Saturday, February 16, 2013

Fastjet yatoa mafunzo kwa Mtanzania wa Kwanza Mmaasai kuongoza ndege aina ya Airbus.


William Zelothe Stepehen akiwa ndani ya ndege aina ya Airbus A319.
William Zelothe Stepehen akiwa na marubani wa ndege ya Fastjet.
 
William Zelothe Stepehen ni Mtanzania wa Kwanza Mmaasai aliyepewa ithibati ya kuiongoza ndege aina ya Airbus A319 punde tu baada ya kupokea mafunzo ya urubani yaliyodhaminiwa na shirika la ndege la fastjet. Alipata mafunzo hayo nchini Uingereza kwa muda wa takriban miezi miwili na amerudi nchini Tanzania hivi karibuni. William alikulia Olosipe jijini Arusha ambapo ni nyumbani kwa wazazi wake.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI



JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA
15 Februari 2013


 
Meli vita tatu (3) kutoka Jeshi la Wanamaji la Urusi zijulikanazo “MARSHAL SHAPOSHNIKOV”, “ALATAU” na “IRKUT” zikiongozwa na Rear Admiral Vladimir Vdovenko, watawasili nchini tarehe 16 February 2013 na kuondoka tarehe 20 Februari 2013 katika bandari ya Dar es Salaam kwa lengo la kufanya ziara ya kirafiki baina ya Jeshi la Wanamaji wa Tanzania na Urusi.
Waandishi wa Habari mnakaribishwa kufanya ‘coverage’ ya tukio hilo
Siku ya Jumatatu, tarehe 18 February 2013 saa 1.00 hadi saa 3.00 usiku.
Imetolewa na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano, Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
SLP 9203, Simu: 0764 742161
Email: ulinzimagazine@yahoo.co.uk
K U M B U K U M B U
MMJ/JB/
Feb 13
DP ADMN
Kufanya mahusiano na uongozi wa Bandari
1. Kurugenzi ya Habari imefanya zoezi la kuwaita waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vifuatavyo TBC, ITV, CLOUDS TV, MLIMANI TV, STAR TV, na CHANEL TEN.
2. Uongozi wa Bandari hauruhusu Waandishi wa Habari kuingia kufanya “coverage” kwenye eneo hilo bila taarifa rasmi.
3. Inaombwa mahusiano yafanyike na bandari kuhusiana na mapokezi ya waandishi wa habari watakao hudhuria siku hiyo ili kukwepa usumbufu kwa waandishi hao.

 
(KM Mgawe)
Col
DIPR

NEY WA MITEGO APATA AJALI MBAYA YA GARI

Usiku wa juzi kuamkia jana, Rapa Ney wa mitego, alipata ajali mbaya ya gari maeneo ya Oysterbay jijini Dar na mguu wake ukshtuka kidogo, ila rafiki yake aliekuwa nae, ameumia kichwani na jana ndio aliruhusiwa kutoka hospitali

ajali hiyo ilitokea maeneo ya mataa ya St Peters, alipokuwa akitokea masaki kuelekea moroko, na  baada ya mataa yake kumruhusu kupita, alikutana na Lori lililokuwa likitokea Mjini kuelekea Moroko pia, likiwa halina taa na kumvaa kwa nyuma na kupelekea gari lake kuingia mtaroni na kuharibika vibaya

ndinga aliyokuwa nayo Ney ni aina ya Altezza, ina thamani ya shilingi millioni 14, kama angekuwa amelipia bima katika kiwango cha Comprehensive, yaani bima kubwa, angerudishiwa gari ndinga mpya, akini kwa bahati mbaya alilipa bima ya kawaida


Friday, February 15, 2013

MKONO WA ALBINO WAPATIKANA SUMBAWANGA

MKuu wa Mkoa wa Rukwa , Stella Manyanya wa tatu kulia akibubujikwa na machozi jana usiku baada ya ya Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa , Peter Ngusa (kulia) akiwa ameushikilia mkono ulionyofolewa hivi karibuni kutoka kwa mwanamke mwenye ulemavu wa
ngozi (hayupo pichani) na kufukiwa poroni kijijini Miangalua wilayani Sumbawanga akiuonesha hadharani mbele ya majengo ya Hospitali ya Mkoa mjini hapa , watatu kushoto ni Mganga Mkuu wa Mkoa , Dk John Gurisha

Mmoja wa askari akifungua majani ya mgomba yaliyoufunga mkono ulionyofolewa hivi karibuni kutoka kwa mwanamke mwenye ulemavu wa ngozi (hayupo pichani) na kufukiwa poroni kijijini Miangalua wilayani Sumbawanga ambao akiuonesha hadharani mbele ya majengo ya Hospitali ya Mkoa mjini hapa jana usiku jana Februari 14.

JAJI MKUU WA KENYA, MHE. MUTUNGA AKUTANA NA WAJUMBE TUME YA KATIBA


Jaji Mkuu wa Kenya, Mhe. Willy Mutunga (katikati) akibadishana mawazo na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba (kulia) na Mjumbe wa Tume, Dkt. Sengondo Mvungi nje ya ukumbi wa Tume Jijini Dar es Salaam mara baada ya kumalizika kwa mkutano kati yake na Wajumbe wa Tume leo Ijumaa (Feb. 15, 2013). Mhe. Mutunga alikutana na Wajumbe ili kubadilishana mawazo na uzoefu katika uandishi wa Katiba Mpya.
Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mkuu mstaafu Augustino Ramadhani (kushoto) akibadilishana mawazo na Jaji Mkuu wa Kenya, Mhe. Willy Mutunga nje ya ofisi za Tume Jijini Dar es Salaam mara baada ya kumalizika kwa mkutano kati yake na Wajumbe wa Tume leo (Ijumaa Feb. 15, 2013). Mhe. Mutunga amekutana na Wajumbe wa Tume kubadilishana mawazo na uzoefu wake kuhusu uandishi wa Katiba Mpya.

Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Prof. Palamagamba Kabudi (kushoto) akimwonyesha nakala ya Kitabu Jaji Mkuu wa Kenya, Mhe. Willy Mutunga (katikati) nje ya ofisi za Tume mara baada ya kumalizika kwa mkutano kati yake na wajumbe wa Tume baina yao uliofanyika katika ofisi za Tume Jijini Dar es Salaam leo (Ijumaa Feb. 15, 2013). Mhe. Mtungi amekutana na Wajumbe wa Tume kuzungumzia uzoefu wake kuhusu uandishi na utekelezaji wa Katiba Mpya. Kulia ni Mwenyekiti wa Tume, Jaji Joseph Warioba. (PICHA NA TUME YA KATIBA)

JESHI LA POLISI WALIVYOWEKA ULINZI MKALI KUFUATIA MAANDAMANO YA WAFUASI WA SHEKH PONDA

5Polisi wakiwa wameimarisha ulinzi nje ya jengo la Sukari lililopo mkabala na Makutano ya Barabara za Ohio na Sokoine Driver Posta jijini Dar es salaam jengo hilo ndmo zilimo ofisi za mwendesha mashtaka wa Serikal Dk.Eliezer Feleshi, Ulinzi huo umeimarishwa kutokana na tishio la wafuasi wa Shekh Ponda kutishia kuandamana kwenda kwa Mwendesha Mashtaka huyokushinikiza Shekh Ponda aachiwe huru.

Baadhi ya wafuasi hao wa Shekh Ponda wamekamatwa katika maeneo mbalimbali wakati wakijaribu kuingia katika eneo la Posta ambapo ulinzi mkali uliimarishwa huku polisi wakitumia Magari, Pikipiki, Mbwahuku makachero wakizunguka kila mahali.
Baadhi ya Barabara zilifungwa ili kuweka eneo hilo katika hali ya usalama zaidi na kuhakikisha linzdhibitiwa na kulidwa kirahisi.
3Poalisi wakiimarisha Doria katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam.
6Askari Polisi wakifanya doria kwa kutumia pikipiki kam wanavyoonekana wakiranda katika mitaa mbalimbali Posta jijini Dar es salaam.

Lady Gaga Cancels World Tour For Hip Surgery.


Lady Gaga has cancelled the remainder of her world tour after discovering she needs surgery for a hip injury.
The announcement was made on Wednesday, one day after the pop superstar lamented having to delay some of her forthcoming North America concerts.
A news release said Gaga, 26, has a tear in the labrum in her right hip that would require surgery followed by a recovery period.
The labrum is a layer of muscle that helps holds the ball-shaped hip joint in place.

NCCR – Mageuzi yapinga hatua zozote za kutaka kuzuia matangazo ya moja kwa moja kutoka bungeni.

Chama cha NCCR – Mageuzi kimesema kimesema kimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya Katibu wa Bunge kwa waandishi wa habari juu ya mpango wa kuzuia kurusha matangazo moja kwa moja na badala yake kuyafanyia kwanza uhariri kabla ya kuwafikia walaji.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini dar es Salaam, Kaimu Katibu Mkuu wa chama hicho Faustin Sungura NCCR – Mageuzi inapinga kwa nguvu zote, hatua zozote zinazotaka kuchukuliwa na mamlaka yeyote za kuzuia matangazo ya moja kwa moja kutoka bungeni.
Amesema wanapinga hatua hizo kwa sababu, hoja na sababu za kutekeleza azma hiyo kama zilivyotolewa na Katibu wa Bunge ni hoja dhaifu na hasi.
Amesema mawazo ya Katibu wa bunge yanakinzana na Ibara ya 18(d) ya katiba ya nchi.(Picha na Maktaba).

Nigerian singer Susan ‘Goldie’ Harvey has died in Lagos.

Nigerian pop singer Susan Oluwabimpe Harvey, popularly known as “Goldie”, has died after a sudden illness.
Her record label said Miss Harvey, 31, had complained of a severe headache shortly after returning to Nigeria from the US where she had attended the music industry’s Grammy Awards.
The star was rushed to a hospital in Lagos, where she was pronounced dead.
Goldie had won several industry awards and appeared in last year’s celebrity Big Brother Africa TV show.

Pope appoints Ernst von Freyberg new Vatican bank head.

Pope Benedict XVI has appointed German lawyer Ernst von Freyberg to head the Vatican’s embattled bank.
Mr Freyburg’s selection is one of the last major appointments of the Pope’s tenure in office.
The bank, officially known as the Institute for Works of Religion, has been dogged by scandal in recent years.
The pontiff, 85, shocked the world’s biggest Christian Church on Monday when he announced his resignation.

AFYA YA MATUMAINI YATENGAMAA



SHIRIKISHO la filamu nchini(TAFF) limesema, limefurahishwa na taarifa iliyotolewa na madaktari wa hospitali ya Amana kuwa afya ya msanii wa vichekesho Bi.Tumaini Mwakibibi ‘Matumaini’iposhwari na wamemruhusu kurudi nyumbani.

Akizungumza  jijini Dar es Salaam jana Rais wa Shirikisho hilo la filamu nchini(TAFF) Simon Mwakifamba alisema kuwa wao kama shirikisho wamepokea kwa furaha taarifa hiyo.

"Tunajisikia poa kwa afya ya msanii huyo kurejea kuwa nzuri,  baada ya kuwa ameruhusiwa na madaktariwa hospitali hiyo ya Amana kwa kuwa amerudi nyumbani kwao Kiwalani jijini Dar es Salaam,"alisema Mwakifamba.


Afya ya msanii huyo ilibadilika na alianza kuumwa alipokuwa ameenda nchini Msumbiji na alipokelewa na wasanii wenzake kibao baada ya kutua  Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwl.Julius Nyerere jijini Dar akiwa hoi kutokana na kusumbuliwa na maradhi kwa muda mrefu.

MKUU WA MKOA WA RUKWA AAHIDI KUWACHUKULIA HATUA KALI WALANGUZI WA NISHATI YA MAFUTA MKOANI HUMO



Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akizungumza katika kikao cha baraza la ushauri la watumiaji wa nishati na maji nchini na wadau wake walipotembelea Mkoani Rukwa kwa ajili ya shughuli mbalimbali za baraza hilo. Mkuu huyo wa Mkoa alitoa pongezi kwa kazi nzuri wanayofanya na kuahidi kuwachukulia hatua walanguzi wa nishati ya mafuta pamoja na wale wanasimamia kwa kushindwa kufanya kazi yao vizuri. Kulia ni Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Alhaj Salum Mohammed Chima.
 
Mwenyekiti wa baraza la ushauri watumiaji wa maji na nishati nchini Eng. Profesa Katima akizungumza katika kikao hicho ambapo alisema kazi kubwa ya baraza hilo ni kutetea na kulinda haki za watumiaji wa maji na nishati ambayo ni maji safi na maji taka, umeme, petroli na gesi asilia.
 
Baadhi ya wadau wa mkutano huo ambao ni vyombo vya ulinzi na usalama, Tanesco, EWURA Mkoa wa Rukwa, wawakilishi wa sheli za mafuta na shirika la Maji safi na Maji taka Mkoa wa Rukwa (SUWASA) 
 
Wawakilishi wa baraza hilo Mkoani Rukwa
 
Picha ya pamoja.
(Na Hamza Temba -Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa)

WAZIRI WA HABARI,VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO ATEMBELEWA NA BRITISH COUNCIL OFISINI KWAKE

  Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara (Mb) akisalimiana na Mkurugenzi wa British Council nchini Sally Robinson (kulia) leo  Ofisini kwa Waziri,alipokwenda kumtembelea na kufanya mazungumzo mbalimbali kuhusu tasnia ya ubunifu wa Sanaa na Utamaduni pamoja na jinsi ya kuwajengea uwezo katika fani mbalimbali za sanaa na ujasiria mali.
Picha ya pamoja
 Waziri wa Habari ,Vijana,Utamaduni na Michezo,Dkt. Fenella Mukangara (Mb)akizungumza na Mkurugenzi wa British Council nchini(kulia) Sally Robinson leo alipomtembelea Ofisis kwake jijini Dar es Salaam na kuzungumza masuala mbalimbali ya tasnia ya Utamaduni,

Rais Jakaya Kikwete Asaini Kitabu Cha Maombolezo na Kutoa Heshima za Mwisho Kwa mwili wa Askofu Thomas Laizer wa Dayosisi ya Kaskazini Kati la Kanisa la Kiinjili cha Kilutheri Tanzania (KKKT)


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akitia saini kitabu cha maombolezo ya Askofu Thomas Laizer wa Dayosisi ya Kaskazini Kati la Kanisa la Kiinjili cha Kilutheri Tanzania (KKKT)jana, Alhamisi, kwenye Kanisa Kuu la KKKT mjini Arusha kabla ya kutoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa Askofu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akitoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa Askofu Thomas Laizer wa Dayosisi ya Kaskazini Kati la Kanisa la Kiinjili cha Kilutheri Tanzania (KKKT)Jana, Alhamisi, kwenye Kanisa Kuu la KKKT mjini Arusha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akiifariji familia ya Askofu Thomas Laizer wa Dayosisi ya Kaskazini Kati nyumbani kwa Askofu mara baada ya kuwa ametoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa marehemu kwenye Kanisa Kuu la KKKT mjini Arusha jana, Alhamisi, Februari 14, 2013. Picha zote na Freddy Maro-IKULU

JAJI MKUU WA UGANDA MHE. ODOKI AKUTANA NA WAJUMBE WA TUME YA KATIBA

UG CJ 1Jaji Mkuu wa Uganda Mhe. Benjamin Odoki (kushoto) akiongea na Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba katika ofisi za Tume jijini Dar es Salaam leo (alhamisi Feb. 14 2013) kuhusu uzoefu wake katika uandishi na utekelezaji wa Katiba. Jaji Odoki aliongoza Tume ya Katiba ya Uganda iliyoundwa mwaka 1989. Kulia ni Mwenyekiti wa Tume Jaji Joseph Warioba.

UG CJ 2Jaji Mkuu wa Uganda Mhe. Benjamin Odoki (kulia) akiongea na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba katika ofisi za Tume jijini Dar es Salaam. Jaji Odoki, ambaye aliongoza Tume ya Katiba ya Uganda iliyoundwa mwaka 1989, amekutana na Wajumbe wa Tume leo (alhamisi Feb. 14, 2013) na kuzungumzia uzoefu wake kuhusu uandishi na utekelezaji wa Katiba Mpya.
UG CJ 5.Katibu wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Bw. Assaa Rashid (kushoto) akimkaribisha Jaji Mkuu wa Uganda, Mhe. Benjamin Odoki (katikati) mara baada ya kuwasili katika ofisi za makao makuu ya Tume hiyo Jijini Dar es Salaam leo (alhamisi Feb 14, 2013) na kulia ni Mjumbe wa Sekretarieti ya Tume, Bw. Joseph Ndunguru. Jaji Odoki, ambaye aliongoza Tume ya Katiba ya Uganda iliyoundwa mwaka 1989, amekutana na Wajumbe wa Tume na kuzungumzia uzoefu wake kuhusu uandishi na utekelezaji wa Katiba Mpya

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...