Saturday, March 30, 2013

Maiti 18 zaopolewa katika jengo lililoporomoka jana katikati ya jiji la Dar es Salaam

Jumla ya maiti 18 zimeopolewa katika kifusi cha jengo la ghorofa zaidi ya kumi lililopromoka jana asubuhi katika mtaa wa Indira Ghandi jijini Dar es salaam, idadi hiyo ya watu waliopoteza maisha ikiwa ni ya kihistoria kwa majanga ya aina hii.

Mwili mmoja umeopolewa muda mfupi uliopita, ikiwa ni masaa kadhaa baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Saidi Meck Sadik kuthibitisha mapema asubuhi kwamba miili 17 ilikuwa imepatikana baada ya kazi za uokoaji ya usiku kucha na inayoendelea hivi sasa.

Makampuni kadhaa ya ujenzi yamejiunga katika zoezi hilo toka usiku kusaidia kuinua vifusi na kuopoa miili ya marehemu. Uwezekano wa kukuta mtu aliye hai hadi sasa ni mdogo sana wakati waokoaji wakiwa ni pamoja ya wanajeshi na vijana wa JKT wakiendelea na kazi.

Tutaendelea kuwapa Updates kila itapobidi.

Mola aziweke roho za marehemu mahala pema peponi - AMEN

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...