Rome wakati serikali mpya ikiapishwa.


Serikali mpya nchini Italia imeapishwa na kumaliza hali ya iliyodumu kwa miezi kadhaa ya wasiwasi wa kisiasa, kufuatia uchaguzi mkuu wa mwezi Februari mwaka huu, ambao ulishindwa kutoa mshindi wa moja kwa moja.
Hata hivyo hafla ya kuapishwa kwa viongozi hao ilifunikwa na tukio la ufyatuaji risasi nje ya ofisi ya waziri mkuu ambapo maafisa wawili wa polisi walishambuliwa.
Watu walioshuhudia tukio hilo wamesema walimuona mwanaume mwenye silaha akifyatua risasi nje ya ofisi ya waziri mkuu katikati ya mji wa Rome, wakati baraza jipya la mawaziri likiendelea kuapishwa, umbali wa kilomita moja kutoka hapo, katika ikulu ya rais.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...