Saturday, July 26, 2014

REINA ATHIBITISHA KUPENDA KUENDELEA KUICHEZEA LIVERPOOL

438662_heroa
MLINDA mlango wa Liverpool, Pepe Reina amejitia kitanzi mwenyewe katika klabu hiyo, licha ya kudai anapenda kustaafu soka la kimataifa nchini Hispania.
 Akicheza kwa mkopo Seria A katika klabu ya Napoli msimu uliopita-Reina alianza kuhusishwa kujiunga na bosi wake  wa zamani wa Anfield Rafael Benitez-na kuzua maswali juu ya hatima yake Liverpool.
 Reina amesisitiza kuwa anaheshimu mkataba wake Anfield-ambao utamalizka mwaka 2016 kabla ya kwenda nchini Hispania.
 “Nina mkataba ambao nahitaji kuuheshimu Liverpool,” Reina aliiambia radio ya Hispania ya Cadena Ser. “Ninafanya mazoezi vizuri na nipo sawa na wachezaji wenzangu”.
 “Nipo hapa kwa ajili ya kukaa”.
 “Sijazungumza na Brendan Rodgers, ni siku nne tu tangu nifike hapa, naangalia kufanya mazoezi vizuri ili kurudi katika kiwango changu”.
 Reina mwenye miaka 31 alianza maisha yake ya soka katika klabu ya Barcelona, kabla ya kwenda Villarreal na kuelekea ligi kuu nchini England, na sasa amekiri kuwa kurudi La Liga itakuwa nafasi nzuri kwake. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
 “Nimekuwa nikiwaza hili kwa muda mrefu kuwa ni vizuri kurudi ulipotoka,” Reina aliongeza.
 “Wakati Rafa Benitez ananisajili Liverpool mwaka 2005, nilikubali na nilisema nitarudi Hispania baadaye”.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...