Sunday, March 24, 2013

MBEYA WABAINI CHANZO CHA WANAFUNZI KUFELI

Na, Modestus Nkulu

OFISA Elimu wa Mkoa wa Mbeya, Juma Kaponda ametangaza kiama kwa watu wanaomiliki vituo vya kufundishia watoto masomo ya awali baada ya kubaini kuwa ndiyo chanzo cha kuwa na wanafunzi wanaongia darasa la kwanza bila kujua kusoma na kuandika.

Kaponda aliyasema hayo jana wakati wa kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika kwenye ukumbi wa Mkapa jijini hapa na kuwahusisha watendaji kutoka wilaya zote za Mkoa wa Mbeya kujadili changamoto za maendeleo zinazowakabili wananchi.

Akitoa ufafanuzi, ofisa huyo aliwaambia wajumbe wa kikao hicho kuwa baada ya kubaini hiyo ni moja ya sababu ya kushuka kwa kiwango cha elimu mkoani hapa, ofisi yake imejipanga kuvikagua vituo vyote vya masomo ya awali.

Alisema vituo vingi vya chekechea ndiyo chimbuko la maandalizi mabovu ya wanafunzi wanaoanza darasa la kwanza ambao licha kusoma miaka miwili, wengi wao wamekuwa hawajui kusoma na kuandika hivyo kukosa sifa ya kujiunga darasa la kwanza.
Kaponda alisema hali hiyo imechangia hata wanafunzi wanaojiunga na elimu ya kidato cha kwanza pia baadhi yao kuwa na uwezo mdogo kutokana na msingi mbovu, hivyo kushindwa kusoma na kuandika.
Aidha, ofisa elimu huyo amewatupia lawama wasimamizi wa mitihani kwa kujihusisha na rushwa na kwamba ofisi yake inaendelea kujipanga kukabiliana na changamoto hiyo.
Dk. Michaeli Kadeghe ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, alisema suala la kufeli kwa wanafunzi na baadhi yao kutojua kusoma na kuandika, ni aibu ingawa tayari taarifa zao zinaonesha kuwa wamefaulu mitihani.

Alisema mfumo wa mitaala ya elimu hapa nchini ndilo chimbuko la ubovu huu kwa kuwa haiwezekani wanafunzi wakaendelea kuwa na mfumo wa kuchagua majibu, hivyo ni mambo yanayopaswa kusitishwa haraka.

Mkuu huyo alisema kwa mfumo wa mitaala hiyo, ndiyo inawafanya hata wasiojua kusoma na kuandika kufaulu kwa staili ya kubahatisha katika mitihani yao, hivyo ni wakati mwafaka wa kufanya mabadiliko katika jambo hilo kwa wanafunzi kupimwa uelewa.

Kikao hicho kilichohudhuriwa na watendaji wa serikali kutoka katika wilaya zote za mkoani hapa pamoja na viongozi wa vyama vya siasa na makundi mengine ya kijamii, kilikuwa chini ya Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Normani Sigala kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, Abasi Kandoro.
Chanzo;Tanzania daima

JACK CHUZI WA BONGO MOVIE AOLEWA BAADA YA KUKUBALI KUBADILI DINI....!!!

 Katika Hali ya Kushtusha na Kufuraisha....Staa wa Bongo Movie Jack Pentezel amewashtusha wengi baada ya Kuamua kubadili dini kuwa Muislamu kisha kuolewa na Mpenzi wake wa Muda Gadner Dibibi....

wadau wengi na wapenzi wa Bongo Movie wamekuwa wakihoji juu ya Ndoa Hiyo iliofungwa kisiri sana na kwa haraka,Je Ndoa Hiyo Itadumu? Je ni kweli wamehamua kukaa kwenye Maadili ya Ndoa..? au Ni kama Mchezo wa Mjini kubadilishana Dini na kuoana mwishowe ni kuachana....Tusubiri Tuone.....

Mpekuzi  inapenda kumtakia Jack Pentezel na Mumewe Gadner Dibibi Baraka Tele,Amani na Upendo utawale kwenye Maisha yao ya Ndoa..





MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AMJULIA HALI MZEE KINGUNGE NYUMBANI KWAKE

1Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Mzee Kingunge Ngombale Mwiru, wakati alipofika kumjulia hali nyumbani kwake Victoria jijini Dar es Salaam jana Machi 23, 2013 baada ya mzee Kingunge kulazwa Hospitali ya Muhimbili kwa uangalizi hivi karibuni alipougua ghafla. Picha na OMR2Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Mzee Kingunge Ngombale Mwiru, wakati alipofika kumjulia hali nyumbani kwake Victoria jijini Dar es Salaam jana Machi 23, 2013 baada ya mzee Kingunge kulazwa Hospitali ya Muhimbili kwa uangalizi hivi karibuni alipougua ghafla. Kulia ni Mke wa Mzee Kingunge. Picha na OMR3Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Mzee Kingunge Ngombale Mwiru, wakati alipofika kumjulia hali nyumbani kwake Victoria jijini Dar es Salaam jana Machi 23, 2013 baada ya mzee Kingunge kulazwa Hospitali ya Muhimbili kwa uangalizi hivi karibuni alipougua ghafla. Picha na OMR

WASICHANA WADOGO NAO WAINGIA KATIKA BIASHARA YA NGONO KWA SH. 5000

Ni usiku wa saa 4 nipo katika eneo maarufu la Buguruni lililopo jijini Dar es Salaam nikiwa nimekaa napata kinywaji kwenye baa moja.

Katika eneo hilo ambalo lipo pembezoni mwa Barabara ya Mandela si tulivu sana kutokana na pilika pilika za magari na watu wanaopita karibu kwa shughuli mbalimbali.
Huku nikiendelea kupata kinywaji mara naona wasichana wadogo wenye umri wa miaka 14 hadi 16 wakizunguka zunguka katika eneo hili la baa.

Awali nilifikiri walikuwa wakitafuta msaada au wakipita kuelekea nyumbani kwao, kwani umri wao haukunipa picha kwamba walikuwa kazini wakati huo wa usiku wa kiza kinene.

Kilichonifanya niwaangalie kwa udadisi zaidi ni kuona jinsi walivyovaa nguo ambazo zilionyesha nusu ya sehemu zao za mapaja, huku kifuani wakiwa wamevaa blauzi zilizobana zikionyesha matiti yao madogo ambayo yanaanza kuchipua.

Kilichonitisha zaidi ni kuona wasichana hawa ambao wakati huo walipaswa kuwa nyumbani wakiwa mkononi wameshika vinywaji vikali aina ya ‘viroba’ na wengine wakivuta sigara.

Hawa ni sehemu ndogo tu ya wasichana wadogo ambao hukesha usiku kucha katika baadhi ya mitaa ya jiji la Dar es Salaam wakitafuta wateja ili wapate fedha za kujikimu.
Mwandishi analazimika kuwadadisi wasichana hawa ili kujua nini kilichosababisha waingie katika biashara hii.

Inavyokuwa
Mwandishi ana mwita mmoja wa wasichana hawa Neema Mashiri (16) (sio jina lake halisi) na kuongea naye katika sehemu tulivu katika baa hiyo huku wakitumia vinywaji kunogesha mazungumzo.
Neema akiwa mwenye kujiamini na kazi yake bila ya kutetereka anasema kazi hiyo aliianza zaidi ya miezi sita nyuma huku akiwa tayari amekutana na idadi ya wanaume ambayo haikumbuki kutokana na wingi wake.
“Kwa siku moja nakutana na wanaume katiya watano hadi saba na hii hutegemea siku na siku, kwani kuna siku huwa na biashara ya kutosha na tunapata fedha za kutosha,”anasema Neema.
Neema akieleza ujira ambao hulipwa anasema ni Sh3,000 hadi Sh5,000 kwa muda usiozidi dakika 30 kwa mwanamume mmoja huku wakati kwa yule anayetaka kulala naye hadi asubuhi hutakiwa kulipa Sh10,000 hadi Sh15,000.
“Baadhi ya wanaume wamekuwa wakitufanyia vitendo vya kikatili kwa kutuingilia kinyume cha maumbile, lakini kutokana na hali ngumu ya maisha hukubali kwani dau huwa kubwa Sh10,000 hadi Sh12,000, lakini wengine hutumia ubabe tu na kututumia bila kutulipa,” anasema Neema na kuongeza;

WANAFUNZI WA CHUO CHA UTUMISHI WAJIPIGA PICHA CHAFU WAKATI WAKIFANYA ZINAA....!!

Wanafunzi  watatu  wa chuo  maarufu  nchini wametia aibu ya mwaka   baada  ya  kunaswa wakivunja  amri ya  sita  huku  wakijipiga  picha  chafu  za  tukio  hilo.....

Kwa mujibu wa ripota wetu, tukio hilo la aibu  linahusisha  wanaume  wawili  na  msichana  mmoja  aliyetambuliwa  kwa  jina  moja  la  Fetty.....

Katika tukio  hilo la aina yake, Fetty  anaonekana  akigawa  penzi  kwa  jamaa    huku  jamaa  mwingine  akiwapiga   picha  hatua  kwa  hatua.....

Kuvuja  kwa  picha:
Picha  hizi  zinadaiwa  kusambaa na kumfikia  mpekuzi wetu  baada  ya  wanafunzi  hao  kutofautina  na  hivyo  kuamua  KUTUBU  DHAMBI  HII  kwa  staili  ya  KUUMBUANA
 

BINTI ABAKWA KIKATILI NA VIJANA WAWILI....


Daily post imepokea   video moja  ya  kusikitisha  sana  ikimuonesha  msichana  mmoja  akibakwa na  wavulana  watatu.....

Katika video hiyo, binti anaoneka  kulia  kwa  huzuni  akiomba  msaada.Bahati  mbaya, shetani  hao  wawili  hawakuwa  na tone la  huruma kwa binti huyo.....
Watu hao  ni wakenya na wanaongea kiyoruba.

Ifuatayo ni sehemu fupi ya video hiyo:

Video inafunguka  kikatili  ikimuonesha  ikimuonesha  binti  akiwa amekabwa  na  anapumua kwa shida...

Binti: Nisaiidiee..( huku nalia)

Mbakaji: Jitahidi usioneshe sura yangu..( alikuwa anamweleza mwenzie aliyekuwa anarekodi)

Anayerekodi: Usijali, siichukui sura yako

Binti: Nimewakosea nini...nakufaaa...!!!

Mbakaji aliendelea  kusisitiza  kuwa  sura yake ifichwe  na  binti  aliendelea  kuomba  msaada bila mafanikio....

Hiyo  ni  picha ya mbakaji kama kuna mtu atafanikiwa kumtambua....
Credit: Dailpost-kenya

SHY - ROSE 'AMVUA NGUO' WAZIRI SITTA

SHY - ROSE
MBUNGE wa Afrika Mashariki Shy-Rose Bhanji amemtaka Waziri wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki (EAC), Samuel Sitta kuacha ubabaishaji kwa kutoa kauli za uongo kwa Watanzania na badala yake aongeze kasi ya uwajibikaji.
Shy-Rose alisema hayo jana akijibu kauli ya Waziri Sitta kwamba baadhi ya wabunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA), akiwemo yeye hawahudhurii vikao vinavyoitishwa na wizara hiyo na kwamba wamekuwa wakidai posho.
Akijibu kauli hiyo kwa maneno makali, Shy-Rose alimtaka Waziri Sitta na naibu wake kutoa vielelezo dhidi ya madai yao.
“Kama nilivyosema kwenye kikao cha Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, wizara imejitenga sana katika kutoa mwongozo na vile vile katika kuwafikia Watanzania walio wengi kwa kigezo kwamba haina fedha.
“Nimekuwa nikiwasiliana moja kwa moja na Naibu Waziri Abdullah Juma Sadallah kuhusu masuala mengi kwa maana ya kushirikiana na kupeana mwongozo, lakini majibu ya Naibu Waziri daima yamekuwa ni ya ubabaishaji na ya kukatisha tamaa, akisema kwamba wabunge wa EALA hawako chini ya wizara,” alisema Shy-Rose.
Mbunge huyo amemtaka Waziri Sitta kukaa na viongozi wa wizara yake ili apate ukweli wa mambo kuliko kurukia kujibu hoja kwa ubabaishaji kwani nia ni kuweka maslahi ya nchi mbele na si binafsi kama alivyofanya juzi yeye na naibu wake kwenye kikao cha kamati.
“Kwa vile amenitaja mimi moja kwa moja kuwa ni kinara wa kutoa udhuru… nasema si kweli hata kidogo… ninamheshimu Waziri Sitta kama kiongozi na kama mzazi wangu, lakini kauli yake imenisikitisha sana sana kwani amenifedhehesha kwenye jamii kwa kutoa kauli za kunichafulia jina langu kwa vile nimesema ukweli.
“Ni Waziri Sitta huyo huyo kwenye kikao cha bajeti mwaka jana bungeni Dodoma nilikuwa miongoni mwa wabunge aliowapongeza kwa kazi nzuri. Leo iweje abadili kauli yake? Au ni kwa vile nimesema ukweli?” anahoji Shy-Rose na kuongeza kuwa penye ukweli hatasita kuwaumbua viongozi ambao hawawajibiki.
Kuhusu suala la posho, alisema walialikwa mara moja tu bungeni lakini waliambiwa kila mtu ajigharamie malazi na usafiri.
“Hivi inaingia akilini kweli ualikwe kwenda safari halafu unaambiwa ujigharamie? Yeye Sitta na Naibu Waziri kwa vile wanatumia magari ya wizara na kuwekewa mafuta na kupewa posho kufika bungeni ndiyo maana inamwia rahisi kuongea kiubabaishaji.
“Licha ya wizara kukataa kutugharimia, lakini nilikuwa miongoni mwa wabunge waliohudhuria kikao cha bajeti ya wizara huko Dodoma… hiki ni kielelezo tosha kabisa suala la posho ni agenda ya uongo ili wizara kujisafisha kwenye kamati na Watanzania kwa ujumla.
“Hivi inaingia akilini kweli eti tunadai posho kuhudhuria vikao vya kupewa mwongozo tena hapa Dar?” anahoji Shy-Rose na kuongeza kuwa suala la posho kwake binafsi halijawahi kuwa agenda kuu hata siku moja.
“Hii hoja ya posho si ya kweli hata kidogo, kilichoongelewa ni vipi tunafika Dodoma iwapo hatujui tutalala wapi na tutakula nini. Sijaomba gharama hizi kama Shy-Rose bali kama Katibu wa Wabunge wa EALA,” aliongeza.
Shy-Rose alisema ni jambo la kusikitisha kwamba Watanzania walio wengi hawaifahamu Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa upana wake, hivyo juhudi za ziada zinahitajika kwa wizara kushirikiana na wabunge wa EALA ili kuwafikia Watanzania wengi kufahamu mtengamano huu.
Mbunge huyo alisema semina pekee iliyowahi kufanyika kwa wabunge wa EALA ilikuwa mara baada ya kuchaguliwa takriban miezi kumi iliyopita.
Katika semina hiyo iliyoandaliwa na Ofisi ya Bunge kwa kushirikiana na wizara, waliambiwa wizara itakuwa inatoa mwongozo kabla ya vikao vya Bunge kuanza ili kuweka maslahi ya taifa mbele na baada ya hapo hawajawahi kuitwa tena na wizara hiyo.
Kwa mujibu wa Shy-Rose, kikao pekee kilichoitishwa na wizara ni Januari mwaka huu jijini Bujumbura wakati ambapo mbunge huyo alikuwa nchini India kwa matibabu.
Juzi wakati Waziri Sitta akitoa ufafanuzi katika kikao cha Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Waziri Sitta alisema madai ya wabunge wa jumuiya hiyo kwamba hawashirikishwi katika vikao vya wizara yake sio ya kweli kwani wengi ni mabingwa wa kutoa udhuru na wanataka posho.
TANZANIA DAIMA

PAPA FRANCIS I AMTEMBELEA PAPA MSTAAFU BENEDICT

Walisali pamoja
walipokeana kwa bashasha
wakazungumza kwa nafasi baada ya chakula

WAZIRI SITTA AWAANIKA WABUNGE WA AFRIKA MASHARIKI KUHUSU POSHO

              Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta 
Na: Beatrice Moses
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta amewajibu wabunge wa Afrika Mashariki akisema wengi hawahudhurii vikao vya kupewa mwongozo kuhusu bunge hilo kwa kuwa “wanataka kulipwa posho”. Kauli hiyo ya Sitta ambaye pia ni Mbunge wa Urambo Mashariki, imekuja siku moja tangu wabunge hao waichongee wizara hiyo kwa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, kwamba imeshindwa kuwapa mwongozo pale wanapokwenda kwenye vikao vya Bunge la Afrika Mashariki. Akizungumza katika kikao cha kamati hiyo jana, Sitta alisema wabunge hao wamekuwa vinara wa kuomba posho kila
wanapotakiwa kuhudhuria kwenye mikutano ya wizara yake.
Katika maelezo yake Sitta alimeshutumu Katibu wa Wabunge hao, Shyrose Bhanji kuwa ndiye anayeongoza kwa kutoa udhuru mara kadhaa, hivyo kutoudhuria vikao vinavyoitishwa na wizara hiyo.
“ Wizara imejiwekea utaratibu mzuri wa kukutana na wabunge hao, lakini nafikiri katibu wao ndiye anayeongoza kwa kutohudhuria,” alisema Sitta na kuongeza:

CHECK OUT PICHA ZA HARUSI YA 2 FACE IDIBIA TAZAMA ILIVYOKUWA.



Celebrity Guests


Ini Edo, Kate Henshaw & Mike Ezuruonye





Tunde Demuren & Banky W



Tunde Demuren, Ubi Franklin & Banky W

photophotophotophoto
photo

photo

photo

photo

photo

photo

photo
photo

Saturday, March 23, 2013

MAKALIO YANGU HUNIFANYA NIKOSE AMANI MTAANII".....AGNESS MASONGANGE



VIDEO Queen maarufu Bongo, Agnes Gerald ‘Masogange’ ambaye muda mwingi amekuwa akiishi Afrika Kusini ameelezea jinsi maisha ya Bongo yalivyomchosha huku usumbufu anaopata kutokana na makalio yake makubwa ikiwa moja ya sababu. 

Akipiga stori mwandishi wetu, Masogange alisema umbile lake hilo limekuwa likimfanya akose amani anapokatiza mitaani, tofauti na Sauzi ambako wanawake wengi wamefungashia huku yeye akionekana ‘cha mtoto’.

“Muda mwingi niko Sauzi, Bongo miyeyusho na hili umbo langu nimekuwa nikisumbuliwa sana na wanaume lakini Sauzi hili langu la kawaida, wengi wamefungashia ile mbaya, kwa hiyo muda mwingi nitakuwa huko, huku nitakuwa nakuja na kuondoka,” alisema Masogange.

HATIMA YA HUKUMU SHEIKHE PONDA KUJULIKANA APRIL 18 MWAKA HUU.


Dar es Salaam. 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, Aprili 18, mwaka huu inatarajiwa kutoa hukumu katika kesi inayomkabili Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda (55) na wenzake 49.

Mbali na kupangwa kwa tarehe ya hukumu hiyo, Hakimu Mkazi, Victoria Nongwa jana aliutaka upande wa mashtaka na utetezi kuwasilisha hoja zao kama washtakiwa hao watakuwa na hatia ama la, Aprili 3, mwaka huu.
Juzi wakati Sheikh Ponda akijitetea aliieleza mahakama hiyo, kuwa yeye hana nyaraka za umiliki wa Kiwanja cha Malkazi Chang’ombe bali historia ya eneo hilo inawafanya wao kuwa wamiliki.
Sheikh Ponda na wenzake hao 49, wanakabiliwa na mashtaka ya kula njama, kuingia kwa jinai, kuvamia ardhi inayomilikiwa na Kampuni ya Agritanza Ltd kwa nia ya kujimilikisha isivyo halali, wizi wa mali yenye thamani ya Sh 59.6 milioni na uchochezi.
Akijitetea dhidi ya mashtaka hayo, Sheikh Ponda, akiongozwa na wakili wake, Juma Nassoro, alidai kuwa awali kiwanja hicho kilikuwa kinamilikiwa na Taasisi ya Jumuiya ya Kiislamu ya East African Muslim Welfare Society (EAMWS) ambayo ilivunjwa na Serikali mwaka 1958 na Serikali kuunda chombo kingine kilichosajiliwa kama Bakwata.
Alidai kuwa Bakwata iliundwa ili kusimamia shughuli zilizokuwa zikiendeshwa na Taasisi ya Jumuiya ya Kiislamu ya East African Muslim Welfare Society na siyo mali kama majengo, viwanja na hata shule.
“Tulitumia njia ya mazungumzo ya kidiplomasia kurejesha kiwanja cha Malkazi Chang’ombe kwa kuzingatia kuwa itatatua mgogoro huo katika njia nyepesi” alidai Sheikh Ponda.
Alidai Sheikh Ponda.Nyerere sasa tusilete mijadala isiyokuwepo.”
Hata hivyo, Sheikh Ponda alikubali kuwa yeye ni miongoni mwa watu waliohusika kutoa taarifa kwa maimamu wa misikiti mbalimbali kuwaeleza waumini wao kushiriki kujitolea katika ujenzi wa msikiti wa muda uliojenga katika eneo la Malkazi Chang’ombe Oktoba 11 na kukamilika Oktoba 14, mwaka jana.
Alidai kuwa walijenga msikiti huo baada ya kufanya makubaliano na mmoja wa wamiliki wa Kampuni ya Agritanza Ltd, Hafidhi, na kukubaliana kuweka alama ambayo kila Muislamu akiiona ataiheshimu na kutofanya shughuli zake binafsi katika eneo hilo na kupendekeza kujenga msikiti huo wa muda.
Kuhusu kukamatwa kwake.
Sheikh Ponda alidai kuwa yeye alikamatwa Oktoba 16, 2012, nyakati za saa 4 kasoro usiku alipokuwa akijiandaa kuingia katika Msikiti wa Tungi Temeke , akipanda ngazi alitokea mtu mmoja aliyekuwa kwenye gari nyeusi aina ya Toyota Harrier akimtaka amfuate.

MIKATABA 17 KUSAINIWA NA RAIS WA CHINA WAKATI WA ZIARA YAKE HAPA NCHINI

Na Eeuteri Mangi na Hussein Makame - Maelezo
Rais wa Jamuhuri ya watu wa China Xi Jinping anataraija kuanza ziara ya kihistoria nchini tangu kuapishwa  kwake kuitumikia  nchi hiyo ambapo katika ziara hiyo atasaini mikataba 17 ya ushirikiano wa  kiuchumi kati ya Serikali za Tanzania na nchi hiyo.
Akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa kimataifa Bernard Membe alisema kuwa  ziara hiyo ni ya kwanza barani Afrika  kwa Rais huyo mpya wa China baada ya kuchaguliwa kuliongoza taifa hilo Machi 14 mwaka huu.
Lengo la ziara hiyo ambayo itaanza tarehe 24 hadi 25 Machi mwaka huu ni kukuza uwekezaji  na biashara baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China.
Baadhi ya Mikataba hiyo itahusiana na uboreshaji wa sekta ya viwanda, kilimo hasa cha tumbaku ikiwemo kuwatafutia soko wakulima kutoka mikoa ya Tabora na Ruvuma ili waweze kuuza zao hilo katika soko la China.
Waziri Membe alisema kuwa; “Mikataba mingine ni ya kulipatia Shirika la Utangazaji Tanzania zana za kufanyia kazi na kuandaa mazingira ya ujenzi wa bandari ya Bagamoyo itakayounganishwa na reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA), reli ya kati na barabara”.  
Rais Xi Jinping pia atazindua na kukabidhi rasmi kituo cha Mikutano cha  Kimataifa cha Mwalimu Julius Nyerere  chenye ghorofa tatu na kumbi nne za mikutano  zenye uwezo  kupokea washiriki zaidi ya 1800 kilichogharimu dola za kimarekani milioni 29.7 zilizotolewa na Serikali ya China kwa lengo la kumuenzi Mwalimu Nyerere.
Waziri huyo alisema kuwa baada ya kufika nchini Rais Xi Jinping atazungumza na mwenyeji wake Rais Dk. Jakaya Kikwete pamoja na Viongozi Waandamizi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na baadaye atahudhuria dhifa ya kitaifa Ikulu Jijini Dar es salaam.
Siku ya pili ya ziara yake Rais Jinping  atazungumza rasmi na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk Ali Mohamed Shein pamoja na ujumbe wa viongozi waandamizi kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Waziri Membe aliongeza kuwa Rais Jinping atatoa hotuba maalumu kwa Tanzania, Afrika na Dunia kwa ujumla na  kuzungumzia sera ya Serikali mpya ya China kwa bara la Afrika ambayo itahudhuriwa na watu kutoka kada mbalimbali ikiwemo Viongozi na Maafisa Waandamizi wa Serikali, Wahadhiri wa Vyuo Vikuu,Wabunge, Viongozi wa Dini na Asasi za Kiraia na Wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali.
“Hotuba hiyo ya Rais wa China ataitoa kwa lugha ya Kichina na kutafsiriwa  kwa lugha ya Kiingereza na Kiswahili ili iweze kuifika dunia nzima, hivyo tunaviomba vyombo vya habari nchini vichukue fursa hiyo kuwa vya kwanza kuutangazia Ulimwengu” alisema Waziri Membe.
Ziara hiyo ya Rais wa Jamhuri ya Watu wa China  ni muendelezo wa uhusiano mzuri kati ya nchi hiyo na Tanzania ulioasisiwa na viongozi  wa mataifa hayo mawili, yaani Mao Zedong wa China na  Mwalimu Julius Nyerere wa Tanzania.
Rais Jinping ataondoka nchini Machi 25 saa 10:40 jioni kuelekea nchini Afrika Kusini kuhudhuria mkutano wa tano wa Wakuu wa Nchi zinazokuwa kwa kasi kiuchumi ambazo ni Brazil, Urusi, India, China na Afrika ya Kusini (BRICS). 

KAMATI YA ULINZI NA USALAMA MKOA WA MBEYA IMEPIGA MARUFUKU MAANDAMANO YALIYOPANGWA NA CHADEMA TAREHE 25 MACHI MWAKA HUU

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Dk. Norman Sigalla




KAMATI ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Mbeya limepiga marufuku maandamano yoyote kufanyika Mkoani hapa yenye lengo la kushinikiza Raisi Kikwete kumfukuza kazi Waziri wa Elimu kutokana na matokeo mabaya ya kidato cha nne.
  
Maandamano hayo yalipangwa kufanywa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo( CHADEMA)  Machi 25, Mwaka huu, ambayo yamepangwa kuhusisha Mikoa yote ya Nyanda za Juu Kusini na kufanyika Jijini Mbeya kwa lengo hilo.
Akitoa taarifa ya Kamati hiyo kwenye Mkutano wa ushauri wa Mkoa (RCC),Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Dk. Norman Sigalla amesema kamati hiyo ilikaaa Machi 19, mwaka huu na kuamua kuwa hakuna mantiki ya kufanyika kwa maandamano hayo.
  
Amesema sababu iliyoonekana ni kwamba tayari tume imeshaundwa kuchunguza madai hayo hivyo hamna sababu ya watu kuandamana kushinikiza waziri kujiuzulu ili hali kamati itakuja na majibu juu ya kile kilichosababisha matokeo kuwa mabaya.
  Sigalla amesema kamati ya Ulinzi na Usalama imeona kuwa kuendelea kufanya maandamano soyo ufumbuzi wa matatizo bali yataathiri shughuli za kujitafutia kipato kwa wananchi wa kawaida pamoja na usalama wa mali.
  
Ameongeza kuwa usalama wa Wananchi wa Mkoa wa Mbeya utaathirika kutokana na wanaotarajiwa kufanya maandamano hayo wamehamasishwa kutoka mikoa ya Iringa, Njombe, Ruvuma  ambako kutajaza idadi kubwa ya watu.

Amesema kamati pia inaamini kuwa maandamano ya aina hiyo yanaweza kusababisha  uvunjifu wa amani hivyo kamati inapiga marufuku maandamano ya aina yoyote kufanyika Mkoani Mbeya na kuongeza kuwa yapelekwe maeneo mengine.
  
Aidha ametoa rai kwa vikundi vya kisiasa, kijamii na vikundi vya dini kuweka mbele maslahi ya wananchi kwa kuhimiza kujitafutia vipato kutokana na fursa za maendeleo zilizopo.
  
Hata hivyo Mwenyekiti huyo wa kamati ya Ulinzi na Usalamaya Mkoa ameviagiza vyombo vyote vya Ulinzi na usalama kuendelea kuhakikisha kwamba Mkoa wa Mbeya unaendelea kuwa tulivu na amani ambayo itawezesha wananchi kuendelea na shughuli za kujiongezea kipato bila bugudha yoyote.
Maandamano hayo yamepangwa kufanyika Machi 25, Mwaka huu kufuatia Mkutano wa Hadhara uliofanyika hivi karibuni wa Chadema katika Viwanja vya Shule ya Msingi RuandaNzovwe Ilomba Jijini Mbeya Februari 28, Mwaka huu, ambapo Mwenyekiti wa Chama hicho taifa Freeman Mbowe aliagiza kufanyika kwa maandamano hayo kwa namna yoyote ile.
  Pia katika kuhakikisha dhana hiyo inatimia Mwenyekiti huyo pia alichangisha zaidi ya Shilingi Milioni Tatu ambazo alidai kuwa zitasaidia wakati wa maandamano katika kununulia maji ya kunawa baada ya kupigwa na mabomu pia kununulia dawa za huduma ya kwanza kwa watakaoathirika na maandamano hayo.

Friday, March 22, 2013

JK aziponda Simba, Yanga


RAIS Jakaya Kikwete amezipiga ‘kijembe’ klabu kongwe hapa nchini, Simba na Yanga, kutokuwa na maendeleo kisoka na kuiacha Azam FC, ikiwapiga kumbo kila idara huku wao wakiendekeza ushirikina mbele na migogoro.
Kikwete aliyasema hayo jana, wakati akiweka jiwe la msingi la klabu ya Azam iliyoko Chamazi nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.

Rais aliipongeza Azam kwa hatua ambayo imefikia, licha ya kuwa na uchanga katika soka na kuzipita klabu za Simba na Yanga.

Alisema endapo Azam inataka kupiga hatua na kuifikisha nchi mbali kwa kulitangaza jina la Tanzania, ifanye mambo yake bila kuzifuata timu kongwe na kudai kuwa itafika mbali kitaifa na kimataifa pia.
“Naamini mna uwezo wa kufika mbali katika ulimwengu wa soka, ila msiwe karibu na hizi timu, mtajikuta mnaishia hapahapa; wao mechi mechi moja wanatolewa,” alisema Kikwete na kuwafanya watu walioshuhudia hafla hiyo kuvunjika mbavu.
Aidha Kikwete alisema kutokana na mafanikio ambayo Azam wameyapata hadi sasa, ikiwemo uwanja na mambo mengine, imeonekana kama wao ndio vigogo na kusababisha kuogopwa na jamaa ambao wanajifanya wakubwa.
 “Mpaka sasa haionekani nani mkubwa, maana kuwa na wanachama wengi sio ishu na nyie nina imani mnaweza kulileta hili Kombe la Shirikisho nyumbani, najua timu kubwa zikiwa na mechi na nyie zinakuwa na wasiwasi, hivyo basi mpaka sasa nyie ndio mtasaidia soka la Tanzania kukua,” alisema Kikwete.

Alikwenda mbali zaidi na kuwataka Azam, kuacha kufuata vivuli vya hizo timu na kujisimamia wenyewe, kwa kuwa timu mbili kongwe zina wanachama wanaopiga kura kwa kuhongwa, sambamba na kutumia muda mwingi kulumbana, wakati hawana kitu wanachoingiza katika timu.

Alisema timu kubwa zikiambiwa kutumia Uwanja wa Chamazi, zinaanza kuleta maneno ya ajabu na kuongeza kuwa ushirikina haufai katika soka, cha muhimu ni kucheza mpira na sio kazi ya kuandaa kamati za ufundi na kushindwa kutazama benchi la ufundi ili kujenga timu.
“Ingekuwa mpira ni ushirikina, basi Afrika tungekuwa mabingwa kila mwaka, kama timu inaona uchawi dili, basi ikusanye wachawi wote dunia nzima ikae nao klabuni kwao tuone!” aliongeza Kikwete.

Aliwataka Azam endapo watakuwa na shida yoyote, wasisite kumjulisha na kudai kuwa ombi lao la kupunguziwa VAT katika bidhaa zao za kisoka, atawasiliana na wahusika ili aweze kulipatia ufumbuzi.
Naye Mkurugenzi wa Azam, Yusuph Bakhressa, alishukuru sana kupata nafasi ya Rais kuzindua mradi wao maalumu, ambao lengo lake ni kukuza na kuendeleza mpira wa miguu nchini.
Alisema hadi sasa wametumia sh bilioni 3 katika mradi huo.
Katika hafla hiyo, Rais aliambatana na mkewe Mama Salma Kikwete, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara, Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam, Mecky Saidi Sadick, na viongozi mbalimbali.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...