Sunday, March 17, 2013

LOWASSA, MENGI KUFANYIWA UMAFIA KAMA ABSALOM KIBANDA.

 EDWARD LOWASSA.
Reginald Mengi.

AFISA IKULU AHUSISHWA NA MKAKATI HUO, AFYA YA LWAKATARE YAZIDI KUDOROLA
 WAKATI sakata la Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wilfred Lwakatare anayetuhumiwa kupanga mikakati ya uhalifu na kurekodiwa kwa video likizidi kuibua maswali, vigogo wengine wanadaiwa kuandaliwa mpango wa kurekodiwa kwenye video ili kuwachafua na kuwanyamazisha, Tanzania Daima Jumapili limebaini.

Vigogo hao ni pamoja na Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi, Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe.

Taarifa za mkakati huo zilisambazwa jana kwenye mtandao maarufu wa Jamii Forum, huku ukihusisha mawasilino ya ofisa mmoja wa Ikulu ya Rais Kikwete akieleza kufurahishwa kwake na kuwapongeza waliofanikisha mpango wa kuandaa video ya Lwakatare ambaye kwa sasa anashikiliwa na Jeshi la Polisi.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...