Baada ya Ney Wa Mitego kutoa Track ya Salam Zao, Kuna tetesi Kuwa
Muandaaji wa BSS Madam Rita anampango kumfungulia Kesi ya Madai Ney wa
Mitego kwa Kumchafua (Defamation)
kwani eti alisema Madam Rita huwa
hatoi zawad anazoziahidi kwa washindi wa shindano
lake la kusaka Vipaji, Je Kama ni kweli kuhusu Kesi hii Ney wa mitego
ataweza kulipa milioni 500? Tayari msanii huyo amesema yuko tayari
kwenda mahakamani na ataweka mwanasheria wa kumtetea.
Thursday, August 22, 2013
HII NDO KAULI KUTOKA KWA NDUGU WA AGNES MASOGANGE, KUHUSU NDUGU YAO KUKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA
Kwa mujibu wa ndugu mmoja wa familia hiyo aliyeomba jina lake lisitiriwe, wameamua kumwachia Mungu ishu hiyo kwani ndiye anayejua ukweli. “Unajua baba wa Masogange (mzee Gerald Waya) ni mlokole, sasa amekabidhi ishu nzima mikononi mwa Mungu kwa hiyo hayuko tayari kusemasema maneno ambayo hayatakuwa na faida,” alisema ndugu huyo.
Habari zinazidi kudai kwamba, mzee huyo aliwahi kuchukizwa na kitendo cha binti yake huyo kujiingiza kwenye sanaa, hadi kuonekana akinengua kwenye muziki.
Hilo liliwahi kubainishwa na Masogange mwenyewe miaka ya nyuma alipohojiwa na gazeti ndugu na hili (Ijumaa) kupitia safu ya Ten Questions (Maswali Kumi) ambapo ilikuwa hivi:
TQ: Inasemekana umetokea kwenye familia ambayo imeiva kidini, walokole, wao wanachukuliaje suala la wewe kuingia kwenye mambo ya kuuza sura tena wakati mwingine kwenye mavazi ya kimitego?
WATUMISHI WA ZAHANATI WATUHUMIWA KUFANYA MAPENZI NA WAGONJWA.
WATUMISHI wawili katika zahanati ya Mwanhala wilayani Nzega, wamekumbwa na kashfa ya kufanya mapenzi na wagonjwa hospitalini.
Kutokana na kashfa hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Nzega, Bitun Msangi, ameiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Nzega, kuchukua hatua kali za kinidhamu kwa watumishi hao.
Agizo la mkuu huyo limetolewa hivi karibuni, baada ya Diwani wa kata ya Utwigu, Sawaka Shita kuwalalamikia watumishi hao mbele ya Baraza la Madiwani, kwa kukithiri kufanya mapenzi na wagonjwa nyakati za kazi, licha ya kuonywa kwa mara kadhaa.
Diwani huyo aliliambia baraza hilo kuwa vitendo hivyo vina hatarisha maisha ya watumishi hao na ya wananchi, hususani waliotembea nao na kutishia kuvunja ndoa za wananchi.
Alidai kuwa taarifa hizo za malalamiko, zilishafika katika ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji, tayari kwa utekelezaji, lakini wananchi wa kata hiyo walitaka kuifunga zahanati hiyo, baada ya kukithiri vitendo hivyo vya kufanya mapenzi katika wodi zilizopo.
MKE AFUMANIWA AKILIWA URODA CHOONI NA RAFIKI WA MUMEWE
Mwanaume aliyetambulika kwa jina moja la Juma, mkazi wa Tegeta A, Dar amejikuta akikamuliwa faini ya Sh. laki tano kufuatia kufumwa ugoni na mke wa mtu.
Katika tukio hilo lililojiri Kimara-King’ong’o, Dar, Jumapili iliyopita, Juma alifumaniwa na mke wa mwanaume aitwaye Swai aliyetajwa kwa jina moja la Cesilia, mkazi wa maeneo hayo.
Ilidaiwa kuwa Cesilia alimwachia mumewe mtoto na kumuaga kuwa anakwenda harusini ambapo mumewe alimkubalia bila kujua kumbe anakwenda kuzini.
Ilisemekana kuwa muda mfupi baadaye, kuna vijana walimfuata Swai na kummwagia ‘upupu’ kuwa mkewe alikuwa akisaliti ndoa yao.
Ilifahamika kuwa vijana hao walimchukua Swai na kumpeleka hadi kwenye nyumba ambayo wenyewe hawajahamia iliyopo karibu na biashara yao ya duka ambapo baada ya mwenye mali kuingia, alimkuta Juma akiwa amevaa ‘singlendi’ na bukta ambapo alizidi kuangaza macho huku na kule ili amuone mkewe.
RAIS KIKWETE AFANYA MABADILIKO YA MAKATIBU WAKUU NA MANAIBU WAKE.... !!!
Kauli hiyo ilitolewa leo jioni na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
“Rais amefanya mbadiliko haya kwa lengo kuu la kuimarisha utendaji wa kazi za Serikali katika ngazi hizo za juu,” alisema Balozi Sefue.
Mabadiliko yaliyofanywa kwa upande wa Makatibu Wakuu ni kama ifuatavyo:
- Dk Florens Turuka amekuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, awali alikuwa Katibu Mkuu Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia.
- Joyce Mapunjo amekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, awali alikuwa Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko.
RWANDA NA UGANDA WAJITOA BANDARI YA DAR ES SALAAM
Chama cha Wasafirishaji wa Mafuta Tanzania (Tatoa), kimesema Rwanda na Uganda zitajitoa kutumia Bandari ya Dar es Salaam kuanzia Septemba Mosi, mwaka huu.
Katibu Mtendaji wa Tatoa, Zacharia Hanspope aliwaambia waandishi wa habari jana baada ya kukutana na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuwa nchi hizo zinajitoa kutokana na matatizo mbalimbali ambayo kwa muda mrefu zimekuwa zikiyalalamikia lakini Serikali haikuchukua hatua.
Hanspope alisema ushuru wa barabara na ushuru wa forodha ni baadhi ya vikwazo ambavyo vimekuwa vikilalamikiwa kwa muda mrefu na wafanyabiashara mbalimbali wa nchi hizo.
“Serikali ipunguze gharama za ushuru wa barabara na ushuru wa forodha ili kuwa na ushindani sawa na bandari nyingine na hivyo kuzivutia kutumia Bandari ya Dar es Salaam,” alisema Hanspope.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Omary Chambo alikataa kuzungumzia lolote kuhusu suala hilo akisema halina mantiki yoyote kwake.... “Hivi hilo jambo unaloniuliza lina sense (mantiki) yoyote? Mie siwezi kujibu lolote nenda ukamuulize mwenyewe (Hanspope) maana wakati akisema mimi sikuwepo.”
Wednesday, August 21, 2013
ALHAJ MWINYI NA MZEE MKAPA WAWASILI ZIMBABWE KUHUDHURIA SHEREHE ZA KUAPISHWA KWA RAIS MUGABE
Marais Wastaafu Alhaj Ali Hassan
Mwinyi na Mzee Benjamin William Mkapa na wake zao, Mama Sitti Mwinyi na
Mama Anna Mkapa, wakiondoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius
Nyerere kuelekea Harare, Zimbabwe, kushiriki katika sherehe ya kuapishwa
kwa Rais wa Zimbambwe, Mhe Robert Mugabe, inayotarajiwa kufanyika kesho
Alhamisi Agosti 22, 2013
Marais Wastaafu Alhaj Ali Hassan
Mwinyi na Mzee Benjamin William Mkapa na wake zao, Mama Sitti Mwinyi na
Mama Anna Mkapa, wakiwasili katioka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa
Harare, Zimbabwe, walikoalikwa kushiriki katika sherehe ya kuapishwa kwa
Rais wa Zimbambwe, Mhe Robert Mugabe, inayotarajiwa kufanyika kesho
Alhamisi Agosti 22, 2013.PICHA NA IKULU
MADIWANI BUKOBA: TUKO TAYARI KUHAMIA CHADEMA....!!!
MADIWANI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliofukuzwa katika Manispaa ya
Bukoba, wamesema wako tayari kujiunga na Chama Cha Demokrasia na
Maendeleo (Chadema), kama chama chao kitaendelea na msimamo wa
kuwafukuza. Akizungumza na MTANZANIA kwa njia ya simu, mmoja wa madiwani
hao (jina na kata yake tumevihifadhi), alisema wako tayari kuhamia
Chadema muda wowote kama hawatarudishiwa uanachama wao.
Alisema, madiwani wote waliofukuzwa wana msimamo mmoja, ambapo wanasubiri vikao vya Kamati Kuu ya CC ili wajue hatima yao, lakini vikishindwa kuwarudisha kwenye chama, watahamia Chadema ili kuendeleza harakati zao walizozianzisha.
Alisema, wanachokifanya wao ni kutetea maslahi ya taifa na wananchi waliowapigia kura na si kulinda biashara za watu binafsi, hata kama wanaungwa mkono na uongozi wa juu wa CCM.
Msimamo huo wa madiwani umekuja siku mbili baada ya Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe, kuwakaribisha madiwani hao katika chama chake na kusema wako tayari kuwafundisha siasa za mageuzi.
Alisema, madiwani wote waliofukuzwa wana msimamo mmoja, ambapo wanasubiri vikao vya Kamati Kuu ya CC ili wajue hatima yao, lakini vikishindwa kuwarudisha kwenye chama, watahamia Chadema ili kuendeleza harakati zao walizozianzisha.
Alisema, wanachokifanya wao ni kutetea maslahi ya taifa na wananchi waliowapigia kura na si kulinda biashara za watu binafsi, hata kama wanaungwa mkono na uongozi wa juu wa CCM.
Msimamo huo wa madiwani umekuja siku mbili baada ya Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe, kuwakaribisha madiwani hao katika chama chake na kusema wako tayari kuwafundisha siasa za mageuzi.
GODBLESS LEMA AUGUA GHAFLA, KESI YAKE YAHAIRISHWA
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Arusha jana imeshindwa kuanza kusikiliza kesi ya uchochezi inayomkabili Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, dhidi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, kutokana na mbunge huyo kuwa mgonjwa.
Wakili wa Lema, Method Kimomogoro, aliieleza mahakama hiyo mbele ya Hakimu Mkazi, Hawa Mguruta, anayesikiliza shauri hilo kuwa Lema anaumwa na alikuwa amelazwa katika Hospitali ya AICC tangu Agosti 14 hadi 19, mwaka huu aliporuhusiwa kutoka hospitali, hivyo ametakiwa apumzike kwa muda wa siku 10 kuanzia Agosti 19, mwaka huu.
Wakili Kimomogoro aliomba shauri hilo liahirishwe hadi siku nyingine, ombi lililokubaliwa na hakimu aliahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 1 na 2 mwaka huu, ambapo mashahidi tisa wanatarajiwa kutoa ushahidi wao.
DIAMOND NAE ATAJWA SAKATA LA UNGA....!!!
*Utajiri, safari zake nje ya nchi vyatiliwa shaka
*Ahusishwa na mtandao hatari wa Masogange
KWA mara ya kwanza tangu lilipoibuka sakata la watu maarufu kujihusisha ama na utumiaji au usafirishaji wa dawa za kulevya, jina la mwanamuziki anayeaminika kuwa na ukwasi mkubwa kwa sasa hapa nchini, Nasseeb Abdulmaliki, maarufu zaidi kwa jina la Diamond, limeanza kutajwa kuwa ni miongoni mwa vigogo wa ‘unga.’
Tayari mjadala mkubwa wa chini chini umeibuka kwa watu mbalimbali wakiwemo mashabiki wake, na taarifa ambazo zimelifikia MTANZANIA Jumatano kutoka vyanzo mbalimbali zimedai kuwa, mwenendo wa maisha ya Diamond sasa unachunguzwa na baadhi ya maofisa wa vyombo vya dola vya ulinzi na usalama.
Kutajwa kwa jina la Diamond katika sakata hili, kunatiwa nguvu zaidi na mwenendo binafsi wa maisha wa msanii huyo maarufu wa muziki wa kizazi kipya, unaokwenda sambamba na ukwasi mkubwa alioupata katika kipindi kifupi.
Kama hiyo haitoshi, safari za nje ya nchi za mwanamuziki huyo unaohusisha ziara zake nchini Afrika Kusini na Uingereza, pia ni mambo ambayo yamechochea wingu la mashaka lililofikia hatua ya jina lake kuingizwa katika mtandao huo ambao katika siku za karibuni, umewagusa pia baadhi ya watu wenye majina makubwa katika jamii.
PONDA AIGHARIMU SERIKALI MILIONI 10...!!!
*Usafiri wa helikopta waitafuna dola mara 71 ya gharama ya gari
ULINZI wa Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu, Sheikh Ponda Issa Ponda, akiwa gerezani na anapopelekwa mahakamani, umeanza kuvitesa vyombo vya Dola. Habari zilizolifikia gazeti hili na kuthibitishwa na Kamanda wa Kikosi cha Anga wa Jeshi la Polisi, zinaeleza kuwa serikali juzi ilitumia kiasi cha shilingi 10,682,031 kama gharama za usafiri wa helikopta za kumpeleka na kumrudisha kiongozi huyo mahakamani mkoani Morogoro.
MTANZANIA Jumatano kupitia vyanzo vyake vilivyoko ndani na nje ya Jeshi la Polisi, limedokezwa kuwa gharama za kurusha helikopta kwa dakika 45 hadi saa moja ni dola za Marekani 3,000 hadi 3,300 ambazo ni sawa na shilingi 5,341,032.85 .
Hivyo gharama za kwenda na kurudi kwa saa jumla yake ni dola za Marekani 6,600 ambazo ni sawa na shilingi 10,682,031.
Akithibitisha hilo, Kamanda wa Kikosi cha Anga wa Jeshi la Polisi, Antony Mwami alisema gharama za kurusha helikopta kwa dakika 45 ni dola 3,000 ambazo ni sawa na shilingi milioni tano.
TSVANGIRAI ATUHUMIWA KUDHARA MAHAKAMA...!!!
Kiongozi wa upinzani nchini Zimbabwe, Morgan Tvangirai anakabiliwa na makosa ya kudharau mahakama kufuatia matamshi aliyoyatoa kuhusiana na idara hiyo.
Jaji wa mahakama kuu Chinembiri Bhunu amesema waendesha mashtaka watafahamishwa kuhusu tuhuma hizo. Haya yanajiri wakati chama cha Tsvangirai cha Movement For Democratic Change kimepoteza kesi mbili kulalamikia uchaguzi mkuu wa Julai 31 mwaka huu.
P.T
Mahakama ya kikatiba ilitangaza kwamba Rais Robert Mugabe alishinda uchaguzi kwa njiya huru na haki. Mugabe alipata asili mia 61 ya kura dhidi ya asili mia 34 alizopata Bw. Tsvangirai.
Viongozi hao wamekuwa katika utawala wa kugawana madaraka ulioafikiwa mwaka 2009 kufuatia uchaguzi mkuu uliokumbwa na utata. Chama cha MDC kiliondoa kesi yake mbele ya mahakama ya kikatiba kikisema hakikua imani ya kupata haki.
RAIS DKT SHEIN AFANYA MABADILIKO YA MAWIZARA ZANZIBAR.
RAIS
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Ali
Mohamed Shein kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya kifungu cha 53 cha
Katiba ya Zanzibar ya 1984 amefanya marekebisho katika muundo na
majukumu ya baadhi ya Wizara za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Kufuatia
marekebisho hayo, baadhi ya shughuli za Wizara zimeunganishwa na
kuundiwa Wizara mpya na baadhi zimehamishiwa katika wizara mpya na
baadhi zimehamishiwa katika wizara nyengine.
Hata hivyo marekebisho hayo hayakuongeza idadi ya Wizara na kwa hivyo zinaendelea kubaki wizara 16. Kwa
mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na
Katibu Mkuu Kiongozi Dkt. Abdulhamid Yahya MzeeMarekebisho ya muundo na
shughuli katika baadhi ya Wizara ni kama ifuatavyo.
Tuesday, August 20, 2013
AJARI KATIKA MSAFARA WA MBIO ZA MWENGE DODOMA
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma Bi. Suzzan Kaganda Akiongea na waandishi wa Habari hawapo pichani, Katika ukumbi wa Mikutano wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma Kuhusia na ajali iliyotokea katika kijiji cha Fufu, Kata ya Fufu, Wilaya ya Chamwino, ambapo takribani magari matano (5) yaliyokuwa kwenye msafara wa Mwenge wa Uhuru, yakitokea Wilaya ya Dodoma kuelekea kwenye makabidhiano Wilaya ya Mpwapwa, ambapo Watu wapatao tisa (9) walijeruhiwa katika ajali hiyo
Mkuu
wa Kikosi cha Usalama Barabarani Wilaya ya Dodoma, Mrakibu wa Jeshi la
Polisi Bw. Bonventure Nsokolo Akikagua moja ya gari iliyoharibika katika
ajali iliyotokea katika kijiji cha Fufu, Kata ya Fufu, Wilaya ya
Chamwino, ambapo takribani magari matano (5) yaliyokuwa kwenye msafara
wa Mwenge wa Uhuru, yakitokea Wilaya ya Dodoma kuelekea kwenye
makabidhiano Wilaya ya Mpwapwa
Baadhi
ya washiriki walikuwa katika msafara wa kwenda kukabidhi mwenge kutoka
wilaya ya Dodoma mjini na kuukabidhi katika wilaya ya Mpwapwa
wakiangalia moja ya magari yaliyoharibika baada ya kutokea ajali hiyo
Gari namba DFP.7178 TOYOTA LAND CRUISER (AMBULANCE) ambayo ni mali ya
Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma. Picha na Luppy Kung’alo wa Jeshi la Polisi Dodoma
KIM AITA 24 STARS KUIVAA GAMBIA
Kikosi cha Taifa Stars.
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen ameita kambini wachezaji 24
kujiandaa kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya Gambia
itakayochezwa Septemba 7 mwaka huu nchini humo.
Wachezaji hao wanatakiwa kuripoti kambini Agosti 29 mwaka huu kabla ya saa 1 kamili usiku. Kambi ya Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itakuwa kwenye hoteli ya Accommondia jijini Dar es Salaam.
Wachezaji hao wanatakiwa kuripoti kambini Agosti 29 mwaka huu kabla ya saa 1 kamili usiku. Kambi ya Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itakuwa kwenye hoteli ya Accommondia jijini Dar es Salaam.
Makipa walioitwa katika timu hiyo Juma Kaseja (Simba), Mwadini Ali (Azam), Ally Mustafa (Yanga) na Aishi Manula (Azam). Mabeki ni Aggrey Morris (Azam), Kelvin Yondani (Yanga), Shomari Kapombe (Simba), Nadir Haroub (Yanga), Erasto Nyoni (Azam), Vincent Barnabas (Mtibwa Sugar) na David Luhende (Yanga).
Viungo Khamis Mcha (Azam), Salum Abubakar (Azam), Said Dilunga (Ruvu Shooting), Frank Domayo (Yanga), Athuman Idd (Yanga), Haruna Chanongo (Simba), Amir Kiemba (Simba), Mrisho Ngasa (Yanga), Simon Msuva (Yanga), John Boko (Azam), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo), Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo) na Juma Liuzio (Mtibwa Sugar).
MWALIMU WA MIAKA 30 AMWEKA KUNYMBA MWANAFUNZI WA MIAKA 14....!!!
MWANAFUNZI wa darasa la saba katika Shule ya Msingi ya Sokoine, Manispaa ya Dodoma (jina linahifadhiwa), anadaiwa kuwekwa kinyumba na mwalimu wake David Macha (30).
Mwanafunzi huyo wa miaka 14 ni kati ya watoto wanaofadhiliwa na shirika lisilo la kiserikali la Compassion International Tanzania kituo cha Tz 807 FPCT kilichoko Chamwino.
Hata hivyo, katika hali ya kushangaza Jeshi la Polisi mkoani hapa, limelalamikiwa na wazazi wa mtoto huyo kwa kitendo cha kumlinda mtuhumiwa licha ya kupewa taarifa za uhalifu huo kwa zaidi ya miezi mitano sasa, limeshindwa kumchukulia hatua.
Uchunguzi wa Tanzania Daima ambao umethibitishwa na wazazi wa mwanafunzi huyo, umebaini kuwa mwalimu Macha amekuwa akifanya mapenzi na mwanafunzi huyo kwa zaidi ya miezi mitano sasa.
Wazazi wa mwanafunzi huyo wanathibitisha kuwa kwa zaidi ya miezi mitano, mtoto wao alikuwa na tabia ya kutoroka nyumbani nyakati za usiku na kulala nje, jambo ambalo lilianza kuwatia mashaka na kuanza kufuatilia nyendo zake.
Walidai kuwa wakati mwingine alikuwa akirudi nyumbani asubuhi kwa ajili ya kujiandaa kwenda shule na anapoulizwa alikolala, alisema alikuwa katika mkesha.
Akisimulia mkasa huo, mjomba wa mwanafunzi huyo, Silas Mjengi, alisema binti yao anaishi na mama yake pekee katika eneo la Area ‘A’ mjini hapa baada ya mzazi huyo kutengana na mumewe.
"MWAKYEMBE ALINDWE" BARAZA LA VIONGOZI WA DINI
Mwenyekiti wa baraza la viongozi wa dini la kupambana na dawa za kulevya nchini Shekhe wa mkoa wa Dar es Salaam Alhad Mussa Salum
BARAZA la Viongozi wa Dini la Kupambana na Dawa za Kulevya nchini, limetaka Jeshi la Polisi kumpa ulinzi Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe, kutokana wa ujasiri alioonesha kupambana na dawa za kulevya.
Kutokana na ujasiri huo, Baraza hilo ambalo Mwenyekiti wake ni Shekhe wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum, limempongeza Dk Mwakyembe na kusisitiza umuhimu wa ulinzi huo kwake, kwa kuwa vita aliyoanza, inaweza kuhatarisha usalama wake.
Shekhe Salum alisema hayo jana alipozungumza na vyombo vya habari Dar es Salaam, akiongeza kuwa kitendo alichofanya waziri huyo kimeonesha uzalendo, ujasiri na upendo alionao kwa Taifa, alilosema linalochungulia kaburi kutokana na dawa hizo.
Maombi maalumu
Kutokana na ujasiri huo na hatari inayomkabili Dk Mwakyembe, pamoja na kutaka ulinzi wa Polisi, Shekhe Salum pia aliomba viongozi wa dini wa imani zote, kumwombea kwa uthubutu huo. Alisema watampa ushirikiano kwa kuunga mkono juhudi anazoonesha ambazo kwa kiasi kikubwa anaamini zitarejesha heshima ya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA).
“Kwa dhati kabisa Baraza linataka mawaziri na viongozi nchini kuiga mfano wake, ili kuliondoa Taifa letu katika sifa mbaya ya dawa za kulevya,” alisema Shekhe Salum.
Kwa mujibu wa kiongozi huyo, viongozi wana uwezo mkubwa wa kujitolea kupambana na dawa hizo, isipokuwa hakuna aliye tayari kuonesha uthubutu wake, suala alilosema kwa kiasi kikubwa limechangia mapambano dhidi ya dawa hizo kutofanikiwa.
MTANDAO WA KAGAME WAZIDI KUMCHOKOZA KIKWETE.... WADAI MAMA SALMA KIKWETE NI MNYARWANDA...!!!
Mtandao wa News of Rwanda umeendelea kutuchokonoa watanzania ili kuupima msimamo wetu.....
Baada ya kukurupuka na madai kwamba Rais Kikwete si mtanzania halisi na kwamba ni mtu mwenye asili ya Burundi, mtandao huo umekuja na kioja kipya....
Taarifa iliyotolewa jana tarehe 19/08/2013 na mtandao huo inadai kwamba mke wa Rais Kikwete aitwaye Mama Salma Kikiwete ni mnyarwanda wa kabila la wahutu ( mhutu )..
Katika maelezo yake, mtandao huo umeenda mbali na kudai kuwa Mama Salma Kikwete ni binadamu wa rais wa zamani wa Rwanda, Juvenal Habyarimana na ndo maana rais Kikwete alitoa ushauri wa mazungumzo ya amani kati ya Kagame na waasi....
VIGOGO WAJUMUISHWA KESI YA LEMA....!!!
Mkuu wa Chuo cha Uhasibu cha Arusha, John Nanyaro na Mkuu wa
Polisi wa Wilaya ya Arusha, Gillis Mroto, leo wanaanza kutoa ushahidi
katika kesi ya tuhuma za uchochezi inayomkabili Mbunge wa Arusha Mjini,
Godbless Lema.
Mashahidi wengine katika kesi hiyo ni, Mkaguzi wa Polisi Bernard Nyambanyana na mwenzake aliyetajwa kwa jina moja la Jane.
Hali kadhalika PC Godfrey na Joachim Mahanyu .
Wakili wa Serikali, Elinenya Njiro, alitaja mashahidi wengine watakaotoa
ushahidi wao mahakamani kuwa Faraji Mnepe, Benjamin Simkanga na Naibu
Hamidu, wote kutoka Chuo cha Uhasibu.
SHOMARY KAPOMBE KUJIUNGA NA AS CANNES YA UFARANSA
Hatimaye beki wa kimataifa wa klabu ya Simba na timu ya taifa ya Tanzania Shomary Kapombe amefuzu majaribio aliyokuwa akifanya barani ulaya kwa kufanikiwa kujiunga na klabu ya AS Cannes ya Ufaransa.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka mwandishi wa BBC - Abdul Mohamed ni kwamba Shomary Kapombe amefuzu majaribio hayo na sasa zimebakia taratibu tu za uhamisho ili ajiunge rasmi na timu hiyo ya AS Cannes inayoshiriki kwenye ligi daraja la nne nchini Ufaransa.
Kapombe aliondoka nchini takribani mwezi mmoja uliopita na kwenda barani ulaya kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa.
Mtandao huu upo katika kujaribu kufanya mawasiliano na uongozi wa Simba ili kupata taarifa rasmi juu ya usajili huu wa Shomary Kapombe.Credits: Shaffih Dauda Blog
Kwa mujibu wa taarifa kutoka mwandishi wa BBC - Abdul Mohamed ni kwamba Shomary Kapombe amefuzu majaribio hayo na sasa zimebakia taratibu tu za uhamisho ili ajiunge rasmi na timu hiyo ya AS Cannes inayoshiriki kwenye ligi daraja la nne nchini Ufaransa.
Kapombe aliondoka nchini takribani mwezi mmoja uliopita na kwenda barani ulaya kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa.
Mtandao huu upo katika kujaribu kufanya mawasiliano na uongozi wa Simba ili kupata taarifa rasmi juu ya usajili huu wa Shomary Kapombe.Credits: Shaffih Dauda Blog
KESI YA MWANARIADHA OSCAR PISTORIUS ALIYEMUUA MPENZI WAKE KWA KUMPIGA RISASI ITAANZA MACHI MWAKANI....!!!
Mwanariadha mlemavu wa Afrika Kusini Oscar Pistorius amefika mahakamani ambapo ameshtakiwa kwa mauaji ya mpenzi wake.
Oscar Pistorius alizingirwa na umati mkubwa wa waandishi wa habari alipofika mahakamani mji wa Pretoria. Akiandamana na jamaa wake mwanariadha huyo alifanya maombi maalum. Punde baada ya kusomewa makosa ya kumuua Mwanamitindo Reeva Steenkamp, Oscar alionekana kupatwa na huzuni kubwa.
Monday, August 19, 2013
CHADEMA WAVAANA NA POLISI KWENYE MAANDAMANO YAO...!!!
Maandamano ya chama cha CHADEMA yaliyokua yanafanyika huko Mwanza yamegeuka vurugu baada ya wandamanaji kuanza kupambana na polisi.
CHADEMA walikua wakiandamana katika kushinikiza Meya wa Ilemela Henry Matata aachie ngazi kwani hana sifa zakua meya, baada ya kuvuliwa uanachama na chama hicho.
Katika picha zilizokirushwa kupitia televisheni ya Barmedas Tv ya Mwanza, barabara zimeonekana zikiwa zimefungwa kwa mawe na miti, huku katika maeneo mengine uchafu ukiwa umejazwa barabarani na matairi kuchomwa.
katika mtaa wa Mission waandamanaji wamefunga barabara kwa uchafu uliokua katika dampo moja kando ya barabara hiyo.
Maandamoano hayo yalikua yamalizikie viwanja vya furahisha ambapo viongozi wa chadema walikua wahutubie.
Chanzo cha vurugu hizo hakijafahamika, ikizingatiwa CHADEMA walikua na kibali cha kufanya maandamano hayo.
Hivi sasa polisi wametanda mitaani katika kudhibiti vurugu hizo na hali inaonekana kutengamaa.
PONDA AFIKISHWA MAHAKAMANI MOROGORO HII LEO ASOMEWA MASHITAKA 3.
Sheikh Issa Ponda Akiwa mahakamani mkoani Morogoro asubuhi ya leo Sheikh Ponda Amesomewa Mashtaka Matatu katika Mahakama ya mkoa wa Morogoro Likiwemo la uchochezi alilolitoa Kwenye Mkutano wa Hadhara Tarehe 10 mwezi huu Ambapo Inadaiwa alisema kwamba ''Ndugu waislamu Msikubali uundwaji wa kamati za ulinzi na usalama za Misikiti kwani kamati hizo zimeundwa na Bakwata ambao ni vibaraka wa Serikali ''katika viwanja vya shule ya kiwanja cha ndege Mkoani Morogoro.
VIONGOZI DECI JELA MIAKA 3 AU FAINI MILIONI 21 KILA MMOJA
SHERIA imewatia hatiani viongozi 4 kati ya 5 wa kampuni
ya Development Entrepreneurship for Community Initiative (DECI)
iliyokuwa ikijihusisha na shughuli za kuvuna na kupanda fedha nchini
kinyume cha sheria.
Hayo
yalibainika hii leo wakati wa hukumu ya kesi hiyo iliyodumu kwa miaka
kadhaa huku mtuhumiwa mmoja katika kesi hiyo akiachiw huru baada ya
upande wa mashitaka kushindwa kuthibitisha makosa yake.
Akisoma
hukumu hiyo iliyo andikwa na Hakimu Mwenzake, Stuart Sanga, Hakimu wa
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, Aloyce Katemana
alitafsiri sheria kadhaa zilizowatia hatiani watuhumiwa hao.
Vigogo
hao waliotiwa hatiani ni pamoja na Jackson Sifael Mtares, Dominick
Kigendi, Timotheo Saigaran ole Loitginye, Samwel Sifael Mtares,Samwel
Mtalis huku sheria ikimwachia huru Arbogast Francis Kipilimba baada ya
kushindwa kumtia hatiani.
SIRI ZA TRAFIKI FEKI ZAFICHUKA, YADAIWA ALIANZA KAZI MKOANI SINGIDA,AKAJIPA UHAMISHO WA KIKAZI HADI DAR...!!!
SIKU chache baada ya kukamatwa kwa
askari 'feki' wa Usalama Barabarani mwenye cheo cha Sajini, akifanya kazi ya
kuongoza magari eneo ya Tabata Kinyerezi, Dar
es Salaam, mambo mapya yamezidi kubainika juu ya
sababu za mtu huyo kujiingiza katika kazi hiyo bila kutambuliwa na Jeshi la
Polisi.
Habari
zilizolifikia gazeti hili kutoka vyanzo vya kuaminika, zinasema trafiki huyo
'feki', ambaye inadaiwa jina lake
halisi ni James Juma
Hussein (45), mkazi wa Kimara Matangini, alianzia kazi hiyo mkoani Singida
kabla ya kujipa uhamisho wa kikazi kwenda Dar es Salaam.
Chanzo
chetu kilieleza kuwa, trafiki huyo alikuwa na shemeji yake aliyeitwa Shaban
ambaye aliajiriwa na Jeshi la Polisi Kitengo cha Usalama Barabarani aliyekuwa
akifanyia kazi mkoani Tabora.Vyanzo
vyetu viliongeza kuwa, baada ya shemeji yake kufariki mkoani Tabora, trafiki
huyo alipata mwanya wa kuchukua nguo za kazini alizokuwa akizitumia shemeji
yake.
MECHI YA NGAO YA JAMII YA YANGA NA AZAM YAINGIZA MIL 208
Mechi
hiyo ya Ngao ya Jamii (Community Shield) kuashiria ufunguzi wa msimu
mpya wa 2013/2014 iliyochezwa jana (Agosti 17 mwaka huu) Uwanja wa
Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 208,107,000. Washabiki 26,084
walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo ambayo ilimalizika kwa Yanga
kushinda Azam bao 1-0.
Mgawanyo
wa mapato ya mechi hiyo uliokuwa kama ifuatavyo; asilimia 18 ya Kodi ya
Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 31,745,135.59, asilimia 10 ya mchango wa
kusaidia jamii sh. 20,810,700, gharama ya tiketi sh. 7,309,866.
Uwanja
sh. 22,236,194.76, gharama za mchezo sh. 13,341,716.86, Chama cha Mpira
wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 5,188,445.44, TFF sh.
13,341,716.86 na Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh.
6,670,858.43. Kila klabu imepata mgawo wa sh. 43,731,183.03.
MAJINA YA WALIOKOSEA KUJAZA FOMU ZA MIKOPO KWENDA CHUO KIKUU
Tizama majina kwa kubofya hapa chini
DEREVA DALADALA AFUMANIWA GESTI AKIWA NA BINTIYE.....!!!
Za mwizi 40:Temba baada ya kufumaniwa na mkewe akiwa na bintiye.
AMA kweli za mwizi arobaini! Mwanaume aliyetajwa kwa jina moja la Temba, mkazi wa Kimara-Rombo, Dar ambaye ni dereva wa daladala amefumaniwa laivu na mkewe akiwa gesti na binti yao wanayemlea.
NI MTEGO
Tukio hilo la aina yake lilijiri wiki iliyopita kwenye gesti hiyo iliyopo maeneo hayohayo ya Kimara-Rombo, majira ya saa 10:00 jioni ambapo Temba ambaye ni dereva wa daladala inayofanya safari kati ya Kimara na Kariakoo alinaswa kiulaini baada ya kuwekewa mtego.
OFM YATAARIFIWA
Baada ya mke wa Temba kuweka mambo vizuri aliitaarifu Oparesheni Fichua Maovu ya Global Publishers ambapo alihojiwa maswali muhimu kisha kutakiwa kuwajulisha polisi ili kuhakikisha kuna usalama wa kutosha.
MWANZO WA YOTE HADI FUMANIZI
Kwa mujibu wa mke wa Temba, siku kadhaa nyuma aligundua kuwepo kwa mawasiliano ya kimapenzi kati ya mumewe na binti yao hivyo akalazimika kufanya uchunguzi wa kina.
BARCELONA YAFANYA KUFURU, YAIGONGA LEVANTE 7-0
Wachezaji wa Barcelona wakishangilia bao lao la kwanza lililofungwa na Alexis Sanchez dakika ya tatu.
Lionel Messi kama kawaida yake katupia mbili katika mechi ya leo.
Sunday, August 18, 2013
HII NDIO SABABU ILIYOFANYA AGNESS MASOGANGE KUSHTUKIWA NA POLISI NA HATIMAE KUKAMATWA NA UNGA AFRIKA KUSINI
Kilichomponza Masogange kukamwatwa ni pale alipochelewa kutoka uwanjani hapo kutokana na kujiremba, kitu ambacho kilisababisha kufanyiwa upekuzi wa dharura na askari ambaye hakujua kuhusu mpango huo. Tembelea http://jambotz8.blogspot.com/ kila siku.
Taarifa zinabainisha kwamba, baada ya Masogange na wenzake kufanikiwa kupita katika maeneo ya ukaguzi ya uwanja wa ndege wa Oliver Tambo nchini Afrika Kusini, mwenzake waliyesafiri pamoja aliyetajwa kwa jina la Mangunga alifanikiwa kuondoka uwanjani hapo na mabegi matatu yenye jumla ya kilo 60 za madawa hayo ya kulevya bila kujulikana.
"Kilichomponza Masogange ni pale alivyokuwa anajiremba baada ya kuruhusiwa kupita katika vizuizi vyote. Kiuhakika hakukamatwa katika mashine, bali ulikuwa ni ukaguzi usio rasmi uliofanywa na Polisi. Nadhani huyu Askari aliyewashika hakujua kuhusu mpango huo." kilisema chanzo kimoja ndani ya jeshi la Polisi kama ilivyonukuliwa katika gazeti la Tanzania Daima la Tarehe 17/8/2013
NEWS OF RWANDA WAANDIKA KUWA RAIS JAKAYA KIKWETE ANAWEZA KUWA NA ASILI YA GITEGA BURUNDI....!!!
Mtandao wa News of Rwanda juzi umeandika
makala yenye kichwa cha habari, ‘If President Kikwete is Tanzanian,
then most Rwandans being expelled are Tanzanians too’ na kuandika kile
linachodai kuwa Rais Kikwete anaweza kuwa na asili ya Burundi.
Kwa mujibu wa wazee wa Burundi waliohojiwa na mtandao huo, umedai Rais Kikwete anaweza kuwa na asili ya Giteka, Burundi.
“They are of Rwandan origin, but speak Kirundi and solely prefer to be viewed as Burundians. By virtual of that country’s laws, they are indeed Burundians,” limeandika. So where did President Jakaya Mrisho Kikwete come from? There are no original residents of Bagamoyo in Tanzania where Kikwete’s parents are traced. Most people from that area are remnants of slaves who were seem as unfit for the market during the slave trade era.
“They are of Rwandan origin, but speak Kirundi and solely prefer to be viewed as Burundians. By virtual of that country’s laws, they are indeed Burundians,” limeandika. So where did President Jakaya Mrisho Kikwete come from? There are no original residents of Bagamoyo in Tanzania where Kikwete’s parents are traced. Most people from that area are remnants of slaves who were seem as unfit for the market during the slave trade era.
Subscribe to:
Posts (Atom)