Chama cha Forum for Democratic Change (FDC) kimepokea na kukubali mpango wa serikali ya Uganda wa kununua toleo jipya kabisa la iPads kwa ajili ya wabunge, lakini kimesema wabunge hao wakopeshwe na sio wapewe bure.
Msemaji wa Chama hicho Wafula Oguttu ambae pia ni mbunge, amesema pendekezo la kununua iPads halikataliwi lakini hakuna sababu ya kuwapa bure na badala yake wapewe kwa mkopo.
Serikali ya Uganda imepanga kununua iPads za kisasa na kuwapatia wabunge kwa lengo la kupunguza gharama ya steshenari.
Uamuzi huo ulichukuliwa hivi karibuni na Kamati ya Bunge na unasubiri utekelezaji kwa Kamati ya Mikataba.