Wednesday, August 27, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMATANO AGOSTI 27, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
.
.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

UKRAINE NA URUSI ZAFANYA MAZUNGUMZO

Marais Vladmir Putin wa Urusi(kushoto) na Petro Poroshenko wa Ukraine(kulia) wakikutana Mensk, Belarusse tayari kwa mazungumzo
Marais wa Urusi na Ukraine wamekuwa na mazungumzo ya kwanza ya moja kwa moja kuhusu mgogoro wa eneo la mashariki mwa Ukraine, lakini inaonekana hakuna welekeo wa mgogoro huo. Kiongozi wa Ukraine Petro Poroshenko amesema "mpango" utaandaliwa haraka iwezekanavyo kumaliza mapigano kati ya majeshi ya Ukraine na waasi wanaotaka kujitenga.
Rais Vladimir Putin wa Urusi amesema nchi yake itasaidia katika mazungumzo, lakini suala la usitishaji mapigano ni la Ukaraine yenyewe. Ukraine imekuwa ikiishutumu Urusi kwa kuwapatia silaha waasi, madai ambayo yanakanushwa na Urusi.
Kabla ya mkutano wao wa ana kwa ana katika mji mkuu wa Belaruse, Minsk, viongozi hao wawili pia walishiriki katika mazungumzo na afisa wa ngazi ya juu wa Umoja wa Ulaya, Catherine Ashton.
Mgogoro nchini Ukraine
Mkutano huo unakuja baada ya askari kumi wa Urusi kukamatwa mashariki mwa Ukraine.
Mwanadiplomasia Ashton ameyaelezea mazungumzo yaliyowashirikia viongozi mbalimbali wa Ulaya kuhusu mgogoro wa Ukraine kuwa una mwelekeo"sahihi".
Umoja wa Ulaya pamoja na Marekani zimeiwekea Urusi vikwazo vya uchumi kwa kushindwa kuwadhibiti waasi. Zaidi ya watu 2,000 wameuawa katika mapigano kati ya majeshi ya Ukraine na waasi katika majimbo ya Donetsk na Luhansk.
Majimbo hayo mawili yamejitangazia uhuru kutoka Kiev kufuatia hatua ya Urusi ya kujinyakulia eneo la kusini la Crimea kutoka Ukraine mwezi March 2014.
Mazungumzo kati ya Bwana Poroshenko na Bwana Putin yalidumu kwa takriban saa mbili bila kuruhusu vyombo vya habari. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

WAKUBALIANA KUSITISHA MAPIGANO GAZA


Mashambulio ya Gaza
Usitishaji wa muda mrefu wa mapigano umekubaliwa kati ya Israel na wapiganaji wa Kipalestina katika Ukanda wa Gaza.
Kusitishwa kwa mapigano hayo, kumehitimisha wiki saba za vita vilivyosababisha vifo vya watu zaidi ya 2,200, wengi wao wakiwa Wapalestina. Mazungumzo hayo yalisimamiwa na Misri na yalianza kutekelezwa jana moja usiku.
Hamas wamesema mpango huo unawakilisha "ushindi wa upinzani wao".
Maafisa wa Israel wamesema Israel italegeza vikwazo ilivyoiwekea Gaza ili kuruhusu misaada na vifaa vya ujenzi kuingia Gaza.

Mahmud Abbas kiongozi wa Wapalestina
Rais wa Wapalestina Mahmoud Abbas ametangaza kukubaliana na mpango wa kusitisha mapigano.
Msemaji wa serikali ya Israeli, Mark Regev amesema: "hebu tuwe na matumaini kwamba mpango huu wa kusitisha mapigano utaheshimika"
Mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja katika masuala yenye utata, ikiwa ni pamoja na wito wa Israel wa kuyataka makundi ya wapiganaji yanapokonywa silaha, yataanza mjini Cairo katika kipindi cha mwezi mmoja. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAN CITY YAIBANA LIVERPOOL 3 - 1


Manchester City yailaza Liverpool 3-0
Mabingwa wa ligi kuu ya Uingereza walifungua kampeini ya kutetea taji lake kwa kuinyuka washindi wa pili msimu uliopita Liverpool mabao 3-1 katika uwanja wao wa nyumbani Etihad.
Stevan Jovetic alipeleka kilio kwa Liverpool kwa kutikisa wavu mara mbili katika kila nusu.
Liverpool ambayo ilijitahidi kucheza vizuri katika kipindi cha kwanza cha mchezo ilishindwa kutumia vizuri fursa ilizopata haswa katika kipindi cha kwanza ilipobainika itambidi Kocha Brendan Rodgers kutafuta mshambulizi mbadala baada ya kumuuza Luis Suarez.
Hata hivyo Rodgers atakuwa akitafuta ufufuo baada ya kumsajili mshambulizi wa Italia Mario Balotelli kwa pauni milioni 16 .
Uwanjani matumaini ya Liverpool kunusurika kichapo yaliambulia patupu , Sergio Aguero sekunde 23 baada ya kuchukua pahala pake Edin Dzeko.
Ushindi huo ni wa pili kwa kwa Man City msimu huu
Liverpool ilipata bao la kufutia machozi baada ya Pablo Zabaleta kujifunga mwenyewe katika dakika 20 za mwisho .
Liverpool itakumbuka Jovetic alipowahangaisha alipokuwa Fiorentina kwa ni jana ndiye aliyekuwa mwiba kwa safu yao ya ulinzi.
Meneja wa Manchester City, Manuela Pellegrini amesema kikosi chake kilionyesha mchezo mzuri ambapo matunda yake ni mabao matatu dhidi ya Liverpool.
Pellegrini anasema ni muhimu kujizolea pointi sita kutoka kwenye michezo miwili ingawa mwanzo ulikua mgumu kwao.
Kwa upande wake Rodgers atajiliwaza na hali ya kuwa wamewasajili wachezaji wapya 9 msimu huu kwa hivyo bado anakisuka kikosi chake kwa niya ya kutetea nafasi yao ya pili ama hata kuiboresha nafasi hiyo ya msimu uliopita.Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Saturday, August 23, 2014

SERIKALI YAOKOA ZAIDI YA MILIONI 40

Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba
Dar es Salaam. Serikali imeokoa zaidi ya Sh40 bilioni tangu ilipoanza kutumia mfumo mpya wa malipo kwa watumishi wake.
Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba alisema hayo jana, wakati akitoa ufafanuzi juu ya kuchelewa kwa malipo ya wafanyakazi wa baadhi ya taasisi za Serikali kwa mwezi uliopita.
“Niliagiza kuanza kwa mfumo mpya wa malipo kwa watumishi wote wa Serikali kuanzia mwaka huu wa fedha ili kubaini malipo hewa yaliyokuwa yakifanywa na wahasibu wasio waadilifu. Tangu mfumo huo uanze Julai, tayari tumeokoa zaidi ya Sh40 bilioni,” alisema Nchemba.
Serikali ilitangaza kuondokana na mfumo wa ‘malipo ya dirishani’ ambao ulikuwa unatoa fursa ya wizi wa fedha za umma kupitia mishahara iliyokuwa ikilipwa kwa wafanyakazi hewa wengi.
“Kuna mishahara mingi ilikuwa inalipwa kwa marehemu au wafanyakazi wasiokuwepo ambayo ilikuwa inawaneemesha baadhi ya watendaji wa idara. Tumeanza kwa kuziba mwanya huo ili kudhibiti upotevu wa fedha,” alisema naibu waziri huyo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Thursday, August 21, 2014

ANGALIA PICHA ZA NYUMBA YA JUSTIN BIEBER YENYE NIGHT CLUB, GYM NA MOVIE THEATER

Hivi sasa Justin Bieber anaweza kujiachia kwenye club bila kupigwa picha na mapaparazi kwa sababu nyumba yake mpya ina night club na bar tatu ndani yake.
Japokuwa pesa alizolipa Bieber kumiliki nyumba hii haijawekwa wazi, sifa zake ni kuwa na ukubwa wa square meter 16,000, vyumba vya kulala 10, gym kubwa, bwawa la kuogelea, movie theater yenye screen ya inch 160 na vitu vingine.
Justin Bieber ameshahama kwenye nyumba aliyokuwa amepanga na kuhamia kwenye nyumba hii mpya aliyonunua. Hizi ni picha 10 zikionyesha nyumba hiyo

0 1
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

HII NDIO STORY MPYA KUHUSU NDEGE YA MALAYSIA ILIYOPOTEA

mala
Mwanamke mmoja mwenye cheo cha juu katika bank kubwa iliyopo Kuala Lumpur Malaysia pamoja na mumewe wameshtakiwa kwa kuiba pesa kutoka katika account za abiria na wafanyakazi wa ndege ya Malaysia iliyopotea kwenye bahari ya Hindi.
Pamoja na kushtakiwa huko mtu na mkewe hao waliepuka makosa mengine 16 kati ya makosa hayo yamo wizi,kukaidi amri ya mahakama na makosa mengineyo.
Ofisa huyo Nur Shila Kanan anatuhumiwa kutumia cheo chake vibaya katika benki ya HSBC nchini Malaysia kwa kuiba pesa za abiria walipotea na ndege.
Mwendesha mashtaka aliiambia mahakama moja mjini Kuala Lumpur,Malaysia kwamba wawili hao walifanikiwa kukwapua dola za kimarekani elfu thelathini kutoka katika account tatu tofauti za abiria waliopotea na account moja ni ya mfanyakazi wa shirika hilo la Malaysia airline. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS AGOSTI 21, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MWINYI: SERIKALI HAIKUFUTA AZIMIO LA ARUSHA

Rais wa mstaafu wa awamu ya Pili Alhaji Ali Hassan Mwinyi
Rais wa Awamu ya Pili Alhaji Ali Hassan Mwinyi amesema serikali haijawahi kufuta Azimio la Arusha kama inavyodaiwa na baadhi ya wananchi, bali ilizimua azimio hilo kuwapatia viongozi wa kati uwezo wa kumudu makali ya maisha.
"Serikali haikufuta Azimio la Arusha. Ililizimua azimio hilo kuwapatia viongozi wa kati kumudu makali ya maisha, lakini baadhi ya viongozi wamekuwa wakitumia vibaya nafasi hiyo kuvunja sheria ya maadili ya viongozi," amesema.
Alhaji Mwinyi ameeleza hayo leo jijini Dar es Salaam katika semina ya siku moja ya maandalizi ya sheria ya kudhibiti mgongano wa maslai miongoni mwa viongozi na watumishi wa umma iliyoandaliwa na Sekretarieti ya Maadili ya viongozi.
"Baadhi ya watu wamekuwa wakitumia vibaya nafasi hiyo kuvunja maadili ya viongozi wa umma kwa kutumia raslimali za umma kujinufaisha. Tabia hii imewafanya wananchi kutokuwa na imani na viongozi wao," amesema.
Kwa mujibu wa Alhaji Mwinyi, mgongano wa maslai ini tatizo kubwa nchini linalotakiwa kuangaliwa kwa umakini vinginevyo baadhi ya viongozi wataendelea kujinufaisha kwa kutumia nafasi zao kazini.
Kwa upande wake Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili ya viongozi Jaji Salome Kaganda amesema lengo na makusudi ya mapendekezo ya sheria hii ni kuleta amani na utulivu wan chi.
Jaji Kaganda amesema, "mapendekezo ya sheria hii hayalengi kuwafanya viongozi kuwa maskini, bali kasi yao ya ukwasi iendane na halii halisi ya kipato chao."
"Sheria hii itakapopitishwa na ngazi husika, itapunguza ubinafsi wa viongozi walioko madarakani kujipendelea wenyewe na maeneo wanayotoka," amesema na kuongeza kuwa, "Lazima kuwepo na hatua uya serikali kurejesha maadili ya maadili. Kama itazingatiwa na kuheshuimiwa, taifa litafikia maendeleoo ya haraka yaliyokusudiwa." Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WAANDAMANAJI WAMTAKA NAWAZ SHARIF AJIUZULU

Waandamanaji wanaotaka waziri mkuu Nawaz Sharif ajiuzulu. Islamabad, Pakistan Aug. 19, 2014.
Waandamanaji wanopinga serikali nje ya bunge la Pakistan, hawaonyeshi ishara yoyote ya kuondoka,hadi pale waziri mkuu Nawaz Sharif atakapojiuzulu, dai ambalo serikali imekataa kwa misingi ya kuwai kinyume na katiba. Wakati huo, huo jeshi lenye nguvu la Pakistan limeonya pande zote kutatua mzozo wao kupitia majadiliano.
Maelfu ya waandamanaji wanopinga serikali wamekuwa katikati ya mji mkuu wa Pakistan kwa karibu wiki moja, katika juhudi za kumshinikiza waziri mkuu Nawaz sharif kujiuzulu.
Wote serikali na viongozi wa maandamano hayo hawaelekei kurudi nyuma, na hivyo kuongeza hofu ya mapambano baina ya polisi na waandamanaji hao kila kuchao.
Mwanasiasa wa upinzani Imran Khan na kiongozi mashuhuri wa kidini Tahir-ul Qadri, wameaanda maandamano ya umma, ingawa si kwa ushirikiano lakini wanamtaka waziri mkuu Sharif kuachia madaraka.
Maandamano hayo dhidi ya serikali yamelazimisha sehemu kubwa ya mji huo kufungwa na kuvuruga maisha ya kila siku pamoja na shughuli za kibiashara. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
CHANZO:VOA

RATIBA LIGI KUU BARA 2014/2015 YAANIKWA HADHARANI, MAXIMO KUANZA NA MTIBWA, PHIRI NA WAGOSI WA KAYA


Kocha mkuu wa Yanga akiongea na msaidizi wake
RATIBA ya ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2014/2015 utakaoanza kutimua vumbi septemba 20 mwaka huu umeanikwa hadharani na Shirikisho la soka nchini Tanzania TFF.
Afisa habari na mawasiliano wa TFF, Boniface Wambura Mgoyo katika taarifa yake amesema ratiba hiyo imezingatia michuano ya Chalenji itakayochezwa Novemba, usajili wa dirisha dogo Nov 15- Des 15, ushiriki wa klabu za Azam na Yanga kwenye mashindano ya Ligi ya Mabingwa (CL) na Kombe la Shirikisho (CC).
Wambura alisema mechi zitachezwa wikiendi ili kuongeza msisimko/kuwapa fursa washabiki wengi zaidi kuhudhuria, na katikati ya wiki imeachwa wazi kwa ajili ya mechi za Kombe la FA (Federation Cup).
DSC_0007-546x291
Kocha mkuu wa Simba sc Patrick Phiri akiongea na wachezaji wake  
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAREKANI YALAANI MAUAJI YA MWANDISHI

James Foley
Rais Barack Obama wa Marekani amesema mauaji ya mwandishi wa habari James Foley raia wa Marekani aliyeuawa na wapiganaji wa kundi la Kiislam yameishtua dunia.
Obama amesema kitendo hicho ni cha kikatili na kisichokubalika mbele za Mungu na kwamba ni matokeo ya mawazo duni yasiyoendana na karne ya sasa.
Kauli hiyo ya Rais Obama inakuja huku wazazi wa mwandishi huyo wakielezea kutoridhishwa kwao na hatua zinazochukuliwa na Marekani kutokana na mauaji ya mtoto wao.
Wazazi hao wamesema wakati mwingine waandishi wa habari huru hawathaminiwi katika aki zao hata pale wanapojitolea maisha yao kwa ujira mdogo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Wednesday, August 20, 2014

PAPA FRANCIS ATABIRI KIKFO CHAKE...!!!


Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis. PICHA|MAKTABA

Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis kwa mara ya kwanza ametabiri hatima ya maisha yake duniani akisema kuwa anaamini Mungu anaweza kumpa muda wa miaka miwili au mitatu ya kuishi.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ndege wakati akitoka ziarani Korea Kusini kurejea Vatican, Papa Francis alisema suala la kuendelea kuishi ni neema ya Mungu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WANAFUNZI BILA KUANDAMANA HAWAPATI HAKI ZAO...???


Sasa ni dhahiri kwamba Jumuiya ya Wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu (Tahliso) imepata mwarobaini wa matatizo yake, ikiwa ni pamoja na wanafunzi kulipwa stahili zao na mamlaka husika. Jumuiya hiyo imegundua kwamba mamlaka zilizopewa dhima ya kuhudumia elimu ya juu na kutatua matatizo ya wanafunzi hao hazifanyi hivyo hadi pale wanafunzi hao wanapotishia kuandamana nchi nzima. Ni utamaduni mpya unaotumiwa na baadhi ya viongozi wetu, kwamba wanafunzi, wakulima, madaktari na wananchi wengine watalipwa madai yao iwapo tu watafanya vurugu au kuandamana na kuitikisa dola.

Hivyo ndivyo ilivyotokea katika suala la madai ya wanafunzi hao ya kulipwa fedha za mafunzo kwa vitendo. Hivi sasa wanafunzi kutoka katika vyuo vya elimu ya juu wako sehemu mbalimbali nchini katika mafunzo kwa vitendo, lakini wanafunzi kutoka vyuo saba hawajalipwa fedha za kujikimu. Wanaishi vipi katika mazingira mageni wakiwa hawana fedha za chakula au malazi ni swali ambalo halina jibu. Viongozi wa Tahliso wamesema ucheleweshwaji wa fedha hizo zinazokadiriwa kuwa Sh6.6 bilioni umesababisha baadhi ya wanafunzi wa kike kudhalilishwa kimapenzi na kutupiwa vyombo vyao nje kwenye nyumba walizopanga.

Kutokana na hali hiyo, viongozi wa Tahliso walipanga kuongoza maandamano keshokutwa kwenda kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda hata kama maandamano hayo yangekosa kibali cha polisi. Pamoja na viongozi hao kukamatwa na polisi na baadaye kuachiwa kwa dhamana, walisisitiza kwamba lazima maandamano hayo yafanyike kwani Tahliso inasimamia haki za wanafunzi ambazo Serikali imeshindwa kuzishughulikia. Msimamo huo uliizindua Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HELSB), ambayo ilitangaza jana katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuwa, wanafunzi hao watakuwa wamelipwa fedha zao ifikapo wiki ijayo.

DR. NCHIMBI KUMRITHI MWIGULU

Dk. Nchimbi kumrithi Mwigulu 
MWELEKEO mpya wa mchakato wa Katiba mpya, adhabu kwa wagombea walioanza mbio za kusaka urais unatarajia unatarajia kujulikana leo baada ya kumalizika kwa kikao cha Kamati Kuu (CC), ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
CC ilikutana jana chini ya uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete, ambaye alisema hana ajenda mfukoni kama ilivyodaiwa na baadhi ya watu.
“Nimekuja, Tuzungumze mambo yetu, tufanye uamuzi…..hivi mara ya mwisho kukutana ilikuwa  lini vile….aah mwezi uliopita” alisema mambo yetu.
Kikao hicho cha CC ambacho kilikuwa kianza saa nane mchana kama ilivyotangazwa kilianza saa tisa na nusu huku wajumbe wote wakiwa tayari ndani ya ukumbu isipokuwa viongozi wakuu.
Viongozi hao wakuu ni Rais Kikwete (Mwenyekiti), Katibu Mkuu Abdulrahman Knana, Makamu  Mwenyekiti (bara), Philip Mangula na Makamu Mwenyekiti (Zanzibar) Dk. Alli Mohamed Shein.
Kabla ya Rais Kikwete, kuingia ukumbini Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, alitoka faragha alikokuwa akizungumza na kwenda kuchukua nyaraka kwa Jenister Mhagama ambaye ni Katibu wa wabunge wa CCM na kurejea faragha ambapo alikaa kidogo kisha kurejea ukumbini kumuita Dk. Asharose Migiro.
Mara baada ya pilika pilika hizo, Rais Kikwete na viongozi wenzake waliokuwa faragha waliingia ukumbini ambapo Kinana alimkaribisha Rais Kikwete afungue mkutano huo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

OKWI: SINA MPANGO WA KURUDI BONGO

Emmanuel Okwi 
WAKATI uongozi wa Yanga ukidai hauna muda kuendelea kulijadili suala la mshambuliaji wa kimataifa wa Uganda, Emmanuel Okwi, mshambuliaji huyo naye amesema hana mpango wa kurudi kucheza soka Tanzania.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kupitia ukurasa wake wa Facebook, Okwi alisema hana mpango wa kurudi nchini kwa sasa, kwani anachoangalia ni kucheza soka barani Ulaya na sio Tanzania.
Awali, Katibu Mkuu wa Yanga, Beno Njovu, alikaririwa akisema, wanachoangalia wao kwa sasa ni wachezaji gani wamefika na maendeleo yao katika mazoezi, sio kumfuatilia yule ambaye hajafika.
Okwi inadaiwa kwa anaidai Yanga zaidi ya sh. milioni 60 zilizotokana na fedha zake za kusajiliwa akitokea Etoile du Sahel ya Tunisia, huku akisaini mkataba wa miaka miwili wenye thamani ya sh. milioni 160.
Hata hivyo klabu hiyo inatakiwa kuvunja mkataba na mchezaji mmoja wa kimataifa kutokana na kuzidi kwa idadi ya wachezaji watano wa kigeni kama zinavyotaka sheria za usajili wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Wachezaji wengine wa kimataifa waliopo katika klabu hiyo ni Andrey Coutinho, Geilson Santos ‘Jaja’ raia wa Brazil, Mbuyu Twite wa Burundi, Hamis Kiiza wa Uganda na Haruna Niyonzima wa Rwanda. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

FURSA YA MIKOPO KATIKA MASOMO YA SAYANSI NA HISABATI

Serikali imetoa fursa ya mikopo kwa wanafunzi watakaojiunga na masomo ya stashahada maalum ya ualimu wa masomo ya Sayansi na Hisabati.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Habari Elimu na Mawasiliano toka Bodi ya Mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya Juu Bw. Cosmas Mwaisobwa wakati wa Mkutano na waandishi wa Habari Leo Jijini Dar es salaam.
" Wanafunzi wapatao 5,000 wanatarajiwa kujiunga na stashahada maalum katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) ambapo wote watanufaika na mikopo ya elimu ya Juu."Alisema Mwaisobwa
Akifafanunua, mwaisobwa alisema kuwa lengo la mpango huo ni kusaidia kuondoa tatizo la walimu wa masomo ya sayansi hapa nchini .
Aidha Mwaisobwa alibainisha kuwa jumla ya maombi 58,037 ya mikopo yalikuwa yamepokelewa hadi kufikia Julai 2014 ambapo maombi 37,689 ni waombaji wa kiume na 19,592 ni waombaji wa kike.
Pia Mwaisobwa alibainisha kuwa majina ya wanafunzi watakaopata mikopo kulingana na udahili yatatangazwa kwenye tovuti ya Bodi ambayo ni www.heslb.go.tz.na taarifa hiyo itatangazwa katika vyombo vya habari.
Bodi ya Mikopo kwa wanafunzi wa Elimu ya juu (HESLB) inakusanya wastani wa shilingi bilioni 3 kwa mwezi ikiwa ni marejesho ya mikopo iliyokwisha tolewa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

PAPA FRANCIS AMRUHUSU PADRI KUOA...!!!

Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis.PICHA|MAKTABA 

Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis amekubali kumuondolea sakramenti ya upadri, Raymond Mosha wa Jimbo Katoliki la Moshi ikiwa ni miaka 20 tangu padri huyo aombe kuachana na daraja hilo.
Barua ya uamuzi wa Papa Francis ilisomwa juzi katika parokia na vigango vyote vya Kanisa Katoliki Jimbo la Moshi katika ibada zilizofanyika katika makanisa ya jimbo hilo.
Miongoni mwa parokia ambazo barua hiyo ilisomwa ni Karanga ambako Paroko wake, John Matumaini alitoa tangazo hilo katika ibada zote. Uamuzi huo ambao ni nadra kutolewa na Papa, unamaanisha kuwa sasa padri huyo yuko huru kuoa na kuwa na familia.
Hata hivyo, wakati uamuzi huo ukitangazwa rasmi juzi, tayari Padri Mosha ambaye ni profesa wa falsafa na maadili katika Chuo Kikuu cha Nelson Mandela Arusha, ana mke na watoto watatu ambao kwa sasa wako vyuo vikuu.
Padri Mosha alisema aliandika barua kuomba kuondolewa daraja hilo mwaka 1994 kabla ya uamuzi kutolewa juzi.
Katika orodha ya mapadre 185 wa Kanisa Katoliki Jimbo la Moshi iliyopo katika tovuti ya jimbo hilo, jina la Padri Mosha linaonekana likiwa ni namba 23.
Akizungumzia hatua hiyo, Padri Mosha alisema: “Ninafurahi kufunguliwa kifugo hiki na hii itanifanya niishi kama Mkristo. Kwa vile hawajaniondolea sifa ya kutoa huduma kama vile ibada za mazishi, sakramenti ya mwisho na ubatizo, nitaendelea kutoa kwa wahitaji kwa sababu ninaupenda ukristo.
“Nashukuru sasa nimekuwa muumini wa kawaida nitaweza kufunga ndoa kanisani kwa kuwa nilikuwa nimefunga ndoa ya kisheria tu kwa DC.”
Kuhusu kwa nini aliamua kuacha upadri, Profesa Mosha alisema ni baada ya kufanya kazi hiyo kwa miaka 20 na akaona ipo haja ya kuwa na familia lakini kanisa lilikuwa haliruhusu.
“Sasa kwa kuwa kanisa haliruhusu mapadri kuoa ndiyo maana nikaamua kuandika barua ambayo hata hivyo, imechukua muda mrefu kujibiwa na tayari nina watoto watatu wako chuo kikuu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATANO AGOSTI 20, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.

.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MWANDISHI WA HABARI AUAWA SYRIA

James Foley enzi za uhai wake akiwa na vitendea kazi vyake.
Kikosi cha kiislam cha kijeshi chenye msimamo mkali kimeachilia video inayoonesha mauaji ya mwandishi habari mwenye asili ya Marekani. James Foley alipotea tangu alipokamatwa mateka na kushikiliwa nchini Syria miaka miwili iliyopita na sasa ameuawa.
Ikulu ya Marekani imesema inaifanyia uchunguzi wa kina video hiyo na ikithibitika kwamba mwandishi huyo wa habari ni wa taifa hilo ,serikali ya Marekani itataka ufafanuzi wa kina ilikuaje na kwanini James Foley auawe.
Katika mtandao wa kijamii wa Facebook familia ya mwandishi huyo iliandika kuwa’tunajua kwamba wengi wenu mnasubiri uthibitisho ama majibu ya maswali yenu,tafadhalini muwe watulivu mpaka nasi sote tupate taarifa tunazo tamia,na tunaomba muendelee kumbumbuka Foleys na kumwombea kila siku.’’
Katika video hiyo iliyobeba ujumbe unaosomeka kua ujumbe kwa Marekani,mwandishi huyo pia alionekana akiwa chini ya ulinzi wa mtu aliyekua amevalia kinyago usoni,askari huyo alikua aku akizungumza ndani ya lafidhi yenye athari za Uingereza,akisema kua kifo cha mwandishi huyo ni matokeo ya mashambulizi ya magurunedi yalowalenga wa Iraq. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ASERNAL YATOKA 0-0 NA BESIKTAS, AARON RAMSEY ALETA MAJANGA KWA KUONESHWA KADI NYEKUNDU


1408480185825_Image_galleryImage_Aaron_Ramsey

Kiungo wa Arsenal Aaron Ramsey alitolewa nje kwa kadi nyekundu katika mchezo wa kwanza wa mtoano wa ligi ya mabingwa barani Ulaya dhidi ya  Besiktas
ASERNAL wamelazimisha suluhu pacha ya bila kufungana na Besiktas ya Uturuki katika mchezo wa kwanza wa mtoano wa ligi ya mabaingwa barani Ulaya uliopigwa jana usiku katika dimba la  Ataturk Stadium
Kutoka sekunde za mwanzo, almanusura Demba Ba afunge bao lakini mpira aliopiga wa adhabu ndogo uligonga mwamba na ilionekana kuwa ni mechi ambayo ingekuw ana magoli mengi. Lakini Aaron Ramsey naye aliwakosa Waturuki hao baada ya kupiga shuti lililogonga mwamba.
Kadi nyekundu ya Aaron Ramsey aliyopata dakika za majeruhi kufuatia kuoneshwa kadi mbili za njano aliwahuzunisha zaidi Asernal kutokana na ukweli kuwa anahitajika sana katika mchezo wa marudiano ndani ya dimba la Emitarates.
Besiktas, na Ba wameonekana kuwa na nia ya kuwaonesha Chelsea kuwa walifanya makosa kumuuza mshambuliaji huyo kwani alionesha kiwango kizuri. Ili kusonga mbele, Asernal wanahitaji ushindi wa bao 1-0 tu mjini London jumanne ijayo.
Silly boy: Ramsey received (left) his second yellow card for bringing down Besiktas' Oguzhan Ozyakup (right)

HARUNA SHAMTE, JABIR AZIZ, JACKSON CHOVE WASAINI MKATABA WA MWAKA MMOJA MMOJA JKT RUVU

SIMBANAYANGA2
Haruna Ramadhan Shamte

MAAFANDE wa JKT Ruvu wamekamilisha usajili wa wachezaji watatu kati ya wengi waliokuwa wanafanya majaribio chini ya kocha mkuu, Fredy Felix Minziro. Beki wa kulia aliyeichezea Simba sc msimu uliopita, Haruna Ramadhan Shamte amesajiliwa na maafane hao na kusaini mkataba mwa mwaka mmoja. Pia nyota wa zamani wa Simba sc na Azam fc, Jabir Aziz ‘Stima’ ameanguka mkataba wa mwaka mmoja kuitumikia klabu hiyo yenye nia ya kuonesha changamoto kubwa zaidi msimu ujao. Katika kuhakikisha lango lake linakuwa mikono salama, klabu hiyo imemsainisha mlinda mlango mzoefu, Jackson Chove mkataba wa mwaka mmoja. Wachezaji hao watatu walikuwa chini ya uangalizi wa kocha Minziro kwa muda mrefu kwa lengo la kujiridhisha na viwango vyao pamoja na suala muhimu la nidhamu.

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz Wachezaji wengine waliokuwa wanafanya majaribio na klabu hiyo ni pamoja na Betram Mombeki na Henry Joseph, wote waliachwa na Simba sc mwishoni mwa msimu uliopita.
 
Jabir Aziz
Pia Athumani Idd ‘Chuji’ alijitokeza mara kadhaa katika mazoezi hayo, lakini aliondoka zake baadaye na sasa anajifua na Mwadui FC ya Shinyanga inayoshiriki ligi daraja la kwanza. Meneja wa JKT Ruvu, Frank Joel Cibaya aliwahi kukaririwa na mtandao huu akisema wachezaji wengi walioachwa na klabu kubwa za Simba na Yanga wanaomba kufanya majaribio klabuni hapo, lakini kocha Minziro yuko makini zaidi kuangalia nani anamfaa.

Cibaya alimtaja Aziz, Shamte na Chove kuwa walionesha juhudi kubwa kwa muda wote wa uangalizi, hivyo kocha amependekeza wasajiliwe rasmi kuitumikia klabu hiyo. Meneja huyo alisema wachezaji wengi wanaotoka timu kubwa huwa wanasumbua sana wanapojiunga na timu ndogo wakitaka kupata kila kitu walichokuwa wanapata Simba na Yanga.
Dirisha la usajili limeongezwa kwa siku 10 hadi Agosti 27 mwaka huu, hivyo bado maafande wana nafasi ya kuongeza au kupunguza wachezaji wanaoona hawana manufaa kwao. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na Baraka Mpenja

Tuesday, August 19, 2014

WAPENZI WA JINSIA MOJA KENYA KUPIGWA MAWE HADI KUFA...!!!

Screen Shot 2014-08-19 at 8.03.13 AM
(Nje ya bunge la Kenya. Picha na Maktaba)
 
Bunge la taifa nchini Kenya linapanga kujadili sheria ya kipekee inayopendekezakupigwa mawe hadi kufa kwa raia wa kigeni atayeshiriki mapenzi ya jinsia moja huku wazawa wakikuhukumiwa kifungo cha maisha jela.

Mwandishi na mdhamini wa sheria hiyo Edward Onwong’a Nyakeriga anapendekeza kuharamishwa kwa ulawiti na kisha kuhukumiwa jela kwa wale wanaotenda kosa hilo huku akisisitiza kuwa upo umuhimu wa kuwalinda watoto na vijana ambao wanalengwa na dhulma ambazo kwa mda mrefu zinaepukwa kutokana na mabadiliko ya teknolojia na habari isiyo chujwa na watoto yatima kukosa mwakilishi pamoja na majaribio ya wanaoshiriki uhusiano wa jinsia moja kuwalea watoto ilihali wanaendeleza uhusiano wao’
 Screen Shot 2014-08-19 at 8.06.26 AM
Muswada huo wa chama cha Republican Liberty Party unaharamisha uhusiano wowote wa jinsia moja na tayari umeungwa mkono na wabunge zaidi ya 78 na wengine zaidi wanaendelea kushawishiwa. Pia spika wa Bunge Mh. Justin Muturi ameupokea na kuuwasilisha katika kamati ya sheria bungeni ambayo inatathmini kisha kutoa ripoti kwa bunge.
 Mmoja kati ya waaandishi wa vitabu maarufu nchini Kenya Binyavanga Wainaina amekua miongoni mwa waliojitokeza hadharani na kukiri kushiriki mapenzi ya jinsia moja na wakati huohuo Mashirika ya kutetea haki za wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja hivi karibuni yaliwasilisha pendekezo la kutaka Wabunge kuondoa sheria zote zinazowazuia kuishi maisha yao kama watu wengine. Muswada huo unatarajiwa kupata upinzani mkali kutoka kwa wanaotetea haki za binadamu.
Kwa upande wa Katiba ya Kenya ya mwaka 2010 imeharamisha ndoa ya jinsia moja japo haiharamishi moja kwa moja uhusiano wa mapenzi ya jinsia moja ambapo pia mwezi uliopita utafiti uliofanywa na kampuni ya Ipsos Synovate umeonyesha kwamba 64% ya Wakenya wanaamini kwamba hisia za kushiriki mapenzi na jinsia sawa ni jambo la kujifunza ilihali 14% kati yao wanaamini watu hao huzaliwa walivyo.

Chanzo: Millard Ayo

UAMUZI MGUMU CCM KATIKA KAMATI KUU LEO

Kamati Kuu (CC) ya Halmashauri Kuu ya CCM inakutana leo mchana mjini Dodoma chini ya mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete huku ikitarajiwa kufanya uamuzi mgumu wa mchakato wa Katiba.

Kikao hicho kinaketi mara ya pili katika muda mfupi, baada ya hivi karibuni kukaa jijini Dar es Salaam na kueleza kuridhishwa na mchakato huo.

Hata hivyo, safari hii kikao hicho kinaketi kukiwa na maswali lukuki ambayo hayajapata majibu: Je, Bunge la Katiba liendelee au livunjwe? Je, lisitishwe kwa muda kupisha maridhiano au la? Je, kuna umuhimu wa maridhiano? Kuna ulazima wa kuwapo Ukawa bungeni?

Akizungumzia kikao hicho, mtaalamu wa sayansi ya siasa na utawala katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Alexander Makulilo alisema jambo kubwa litakalojadiliwa katika kikao hicho ni kauli tofauti zilizotolewa na wananchi kuhusu mchakato wa kupata Katiba Mpya. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

"KAULI YA WEREMA NI YA KINAFIKI" MBATIA


Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia (kulia) akizungumza na waandishi jijini Dar es Salaam jana. Kushoto ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Mosena Nyambabe.


Siku moja baada Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema kueleza kuwa hakuna mwenye mamlaka kisheria kuvunja au kusitiza Bunge la Katiba, mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi amesema kauli hiyo imejaa unafiki na kwamba upo uwezekano wa kuahirisha vikao kwa muda mpaka mwafaka wa kitaifa utakapopatikana.

Mwenyekiti huyo, James Mbatia amesema kuahirisha Bunge kunawezekana kama ambavyo iliwezekana kusitishwa vikao vya Bunge hilo Aprili mwaka huu kupisha Bunge la Bajeti na kubadilishwa kwa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba kinyemela kwa kuongeza idadi ya siku za Bunge la Katiba kutoka 70 hadi 90 mpaka kuwa muda wowote ambao utaonekana unafaa.

Wakati Mbatia akieleza hayo, jana waliibuka wazee wa Jiji la Dar es Salaam wakiwataka Watanzania kuyaombea makundi yanayovutana na moja likisusia vikao vya Bunge hilo vinavyoendelea mjini Dodoma, ili yakutane na yakubali kufikia mwafaka kwa pamoja.

Kauli ya Mbatia

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mbatia alisema kauli iliyotolewa juzi na Jaji Frederick Werema imejaa unafiki. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...