Friday, June 28, 2013

BAADA YA MIAKA KUPITA LADY JAY DEE NA Q CHIEF WAINGIA STUDIO TENA

 
Wakali wa bongo fleva wenye vocal zenye ladha na nguvu ya aina yake Lady JayDee ‘Anaconda’ na Q-Chillah, wamekutana tena studio kurekodi wimbo mpya ikiwa ni miaka kadhaa imepita walipotisha na wimbo wao ‘Zamani’. 
Lady JayDee alipost picha kupitia akaunti yake ya Twitter ikimuonesha yeye na Q-chilla wakiwa ndani ya studio za Combination sound na Man Walter, na kuisindikiza na maelezo. 
"Mtu 3 ndani ya studio. Mwaikumbuka Zamani - Q Chief feat Jide?? Nikilala naotaa, naota km unaniita. Sasa yaja mpya."Alitweet Jide June 26.

Hakuchelewa kutaja jina la wimbo huo “Sukari” na kuonesha kuikubali sana, hii inatoa picha kuwa kitu kikubwa kinakuja.
“Sukari - Qchillah & Jide another hit ??? ☺ #Justasking.” Aliongeza.

Tuisubiri hiyo sukari tuonje ladha yake kwa masikio.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...