Saturday, March 23, 2013

KAMATI YA ULINZI NA USALAMA MKOA WA MBEYA IMEPIGA MARUFUKU MAANDAMANO YALIYOPANGWA NA CHADEMA TAREHE 25 MACHI MWAKA HUU

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Dk. Norman Sigalla




KAMATI ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Mbeya limepiga marufuku maandamano yoyote kufanyika Mkoani hapa yenye lengo la kushinikiza Raisi Kikwete kumfukuza kazi Waziri wa Elimu kutokana na matokeo mabaya ya kidato cha nne.
  
Maandamano hayo yalipangwa kufanywa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo( CHADEMA)  Machi 25, Mwaka huu, ambayo yamepangwa kuhusisha Mikoa yote ya Nyanda za Juu Kusini na kufanyika Jijini Mbeya kwa lengo hilo.
Akitoa taarifa ya Kamati hiyo kwenye Mkutano wa ushauri wa Mkoa (RCC),Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Dk. Norman Sigalla amesema kamati hiyo ilikaaa Machi 19, mwaka huu na kuamua kuwa hakuna mantiki ya kufanyika kwa maandamano hayo.
  
Amesema sababu iliyoonekana ni kwamba tayari tume imeshaundwa kuchunguza madai hayo hivyo hamna sababu ya watu kuandamana kushinikiza waziri kujiuzulu ili hali kamati itakuja na majibu juu ya kile kilichosababisha matokeo kuwa mabaya.
  Sigalla amesema kamati ya Ulinzi na Usalama imeona kuwa kuendelea kufanya maandamano soyo ufumbuzi wa matatizo bali yataathiri shughuli za kujitafutia kipato kwa wananchi wa kawaida pamoja na usalama wa mali.
  
Ameongeza kuwa usalama wa Wananchi wa Mkoa wa Mbeya utaathirika kutokana na wanaotarajiwa kufanya maandamano hayo wamehamasishwa kutoka mikoa ya Iringa, Njombe, Ruvuma  ambako kutajaza idadi kubwa ya watu.

Amesema kamati pia inaamini kuwa maandamano ya aina hiyo yanaweza kusababisha  uvunjifu wa amani hivyo kamati inapiga marufuku maandamano ya aina yoyote kufanyika Mkoani Mbeya na kuongeza kuwa yapelekwe maeneo mengine.
  
Aidha ametoa rai kwa vikundi vya kisiasa, kijamii na vikundi vya dini kuweka mbele maslahi ya wananchi kwa kuhimiza kujitafutia vipato kutokana na fursa za maendeleo zilizopo.
  
Hata hivyo Mwenyekiti huyo wa kamati ya Ulinzi na Usalamaya Mkoa ameviagiza vyombo vyote vya Ulinzi na usalama kuendelea kuhakikisha kwamba Mkoa wa Mbeya unaendelea kuwa tulivu na amani ambayo itawezesha wananchi kuendelea na shughuli za kujiongezea kipato bila bugudha yoyote.
Maandamano hayo yamepangwa kufanyika Machi 25, Mwaka huu kufuatia Mkutano wa Hadhara uliofanyika hivi karibuni wa Chadema katika Viwanja vya Shule ya Msingi RuandaNzovwe Ilomba Jijini Mbeya Februari 28, Mwaka huu, ambapo Mwenyekiti wa Chama hicho taifa Freeman Mbowe aliagiza kufanyika kwa maandamano hayo kwa namna yoyote ile.
  Pia katika kuhakikisha dhana hiyo inatimia Mwenyekiti huyo pia alichangisha zaidi ya Shilingi Milioni Tatu ambazo alidai kuwa zitasaidia wakati wa maandamano katika kununulia maji ya kunawa baada ya kupigwa na mabomu pia kununulia dawa za huduma ya kwanza kwa watakaoathirika na maandamano hayo.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...