Monday, April 02, 2018

AL SHABAAB WAVAMIA KAMBI YA AU NA KUDAI KUUA WANAJESHI 59

Wanamgambo wa kiislamu (Al-Shabaab) wamefanya shambulizi kwenye kambi ya wa jeshi la Muungano wa Afrika AU nchini Somalia.

Wanamgambo hao walilipua mabomu yaliyokuwa yametegwa ndani ya magari mawili nje ya kambi ya jeshi kwenye mji wa Bulamarer, kusini magharibi mwa Mogadishu.

Wenyeji wanasema kuwa walisikia makabiliano makubnwa ya risasi ambayo yalidumu kwa zaidi ya saa tatu.

Msemaji wa Al Shabaab alisema wapiganaji wake 14 waliuawa huku wanajeshi 59 wa AU wakiuawa. Bado madai hayo hayajathitishwa.

Miaka ya hivi karibuni, wanamgambo wa kislamu wamepoteza udhibiti wa miji ya Somalia lakini mara kwa mara hulipua mabomu na kuswashambulia walinda amani.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...