Tuesday, August 18, 2015

SAUTI SOL KUTAFUTA WACHUMBA TANZANIA


KUNDI linalofanya vizuri na wimbo wao wa ‘Nerea’ kutoka nchini Kenya, Sauti Sol, limetangaza kutafuta wachumba wa kuoa nchini Tanzania, huku wakiwaomba radhi wasichana wa Kenya. 

“Samahani kwa wasichana wa nchini Kenya kutokana na maamuzi yetu ya kutaka kuoa huku Tanzania. Dar es Salaam. Kwa sasa tunatafuta warembo wa kuwaoa,” waliandika wasanii hao kupitia akauti yao ya Twitter. 

Wasanii hao kwa sasa wanafanya vizuri nchini humo na wamefanikiwa kuchukua tuzo mbalimbali nje ya nchi ya Kenya.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...