Wednesday, February 27, 2013

Leo ni kilele cha maadhimisho ya kumbukumbu ya mashujaa wa vita vya majimaji nchini Tanzania.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Said Thabiti Mwambungu.
Maadhimisho ya vita vya Majimaji yenye lengo la kuwakumbuka mashujaa zaidi ya 67 walionyongwa Februari 27 mwaka 1906 na kuzikwa katika kaburi moja wakiwa katika harakati za kuung’oa ukoloni wa Wajerumani yamafikia kilele leo mkoani Ruvuma.
Maadhimisho hayo yameandaliwa kitaifa na Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na mkoa wa Ruvuma yanafikia kilele leo katika makumbusho ya Vita vya Majimaji mjini Songea.
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Said Thabiti Mwambungu amesema wakazi wa mji wa Songea na viunga vyake pamoja na wananchi kutoka mikoa ya jirani wamejitokeza katika maadhimisho hayo.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...