Sunday, March 17, 2013

AZAM FC YAMJIBU SHAFFIH DAUDA


UONGOZI WA SSB na Azam FC umesikitishwa na makala iliyotolewa na Blogu ya Shaffihdauda eti, klabu zimekuwa zikidhulumiwa na SSB na Azam FC kwa mechi zao kurushwa Live na Star TV. 

Tungependa ieleweke kuwa Azam FC ingependa kuona mashabiki wake nchini na nje ya nchi wakiiona mechi live na ndiyo maana tumekuwa tukilipia matangazo hayo, pia tunadhani hili ni jambo jema la kuungwa mkono na wadau.

Pia tungependa ifahamike kuwa kwenye kipengele cha mkataba kati ya SSB na Star TV, kuna kipengele kinachoilazimisha Star TV kutoa sehemu ya pato lake na kuvilipa vilabu ambapo kwa mechi moja klabu hupata shilingi milioni moja (1,000,000)

Kwa mechi zinazochezwa chamazi, klabu hupata mgao wa kiingilio wa chini ya shilingi laki tatu hivyo nyongeza ya milioni moja kwa mechi kurushwa live ni pesa ya kutosha angalau kwa kuanzia

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...