Monday, March 18, 2013

HUYU HAPA YULE MWANAUME AMBAYE ANATARAJIWA KUFANYIWA OPARESHENI ILI KUWEKEWA UUME...

 
Historia mpya inakaribia kuandikwa duniani baada ya mwanaume ambaye anajulikana kwa jina Andrew Wardle, kutoka Stalybridge, Greater Manchester huko Uingereza ambaye alizaliwa bila uume, kufanya mpango wa kutengenezewa na kuwekewa kiungo hicho kwa njia ya oparesheni.

Mwanaume huyu ambaye kwa sasa anaumri wa miaka 39, anatarajiwa kuwa mwanaume wa kwanza kabisa duniani kufanyiwa oparesheni kama hii na ajabu zaidi ni kwamba, kiungo hiki kitatengenezwa kutoka sehemu ya mkono wake.
 
Andrew Wardle Katika mahojiano yake na mtandao wa The Sun, Wardle mwenyewe anasema kuwa, hakuwahi kufikiria kutokea kwa siku ambayo anaweza kupata kiungo hiki muhimu kwa mwanaume na ambacho kinafanya kazi sawasawa, na endapo itakuwa ni ya mafanikio, ataanza kuishi kama mtu wa kawaida. Madaktari kutoka chuo kikuuu cha London tayari wameshakiri ugumu wa zoezi ili lakini wamesema kuna uwezekano mkubwa wa kufanikiwa.
Katika hali yake aliyokuwa nayo sasa, Wardle anadai kuwa amekwishawahi kulala na zaidi ya wanawake 100, na asilimia 20% tu ya wanawake hawa ndio alioweza kuwaambia ukweli.
Wardle kwa sasa anafanya kazi kama mlinzi, mpishi na mhudumu na katika historia yake, amekwishapata matukio mbalimbali ya kunyanyaswa kutokana na hali yake na kupoteza marafiki kadhaa wa kike, na amekwishakuwa akijihusisha na matumizi ya madawa ya kulevya kama kitu cha kumfariji.

ANGALIA ANGALIZO ALILOTOA JOHN MNYIKA

MUHIMU: Tahadhari kuna mtu amefungua akaunti kwa jina langu na picha ambayo si halali na tayari anafanya mawasiliano na kuandika vitu mbalimbali. Ifahamike wazi katika Facebook nina akaunti hii tu: http://www.facebook.com/john.mnyika?fref=ts na fan page: http://www.facebook.com/pages/John-Mnyika/113913842009362 na upande wa Twitter akaunti yangu ni: @jjmnyika pia; @TeamJohnMnyika na @TeamUbungo ambazo zipo chini ya Ofisi yangu! na blogu ni: www.mnyika.blogspot.com

Kwa wale ambao wanaona wanashindwa kuwa friends katika akaunti yangu kwasababu ya kufika ukomo basi nawaomba mjiunge na fan page yangu kwa kupitia link hii:http://www.facebook.com/pages/John-Mnyika/113913842009362na si akaunti nyingine!

Naomba tuchukue tahadhari kwa mawasiliano yoyote nje ya akaunti hizo tajwa.

Asanteni na naomba radhi kwa kadhia au usumbufu wowote uliotokea kwa yeyote kutokana na akaunti feki zilizofunguliwa kwa jina langu.

MKE WA MTU AFUMANIWA AKIZINI NA MDOGO WA MUME WAKE ( SHEMEJI YAKE)

Na Dustan Shekidele, Morogoro
MWANAMKE aliyefahamika kwa jina la Bahati ambaye ni mke wa Mrisho Juma, hivi karibuni alikumbwa na aibu ya aina yake baada ya kunaswa laivu ‘akingonoka’ na shemeji yake.
  
Tukio hilo lililoshuhudiwa na umati wa watu lilijiri Machi 11, mwaka huu mchana kweupee katika eneo la Mafisa kwa Mbambi ndani ya chumba cha Mbaji Hamis ambaye ni mdogo wa Mrisho.
Akizungumza na mwandishi wetu, Mrisho ambaye anafanya kazi ya kupiga debe katika stendi ya mabasi ya Msamvu alisema, fumanizi hilo halikutokea kwa kuweka mtego bali ni Mungu tu.

Alieleza kuwa alikamatwa Ijumaa na kutupwa mahabusu kwa kosa la kutovaa ‘yunifomu’. Mkewe na mdogo wake wakawa wanampelekea chakula.


“Jumapili jioni walikuja tena kuniletea chakula ila kwa bahati nzuri Jumatatu nikapewa onyo na kuachiwa. Cha ajabu nilipofika nyumbani nilimkuta mtoto wangu wa miaka 2 analelewa na majirani.

“Nilipowauliza mke wangu yuko wapi walidai tangu Jumamosi hajaonekana kwa maelezo kwamba amekwenda kushughulikia dhamana yangu,” alisema Mrisho na kuongeza kuwa aliendelea kumtafuta sehemu mbalimbali hadi alipoamua kwenda nyumbani kwa mdogo wake.

“Nilipofika nilimkuta mke na mdogo wangu wakiwa pamoja kitandani. Baada ya mdogo wangu kuniona alinyanyuka na kuvaa bukta kisha akatoka nduki,” alisema Mrisho. 


Ikaelezwa kuwa, baada ya mwanaume huyo kumfumania mkewe huku majirani wakishuhudia, alimshushia kipigo kisha akampa talaka kabla ya kuamua kumrudisha kwao Tabora.

Akizungumza na mwandishi wetu kuhusiana na kufumaniwa huko, Bahati alisema shemeji yake alimlazimisha kulala naye baada ya kutoka polisi kumpelekea chakula mumewe.

Mjumbe wa Serikali ya Mtaa, Rehema Dimoso alikiri kutokea kwa tukio hilo kwenye mtaa wake.

TRAFIKI AFARIKI BAADA YA KUGONGWA NA GARI ENEO LA BAMAGA


Trafiki Elikiza baada ya kugongwa na gari eneo la Bamaga muda huu

Trafiki wa kike aliyejulikana kwa jina moja la Elikiza aliyekuwa akiongoza magari 
eneo la Bamaga, Mwenge jijini Dar, akifunikwa na wasamaria wema baada ya kugongwa na gari na inadhaniwa kuwa amekufa papo hapo.

SOURCE GLOBAL PUBLISHER

DEREVA ANUSURIKA KUCHARANGWA MAPANGA KWA KUMCHOMEKEA MWENZAKE IRINGA


 Dereva  wa daladala  ambae  jina lake  halikuweza  kupatikana mara moja akiwa ameshika panga mkononi akitoka kumkoromea dereva  mwenzake aliyetaka kumsababishia ajali kwa kumchomekea  eneo la Mshindo mjini Iringa  leo. PICHA NA MAELEZO FRANCIS GODWIN


 Hapa akitaka  kumcharanga mapanga  dereva  mwenzake  ,huku mwenyewe akinyosha  mikono  juu  kuomba  kusamehewa

Tabia ya  madereva  daladala  mjini Iringa  kuendesha  vyombo  hivyo bila kuzingatia  sheria limeendelea  kuongezeka na ajali   pia  kila kukicha

TUMEKUWA TUKILEA MTOTO MCHAWI KWA MUDA MREFU BILA KUJUA".....NIKITA WA BONGO MOVIE

 KELVIN....

STAA wa filamu za Kibongo, Ahmed Khalfan ‘Kelvin’ na mkewe mwigizaji, Elizabeth Chijumba ‘Nikita’ wamesema mmoja wa watoto pacha waliowaasili (adopt) mwenye umri wa miaka sita, ameonesha matendo ya kichawi...
  

Akizungumza na mwandishi wetu, Kelvin alisema waliwachukua watoto hao mapacha kwa bibi yao Mtwara mwaka 2009 kwa lengo la kuwalea kutokana na mazingira magumu waliyokuwa nayo lakini walipofika Dar, mmoja alianza kuonesha vitendo tofauti vya kichawi.

“Wakati tukiendelea kuishi nao, tulimuona mmoja ana vitukovituko mara kwa mara na tuligundua kuwa mke wangu alikuwa akiumwaumwa kila alipomgombeza mtoto huyo.

“Kuna siku niliamka usiku kwenda kwenye chumba walichokuwa wakilala watoto hao, nikamkuta akiwa uchi akirukaruka kitandani na nilipomshtua alijilaza kitandani na asubuhi tulipomuuliza, alisema muda ule bibi yake alikuwa akimrudisha kutoka kuroga Tanga."

Kwa upande wake, Nikita alipomdadisi mtoto huyo kuhusu vitendo hivyo vya kichawi, alimwambia kuwa bibi yake anataka kumuua kwa sababu wanamzuia asirudi kijijini kwao Mtwara akaendelee kufanya kazi za kichawi. 

“Kwa kweli nampenda sana lakini sina budi kumrudisha nyumbani kwao, roho inaniuma kwa sababu nilimzoea,”alisema Nikita.

Mwandishi wetu alipomuuliza mtoto huyo kuhusiana na sakata hilo, alikiri kuwa ni kweli bibi yake ni mchawi na huwa anamchukua kwenda sehemu mbalimbali kuroga kwa kutumia usafiri wa ungo na ndiye anayemroga Nikita.

KAMPUNI YA SIMAMIA YASHUSHA MABANGO YA MATANGAZO YA KAMPUNI YA COCACOLA TAWI LA MBEYA KUTONANA NA KUDAIWA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 102

Wafanaya kazi wa kampuni ya Simamia wakishusha mabango ya matangazo ya biashara ya kampuni ya Cocacola tawi la Mbeya kazi ya kushusha mabango hayo imeanza maeneo ya kituo kiku cha mabasi yaendayo mikoani


Kampuni hiyo ya simamia ikiendelea na kazi ya kufuta maandishi ya kampuni ya cocacola kwa kutumia rangi nyeusi

Moja ya wakurugenzi wa kampuni ya simamia akiongea na mfanyakazi wa kampuni ya cocacolamwenye kitambulisho shingni akiulizia kulikoni mbona mnatoa mabango yetu? alipata jibu la halaka toka kwa mkurugenzi huyo kuwa mnadaiwa matangazo ya mabango tunayotoa

Mtumishi huyo wa kampuni ya cocacola nae akaungana na sisi katika kupiga picha utoaji wa mabango hayo ya kampuni yao 


Moja ya maafisa wa kampuni ya cocacola alipita hapo kituo kikuu cha mabasi ya kwenda mikoani na kujionea mwenyewe mabango yakitolewa cha ajabu mbeya yetu iliwasiliananae kwa simu jibu alilotupa kuwa hana habari kama mabango yao yanatolewa ilibidi tushangae maana picha ni hii wakati akipita standi hiyi ya mabasi akijionea uondoaji wa mabango yao


Mbali na hapo alienda moja kwa moja katika kampuni ya simamia lakini hakushuka kwenye gari yake akaondoka  kwa kasi mambo hayo




Kazi inaendelea ya kushusha mabango ya matangazo ya biashara ya kampuni ya cocacola mbeya


Mkurugenzi wa   Wakala wa kukusanya ushuru wa mabango ya biashara na Hoteli  Jiji la Mbeya Simamia Company Limited, Ndugu  Aloyce Mrema amesema kampuni yake inatekeleza sheria ya jiji ambayo inataka kila bango la tangazo linatakiwa kulipiwa.




Halimashauri ya jiji la Mbeya kupitia wakala wa ukusanyaji wa  ushuru wa mabango SIMAMIA imeyashusha mabango ya kampuni  ya Vinywaji baridi ya Cocacola tawi la Mbeya kutokana na kudaiwa zaidi ya shilingi milioni 102.
Hata hivyo kampuni hiyo iko   hatiani kuburutwa mahakami kwa kushindwa kulipia gharama za mabango ya matangazo  yaliyowekwa maeneo mbali mbali ya Jiji hilo .
Kampuni hiyo imeshindwa kulipia gharama za kuweka matangazo hayo kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2012 – 2013 ambapo deni limefikia Shilingi Milioni 102 ambazo walitakiwa kuzilipa kutokana na wingi wa mabango hayo.
Akithibitisha kudaiwa kwa kampuni hiyoMkurugenzi wa   Wakala wa kukusanya ushuru wa mabango ya biashara na Hoteli  Jiji la Mbeya Simamia Company Limited, Ndugu  Aloyce Mrema amesema kampuni yake inatekeleza sheria ya jiji ambayo inataka kila bango la tangazo linatakiwa kulipiwa.
Amesema kutokana na Kampuni ya Cocacola kushindwa kulipia mabango hayo kampuni ya Simamia imeamua kutoa mabango yote yaliyondani ya Jiji la Mbeya ambapo alisema hatua itakayofuata ni kuifikisha mahakamani kampuni hiyo kwa kushindwa kutekeleza agizo la Halmashauri ya Jiji.
Amesema kabla ya kuanza kutoa mabango hayo wameshapeleka  barua za kuwakumbusha zaidi tatu lakini bado hawakuitikia wito wa kulipa mapema gharama hizo zilizowataka hadi ifikapo Machi 18, Mwaka huu kutoa majibu au kulipia mabango hayo.
Mrema amesema utaratibu wa kampuni hiyo ni kuhakikisha kuwa kila kampuni iliyoweka bango la biashara katikati ya Jiji la Mbeya inalipa gharama kwa mujibu wa Sheria za Jiji ambapo kwa takayeshindwa kufanya hivyo atachukuliwa hatua ikiwa ni pamoja na kufikishwa mahakamani.
Aidha ametoa wito kwa makampuni makubwa kuheshimu sheria za nchi na siyo kukiuka kutokana na kuwa na fedha nyingi ambapo aliongeza kuwa kwa sasa zaidi ya makampuni sita makubwa ya Jiji la Mbeya yameshapewa barua za kuwakumbusha kulipia mabango hayo.
Hata hivyo ameyataja makampuni hayo kuwa ni pamoja na makampuni ya simu za mkononi ya Tigo, Vodacom, Airtel,Zantel, Tbl na Pepsi ambayo yameshapewa barua za kuwakumbusha kulipia mabango hayo yakiwemo makampuni ya watu binafsi.
Akizungumzia hatua hiyo Ofisa wa Cocacola aliyejitambulisha kwa jina moja la Zekaria amesema hajui lolote kuhusu kuondolewa kwa mabango ya kampuni yake na wakala wa Jiji Simamia ambapo amesema atalifuatilia na kulipeleka kitengo kinachohusika kwa ajili ya kulitolea taarifa.
Hata hivyo Ofisa huyo alionekana kukwepa kutokuwa na taarifa juu ya kampuni hiyo kung’oa mabango ili hali baadhi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo walionekana wakipiga picha na kufuatilia hatua zote zilizokuwa zikifanyika.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Haslmashauri ya Jiji la Mbeya Juma Iddi alipoulizwa juu ya utaratibu wa kampuni hiyo wa kutoa mabango ya biashara ya kampuni ya Cocacola amesema hajui lolote kwa sababu kampuni ya Simamia  ilishinda tenda ya kukusanya ushuru wa Hoteli na mabango ya biashara hivyo yeye hana uwezo wa kuingilia.
Na Mbeya yetu

TAARIFA YA RIDHIWANI KIKWETE KUKANUSHA YALIYOANDIKWA DHIDI YAKE KATIKA MITANDAO YA JAMII

Ndugu zangu habari za wikiendi. 

Yapo mambo machache ningependa kuwashirikisha ili kuweka kumbukumbu sawa na pia kuzuia upotoshaji ambao unaweza kujitokeza siku za usoni iwe kwangu, kwako au kwa mtu mwingine.

Mojawapo ya mambo makubwa ambayo yamejitokeza siku za karibuni hasa katika suala la Teknolojia na habari ni jambo la sheria za faragha (privacy and privacy lawas). 

Tumeshuhudia kufungwa kwa gazeti za News of The World, mali ya bilionea Rupert Murdoch wa Kimarekani baada ya kudhihirika alitumia wataalam wa teknolojia (hackers) kutafuta siri za watu mashuhuri kwa kuingia katika simu zao za mkononi kinyume cha utaratibu na sheria za faragha (Privacy Laws). Tumeshuhudia pia wahalifu hao hao wa mtandao wakifanya mengi kama kuvamia kwa mitandao ya makampuni makubwa kama Sony na mengineyo na hata katika mitandao hii ya kijamii upo wakati marafiki zako wanakwambia mbona umenitumia kitu kisichoeleweka, na baadaye kuja kugundua kwamba si wewe uliyefanya hivyo.

Tarehe 1, 8 na 9 mwezi huu wa Machi nilikuwa Dar es Salaam kwa shughuli zangu za kawaida kimaisha lakini ziko updates 5 zilifanyika hapa moja ikimhusu ndugu Absalom Kibanda. Ni ajabu kwamba baadhi ya waandishi tena waliojivika taji la usahihi katika uandishi waliiandika habari hiyo bila hata kuniuliza kwamba ni nini kinatokea. Tunajitahitahidi na kutamani kuwa na Taifa la waandishi makini na wenye kufuata maadili lakini wapo wanaoturudisha nyuma. 

Ni ajabu gazeti kuandika jambo lisilo la kweli huku wahusika wakiwa na kila uwezo wa kumfikia yule wanayedhani kwamba ameandika na kumhoji ili kuhakiki habari. Kazi ya uhariri ni kuhakiki. Ikiwa mtu atakimbilia kuandika jambo likuhusulo ambalo hana hakika nalo na alikuwa na kila uwezo wa kuwasiliana na wewe na kukuuliza lazima utajiuliza maswali mengi. Kwanza: Nini hasa lengo lake na pili ufahamu wake wa kile anachokifanya kwa maana ya taaluma yake katika kazi anayoifanya.

Napenda kuwaambia kwamba katika tarehe tarehe hizo mwezi huu wa Machi, wahalifu wa mtandao wakiwa eneo la Njiro na baadaye Kijenge mjini Arusha (Kila post ilionyesha eneo ilipotoka), (wakati huo mimi nikiwa Dar es Salaam) waliingia bila idhini kwa njia haramu (Hacking) katika anuani yangu ya Facebook na ku-post habari hizo tano. Sasa nimeliacha jambo hilo katika vyombo stahiki vya ulinzi na usalama ili kufuatiliwa kadiri ya taratibu zao.

Natoa wito kwa ndugu zangu waandishi kujitahidi kuhakiki habari kabla ya kuzipeleka katika vyombo vyao. Hii itasaidia 1. Wao kujenga heshima mbele ya jamii 2. Kufikisha kile hasa ambacho ni habari 3. 

Kuzuia mikanganganyiko isiyo ya lazima. Haya yakizingatiwa nadhani hata sintofahamu hizi za uandishi wa habari unaotokana na hisia na  vyanzo vumbi na  ufahamu mdogo wa jambo utaondoka na tutakuwa na jamii ambayo haki na uwajibikikaji wa wanahabari kwa jamii utaonekana kutendeka

Niombe radhi kwa ndugu yangu, rafiki yangu na pia mwalimu wangu, Ndugu Absalom Kibanda kwa usumbufu wowote uliojitokeza ambao naamini watu wasio na nia njema walitaka kuutumia kuleta hisia tofauti katika jamii na pia kumpa pole kwa mara nyingine tena kwa maumivu yaliyosababishwa na ujangili huo.

 Namuombea kwa Mungu ampe unafuu mapema zaidi ili arudi katika meza yake kuendeleze harakati za kupambana na mchango wake katika kuleta maendeleo ya kweli kwa nchi yetu. Pili, pole pia kwa wote ambao kwa namna moja au nyengine walikwazwa na uzushi huo, kwa kuwa sina tatizo lolote na Bwana Kibanda na wala nisingependa lililomtokea limtokee yeye wala mtu mwengine yeyote.

Ni imani yangu ya dhati kwamba vyombo husika katika nchi yetu havitasita kulitalifanyia kazi jambo hili na ukweli juu ya nini kimemtokea Bwana Absalom Kibanda utajulikana na kuwekwa bayana.

Mwisho, shukrani kwa wote mlionipigia simu kuhusu hili, tuko pamoja na nawatakia kila la kheri katika shughuli za uajenzi wa Taifa letu hili la Tanzania ambalo msingi wake umejengwa katika haki, umoja, amani na kujali hali za watu wake.
Asanteni sana.

Ndugu yenu,
Ridhiwani Kikwete,
Jumapili Machi 17, 2013.

Sunday, March 17, 2013

LOWASSA, MENGI KUFANYIWA UMAFIA KAMA ABSALOM KIBANDA.

 EDWARD LOWASSA.
Reginald Mengi.

AFISA IKULU AHUSISHWA NA MKAKATI HUO, AFYA YA LWAKATARE YAZIDI KUDOROLA
 WAKATI sakata la Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wilfred Lwakatare anayetuhumiwa kupanga mikakati ya uhalifu na kurekodiwa kwa video likizidi kuibua maswali, vigogo wengine wanadaiwa kuandaliwa mpango wa kurekodiwa kwenye video ili kuwachafua na kuwanyamazisha, Tanzania Daima Jumapili limebaini.

Vigogo hao ni pamoja na Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi, Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe.

Taarifa za mkakati huo zilisambazwa jana kwenye mtandao maarufu wa Jamii Forum, huku ukihusisha mawasilino ya ofisa mmoja wa Ikulu ya Rais Kikwete akieleza kufurahishwa kwake na kuwapongeza waliofanikisha mpango wa kuandaa video ya Lwakatare ambaye kwa sasa anashikiliwa na Jeshi la Polisi.

AZAM FC YAMJIBU SHAFFIH DAUDA


UONGOZI WA SSB na Azam FC umesikitishwa na makala iliyotolewa na Blogu ya Shaffihdauda eti, klabu zimekuwa zikidhulumiwa na SSB na Azam FC kwa mechi zao kurushwa Live na Star TV. 

Tungependa ieleweke kuwa Azam FC ingependa kuona mashabiki wake nchini na nje ya nchi wakiiona mechi live na ndiyo maana tumekuwa tukilipia matangazo hayo, pia tunadhani hili ni jambo jema la kuungwa mkono na wadau.

Pia tungependa ifahamike kuwa kwenye kipengele cha mkataba kati ya SSB na Star TV, kuna kipengele kinachoilazimisha Star TV kutoa sehemu ya pato lake na kuvilipa vilabu ambapo kwa mechi moja klabu hupata shilingi milioni moja (1,000,000)

Kwa mechi zinazochezwa chamazi, klabu hupata mgao wa kiingilio wa chini ya shilingi laki tatu hivyo nyongeza ya milioni moja kwa mechi kurushwa live ni pesa ya kutosha angalau kwa kuanzia

Dk. Slaa aivuruga CCM


CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kauli ya Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa kwamba kuna baadhi ya watumishi wa vyombo vya dola wanaripoti kwake, kimesababisha baadhi ya wananchi kukosa imani na vyombo hivyo.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Mkoa Maalum wa CCM Dar es Salaam baada ya kikao chao kutathimini mambo na matukio mbalimbali yanayolitikisa taifa kwa sasa.
Katika taarifa yao iliyosainiwa na Katibu wa Wilaya ya Dar es Salaam (ya kisiasa - CCM), Daniel Zenda ilisema kuwa Dk. Slaa amekuwa akitoa kauli hizo mara kwa mara tangu wakati wa kampeni za urais mwaka 2010, lakini hajaitwa kuulizwa wala kuchukuliwa hatua.
“Lakini pia kauli ya Dk. Slaa imesababisha wananchi wakose imani na Idara ya Usalama na zaidi kupoteza imani juu ya uwezo wa serikali kuwalinda na kuwahakikishia usalama wa maisha yao, ambapo ni jukumu la kikatiba la serikali,” ilisema taarifa hiyo.

Rais Kikwete apokea Ujumbe maalumu toka kwa Rais wa Botswana.


 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokea ujumbe maalumu kutoka kwa Rais wa Botswana uliowasilishwa na  Waziri wa Mambo ya Nje ya nchi hiyo Mhe Pandu Skelemi Ikulu jijini Dar es salaam.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisoma ujumbe maalumu kutoka kwa Rais wa Botswana uliowasilishwa na Waziri wa Mambo ya Nje ya nchi hiyo Mhe. Pandu Skelemi Ikulu jijini Dar es salaam.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na  Waziri wa Mambo ya Nje wa Botwana Mhe Pandu Skelemi baada ya kupokea ujumbe maalumu kutoka kwa Rais wa nchi hiyo jana Ikulu jijini Dar es salaam.(PICHA NA IKULU).

Papa Francis akataa vitu vya kifahari

Siku chache baada ya kuchaguliwa kuwa Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis amewashangaza wengi mengi kwa kukataa kuvaa viatu vya kifahari na msimamo wake kuwekwa wazi kuwa hatavumilia makasisi watakaotenda uovu.
 
 Papa Francis 1
Tayari, Papa Francis ameelezwa kuwa kiongozi asiyetaka makuu, mhafidhina na mtu ambaye hataweza kubadili mengi katika kanisa hilo lenye waumini bilioni 1.2 duniani.
Katika siku mbili za uongozi wake, Papa Francis amelithibitisha hilo kwa kutokea hadharani akiwa amevaa viatu rahisi, vyeusi na kuachana na vyekundu vya kifahari vilivyopendelewa na mtangulizi wake, Benedict VXI.
Kutoka Uk 1

Katika uongozi wake, siku zote Papa Benedict, alivaa viatu vyekundu vilivyotengenezwa kwa mkono, jambo ambalo Papa Francis anaonekana kuachana nalo.
Watu walio karibu naye Papa Francis, wanaeleza kuwa kabla ya kuondoka Buenos Aires, Argentina kwenda Rome, Kardinali Jorge Mario Bergoglio, kama alivyojulikana awali, alivaa viatu rahisi vya rangi nyeusi, na kuwafanya marafiki zake, wakiwamo mapadri kutaka kumnunulia viatu vingine vipya.

“Siku ile aliyoondoka mjini Buenos Aires kuelekea Rome kwa ajili ya mkutano wa uchaguzi wa Papa (conclave), marafiki zake walimpa zawadi ya viatu. Yeye, siku zote amekuwa akitokea hadharani akiwa amevaa nguo rahisi, viatu vya kawaida,” walieleza mapadri hao kutoka Amerika Kusini walipozungumza na Kituo cha Redio Vatican.
Mbele ya makardinali 106
Juzi Ijumaa alipokutana na makardinali 106, kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 76, licha ya kuonyesha uso wa furaha na kuwatania aliwaonya makardinali hao kuhusu wajibu wao kama viongozi wa kanisa maeneo mbalimbali duniani akiwataka kutosahau kuwa hawarudi kwenye ujana.


Katika ukumbi wa Sala Clementina, ulioko Vatican Papa Francis pia aliwataka makardinali hao wakiwamo waliomchagua kuwategemea zaidi vijana aliosema ndio nguzo kuu muhimu ya ustawi wa Kanisa Katoliki, huku aliwashauri makardinali kusaka njia sahihi ya kueneza Ukristo pande zote za uso wa dunia katika karne ya 21.
Aidha, alimsifu mtangulizi wake, Papa Benedict kwa uamuzi wa kijasiri wa kustaafu, akieleza kuwa ni uamuzi wa busara, wenye kuonyesha ukomavu na kuwataka wasichoke kuiga matendo mema.
Yaliyomo kitabuni mwake

Kupitia kitabu, On Earth and Heaven (Duniani na Mbinguni) alichokiandika akiwa kardinali, Papa Francis alitoa taswira yake kama mtu mwenye dhamira safi hasa katika masuala ya kusaidia jamii, muumini thabiti anayeamini katika majadiliano baina ya makundi ya imani tofauti.

Msimamo kuhusu makasisi
Papa Francis ameonyesha wazi kuchukizwa na matendo ya makasisi (mapadri) wasio waadilifu, ambao kwa miaka mingi wamelifedhehesha kanisa na kwamba yeye hakubaliani na wanaoficha maovu ya baadhi ya mapadri ukiwamo ulawiti.
“Suala la useja (mapadri kutokuoa) kwamba ndicho chanzo cha ulawiti linaweza kusahaulika,” anaeleza katika kitabu hicho. “Endapo padri ni mlawiti, alikuwa hivyo hata kabla ya ukasisi wake. Lakini, hili linapotokea, lisiangaliwe kwa mtazamo tofauti, lisifichwe. 

Kama kiongozi, hutakiwi kutumia madaraka yako kuangamiza maisha ya mwingine.”
Kuhusu hatua gani atachukua, wakati akiwa Kardinali Bergoglio, alijibu kuwa hawezi kukubaliana na waovu, lakini alipoulizwa kama askofu angechukua hatua gani dhidi ya mapadri wa aina hiyo, alijibu,” Nitamfukuza kazi, kisha kumshtaki, jukumu langu ni kuweka usafi wa kanisa mbele.
“Hili ni suluhisho kwa matukio kama hayo kama jinsi ilivyopendekezwa Marekani; lakini si kuwahamisha wakosaji kutoka parokia moja kwenda nyingine.
“Huu ni upuuzi, kwani hata huko wataendeleza tatizo hilo. Jibu sahihi kwa tatizo hili ni kutowavumilia.”

Katika kitabu hicho, Papa Francis anazungumzia maisha ya utauwa (usafi wa moyo), uadilifu na maovu akiweka wazi msimamo wake usio wa mzaha na kuruhusu mijadala baina ya makundi ya imani tofauti, msimamo ambao unaweza kupingwa na baadhi ya Wakatoliki wenye msimamo mkali.Kwa maneno yake, Papa Francis anaonyesha kuwa mtu mwenye akili, anayefikiri haraka, mjuzi wa mambo, anayechanganya uhafidhina wa kijamii na akiwa mwenye msimamo mkali wala kutokukubali upuuzi kwa mambo asiyoyapenda au kuyakubali.

Kiongozi huyo ameahidi kutumia Jumamosi ya Machi 23 kumtembelea mtangulizi wake, Papa Benedict katika jumba analoishi huko Castel Gandolf, kusini mwa Rome na anaeleza kuwa kanisa limepitia nyakati ngumu. “Kumekuwa na vipindi vingi, majaribu mengi. Kumekuwa na vipindi vigumu, lakini, kanisa limesimama imara.”
Hata hivyo, katika misa yake ya kwanza, Alhamisi, Papa Francis alieleza kuwa kanisa hilo halina budi kwenda na wakati, kukubali mabadiliko.

“Ni dhahiri kuwa katika historia yake, kanisa limebadilika mno, sioni sababu za kwa nini tusikubali mabadiliko na kuwa utamaduni wetu wa sasa,” anaeleza.
Alieleza kuwa mafundisho ya msimu ya Kikatoliki, msimamo kuhusu mashoga, ndoa za jinsia moja, hayawezi kubadilika.
Pia, anaeleza kuwa utoaji mimba ni tatizo la kisayansi zaidi, lakini ambalo haliwezi kukubaliwa na kanisa.
Kuhusu utandawazi, Papa Francis alieleza kwamba hakubaliani nao kwa kuwa mfumo huo hauheshimu tamaduni. “Aina ya utandawazi unaofanya vitu vyote kuwa sawa ni aina ya unyama,” anaeleza akiongeza kwamba tofauti za kitamaduni hazina budi kudumishwa.
“Hatimaye, utandawazi unageuka njia ya kuwatumikisha wengine,” alisema.

BALOZI KAMALA AKUTANA NA WATANZANIA WAISHIO UHOLANZI

IMG_1539Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Watanzania waishio Uholanzi (TANE), Bw. Musuto wa Chirangi  (aliyesimama) akizungumza wakati wa kumkaribisha Balozi Kamala.IMG_1548Mwenyekiti wa TANE, Bw. Kweba Bulemo (aliyesimama Kulia), akisema machache kabla ya kumkaribisha Mhe. Balozi.

Mwenyekiti wa Chadema na Mbunge wa Hai Freeman Mbowe Atua Shinyanga, tayari kuzindua Kanda ya Ziwa Mashariki

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, akifurahia jambo na Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Kakola, mahali ambapo mgodi wa dhahabu wa Buzwagi unapatikana, Emmanuel Bombeda anayetokana na chama hicho, wakati kiongozi huyo mkuu wa CHADEMA alipokuwa akisalimiana na viongozi mbalimbali wa chama hicho, baada ya kuwasili mkoani Shinyanga, kwenye kikao cha Baraza la Uongozi Kanda ya Ziwa Mashariki (Mara, Shinyanga na Simiyu). Mbowe anatarajiwa kufanya mkutano wa hadhara Mjini Shinyanga, kufanya uzinduzi wa kanda hiyo.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...