Wednesday, August 28, 2013

MADIWANI WALIOTIMULIWA BUKOBA WARUDISHWA


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa imejadili na kutolea maamuzi pamoja na mambo mengine suala la Madiwani wanane waliotangazwa kufukuzwa uanachama na Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kagera.

Katika maamuzi yake, Kamati Kuu imebatilisha uamuzi uliofanywa na Halmashauri Kuu CCM ya Mkoa wa Kagera Agosti 13, 2013 wa kuwafukuza uanachama Madiwani hao. Hivyo Madiwani hao wanane ni wanachama halali wa CCM.

Kamati Kuu imetoa uamuzi huo, baada ya kubaini kuwa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kagera haikuzingatia Katiba ya CCM ya 1977 Toleo la 2012 Ibara ya 93 (15). Ibara hiyo inasomeka kuwa moja ya kazi ya Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa ni:-

“Kumwachisha au kumfukuza uongozi kiongozi yeyote ambaye uteuzi wake wa mwisho unafanywa na Halmashauri Kuu ya CCM ya Mkoa, isipokuwa kwa suala la kumvua uanachama au uongozi Diwani lisifanyike hadi Kamati Kuu imearifiwa na kutoa maelekezo”.

Tuesday, August 27, 2013

HII NDILO JENEZA LENYE KIYOYOZI NDANI, WACHA LILE LA MSUYA LINALOFUNGULIWA KWA RIMOTI

Hili ni sanduku ya aliyekua Mfalme wa Roma(self-appointed Roma king),Florin Cioaba aliyefariki wiki moja iliyopita kwa mshtuko wa moyo huko Uturuki. Sanduku lake lilikua na Kiyoyozi kama lionekanavyo pichani.
Hivi karibuni watanzania tulishangazwa pale tulipoona sanduku la Billionea wa Arusha ambalo lilikua likifunguliwa kwa 'Remote Control'. Nadhani sanduku hili pia litawashangaza wengi.


MAGAZETI YA LEO JUMANNE AGOSTI 27, 2013

DSC 0048 a976f
DSC 0049 e302d
DSC 0050 81f49
DSC 0051 86967

EAC KUJITOSA MZOZO WA TANZANIA, RWANDA

sezi_cbe2f.jpg
Wakati Tanzania ikisema kuwa iko tayari kukaa meza moja na jirani yake Rwanda kumaliza hali ya uhasama iliyoanza kujitokeza katika siku za hivi karibuni, Katibu Mkuu wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dk Richard Sezibera amesema jitihada za kidipolomasia zinafanyika kutatua tofauti hizo za kimawazo.

Bila kutaja taasisi wala wanaohusika katika jitihada hizo za kidiplomasia, Dk Sezibera aliwaambia waandishi wa habari jijini Arusha jana kuwa jitihada hizo zinafanyika kimya kimya bila kushirikisha vyombo vya habari "Migongano na tofauti za kimtazamo miongoni mwa viongozi wakuu wa nchi wanachama wa EAC ni jambo lisilo la afya kwa Jumuiya na linastahili kushughulikiwa kidiplomasia," alisema Dk Sezibera.


Akizungumza kwa tahadhari kubwa kukwepa kuingia kwa undani kuhusu suala hilo, Katibu Mkuu huyo alisema inafaa kila linalowezekana lifanyike kutatua mgongano wowote unaotokea kati ya viongozi wakuu.
Mjini Dar es Salaam, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe naye alisema katika mahojiano kuwa iwapo Rwanda itaomba kukutana na Tanzania kwa ajili ya kumaliza mzozo huo Serikali itakuwa tayari kutoa ushirikiano.

TAARIFA KAMILI KUHUSU BOMU KATIKA KANISA LA KKKT DAR ES SALAAM


POLISI Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, imebaini kuwa chombo kilichodhaniwa kuwa bomu katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kijitonyama hakikuwa bomu, bali ni kifaa cha Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) cha kuchunguza anga.
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleman Kova alisema hayo jana alipozungumza na waandishi wa habari, baada ya kufanya uchunguzi kwa kushirikiana TMA.
"Baada ya kupata taarifa, polisi walifika eneo la tukio na kukuta kifaa kilicho katika umbo la kasha kikining'inia kwenye transfoma karibu na Kanisa kikiwa kinawaka taa.

“Katika kasha hilo kulikuwa na maandishi ya kalamu ya wino yaliyosomeka TMA na Airport," alisema Kamanda Kova.
Alisema baada ya uchunguzi wa awali, polisi walibaini kuwa kifaa hicho si bomu na kuondoka nacho kwa uchunguzi zaidi. Mtabiri Mwandimizi wa hali ya hewa kutoka TMA, Augustino Kanemba, alisema kifaa hicho kinaitwa Radio Sound na hutumiwa na Mamlaka hiyo kufanya utafiti wa hali ya anga za juu.

DADA YAKE FREEMAN MBOWE AIKIMBIA CHADEMA NA KUJIUNGA CCM, ADAI CHADEMA HAINA JIPYA



DADA wa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Grace Mbowe, amejiunga na Chama Cha Mapinduzi ( CCM) akitokea Chadema, kwa kile alichodai haoni jambo jipya katika chama hicho.

Grace amesema amehama kutokana na kuwepo propaganda zisizotekelezeka. Hata hivyo, amesisitiza kwamba kuwepo kwake katika Chadema, siyo kwa sababu ya familia.

Alikabidhi kadi hiyo jana kwenye ofisi za CCM Wilaya ya Hai. Alisema itikadi za kisiasa, zisihusishe masuala ya kifamilia, kwani upendo wao uko pale pale.

Alisema kilichomfanya kujiunga na chama hicho ni utashi wake. Alidai CHADEMA wanafanya propaganda za 



kuwadanganya wananchi.

Alisema itikadi za chama, haziwezi kuingilia masuala ya kifamilia, hivyo kwake siyo ajabu kuondoka CHADEMA, kwani kila mtu ana utashi wake wa kisiasa.

MAN U, CHELSEA HAKUNA MBABE



Beiki wa Chelsea, Ashley Cole (kushoto) akikwaana na Wyne Rooney wa Manchester United.
Mshambuliaji wa Manchester United, Wyne Rooney (kushoto)  akijaribu kupiga shuti langoni mwa Chelsea.
Mourihno na Moyes wakisalimiana kabla ya mechi hiyo.

MANCHESTER UNITED VS CHELSEA 0-0 FULL HIGHLIGHTS

Monday, August 26, 2013

WANAUME WAWILI WAAMUA KUOA MWANAMKE MMOJA ILI KUEPUSHA UGOMVI WA KUMGOMBEA


Wanaume wawili nchini Kenya wameibuka na mbinu isiyo ya kawaida ya kupata suluhu ya kupigania mwanamke ambaye wote wanampenda Wamesaini mkataba wakikubaliana kuishi nae kwa zamu.


Silvester Mwendwa ni mmoja wa wanaume hao anayeanza kwa kueleza kwa nini binafsi anamuhusudu mwanamke huyo.

Mmoja ya wa wanaume hao alisema haoni ubaya wowote kwa yeye na
mwenzake kumuoa mwanamke mmoja.

Amehoji sheria ya sasa inayoruhusu wanaume kuoa wanawake wengi na wakati huo huo kuharamisha mpango kama huo kwa kina mama.

Sylvester Mwendwa anasema wazazi wake wamekubali na mpango wake na wakotayari kumtolea mahari

MBWA AZIKWA NA MAELFU YA WATU......! APEWA HESHIMA ZOTE


dog hero

 
Unacho kiona katika picha hapo chini ni mazishi shujaa ambayo yalitolewa kwa mbwa. Jina la mbwa alikuwa akiitwa Zanjeer na yeye kuokoa maelfu ya maisha ya watu wakati wa milipuko Mumbai Serial Machi 1993. Yeye alikua na  kilo zaidi ya 3329 ya RDX kulipuka, detonatorer 600, mabomu 249 mkononi na raundi ya 6406 ya risasi kuishika kusudi watu wasilipuke.
Kusema kwaheri kwa Zanjeer baada ya yeye kupita, alizikwa kwa heshima kamili.

ANGALIA VIDEO YA MWANAFUNZI ALIYESHITAKIWA KWA KUIBA SADAKA....!!!


 
Tembelea http://jambotz8.blogspot.com/ kila siku.

MSICHANA AMEJIKUTA AKIZOMEWA NA KUCHAPWA VIBOKO BAADA YA KUVAA NGUO FUPI...!!!


Msichana mmoja ambaye jina lake halikujulika amejikukuta katika wakati mgumu baada ya kuzomewa na   kuchapwa viboko na kundi la watu katika eneo la soko la nmc jiji arusha kwa madai ya kuvaa nguo fupi hali iliyowalazimu wasamariawema kuingilia kati  na kutumia nguvu kubwa ili  kumwokoa na kumsitili kwa kumfunika na nguo zingine.

 Mwandishi wetu Halfani Lihundi  kutoka arusha alikuwapo katika sakata hilo na ametuma taarifa hii iliyosema,  watu walio shuhudia tukio hilo wamesema wamechukizwa na aina ya nguo alizizovaa msichana huyo ambazo haziendani na maadili ya Kitanzania, ndiyo maana wameamua kumwadabisha ili kukomesha tabia hiyo. Tembelea http://jambotz8.blogspot.com/ kila siku.

Kwa upande wao wanawake waliyo msitili msichana huyo kwa kumpa nguo za heshima na kumhifadhi katika Gareji ya jirani kabla ya kumkimbiza kwa gari aina ya Toyota Hiace wamesema hawaridhishwi na tabia hiyo inayowazalilisha wanawake na kuwataka wasichana kuavaa nguo za kujisitili ili kujenga heshima katika jamii.
Source ITV

AHUBIRI ZAIDI YA MASAA MATATU BILA WAUMINI...!!!

Mhubiri wa injili akitoa neno pembeni ni viti kwa ajili ya waumini japo hakuna aliyejitokeza.
...Akizidi kumwaga injili.
 ...Akielezea umuhimu wa kumtukuza bwana.

CHAZ BABA AFUNGA NDOA, ATINGA UKUMBI WA ‘TWANGA’ KUJINAFASI AKIWA PEKE YAKE


 Rehema akikubali kuolewa na Chaz.

 
Chaz akimvisha pete mkewe.

CCM KWAWAKA MOTO MMOJA ATIMULIWA UANACHAMA


Nape Moses Nnauye,

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) iliyomalizika leo imejadili kwa kina Masuala mbalimbali likiwemo pendekezo la Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Magharibi - Zanzibar la kumvua uanachama Ndugu Mansoor Yussuf Himid, Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi wa Kiembesamaki.
Baadhi ya tuhuma za Ndugu Mansoor Yussuf Himid ni pamoja na:-
1.   Kushindwa kusimamia malengo ya CCM na kutekeleza masharti ya uanachama.
2.   Kushindwa kutekeleza wajibu wa mwanachama na kukiuka Maadili ya Kiongozi wa CCM.
3.   Kuikana Ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010-2015 na kuisaliti CCM.
Baada ya kujiridhisha vya kutosha na tuhuma dhidi ya Ndugu Mansoor Yussuf Himid, Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) imeridhia uamuzi wa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Magharibi Zanzibar wa kumfukuza uanachama. Kwa uamuzi huo wa kumvua uanachama wa CCM Ndugu Mansoor Yussuf Himid, yeye kwa sasa sio Kiongozi tena wa CCM.
Imetolewa na:
Nape Moses Nnauye,
KATIBU WA NEC ITIKADI NA UENEZI CCM TAIFA
26/08/2013

Tembelea http://jambotz8.blogspot.com/ kila siku.

DILLISH TOKA NAMIBIA AIBUKA MSHINDI WA BIG BROTHER AFRICA 2013

 
Fainali za Big Brother zimefikia  tamati  usiku  huu  zikiwa  na  washiriki  watano  ambao  ni  Beverly, Melvin, Cleo, Elikem  na  Dillish.

Mshiriki  wa  kwanza  kutolewa  alikuwa  ni  Beverly  akifuatiwa  na  Melvin  huku  Elikem  akiwa  ni  mshiriki  wa  tatu  kutolewa..

Mchujo  huo  uliwafanya  Cleo  na  Dillish  waingie  katika  masaa  ya  fainali za  mwisho  ambapo  Cleo  alielemewa  na  kutolewa  huku  akimwacha  Dillish  akichekelea  $300,000  za  ushindi  wa  shindano  hilo....

Agalia  jinsi  kura  zilivyopigwa:
 Angola: Dillish
Botswana: Cleo
Ghana: Elikem
Kenya: Dillish
Ethiopia: Beverly
Malawi: Cleo
Namibia: Dillish
Nigeria: Melvin
South Africa: Cleo
Sierra Leone: Elikem
Tanzania: Dillish
Uganda: Dillish
Zambia: Cleo
Zimbabwe: Elikem
Rest of Africa: Melvin
Total

Dillish = 5, Cleo = 4, Elikem = 3, Melvin = 2, Beverly = 1.
 
Hongera sana Dillish

MAGAZETI YA LEO JUMATATU AUGUST 26, 2013 YA UDAKU, MICHEZ0 NA HARD NEWS

DSC 0063 d67d6
DSC 0064 188c0

TANGAZO LA USAILI NAFASI ZA JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA



TANGAZO                            TANGAZO                            TANGAZO                   TANGAZO
 
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA DIWANI ATHUMANI – ACP ANAWATANGAZIA WANANCHI WOTE YA KUWA ORODHA YA MAJINA YA VIJANA WALIOMALIZA KIDATO CHA NNE MWAKA 2012 NA CHA SITA MWAKA 2013 NA KUCHAGULIWA KUFANYA USAILI WA KUJIUNGA NA JESHI LA POLISI INAPATIKANA KWENYE TOVUTI YA POLISI www.policeforce.go.tz.
MUHIMU.                                                                                                          
       i.            MWOMBAJI ANARUHUSIWA KUFANYA USAILI KWENYE KITUO CHOCHOTE CHA USAILI KILICHO KARIBU NAE KULINGANA NA TAREHE ZINAVYOONYESHA KWENYE TANGAZO LA USAILI.
     ii.            KWA MKOA WA MBEYA NA IRINGA KITUO CHAO NI MBEYA NA USAILI UTAFANYIKA KUANZIA TAREHE 16/09/2013 HADI 19/9/2013 SAA 2:00 ASUBUHI HADI SAA 10:00 JIONI KATIKA OFISI YA KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.
  iii.            MWOMBAJI ALIYEITWA KWENYE USAILI AJE NA VYETI VYOTE VYA MASOMO(ACADEMIC CERTIFICATES),RESULTS SLIP(S) NA LEAVING CERTIFICATE(S), NAKALA HALISI YA CHETI CHA KUZALIWA(ORIGINAL BIRTH CERTIFICATE). HATI YA KIAPO CHA KUZALIWA HAITAKUBALIWA.
  iv.            MWOMBAJI AWE NA NANMBA YA SIMU AMBAYO ITAMJULISHA ENDAPO ATAKUBALIWA.
     v.            KILA MWOMBAJI ALIYEITWA KWENYE USAILI ATAJIGHARAMIA USAFIRI, CHAKULA, NA MALAZI KWA MUDA WOTE WA ZOEZI LA USAILI.
  NI MUHIMU SANA KILA MWOMBAJI KUZINGATIA MUDA WA KUANZA USAILI.

Saturday, August 24, 2013

KUWA WAKWANZA KUSIKILIZA NA KUDOWNLOAD WIMBO WA MSANII MPYA WA HIP HOP CHATTA RYMES KUTOKA SHY TOWN

Ujio mpya katika mziki wa kizazi kipya katika miondoko ya hiphop.. Anaitwa ISSA ALLY  a.k.a CHATTA RYMES  ni kijana mdogo mwenye uwezo wa kushangaza katika mziki Anakuja na wimbo wake mpya  aliofanya na KING DIZZO unaitwa SEMA NAO ameufanyia katika Studio  za SHY TOWN REC pande za SHINYANGA Tz


Kwa muonekano ni mdogo lakini kiuandishi ni hatari sana na anaplan ndefu ya kuhakikisha mziki unaweza kumlipa na kumfanya aendeshe maisha yake kupitia mziki na hatimae kuitangaza Tanzania kimataifa zaidi.


SUPORT YAKO NDIO ANAYOIHITAJI 



                   ARTIST: Chatta Rymes Ft King Dizzo

                   TRACK:Sema nao

                   STUDIO:Shy Town Recs

                   PRODUCER:Hance Q

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI AUGUST 24, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

CHANZO CHA MAUAJI YA BILIONEA ERASTO MSUYA HIKI HAPA


 Mbunge wa Simanjiro Ole Sendeka alipo wasili Msibani.



Mc wa Shughuli ya Mazishi alikua ni JB.



Friday, August 23, 2013

MADAM RITA: "NAY WA MITEGO HANA PESA ZA KUNILIPA HATA NIKIMFUNGULIA KESI"


                                        Madam Rita

 Mratibu wa shindano la Epic Bongo Star Search(EBSS) Rita Paulsen (Madam Rita ) ameshangazwa na taarifa zilizoenea katika vyombo mbalimbali vya habari ikiwemo mitandao ya kijamii ,kuhusiana na yeye kutaka kumfungulia mashtaka msanii Nay Wa Mitego ambaye anadaiwa kumchafua (defamation) katika wimbo wake mpya unaotamba sasa (Salamu Zao). Amesema hana mpango
wa kumfungulia mashitaka kwa kuwa hatakuwa na pesa za kumlipa kwa maana itakuwa kesi ya kumchafua na inaweza kumgharimu pesa nyingi.
.
Madam Rita ameyasema hayo wakati akifanya mahojiano katika kipindi cha burudani cha The Strengo Saturday kinachorushwa na Radio Victoria fm kupitia 90.6 kilichopo Musoma, Mara. Ambapo mtangazaji wa kipindi hicho Patrick Derrick Mwankale alitaka kujua sababu kubwa ya EBSS kuhamishiwa katika kituo cha televisheni cha TBC1 ikitokea ITV na vipi kuhusiana na habari zilizopo za yeye (Madam Rita) kutaka kumfungulia Nay Wa Mitego kesi ya kumchafua .

JK AAPISHA MAKATIBU WAKUU NA NAIBU MAKATIBU WAKUU IKULU DAR ES SALAAM LEO

 Rais Jakaya Kikwete na Katibu Mkuu Kiongozi Mhe Ombeni Sefue wakiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa ofisi ya Sekretariate ya Baraza la Mawaziri ambako watumishi wake wawili wameteuliwa kuwa manaibu Makatibu wakuu, ambao ni Injinia Angelina Madete (kulia kwa Rais) na Mhe. Consolata Mgimba (kushoto kwa Rais) mara baada ya kuapishwa Makatibu wakuu na Manaibu Katibu wakuu Ikulu jijini Dar es salaam leo.
 Rais Jakaya Kikwete, Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilal na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue katika picha ya pamoja na Makatibu wakuu na manaibu Katibu wakuu wapya mara baada ya kuapishwa Makatibu wakuu na Manaibu Katibu wakuu Ikulu jijini Dar es salaam leo.
 Rais Jakaya Kikwete, Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilal na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue katika picha ya pamoja na Makatibu wakuu wapya mara baada ya kuapishwa Makatibu wakuu hao na Manaibu Katibu wakuu Ikulu jijini Dar es salaam leo.

HIKI NDICHO KILICHOMPONZA LULU MPAKA FILAMU YAKE YA FOOLISH AGE KUPIGWA STOP





Bodi ya ukaguzi wa filamu na michezo ya kuigiza nchini imeipiga stop filamu ya Foolish age ya msanii wa kike mwenye mvuto Bongo Elizabeth Michael ‘Lulu’ baada ya kukuta picha zilizo nje ya maadili ya Kitanzania katika filamu hiyo, filamu hiyo ambayo ilipanga kuzinduliwa mwezi huu tarehe 30 katika ukumbi wa Mlimani City inahitaji marekebisho.

Kikwazo kilichoikumba filamu hiyo ni nguo fupi zilizotumika katika waigizaji walioshiriki katika filamu hiyo ambayo inatabiriwa kufanya vizuri katika soko la filamu Bongo kama itafanikiwa kuzinduliwa na kuingia sokoni, juhudi zinafanyika kuhakikisha kuwa marekebisho yanafanyika ili kwenda na ratiba kama ilivyopangwa.

Hivi sasa baada ya urasimishaji wa filamu mamlaka na taasisi zinazohusika na masuala ya filamu zimekuwa makini na kuhakikisha kuwa filamu zinazoingia sokoni na zile zinazozinduliwa kukaguliwa kabla ya kufanyika kwa matukio hayo kama ilivyokuwa awali, kama filamu hiyo ya Foolish age itashindwa vigezo vya madaraja yanayotolewa na Bodi hiyo haitaonyeshwa.

Lulu ndio mwigizaji bora wa kike kwa mwaka 2013 kupitia tamasha la filamu la kimataifa la ZIFF katika kipengere cha tuzo za Bongo movie kilichopewa jina la Zuku Bongo movie Awards zilizotolewa katika ukumbi wa Ngome Kongwe.

TFF: YANGA WAMEONGEZA ADHABU YA MRISHO NGASSA

 
Mrisho Ngassa.
Na Khatimu Naheka
IMEFAHAMIKA kuwa Klabu ya Yanga, ndiyo iliyochangia ukubwa wa adhabu aliyopewa kiungo wake mshambuliaji Mrisho Ngassa, Championi Ijumaa limebaini.
Taarifa hiyo inakuja wakati ambao Ngassa amefungiwa kucheza mechi sita za mashindano pamoja na kuilipa Simba jumla ya shilingi milioni 45, sababu kubwa ikiwa ni kusaini mikataba miwili, ule wa Yanga na ule wa Simba.

Boniface Wambura ambaye ni Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), ameliambia Championi Ijumaa kuwa, adhabu ya kufungiwa michezo sita kwa Ngassa imewekwa maalum, kutokana na Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji kutaka mchezaji huyo apate uchungu wa makosa aliyoyafanya na siyo kutegemea kulipiwa na klabu.
Wambura alisema adhabu hiyo imetokana na kasumba ya klabu mbalimbali ambazo zimekuwa zikiamua kulipa faini wanazokatwa wachezaji wao kwa makosa mbalimbali, maamuzi ambayo yanasababisha wachezaji kurudia makosa hayo.

SHAHIDI KESI YA WEMA AGEUKA ‘BUBU’ GHAFLA

KESI inayomkabili staa wa filamu Bongo, Wema Isaac Sepetu ya kudaiwa kumtukana matusi ya nguoni na kumpiga vibao meneja wa hoteli, Goodluck Kayumbu ilizua kituko baada ya shahidi kugeuka ‘bubu’ ghafla.
 
Kituko hicho kilijiri Agosti 20, mwaka huu katika Mahakama ya Mwanzo Kawe jijini Dar ambako kesi hiyo inaunguruma.
Mmoja wa makarani wa mahakama hiyo aliyeomba hifadhi ya jina lake, alisema kitu kilichoonekana kituko ni pale shahidi wa mwisho aliposhindwa kutoa ushahidi baada ya sauti kukauka ghafla.
 “Mlalamikaji alifika hapa na mashahidi wake watatu, Boniface Mati, Taito Osa na Melao  ambapo wawili walitoa ushahidi lakini Taito alishindwa kutoa ushahidi wake kwani sauti ilikata ghafla na ndipo hakimu Bernice akamuamuru anyamaze na kupanga tarehe nyingine ya kuwasikiliza mashahidi hao,” alisema karani huyo.


Mlalamikaji wa kesi hiyo, alipoombwa na paparazi wetu azungumzie ‘ ishu’ ya shahidi wake kushindwa kuzungumza alisema amekubaliana na uamuzi wa mahakama  na anasubiri tarehe ya kurudi mahakamani ambayo ni Septemba 30, mwaka huu.

MAGAZETI YA LEO IJUMAA AGOSTI 23, 2013

DSC 0244 1381a
DSC 0245 1e04d

MUNGU ALINIAMURU NIJIUZULU, ASEMA PAPA BENEDICT XVI

pope_37848.jpg
Rome, Italia. Miezi sita baada ya kujiuzulu, Papa Benedict XVI, amefungua mdomo na kueleza sababu za kufikia uamuzi huo wa kushangaza.
Jana, vyombo vya habari vilimkariri Papa Mstaafu Benedict akimweleza mgeni wake kuwa aliitwa na Mungu kwa miujiza.
P.T

Kiongozi huyo ambaye alishangaza watu kwa uamuzi huo wa Februari 8, mwaka huu, hata hivyo alisema sauti ya Mungu imejibu kupitia kwa mfuasi wake, Papa Francis.
Papa Benedict alitangaza uamuzi wa kujiuzulu Februari 11, maelezo yake yalielekeza katika afya yake.
Alisema nguvu zake zilikuwa zimepungua kiasi cha kutokuweza kumudu majukumu yake ipasavyo.

ANGALIA PICHA ZA RAIS ROBERT MUGABE WA ZIMBABWE ALIPOKULA KIAPO JANA

 Rais wa Zimbabwe Robert Gabriel Mugabe akila kiapo cha kuongoza nchi hiyo kwa miaka mitano ijayo katika sherehe zilizofana sana katika Uwanja wa Taifa wa Michezo wa Harare Agosti 22, 2013
  Rais wa Zimbabwe Robert Gabriel Mugabe akivishwa shada na medali baada ya kula kiapo cha kuongoza nchi hiyo kwa miaka mitano ijayo katika sherehe zilizofana sana katika Uwanja wa Taifa wa Michezo wa Harare Agosti 22, 2013

MKENYA AKIRI KUUA NA KULA MOYO NA UBONGO WA MAREHEMU, MAREKANI


Alexander Kinyua (kushoto) na mwanamume aliyekuwa akiishi naye nyumba moja Kujoe Bonsafo Agyei-Kodie. Picha/MAKTABA



Mwanafunzi kutoka Kenya aliyekuwa akiishi Marekani amekiri kwamba alimuua mwanamume waliyekuwa wakiishi nyumba moja na kula moyo wake na ubongo wake.

MWANAFUNZI kutoka Kenya aliyekuwa akiishi Marekani amekiri kwamba alimuua mwanamume waliyekuwa wakiishi nyumba moja na kula moyo wake na ubongo wake.
Alexander Kinyua, 22, alikiri mashtaka ya mauaji ya Kujoe Bonsafo Agyei-Kodie, 37, katika jimbo la Maryland mwaka jana lakini Jaji akasema hafai kulaumiwa aliposhtakiwa Jumatatu wiki hii.

Thursday, August 22, 2013

HATIMAYE MWANAMUZIKI MKONGWE WA DANS MUHIDIN GURUMO AKUBALI YAISHE NA SASA ASTAAFU RASMI MUZIKI



Mwanamuziki mkongwe wa muziki wa dansi wa bendi ya Msondo Ngoma, Mzee Muhidin Gurumo, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uamuzi wake wa kustaafu rasmi kazi ya muziki aliyoifanya kwa muda wa miaka 53 sasa. Gurumo alitoa kauli hiyo leo katika ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo jijini Dar es Salaam. Picha na Magreth Kinabo.


************************************


Na Jennifer Chamila, Maelezo.


MWANAMUZIKI mkongwe wa bendi ya Msondo Ngoma Mzee Muhidin Gurumo amestaafu rasimi kazi ya muzika alioifanya kwa muda wa miaka 53.




Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Mzee  Gurumo mwenye umri wa miaka 73 amesema ameamua kustaafu kazi hiyo kwa hiari yake mwenyewe kutokana na umri wake kuwa mkubwa.




“Muziki kwangu umekuwa kama asili yangu na kazi yangu lakini nimeamua kustaafu kutokana na umri wangu na nitabaki kuwa mshauri tu kwa mwanamuziki yeyote atakayetaka ushauri wangu,”alisema  Mzee Gurumo.

MAAFISA WA JESHI LA POLISI WAVULIWA MADARAKA NA KUSIMAMISHWA KAZI

pic 2
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt.Emmanuel Nchimbi akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu hatua  ya kuwavua madaraka Maafisa wanne wa Jeshi la polisi nchini na kumsimamisha kazi mmoja kutokana na kukiuka maadili na taratibu za Jeshi la Polisi.
……………………………………………………………….
Na Lydia Churi, MAELEZO

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewavua madaraka Maafisa wanne wa Jeshi la Polisi nchini na kumsimamisha kazi mmoja ambaye atafunguliwa mashtaka ya kijeshi kutokana na kukiuka maadili na taratibu za jeshi hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo, Waziri Nchimbi amesema hatua hiyo ni katika kuendeleza vita ya kuhakikisha kuwa jeshi la polisi linakuwa na nidhamu, linatekeleza wajibu wake wa kutenda haki na kuwalinda raia na mali zao.
Alisema amewachukulia hatua Maafisa hao baada ya kuridhia maoni ya kamati aliyoiunda kufanya uchunguzi wa matukio yaliyolalamikiwa dhidi ya askari polisi katika mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Morogoro na Kigoma kati ya Desemba 2012 na Mei, 2013.

FILAMU YA “FOOLISH AGE” YAIKUTANISHA LULU NA BODI YA FILAMU...!!!



 Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Tanzania Bi. Joyce Fissoo akiwaonyesha wajumbe pamoja na wahusika wa Kampuni ya Proin Promotions baadhi ya maeneo muhimu ya kufanyiwa marekebisho wakati walipowasilisha filamu yao ya “Foolish Age” katika Bodi ya Filamu kwa ajili ya ukaguzi.
 Msanii wa filamu Elizabeth Michael (Lulu) akieleza jambo mbele ya Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Tanzania Bi. Joyce Fissoo wakati kampuni yake ya Proin Promotions ikiwasilisha filamu yake ya “Foolish Age” kwa ajili ya ukaguzi.
 Msanii wa filamu Elizabeth Michael (Lulu) akiweka sahihi yake kuashiria amekubaliana na taratibu zote alizoelekezwa na Bodi ya Filamu wakati wa ukaguzi wa filamu yake ya “Foolish Age”.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...