Tuesday, August 18, 2015

IRENE UWOYA AFANYIWA SHEREHE YA KUPONGEZWA

Irene Uwoya

MWIGIZAJI wa filamu ambaye jina lake limepitishwa nafasi ya ubunge viti maalumu Mkoa wa Tabora kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Irene Uwoya, amesema malezi aliyopewa na wazazi wake ndiyo yatakayomsaidia kuwa kiongozi bora. 

 Irene alisema hayo juzi katika hafla fupi iliyoandaliwa na wazazi wake kumpongeza kupitishwa katika nafasi hiyo ambapo pia marafiki zake wa karibu walihudhuria sherehe hiyo.

“Nisingekuwa hapa nilipofika kama wazazi wangu wasingenionyesha moyo na ushirikiano wa kutosha, najivunia kwani wamenisaidia kujenga moyo wa ujasiri ndani yangu na naamini nitawatendea haki kwa kuhakikisha ninakuwa kiongozi bora,” alisema Irene.

Irene alieleza kuwa lengo lake la kugombea nafasi hiyo ni kuhakikisha anaingia bungeni kuwatetea vijana wanaokabiliwa na matatizo mbalimbali, hasa katika Mkoa wa Tabora.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...