Wednesday, November 26, 2014

HALIMA MDEE AMKANA MKONO


Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee. PICHA|MAKTABA 

Siku moja baada ya Mbunge wa Musoma Vijijini (CCM), Nimrod Mkono kusema amelishwa sumu akiwa London, Uingereza, Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee amemtaka kusema ukweli na si kulihadaa Taifa kwa uongo.

Mkono akizungumza na waandishi wa habari juzi kuelezea mwenendo wa afya yake, alisema lengo la kulishwa sumu ilikuwa ni kutaka kuharibu figo zake ndani ya saa 72 kitendo kilichoshindikana.

Mdee aliyekuwa na Mkono katika ziara hiyo alisema: “Hakuna ukweli wowote kwamba alilishwa sumu, nilikuwa naye kule na mazingira aliyoanza kuumwa hadi kupona kwake ni utata... awaeleze Watanzania anaumwa nini na si kusema alilishwa sumu.

“Nilikaa kimya baada ya kuripotiwa na gazeti moja (The Citizen) kwamba Mkono kalishwa sumu, sasa amezungumza tena nikaona si busara kukaa kimya wakati alilidanganya Taifa. Mkono waeleze ukweli watu mbona unawadanganya.” Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Mdee aliwataja baadhi ya wajumbe wa msafara huo wa watu 11 kuwa ni William Ngeleja (Mwenyekiti wa kamati hiyo), Mkurugenzi wa Kupambana na Kuzuia Rushwa Tanzania (Takukuru), Dk Edward Hoseah, Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), George Mkuchika.

“Dk Hoseah ndiye aliyezungumza na daktari wa Mkono kwa kina zaidi na alimweleza kuwa ampatie dawa fulani, sasa kama kweli alilishwa sumu daktari wake alijuaje kuwa sumu hiyo inaondolewa na dawa hiyo aliyomwambia Hoseah ampe.

“Kama ni kutaka kutumia kivuli cha sakata la escrow, arudi bungeni tuijadili na tuimalize ila asiseme kuwa sijui wanataka kumuua ni uongo,” alisema Mdee.

Kuhusu vitisho alivyodai Mkono kutumiwa kabla ya safari hiyo, Mdee alisema: “Kama kweli ni vitisho iweje tulivyokwenda aliamua kulala peke yake, wewe upo safarini na wenzako halafu ukatishwa kuuawa utakwenda kulala peke yako au utalala na wenzako?”

Mkono alisema anaendelea vizuri na anasubiri kujua hatima ya uchunguzi unaoendelea ili kubaini chanzo cha kulishwa sumu.

“Niko vizuri na afya njema... kama kuna mtu anawinda jimbo langu, mwambieni ameshindwa na wananchi wangu nawaeleza kuwa niko salama wasiwe na hofu. Ninataka kujua nani kanilisha sumu na kwa nini?

“Tukiwa uwanja wa ndege nilipokea ujumbe mfupi wa maandishi (hakutaka kuuweka wazi kwa sababu upelelezi haujakamilika), ukinitahadharisha kuwa makini, ujumbe ule ulinishtua kwa kweli,”alisema. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...