Thursday, February 21, 2013

SIMBA 1 TZ PRISONS 0



KIKOSI CHA SIMBA

MASHABIKI WA SIMBA

KIKISI CHA TZ PRISONS
MASHABIKI WA PRISONS


WAANDISHI WA HABARI


WAANDISHI WENGINE WAKITUMA STORY ZA MCHEZO HUO KWA KUTUMIA SIMU





WAHUSIKA WA UWANJA HUU WA SOKOINE TUNAOMBA BARABARA HII IWE KATIKA HALI  NZURI HASA ZINAPONYESHA MVUA KWANI HAIFAI KABISA 




PICHA NA MBEYA YETU

Pinda akutana na msimaizi mwendeshaji wa USAID.


Waziri Mkuu,Mizengo Pinda akisalimiana na Msimamizi Mwendeshaji wa Shirika la  la Maendeleo la Marekani USAID, Dr. Rajiv Shah kabla ya mazungumzo yao, Ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam Februari 20, 2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  na Katibu Mkuu katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Peniel Lymo wakizungumza na Msimamizi Mwendeshaji wa Shirika  La Maendeleo la Marekani (USAID), DR. Rajiv Shah (kushoto ) na Balozi wa Marekani nchini,  Alfonso Lenhardt Ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam Februari 20 2012. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Wednesday, February 20, 2013

Dkt. Shein aongoza Wazanzibar kutoa heshima za mwisho kwa Padri Evarest Mushi.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Ali Mohamed Shein, akitia saini kitabu cha maombolezi ya Padri Evarist Gabriel Mushi, katika Kanisa la Minaramiwili Mjini Zanzibar, ambapo alifika kutoa salamu ya mwisho kwa Padri huyo aliyefariki kwa kupigwa risasi na watu wasijuilikana Jumapili iliyopita, na atazikwa leo Kijini Kitope Wilaya ya Kaskazini B Unguja,(kushoto)  Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Zanzibar Augustino Shao.

  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Ali Mohamed Shein,(kushoto) akitoa salamu ya Mwisho kwa mwili wa Marehemu Padri Evarest Mushi,katika Kanisa la Minaramiwili Mjini Zanzibar, Padri Gabriel Mushi, aliyefariki kwa kupigwa risasi na watu wasijuilikana Jumapili iliyopita,na atazikwa leo Kijini Kitope Wilaya ya Kaskazini B Unguja,(katikati) Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Zanzibar Augustino Shao.

Baadhi ya Waombolezaji wakiwa ndani ya Kanisa la Minaramiwili Mjini Zanzibar wakati wa kutoa salamu ya Mwisho kwa Padri Evarist Gabriel Mushi,aliyefariki kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana Jumapili iliyopita,na atazikwa leo Kijijini Kitope Wilaya ya Kaskazini B Unguja.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Zanzibar Augustino Shao wakati alipofika katika Kanisa la Minaramiwili Mjini Zanzibar kutoa salamu ya Mwisho kwa Padri Evarist Gabriel  Mushi,aliyefariki kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana Jumapili iliyopita,na atazikwa leo Kijijini Kitope Wilaya ya Kaskazini B Unguja.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Ali Mohamed Shein, akiwasalimia wananchi wakati alipofika katika Kanisa la Minaramiwili Mjini Zanzibar kutoa salamu ya Mwisho kwa Padri Evarist Gabriel Mushi,aliyefariki kwa kupigwa risasi na watu wasijuilikana Jumapili iliyopita,na atazikwa leo Kijini Kitope Wilaya ya Kaskazini B Unguja.[Picha na Ramadhan Othman Ikulu.]

Naibu Waziri wa TAMISEMI ataka watendaji wa vijiji Singida kufanya kazi ya kuandikisha wanafunzi wa madarasa ya awali na msingi.


Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Kassim Majaliwa (Mb), akizungumza na walimu wakuu wa shule za sekondari mkoa wa Singida na baadhi ya watendaji wa sekta ya elimu. Mazungumzo hayo ambayo yalikuwa ni pamoja na kuweka mikakati ya kuinua taaluma mkoani Singida yamefanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa mkoa mjini Singida. Kushoto ni kaimu mkuu wa mkoa wa Singida ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Ikungi, Manju Msambya na Kulia ni katibu tawala mkoa wa Singida, Liana Hassan.
Baadhi ya walimu wakuu wa shule za sekondari mkoa wa Singida wakimsikiliza kwa makini Mh. Kassim Majaliwa (hayupo kwenye picha). (Picha na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Kassim Majaliwa, amesema kuanzia sasa kazi ya kuandikisha wanafunzi kuanza madarasa ya awali na yale ya msingi, itafanywa na watendaji wa vijiji na si walimu wakuu wa shule za msingi.
 Majaliwa amesema hayo wakati akizungumza na walimu wakuu wa shule za sekondari na baadhi ya viongozi wa sekta ya elimu mkoani Singida.
Amesema kutokana na ukweli huo, serikali  itafanya kazi ya uandikishaji watoto wenye sifa ya kuanza madarasa ya awali na yale ya msingi, ni watendaji wa vijiji na kazi hiyo, itakuwa na ufanisi mkubwa kuliko kipindi cha miaka ya nyuma.
Aidha, Naibu Waziri huyo amesema kuwa kila mtendaji wa kijiji anapaswa kuwakilisha ripoti ya kazi ya uandikishaji wanafunzi wa shule za awali na wale wa msingi mbele ya kikao cha maendeleo ya kata (WDC)  ili kupata Baraka ya kikao hicho.
 Majaliwaa mesema ili kuipa umuhimu mkubwa elimu ya awali ni lazima kuwepo na bajeti ambazo zitaonyesha ongezeko la shule za awali.
 Katika hatuna nyingine, Naibu Waziri huyo amekumbusha kuwa kila shule ya msingi ni lazima iwe na vyumba vya kutosha vya madarasa ya awali.
Mh. Majaliwa amesema wanafunzi wa shule za awali sio walundikwe tu madarasani au wawe wa kucheza tu kipindi chote wawapo shuleni, hapana, ihakikishwe wanasoma kikamilifu ili wakianza darasa la kwanza katika shule za msingi, wawe wameiva barabara.

NDALICHAKO AISHUTUMU CLOUDS FM WAMECHANGIA MATOKEO MABAYA YA KIDATO CHA NNE


Joyce Ndalichako adai
Clouds FM imechangia
yaliyotokea Kidato cha
Nne!
- Adai walimpa 'Promo'
kijana aliendika matusi na
"Bongo Flavor" katika
mtihani wake wa Kidato
cha Nne Mwaka jana kwa
kumfanyia interview katika
moja ya vipindi vyake.
- Adai kuwa hatua hiyo ya
Clouds FM imechangia
uandikaji wa matusi kwa
watahaniwa wa mwaka
huu

Albino wapendekeza adhabu ya kifo kwa wanaowauwa

 Mwenyekiti wa chama cha watu wenye ulemavu Tanzania (TAS) “Tanzania Albino Society” ndugu Ernest Kimaya akizungumza kwa uchungu mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya (Pichani chini) kuelezea juu ya tukio la kinyama alilofanyiwa Maria Chambanenge (39) la kukatwa mkono wake wa kushoto kwa kile kinachodaiwa kwa imani za kishirikina kuwa ni kupata utajiri. Watuhumiwa waliohusika na tukio hilo ambao pia yupo mume wake na muathirika wameshakamatwa na polisi na kuonyesha mkono huo, taratibu za mashitaka zinaendelea ili haki iweze kupatikana. Mwenyekiti huyo ameiomba Serikali kufkiria adhabu kali kwa watuhumiwa kama ho ikiwepo kunyongwa ili fundisho kwa wengine na Albino waweze kuishi katika nchi yao kwa amani.



 Mwenyekiti wa TAS akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa ofisini kwake. Kulia ni Katibu Mkuu wa chama hicho ndugu Mohammed Chanzi.

 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akizungumza kwa uchungu na kutoa onyo kali kuwa vitendo hivyo vya kinyama havitavumiliwa. Alitoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kutokomeza vitendo hivyo.
 Kabla ya kwenda kumtembelea mgongwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa aliandaa chakula kwa wageni wake.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya na msafara wake pamoja na viongozi wa chama cha Albino Tanzania (TAS) wakimfariji Mama Maria Chambanenge walipomtembelea katika hospitali kuu ya Mkoa Rukwa ambapo hali yake kwa sasa inaendelea vizuri japo ameongezewa ulemavu mwingine wa viungo kwa kukatwa mkono wake wa kushoto. 

 Mwenyekiti wa chama cha watu wenye ulemavu Tanzania (Albino) ndugu Ernest Kimaya akimfariji Mama Maria Chambanenge ambaye anaendelea kupatiwa matibabu katika hospitali kuu ya Mkoa Rukwa kufuatia kukatwa mkono wake wa kushoto na watu walioshirikiana na mume wake na ambao tayari wapo mikononi mwa polisi.
NA HAMZA TEMBA – OFISI YA MKUU WA MKOA RUKWA
………………………………………………………………………………………………………………………………………

Mwenyekiti wa chama watu wenye ulemavu wa ngozi Tanzania “Tanzania Albino Society” (TAS) ndugu Ernest Kimaya ameiomba serikali kupitia upya sheria ya haki ya kuishi kwa kuwapatia adhabu kali ya kifo wale wote wanaohusika kwa vitendo vya kinyama dhidi ya albino ikiwepo mauaji na ukataji wa viungo vyao wakiwa hai kwa kile kinachoaminika katika imani za kishirikina kuwa ni kujipatia utajiri.

Aliyasema hayo jana akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya ofisini kwake alipomtembelea akiongozana na viongozi wengine wa chama hicho kumpa pongezi zake za dhati kwa kile alichosema ni mfano wa kuigwa kwani tangu vitendo hivyo vianze hapa nchini kwa muda wa miaka mitano iliyopita ni Mkoa wa Rukwa pekee umefanikiwa kuwakamata wahalifu wa namna hiyo pamoja na kiungo husika kwa muda mfupi usiozidi siku tatu.

Amesema kuwa maalbino wamenyanyasika sana katika nchi yao kwa kukosa uhuru na amani kama watu wengine jambo ambalo ni kinyume na haki za binadam. “Watu waliokamatwa sio wa kuachiwa huru, wabanwe hata kuchomwa moto wataje wahusika wengine kwani mtandao wao ni mmoja na inatia uchungu sana kwa sisi maalbino” alisema mwenyekiti huyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Rukwa alimshukuru mwenyekiti wa chama hicho na viongozi wenzake kwa kufika Mkoani kwake kujionea hali halisi baada ya kuskika kwa matukio hayo ya kinyama kwa Albino wenzao na pia kuwashukuru wananchi na jeshi la Polisi kwa ushirikiano mzuri walioutoa kufanikisha watuhumiwa kutiwa mbaroni ili haki iweze kutendeka. Mkuu huyo wa Mkoa alisema vitendo kama hivo kaamwe havitaweza kuvumilika Mkoani kwake.

Kumekuwepo na matukio ya kusikitisha hivi karibuni ya ukatili kwa Albino ambapo mama mlemavu wa ngozi Maria Chambanenge (39) mkazi wa kijiji cha kavifuli katika Wilaya ya Sumbawanga alivamiwa nyumbani kwake usiku wa manane na kukatwa mkono wake wa kushoto na watuhumiwa ambao wameshakamatwa na jeshi la polisi na taratibu za mashitaka yao zinaendelea.

Vilevile katika bonde la ziwa Rukwa kata ya Milepa mtoto wa kiume mwenye ulemavu wa ngozi ‘albino” Mwigulu Matomange Magessa mwenye umri wa miaka saba ameshambuliwa na vijana watatu waliovaa kininja na kumkata mkono wake mmoja na kutokomea na kusikojulikana. Polisi wanaendelea na uchunguzi kuwabaini wahusika.

Matukio yote hayo yanahusishwa na wahalifu kutoka Mkoa jirani wa Mbeya ambapo vitendo hivi vya imani za kishirikina vimeshamiri

Mtoto wa miaka 6 afariki nchini Uganda kwa kukosa hewa baada ya mama wa kambo kufungia watoto ndani na kuchoma moto nyumba.


Baba wa watoto hao Kanakulya akiwa na mmoja wa watoto zake aliyeokolewa katika janga hilo.(Picha kwa hisani ya newvision.co.ug)
Mtoto asiye na hatia amefariki dunia baada ya mama yake wa kambo kumfungia ndani ya nyumba pamoja na ndugu zake watatu wakiwa wamelala kisha akachoma nyumba moto.
Tukio hilo la kusikitisha limetokea usiku katika kijiji cha Namuyenje kilichopo katika wilaya ya Mukono.
Mtoto huyo Shafik Jjuuko mwenye umri wa miaka 6 alifariki kwa kukosa hewa wakati mama yake wa kambo Margaret Nampiima mwenye umri wa miaka 27 alipochoma moto nyumba waliokuwemo watoto hao huku baba yao ambaye ni dereva akiwa safarini.
Watoto wengine Sulaiman Mutebi 8, Shamim Nakimera, 9 na Hassan Geserwa ,11 waliokolewa wakiwa na majeraha yaliyosababishwa na moto huo ambao pia umeteketeza mali kadhaa.

Pinda afungua kiwanda cha kusindika mbegu za Pamba.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akifungua kiwanda cha kusindika mbegu za pamba za kisasa  cha Quton kilichopo Bariadi Februari 18, 2013. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Paschal Mabiti  na Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa kiwanda hicho, Morgan Nzwele. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Wziri Mkuu, Mizengo Pinda akitazama mbegu za pamba wakati alipofungua kiwanda cha kusindika mbegu za pamba za kisasa cha Quton kilichopo Bariadi Februari 18, 2013. Kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Paschal Mabiti.

Tuesday, February 19, 2013

WAFUASI WA SHEKHE PONDA WAZUA KIZUNGUMKUTI PALE SHEKHE PONDA ALIPOKUWA AKIRUDISHWA RUMANDE MUDA MFUPI ULIOPITA

 Basi la jeshi la magereza lililowabeba mahabusu wanaokabiliwa na kesi ya uchochezi ambayo inamuhusisha Shekhe Ponda Issa Ponda likiwa linatoka Mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu Kuwarudisha Rumande mahabusu Hao huku wafuasi wake wakizomea askari wa kutuliza ghasia muda mfupi uliopita
 Baadhi ya Askari wa Kutuliza Ghasia FFU wakiwa kwenye gari tayari kwa kupambana na lolote litakalojitokeza wakati Shekhe Ponda akirudishwa Mahabusu muda mfupi uliopita
 Wafuasi wa Shekhe Ponda wakiwa Nje ya Mahakama ya Kisutu na Maktaba ya Taifa wakizomea askari wa Kutuliza Ghasi wakati wakisindikiza basi lililobeba mahabusu akiwemo Shekhe Ponda Issa Ponda Muda mfupi uliopita kwenye Barabara ya Bibi Titi Mbele ya Maktaba Kuu ya Taifa
 Wafuasi wa Ponda wakiwa na mabango mbele ya Maktaba Kuu ya Taifa pembeni kidogo ya mahakama ya hakimu mkazi Kisutu muda mfupi uliopita huku wakiwazomea askari wa kutuliza ghasia
 Gari la maji ya kuwasha likiwa linaishia huku likiwa kwenye msafara wa basi linalowarudisha mahabusu rumande huku Shekhe Ponda akiwa Mmoja wao
 Askari wa Kutuliza Ghasia wakiwa Kazini Muda mfupi uliopita
Askari wa Kutuliza ghasia wakiwa kazini
Gari la magereza likiwa linaongoza msafara wa kurudisha mahabusu rumande.
 Wafuasi wa Shekhe Ponda wakiwa wamekaa nje ya Mahakama ya Kisutu na Mbele ya Maktaba Kuu
 Wafuasi wa Shekhe Ponda wakisubiri Shekhe Ponda kutoka Mahakamani

BALOZI WA TANZANIA NCHINI MAREKANI AMALIZA MUDA WAKE AAGA RASMI NA KUONDOKA KUREJEA NCHINI JANA


Mhe. Balozi Mwanaidi Maajar na Mumewe Bw. Shariff Maajar, wakipata picha ya pamoja na Maofisa na wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani waliofika nyumbani kwake mapema jana asubuhi ya Jumatatu Feb 18, 2013 kuwaaga na kuwasindikiza uwanja wa ndege wa kimataifa wa Dulles uliopo Sterling, Virginia.
Juu ni Mhe, Balozi na mumewe wakiwa kwenye gari tayari kwa safari ya uwanja wa ndege wa kimataifa wa Dulles.
Mhe. Balozi katika picha ya pamoja na maofisa na wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani waliofika uwanja wa ndege wa kimataifa kuwasindikiza yeye na mumewe (hayupo pichani) waliokua wanaondoka nchini Marekani jana Jumatatu Feb 18, 2013 kurejea Tanzania baada ya Mhe. Balozi Mwanaidi Maajar, kumaliza muda wake.
Mhe. Balozi Mwanaidi Maajar na mumewe,  Shariff Maajar, wakiwa wanaelekea kupanda ndege.
Maofisa na wafanyakazi wakiwa na masikitiko huku wakiwaaga kwa macho.
Baadhi ya Maofia wa Ofisi za Ubalozi wa Tanzania, nchini Marekani, wakiwapungia kuwaaga Balozi na familia yake, wakati wakiondoka.
Container likiletwa kwa ajili ya kupakia mizigo ya Mhe. Balozi Mwanaidi Maajar, Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico aliyemaliza muda wake na RODGERS EXPORTS LLC ya North Carolina ndio imepewa jukumu la kusafirisha mizigo ya Mhe. Balozi. Picha na Vijimambo Blog

Dk. Kamala awa mwenyekiti mabalozi wa Afrika Ubeligiji.

Balozi Joel M Nheleko wa Swaziland nchini Ubeligiji, ambaye alikuwa Rais wa Mabalozi wa Afrika nchini Ubeligiji aliyemaliza muda wake, akimkabidhi Balozi wa Tanzania Dk. Diodorus Kamala mfuko wenye vitendea kazi kama ishara ya kumkabidhi Urais wa Mabalozi wa Afrika Ubeligiji jijini Brussels.
Balozi wa Tanzania nchini Ubeligiji, Dk. Diodorus Kamala ameteuliwa na mabalozi wa nchi za Africa wanaoziwakilisha nchi zao nchini humo kuwa Mwenyekiti wao.
Balozi Kamala amepokea uenyekiti huo kutoka kwa Balozi wa Swaziland nchini Ubeligiji, Joel Nheleko aliyemaliza muda wake. Tanzania itashikilia kiti hicho kwa muda wa miezi sita hadi Julai 1, 2013.
“Nimefurahi kupewa heshima hii, na naamini nitaitumia fursa hii kufahamiana vizuri na mabalozi wenzangu na kuvutia fursa za kiuchumi kwa nchi yetu,” alisema Balozi Kamala.
Wakati huo huo, juzi mabalozi wa nchi tano zinazozunguka Bonde la Ziwa Tanganyika, walimchagua Balozi Kamala kuwa mwenyekiti wao.
Nchi wanachama wa Bonde la Ziwa Tanganyika ni Burundi, Rwanda, Tanzania, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo na Zambia.
Nchi hizi zimeunganisha nguvu kutafuta wafadhili kwa ajili ya maendeleo ya Bonde la Ziwa Tanganyika, ambapo eneo la bonde hili lenye wakazi wastani wa milioni 40 wanalenga kuliendeleza kwa ajili ya kujenga miundombinu, kurahisisha usafiri na usafirishaji, kujenga reli mpya na kuendeleza utalii.
Chini ya mpango huu wanalenga pia kuboresha viwanja vya ndege vya nchi wanachama vya Mbala, Kalemie, Bujumbura, Kigoma na Kasanga kwa nia ya kurahisisha usafiri wa anga katika ukanda huu.
Dk. Kamala amekabidhiwa jukumu la kuratibu mpango huu na kwa pamoja watatafuta fedha kutoka kwa wafadhili kwa ajili ya mradi huu.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...