Tuesday, June 18, 2013

BANANA ZORRO KURUDI KWENYE GAME KWA KISHINDO

 
Msanii na mmiliki wa Band ya B-band Banana Zorro amefunguka kuwa kimya kingi siku zote kina mshindo na kueleza kuwa alikuwa kimya kwa sababu alikuwa busy na kazi za Band lakini kwa sasa anatarajia kudodosha ngoma nyingine siku za karibuni kwa wale fans wake kaeni mkao wa kura. Banana amefunguka hayo leo alipokuwa katika Show ya Kikaangoni Live inayofanyika kila siku ya Ijumaa kupitia Accounts za Facebook za Eatv na East Africa Radio ambapo mashabiki wake wanapata nafasi ya kuuliza maswali na yeye kuwajibu. 
Moja ya shabiki aliuliza akitaka kujiunga katika B-band afanyaje na jibu lilikuwa anapaswa kufanya mazoezi ya kutosha na akiwa teyari awasiliane na meneja wake Allan Lucky na mambo yatakuwa poa.
Akizungumzia moja ya fanikio aliyopata katika Muziki ni pamoja na kumiliki Band yake mwenyewe ambayo ni B-band ambayo inaendelea kukuwa kila siku na kufanya vizuri pia.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...