Thursday, February 14, 2013

Zimbabwe kuipigia kura Katiba mpya.


Waziri mkuu wa Zimbabwe Morgan Tsvangirai anasema nchi hiyo inatarajiwa kufanya uchaguzi wa bunge na urais mwezi Julai baada ya kupiga kura  maoni juu ya katiba mpya mwezi Machi.
 Alisema hayo  Jumatano baada ya waziri wa maswala ya katiba Eric Matunenga  kupanga tarehe ya Machi 16 kwa ajili ya kupiga kura ya maoni.
 Katika mkutano na waandishi wa habari huko Harare , Matinenga alieleza wasi wasi wake kuwa muda hautoshi na pengine muda zaidi huenda ukahitajika kwa ajili ya uchaguzi wa Machi.
 Baraza la kitaifa la bunge (NCA) ambalo linajumiwsha makundi  ya harakati za kidemokrasia   huko Zimbabwe  limesema  litapinga tarehe  upigaji kura wa maoni  hapo Machi 16 mahakamani .
Katika mahojiano na Sauti ya Amerika mwenyekiti NCA Lovemore  Madhuku amesema kundi lake linataka serikali itoe kipindi cha mdahalo cha  miezi miwili hivi  kabla ya wapiga kura kufanya uamuzi wao juu ya katiba mpya.
 Chama cha Bw. Tsvangirai cha MDC na kile cha  rais Robert Mugabe cha ZANU PF wote wanaunga mkono  mabadiliko hayo mapya.
 Jumuiya ya maendeleo ya Afrika Kusini inataka  katiba mpya  iidhinishwe kabla  ya Zimbabwe kufanya uchaguzi mkuu.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...