Wednesday, February 27, 2013

MSANII AMTELEKEZA MTOTO STENDI YA UBUNGO



MREMBO aliyewahi kupamba video kadhaa za wasanii wa Bongo Fleva ukiwemo wimbo wa Kidato Kimoja ulioimbwa na J.I, anayekwenda kwa jina la Maya Silemwe, amedaiwa kumtelekeza mwanaye wa kumzaa aitwaye Junior Justine (3). 


Tukio hilo la kusikitisha lilitokea hivi karibuni katika kituo cha mabasi yaendayo mikoani, Ubungo jijini Dar es Salaam ambapo mtoto huyo aliokolewa na msamaria mwema.


Akisimulia mkasa mzima ulivyokuwa, shangazi wa mtoto huyo aliyejitambulisha kwa jina moja la Monalisa, alisema wao kama familia wameumizwa sana na kitendo kilichofanywa na Maya.

KUTOKA IKULU,TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Jaji na Balozi Mstaafu Mheshimiwa Hamis Amiri Msumi kuwa Mwenyekiti wa BARAZA LA MAADILI.

Taarifa iliyotolewa leo, Jumanne, 26 Februari, 2013 jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu Kiongozi (KMK) Balozi Ombeni Y. Sefue, inasema kuwa uteuzi huo ulianza Februari 18, mwaka huu, 2013.
 “Mwisho”
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
DAR ES SALAAM.
26 Februari, 2013

Leo ni kilele cha maadhimisho ya kumbukumbu ya mashujaa wa vita vya majimaji nchini Tanzania.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Said Thabiti Mwambungu.
Maadhimisho ya vita vya Majimaji yenye lengo la kuwakumbuka mashujaa zaidi ya 67 walionyongwa Februari 27 mwaka 1906 na kuzikwa katika kaburi moja wakiwa katika harakati za kuung’oa ukoloni wa Wajerumani yamafikia kilele leo mkoani Ruvuma.
Maadhimisho hayo yameandaliwa kitaifa na Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na mkoa wa Ruvuma yanafikia kilele leo katika makumbusho ya Vita vya Majimaji mjini Songea.
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Said Thabiti Mwambungu amesema wakazi wa mji wa Songea na viunga vyake pamoja na wananchi kutoka mikoa ya jirani wamejitokeza katika maadhimisho hayo.

Serikali ya Uganda yakusudia kuwanunulia wabunge wote toleo jipya la iPads kupunguza gharama za steshenari.

Chama cha Forum for Democratic Change (FDC) kimepokea na kukubali mpango wa serikali ya Uganda wa kununua toleo jipya kabisa la iPads kwa ajili ya wabunge, lakini kimesema wabunge hao wakopeshwe na sio wapewe bure.
Msemaji wa Chama hicho Wafula Oguttu ambae pia ni mbunge, amesema pendekezo la kununua iPads halikataliwi lakini hakuna sababu ya kuwapa bure na badala yake wapewe kwa mkopo.
Serikali ya Uganda imepanga kununua iPads za kisasa na kuwapatia wabunge kwa lengo la kupunguza gharama ya steshenari.
Uamuzi huo ulichukuliwa hivi karibuni na Kamati ya Bunge na unasubiri utekelezaji kwa Kamati ya Mikataba.
 

Benedict XVI to hold final papal audience in Vatican.

Crowds have begun gathering in St Peter’s Square in the Vatican for the Pope’s final general audience before his resignation on Thursday.
Papal audiences are normally held inside a Vatican hall in the winter.
But such is the level of interest that the event is being held outdoors and 50,000 tickets have been requested.
 As many as 200,000 people may attend.
After Benedict XVI steps down on Thursday, he will become known as “pope emeritus”.
There has been no papal resignation since Pope Gregory XII abdicated in 1415.
The surprise announcement of Benedict’s abdication has required the rules of electing a successor to be changed to allow the next pope to be chosen before Holy Week, which leads up to Easter.
On Wednesday, the Pope, 85, will be making one of his last public appearances – using his trademark white “popemobile” to greet pilgrims in St Peter’s Square.
 

Waziri Mkuu afanya mazungumzo na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali kutoka Sweden.

Waziri Mkuu wa Tanzania Mh. Mizengo Pinda akifurahia jambo wakati wa mazungumzo na Mdhibiti na Mkaguzi  Mkuu wa Hesabu za Serikali Bw. Ludovick Utouh (kushoto) na Mkaguzi  Mkuu  wa hesabu za Serikali wa Sweden  Jan Lindahr Hjelmaker. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Tuesday, February 26, 2013

CRDB yawa benki pekee Tanzania kupata cheti cha Superbrands kwa miaka miwili mfululizo.


Mkurugenzi kutoka taasisi ya Superbrand, Jawad Jaffer akitoa maelezo kwa wageni waalikwa juu ya kitabu cha orodha ya kampuni zilizotunukiwa hadhi ya Superbrand.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB-Uendeshaji na huduma kwa wateja Saugata Bandyopadhyay(kulia) akipokea cheti cha Superbrand kutoka kwa mkurugenzi wa Superbrands ukanda wa Afrika Mashariki, Jawad Jaffer.
Baadhi ya wageni walio hudhuria tafrija hiyo.
Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa wateja wa Benki ya CRDB, Tully Esther Mwambapa akizungumza na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB-Uendeshaji na huduma kwa wateja Saugata Bandyopadhyay wakati wa tafrija ya kupokea cheti cha Superbrand
Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa wateja wa Benki ya CRDB, Tully Esther Mwambapa akizungumza na waandishi wahabari juu ya sababu zilizoipaisha Benki ya CRDB hadi kutunikiwa cheti cha Superbrand kwa mara ya tatu mfululizo pia mikakati ya benki hiyo katika kuboresha huduma zake ili kuendeleza rekodi yake ya kupata cheti hicho kila mwaka.

WAZIRI WA MAMBO YA NJE YA NCHI WA OMAN AKUTANA NA RAIS WA ZANZIBAR


 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akimkabidhi zawadi ya Mlango wa Zanzibar, Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman,Yussuf bin Alawi Bin Abdullah,alipofika Ikulu Mjini Zanzibar akiwa na Ujumbe wake leo. 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akizungumza na Ujumbe wa Serikali ya Watu wa Oman,ukiongozwa na  Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman,Yussuf bin Alawi Bin Abdullah,(wa pili kulia) alipofika Ikulu Mjini Zanzibar akiwa na Ujumbe wake leo,kwa ajili ya Mazungumzo na Rais. Picha na Ramadhan Othman,IKulu.

Kocha wa Azam afungiwa na kupigwa faini kwa kuchojoa bukta.


Kocha Mkuu wa Azam, Stewart John Hall (pichani) amefungiwa mechi tatu na kupigwa faini ya sh. 500,000 kwa kushusha bukta yake na kumlalamikia mwamuzi msaidizi wakati wa mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya timu yake na Kagera Sugar iliyochezwa Januari 26 mwaka huu Uwanja wa Azam Complex ulioko Chamazi, Dar es Salaam.
 Adhabu hiyo imetolewa na Kamati ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyokutana mwishoni mwa wiki kupitia ripoti za michuano ya VPL na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu wa 2012/2013 inayoendelea hivi sasa na kufanya uamuzi mbalimbali.
Naye Kocha Msaidizi wa timu ya Mgambo Shooting, Denis Mwingira ametozwa faini ya sh. 500,000 kwa kumtolea lugha chafu mwamuzi kwenye mechi dhidi ya Mtibwa Sugar iliyochezwa Oktoba mwaka jana katika Uwanja wa Manungu.
Ally Jangalu ambaye ni Kocha Msaidizi wa Polisi Morogoro naye ameangukiwa na rungu la Kamati ya Ligi kwa kupigwa faini ya sh. 500,000 baada ya kutolewa kwenye benchi kwa kupinga uamuzi wa refa kwa sauti ya juu. Alitenda kosa hilo kwenye mechi kati yao na Kagera Sugar iliyochezwa Novemba 10 mwaka jana Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.
Matukio ya aina hiyo kwa kocha Jangalu yamekuwa ya kujirudiarudia ambapo Oktoba 13 mwaka jana katika mechi dhidi ya Azam iliyochezwa mjini Morogoro aliondolewa na mwamuzi kwenye benchi kwa kuchochea wachezaji wa timu yake wacheze rafu.
Naye Kocha wa timu ya Moro United inayoshiriki FDL, Yusuf Macho amepigwa faini ya sh. 200,000 kwa kumtolea lugha chafu refa baada ya mechi dhidi ya Transit Camp iliyofanyika Novemba 4 mwaka jana Uwanja wa Mabatini mjini Mlandizi.
Pia Kocha wa Burkina Faso, Hasheem Mkingie amepigwa faini ya sh. 200,000 baada ya kutolewa kwenye benchi kwa kutoa lugha chafu katika mechi ya FDL dhidi ya Mkamba Rangers.
Kiongozi wa Majimaji, Joseph Nswila ambaye aliingia uwanjani baada ya mechi dhidi ya Mlale JKT kumalizika na kuvamia waamuzi amefungiwa miezi sita.
Vilevile timu ya Azam imepigwa faini ya sh. 300,000 kwa kuchelewa kufika uwanjani kwenye mechi kati yao na JKT Oljoro iliyochezwa Novemba 7 mwaka jana katika Uwanja wao wa Azam Complex ulioko Chamazi, Dar es Salaam.
Pia Coastal Union imetozwa faini ya sh. 500,000 kutokana na washabiki wake kumrushia chupa za maji mwamuzi msaidizi namba mbili wakati wa mechi yao dhidi ya Simba iliyochezwa Oktoba mwaka jana Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.
Nayo klabu ya African Lyon imepigwa faini ya sh. 500,000 kwa timu yake kugoma kuingia kwenye chumba cha kubadilishia nguo wakati wa mapumziko katika mechi dhidi ya Coastal Union iliyochezwa Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga, Oktoba 24 mwaka jana.
Timu ya Burkina Faso ya Morogoro imepigwa faini ya sh. 200,000 kutokana na kuonesha vitendo vya ushirikina kabla ya mechi yao dhidi ya Mbeya City iliyochezwa Oktoba 24 mwaka jana Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Faini ya ushirikina ya sh. 200,000 pia imepigwa timu ya Pamba baada ya kuonesha vitendo hivyo kwenye mechi yao dhidi ya Mwadui iliyochezwa Novemba 4 mwaka jana Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.
Nayo Mkamba Rangers imepigwa faini ya sh. 200,000 baada ya washabiki wake kumtolea lugha chafu Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Morogoro (MRFA), Hamis Semka na kumrushia chupa za maji mwamuzi wa mezani katika mechi dhidi ya Mbeya City iliyochezwa mjini Morogoro.
Polisi Dodoma imepigwa faini ya sh. 200,000 kutokana na washabiki wake kuvamia uwanjani na kutaka kuwapiga waamuzi katika mechi yao dhidi ya JKT Kanembwa na kusababisha mipira miwili ya Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dodoma (DOREFA) kupotea.
Pia klabu kadhaa zimeandikiwa barua za onyo kwa timu zao kuchelewa kufika uwanjani au kutofika kwenye mkutano wa maandalizi ya mechi (Pre-match meeting). Klabu hizo ni Coastal Union, JKT Ruvu, Toto Africans, Simba, Green Warriors, Majimaji, Mkamba Rangers, Polisi Dodoma, JKT Kanembwa, Moro United.
Mchezaji Stanley Nkomola wa JKT Ruvu baada ya mechi dhidi ya Coastal Union alikwenda jukwaani na kuanza kupigana na washabiki. Pia kipa wa timu ya Transit Camp, Baltazar Makene baada ya mechi dhidi ya Tessema aliruka uzio na kwenda kupigana na washabiki.
Kwa vile masuala ya wachezaji hao ni ya kinidhamu yamepelekwa kwenye Kamati ya Nidhamu inayoongozwa na Kamishna wa Polisi (CP) mstaafu Alfred Tibaigana kwa ajili ya kuchukuliwa hatua.

MeTL GROUP yapokea tuzo ya ubora na thamani ya nembo ikiwa ni ishara ya kukubalika na walaji.


Mkurugenzi kutoka taasisi ya Superbrands ukanda wa Afrika Mashariki, Jawad Jaffer akitoa maelezo kwa wageni waalikwa juu ya kitabu cha orodha ya kampuni zilizotunukiwa hadhi ya Superbrands wakati wa hafla ya kukabidhi vyeti vya tuzo za ubora na thamani ya nembo kwa makampuni bora 2013/14 iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa taasisi huru ya Superbrands Ukanda wa Afrika Mashariki Jawad Jaffer akimkabidhi Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo wa Makampuni ya MeTL Group Hussein Dewji cheti cha tuzo ya ubora na thamani ya nembo kwa kampuni zinazotoa huduma bora kwa walaji katika hafla fupi iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo wa Makampuni ya MeTL Group Hussein Dewji.
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Raha  Aashiq Sharrif (Kulia) akiwa Mwakilishi wa Masoko na Mauzo wa kampuni ya Raha Preetkamal Bansal ( wa pili kulia) wakati wa hafla fupi ya Superbrands kukabidhi vyeti kwa makampuni bora kwa mwaka 2013/14 iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa ITV na Radio One Bi. Joyce Mhaville ( wa pili kulia) aliyembatana na Mkuu wa Kitengo cha Masoko cha IPP Bi. Joyce Luhanga ( wa tatu kulia) wakati wa hafla ya utoaji wa cheti cha tuzo ya ubora na thamani ya nembo iliyoendeshwa na Taasisi ya Superbrands.
Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo wa Makampuni ya MeTL Group Hussein Dewji  akibadilishana mawazo na mmoja wa wageni waalikwa katika hafla hiyo.
Na.Mo Blog Team
Taasisi huru ya Superbrands ambayo ni kubwa kuliko zote duniani, inayoratibu ubora na thamani ya nembo kwa kampuni zinazotoa huduma bora kwa walaji, leo imekabidhi vyeti vinavyotambuliwa kimataifa vya utambuzi wa ubora wa bidhaa kwa kampuni zilizofanya vizuri nchini Tanzania kwa mwaka 2013/2014.
Tuzo za Superbrands ni miongoni mwa tuzo zenye thamani kubwa na zinazoleta heshima ya pekee ndani ya kampuni.
Hii ni mara ya tatu kwa tuzo hizo kutolewa ndani ya Ukanda wa Afrika Mashariki tangu kuanzishwa kwake yapata miaka mine iliyopita.
Uamuzi na hatimaye utoaji wa tuzo husika unatoka baraza huru la wataalamu waliobobea katika masuala ya biashara, lakini lengo hasa likiwa ni ni kustawisha na kuhamasisha ari katika utoaji huduma zinazo zingatia ubora.
MeTL imekuwa moja wapo kati ya Makampuni yaliyopokea vyeti vya tuzo hizo zilizofanyika kwa mara ya tatu hapa nchini.

Tigo yaongeza kifurushi cha ziada kwenye huduma za Blackberry!

Tigo Tanzania imezindua kifurushi kipya cha Blackberry ambacho kitawapa wateja  fursa ya kutumia mitandao ya kijamii kwa bei nafuu zaidi kijulikanacho kama Blackberry Social Plan.
Kifurushi hiki kitawawezesha wateja wa Tigo kutumia mitandao ya kijamii kama Twitter, Facebook, Whatsaap na mingineyo  ipasavyo kwa gharama nafuu zaidi. Watumiaji wanaweza kujiunga na kifurushi cha siku, wiki au mwezi kutokana  na matumizi yao.
Ndg. William Mpinga, meneja wa chapa ya Tigo alisema kuwa “Mitandao ya kijamii imezidi kuja juu baada ya watumiaji kuongezeka maradufu na kuitumia kwa matumizi mbalimbali kama kutafuta habari, kutumiana ujumbe n.k.  Mitandao hii hupatikana kiurahisi sana bila gharama yeyote hivyo kuifanya idadi ya watumiaji kukua kwa kasi kubwa sana. Watumiaji wa kifurushi cha blackberry watanufaika na huduma mbalimbali muhimu ambazo zitawasaidia kujiendeleza kibiashara na kikazi kwa kuwaweka karibu na wafanyabiashara au wafanyakazi wenzao pamoja na wateja  wao. Huduma kama BBm na Whatsapp zitawawezesha kujadili mambo mbalimbali kama vile wako mahali pamoja hivyo kupunguza haja ya mikutano ya kila mara. Watumiaji wataweza kufanya haya yote wakiwa majumbani kwao, au kwenye mizunguko yao mbalimbali.”
Mr. Mpinga aliendelea kwa kusema kuwa “tuliamua kuzindua kifurushi hiki  ili kuwapatia wateja wetu huduma mbadala juu ya kifurushi cha Blackberry na hivyo kuongeza thamani ya huduma zetu.”
Kutumia huduma hii mteja inabidi ajiunge kwa kutuma ujumbe kwenda 15518 wenye neno BBS1 kutumia kifurushi cha siku, BBS7 kutumia kifurushi cha wiki, na BBS30 kutumia kifurushi cha mwezi.  Gharama za siku ni shilingi 499, za wiki shilingi 2,999 na za mwezi shilingi 11,999. Kwa kutumia kifurushi hiki wateja wataweza kutumia mitandao ya kijamii ipasavyo kabisa.

Khadija Kopa, Isha Mashauzi Watoana Kijasho DAR LIVE.

Malkia wa mipasho, Khadija Kopa, akionesha umahiri wake wa kutikisa nyonga.
Mashabiki wanaomfagilia Isha Mashauzi wakiwa wamevamia steji baada ya kuwadatisha.
Aziza Abul ‘Bonge’ wa TOT Taarab akikamua.
Malkia wa mipasho akiserebuka na mmoja wa mashabiki wake aliyepanda jukwaani kumtunza.
Wakali Dancers wakiwajibika jukwaani.
Shabiki akimtunza Malkia wa mipasho baada ya kukunwa na mipasho.
Isha Mashauzi akikamua.
Mashabiki wakijimwaya kwa raha zao.
WAKALI wa miondoko ya muziki wa mwambao nchini, Malkia wa miondoko hiyo, Khadija Kopa akiwa na Kundi la TOT Taarab na Isha Ramadhani ‘Mashauzi’ jana waliugeuza Uwanja wa Taifa wa Burudani wa Dar Live kuwa uwanja wa mapambano baada ya kushindana kutoa burudani kwa kuonesha makali yao na kuwafanya mashabiki kila mmoja kumtaja mshindi wake.
Kabla ya wakali hao kuanza kuhenyeshana jukwaani burudani hizo zilianza kwa kunogeshwa na shoo kali ya washiriki wa shindano la Mic King linaloendeshwa ukumbini hapo kila Jumapili. Baada ya washiriki hao wanaowania gari, kundi la Wakali Dancers lilivamia jukwaa na kufanya vitu vyake pia.
(PICHA : RICHARD BUKOS / GPL )

SIMBA SC WAITISHA MKUTANO MKUU WA DHARURA


Msemaji wa klabu ya simba Ezekiel Kamwaga akizungumza na Waandishi wa Habari  leo mchana 


KIKAO cha Kamati ya Utendaji ya Simba SC jana, kimefikia uamuzi wa kuitisha Mkutano Mkuu wa dharula wa klabu hiyo, ambao ajenda yake itakuwa moja tu, kujadili mwenendo wa timu katika mashindano mbalimbali inayoshiriki.
Akizungumza na Waandishi wa Habari mchana wa leo, makao makuu ya klabu, Mtaa wa Msimbazi, Dar es Salaam, Ofisa Habari wa Simba SC, Ezekiel Kamwaga amesema kwamba siku na mahali ambako Mkutano huo utafanyika vitatajwa wakati wowote kuanzia sasa.
Aidha, Kamwaga alisema kwamba hadi sasa hakuna kiongozi yeyote wa Simba SC aliyejiuzulu na kwamba uongozi upo pamoja. “Hadi sasa hakuna kiongozi yeyote wa klabu ya Simba aliyejiuzulu. Uongozi upo pamoja na mambo yote yatajadiliwa kwenye mkutano huo wa dharula,”alisema.
Akiuzungumzia mchezo wa marudiano, Raundi ya Kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Kamwaga alisema kwamba timu itaondoka Alfajiri ya Ijumaa kwenda Angola kuwavaa wenyeji wao, Recreativo de Libolo.
Alisema mechi hiyo itafanyika Jumapili mjini Calulo, umbali wa kilomita 200 kutoka mji mkuu wa Angola, Luanda.
“Kwa mujibu wa kanuni za CAF (Shirikisho la Soka Afrika) kama umbali wa mji ambao inachezwa mechi unakuwa ni zaidi ya kilomita 200, timu mwenyeji inatakiwa kumsafirisha mgeni kwa ndege, kwa hivyo ni matumaini yetu, wenyeji wetu watakuwa tayari wametutayarishia ndege, kwa kuwa hatuwezi kusafiri kwa basi kwa zaidi ya saa nne,”alisema Kamwaga.
Kamwaga alisema kwamba, Mkuu wa msafara wa timu atakuwa Mjumbe wa Kamati ya Utendaji na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya klabu, Zacharia Hans Poppe, wakati upande wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) utawakilishwa na Mjumbe wake wa Kamati ya Utendaji pia, Muhsin Balhabou.
Kamwaga alisema kikosi kamili cha Simba kitakachokwenda Angola kitatajwa Alhamisi kwa kuwa leo ni mapema sana, kwani wanahofia anaweza kuumia mchezaji yeyote wakati amekwishatajwa kuwemo kwenye safari.
Simba SC ilifungwa bao 1-0 katika mchezo wa kwanza na Libolo wiki iliyopita Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na ili isonge mbele, inatakiwa kushinda 2-0.
Mwaka 1978, Simba iliwahi kufanya maajabu ikitoka kufungwa 4-0 na Mufulira Wanderers ya Zambia mjini Dar es Salaam katika michuano hiyo hiyo na kwenda kushinda 5-0 ugenini, hivyo kusonga mbele. 

Baada ya habari kuenea kuwa kakamatwa na MADAWA ,MSANII TIMBULO HUU NDO UJUMBE ALIO UANDIKA BBM


VODACOM MAHELA YAWAKUTA WAFANYABIASHARA NDOGONDOGO


 Meneja Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Bi.Rukia Mtingw(kulia) akiongea na Mshindi kwenye simu ya mezani wakati wa Droo  ya  kuwapata washindi wa shilingi Milioni 5 na Milioni moja  katika  Promosheni ya"MAHELA"inayoendeshwa na kampuni hiyo,ambapo wafanyabiashara ndogondogo wa Kagera na Dar es Salaam Bw.Rashid Kagombora na Adam Ramadhan wamejinyakulia kitita cha shilingi Milioni 5.wanaoshuhudia kushoto kulia ni Matina Nkurlu Meneja Uhusiano,Benjamin Michael Maneja wa Huduma za Ziada na Afisa Mkaguzi kutoka bodi ya michezo ya kubahatisha Tanzania Bi.Chiku Salehe,Mteja anatakiwa kutuma neno"MAHELA"kwenda namba 15544 na kuweza kujishindia.Zaidi ya shilingi Milioni 400 zinaendelea kushindaniwa.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...