Saturday, January 07, 2017

NANA AKUFO ADDO AAPISHWA RASMI KUWA RAIS WA GHANA

Nana Akufo-Addo akila kiapo wakati akiapishwa 
 
Viongozi kadha wa Afrika leo wamekusanyika katika mji mkuu wa Ghana, Accra, kuhudhuria sherehe za kutawazwa rais mpya, Nana Akufo Addo.

Maelfu ya wageni walialikwa kwenye sherehe katika Medani ya Uhuru mjini Accra. Bwana Akufo Addo, aliyewahi kuwa wakili wa haki za kibinaadamu, alimshinda Rais John Dramani Mahama, katika uchaguzi wa mwezi uliopita.
Madaraka yanakabidhiwa kwa kiongozi mwengine kwa salama, jambo linaloonekana kuwa mfano mwema wa demokrasi Afrika ambako katika baadhi ya nchi, viongozi hawataki kun'gatuka.

Baada ya kuapishwa kwa rais, sasa viongozi waliohudhuria sherehe hiyo, watajadili namna ya kuhakikisha kuwa Rais wa Gambia, Yahya Jammeh, anaondoka madarakani. Kiongozi huyo amekataa kustaafu ingawa alishindwa katika uchaguzi wa Mwezi Disemba.

Tuesday, January 03, 2017

MKULIMA MWINGINE AJERUHIWA KWA SIME KILOSA

524332cd04985aff0de9f1e645398d62

MTU mmoja mkazi wa Kijiji cha Mamoyo, Kata ya Mabwerebwere, Wilaya ya Kilosa, Mkoa wa Morogoro, Omary Sululu (52), amenusurika kifo baada ya kukatwakatwa na sime kichwani na watu wanaodaiwa kuwa ni wafugaji.

Taarifa zilizopatikana kijijini hapo, zinasema Sululu alijeruhiwa na wafugaji hao wakati alipokuwa akizuia mifugo isile mazao katika shamba lake.

Tukio hilo limetokea siku chache baada ya Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha Wafugaji Tanzania, Joshua Lugaso, kutoa tamko la  kulaani matukio ya kikatili yanayofanywa  na  wafugaji dhidi ya wakulima wilayani Kilosa.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii akiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kilosa, Sululu alisema alijeruhiwa Januari mosi, saa za mchana wakati alipokuwa katika shamba lake la mahindi na migomba. Tangaza biashara yako hapa. Pia like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

ANGALIA PICHA ZA BABU MWENYE MIAKA 77 MWENYE NGUVU ZA AJABU AKIVUTA GARI KWA SHINGO....!!!

meet-the-77-years-old-strongest-man-in-akwa-ibom-photos-2
 
Babu wa miaka 77 kutoka mji wa Akwa Ibom, nchini Nigeria ambaye ana uwezo wa kuvuta gari kwa kutumia shingo yake.

Babu huyo amefahamika kwa jina la Sampson, ila yeye anataka afahamike kwa jina la African Superman, ana uwezo pia wa kuweka mkono wake juu na wanaume 10 wakabembea bila kuushusha mkono wake chini.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE JANUARI 03, 2017 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

04dafa6a-93c3-49cf-be2f-ccff44ac58ae

PLUIJM AKARIBIA KUPEWA MIKOBA YA UKOCHA AZAM FC

Mabingwa watetezi wa Kombe la Kagame, Azam FC wamebakiza hatua chache kukamilisha mpango wa kumkabidhi timu hiyo aliyekuwa kocha wa zamani wa Yanga, Hans Pluijm.

Habari za kuaminika kutoka vyanzo makini ndani ya Azam zilithibitisha kuwa tayari Azam imekuwa na mazungumzo ya kina na kocha huyo Mdachi ambaye kwa sasa ni mkurugenzi wa ufundi Yanga.
Awali, Azam ilipanga kumpa timu hiyo kocha wa Majimaji, Kally Ongala ambaye amewahi kuitumikia klabu hiyo kama kocha msadizi, lakini wakabadilisha mawazo kutokana na kocha huyo kuwa na uzoefu mdogo na michezo ya kimataifa.

Mwenyekiti wa Azam, Nassoro Idrissa ‘Father’ amesema Pluijm ni kocha wa kiwango cha juu na amethibitisha hilo nchini kwa kuipa Yanga mataji manne tofauti, hivyo watafurahi kama atafanya nao kazi. Tangaza biashara yako hapa. Pia like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

Sunday, January 01, 2017

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...