Saturday, March 23, 2013

HATIMA YA HUKUMU SHEIKHE PONDA KUJULIKANA APRIL 18 MWAKA HUU.


Dar es Salaam. 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, Aprili 18, mwaka huu inatarajiwa kutoa hukumu katika kesi inayomkabili Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda (55) na wenzake 49.

Mbali na kupangwa kwa tarehe ya hukumu hiyo, Hakimu Mkazi, Victoria Nongwa jana aliutaka upande wa mashtaka na utetezi kuwasilisha hoja zao kama washtakiwa hao watakuwa na hatia ama la, Aprili 3, mwaka huu.
Juzi wakati Sheikh Ponda akijitetea aliieleza mahakama hiyo, kuwa yeye hana nyaraka za umiliki wa Kiwanja cha Malkazi Chang’ombe bali historia ya eneo hilo inawafanya wao kuwa wamiliki.
Sheikh Ponda na wenzake hao 49, wanakabiliwa na mashtaka ya kula njama, kuingia kwa jinai, kuvamia ardhi inayomilikiwa na Kampuni ya Agritanza Ltd kwa nia ya kujimilikisha isivyo halali, wizi wa mali yenye thamani ya Sh 59.6 milioni na uchochezi.
Akijitetea dhidi ya mashtaka hayo, Sheikh Ponda, akiongozwa na wakili wake, Juma Nassoro, alidai kuwa awali kiwanja hicho kilikuwa kinamilikiwa na Taasisi ya Jumuiya ya Kiislamu ya East African Muslim Welfare Society (EAMWS) ambayo ilivunjwa na Serikali mwaka 1958 na Serikali kuunda chombo kingine kilichosajiliwa kama Bakwata.
Alidai kuwa Bakwata iliundwa ili kusimamia shughuli zilizokuwa zikiendeshwa na Taasisi ya Jumuiya ya Kiislamu ya East African Muslim Welfare Society na siyo mali kama majengo, viwanja na hata shule.
“Tulitumia njia ya mazungumzo ya kidiplomasia kurejesha kiwanja cha Malkazi Chang’ombe kwa kuzingatia kuwa itatatua mgogoro huo katika njia nyepesi” alidai Sheikh Ponda.
Alidai Sheikh Ponda.Nyerere sasa tusilete mijadala isiyokuwepo.”
Hata hivyo, Sheikh Ponda alikubali kuwa yeye ni miongoni mwa watu waliohusika kutoa taarifa kwa maimamu wa misikiti mbalimbali kuwaeleza waumini wao kushiriki kujitolea katika ujenzi wa msikiti wa muda uliojenga katika eneo la Malkazi Chang’ombe Oktoba 11 na kukamilika Oktoba 14, mwaka jana.
Alidai kuwa walijenga msikiti huo baada ya kufanya makubaliano na mmoja wa wamiliki wa Kampuni ya Agritanza Ltd, Hafidhi, na kukubaliana kuweka alama ambayo kila Muislamu akiiona ataiheshimu na kutofanya shughuli zake binafsi katika eneo hilo na kupendekeza kujenga msikiti huo wa muda.
Kuhusu kukamatwa kwake.
Sheikh Ponda alidai kuwa yeye alikamatwa Oktoba 16, 2012, nyakati za saa 4 kasoro usiku alipokuwa akijiandaa kuingia katika Msikiti wa Tungi Temeke , akipanda ngazi alitokea mtu mmoja aliyekuwa kwenye gari nyeusi aina ya Toyota Harrier akimtaka amfuate.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...